Njiwa Media

Njiwa Media Njiwa Media ni ukurasa unaomilikiwa na Kanisa la Moravian Tanzania-JK.

TANZIA: MZEE DAUDI WALUGANO MWANJA AFARIKI DUNIANjiwa Media tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mzee Da...
26/07/2025

TANZIA: MZEE DAUDI WALUGANO MWANJA AFARIKI DUNIA

Njiwa Media tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mzee Daudi Walugano Mwanja, ambaye ni Baba Mkwe wa Askofu Kenan Salim Panja wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini (KMT-JK).

Mzee Daudi Mwanja hakuwa tu mkwe wa Baba Askofu Panja, bali pia ni mzazi wa Mchungaji George Mwanja anayehudumu katika Ushirika wa Katumba, Jimbo la Kusini.

Taarifa za awali kuhusu msiba huu zimetolewa na mmoja wa wanafamilia wa karibu, na kwa jitihada za kumpata Makamu Mwenyekiti KMT-JK, Mch. Jair Sengo zimefanyika, ambapo amethibitisha kutokea msiba huu na kwamba Ibada ya mazishi itafanyika siku ya Jumatatu 28/07/2025 huko Kijiji cha Ibungu Wilaya ya Ileje.

Njiwa Media inaendelea kufuatilia kwa karibu taarifa za msiba huu, na itakuwa ikikuletea habari zaidi kadri zitakavyopatikana.

Apumzike kwa Amani Mzee wetu Daudi Mwanja. Amina.

KANISA LA MORAVIAN TANZANIA JIMBO LA KUSINI LAMUAGA MCH. JOHANNES KLEMM KWA HESHIMA KUBWA.Rungwe, Tanzania.Kanisa la Mor...
22/07/2025

KANISA LA MORAVIAN TANZANIA JIMBO LA KUSINI LAMUAGA MCH. JOHANNES KLEMM KWA HESHIMA KUBWA.

Rungwe, Tanzania.
Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini limemuaga rasmi aliyekuwa Team Leader Africa na Program Manager Tanzania wa Shirika la Mission 21 lenye makao yake makuu nchini Uswisi, Mchungaji Johannes Klemm.

Hafla hiyo imefanyika katika viunga vya Butusyo Guest House, yaliyopo Makao Makuu ya Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini – Rungwe Mission, chini ya uratibu wa Kamati Tendaji ya Jimbo hilo.

Tukio hilo limehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya za Kanisa la Moravian Tanzania pamoja na wakuu wa Idara na Taasisi zake, ikiwa ni ishara ya kuthamini mchango mkubwa uliotolewa na Mch. Klemm katika kipindi chote alichohudumu nchini Tanzania.

Shirika la Mission 21 limekuwa mshirika muhimu wa maendeleo katika Jimbo la Kusini, likifadhiri miradi mbalimbali ya kijamii hususan katika sekta ya elimu na afya.

Wakizungumza katika hafla hiyo, viongozi wa Jimbo wamemshukuru Mch. Klemm kwa moyo wake wa kujitoa, ushirikiano wa karibu, na uongozi wenye maono. Wamesisitiza kuwa mchango wake utaendelea kudumu katika historia ya maendeleo ya Kanisa na jamii kwa ujumla.

Hafla hiyo pia imehudhuriwa na Mratibu wa Miradi ya Mission 21 nchini Tanzania, Bi. Adrianne Sweetman, pamoja na msaidizi wake, Ndugu Isaack Eliakimu.

PICHA ZAIDI: Ibada ya harambee ya ununuzi wa basi la kwaya ya ST. John Hus Choir Kyela Moravian hapa Kanisa la Moravian ...
20/07/2025

PICHA ZAIDI: Ibada ya harambee ya ununuzi wa basi la kwaya ya ST. John Hus Choir Kyela Moravian hapa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini, Ushirika wa Kyela Mjini.

20/07/2025

Ibada inaendelea hapa Kanisa la Moravian Ushirika wa Kyela Mjini. Ibada hii ni maalumu kwa uchangiaji wa ununuzi wa basi jipya la ST. John Hus Choir Kyela Moravian .

PICHA: Kutoka hapa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Ushirika wa Kyela Mjini, panapofanyika Ibada ya Harambee ...
20/07/2025

PICHA: Kutoka hapa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Ushirika wa Kyela Mjini, panapofanyika Ibada ya Harambee ya kuchangia ununuzi wa basi jipya la Kwaya ya ST. John Hus Choir Kyela Moravian.

20/07/2025

Kwaya ya Paradise ikiwa madhabahuni hapa Kanisa la Moravian Ushirika wa Kyela mjini, kwenye Harambee ya kuchangia ununuzi wa basi la ST. John Hus Choir Kyela Moravian .

20/07/2025

Hali ilivyo ndani ya Kanisa la Moravian Ushirika wa Kyela Mjini katika Harambee ya kuchangia ununuzi wa basi la ST. John Hus Choir Kyela Moravian

Picha kadhaa ndani ya Kanisa la Moravian Tanzania Ushirika wa Kyela Mjini, ST. John Hus Choir Kyela Moravian wakiwa wana...
20/07/2025

Picha kadhaa ndani ya Kanisa la Moravian Tanzania Ushirika wa Kyela Mjini, ST. John Hus Choir Kyela Moravian wakiwa wanaimba wimbo wao wa kwanza katika harambee yao ya kuchangia ununuzi wa basi lao.

Kwaya mbalimbali zipo Ibadani hapa kushiriki harambee hii. Njiwa Media tupo hapa kukuhabarisha kile kitakachokuwa kinaendelea.

20/07/2025

Nje ya Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini Ushirika wa Kyela mjini, ambapo leo panafanyika Ibada kubwa ya Harambee ya uchangiaji ununuzi wa basi jipya la Kwaya ya ST. John Hus Choir Kyela Moravian.

Kwaya kutoka pande mbali mbali zipo Kanisani hapa. Njiwa Media tumeweka kambi hapa, tafadhali endelea kuwa nasi.

Address

Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Njiwa Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Njiwa Media:

Share