BOMBA Fm RADIO 104.1 Mhz

PUMZIKA KWA AMANI
06/08/2025

PUMZIKA KWA AMANI

20/06/2025

HII SIO YA KUKOSA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ame...
04/02/2025

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amefunga rasmi Kongamano la Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) lililofanyika leo tarehe 4 Februari 2025 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Center jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 48 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Katika hotuba yake, Dkt. Tulia amewahimiza wanawake kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika jamii na ndani ya CCM. Akiwasisitiza umuhimu wa maandalizi kabla ya kushiriki katika vinyang’anyiro hivyo, amesema kuwa uongozi unahitaji watu wenye uwezo, dhamira na sifa stahiki na si kwa misingi ya jinsia pekee.

“Ni muhimu kwa wanawake kujiandaa mapema, kujijengea uwezo na kushiriki kikamilifu katika siasa na uongozi. Nafasi za uongozi zinahitaji watu wenye uwezo wa kuleta mabadiliko chanya, si kwa sababu ya jinsia bali kwa uwezo na dhamira ya kweli ya kuwatumikia wananchi,” alisema Dkt. Tulia.

Aidha, Dkt. Tulia amewakumbusha wanawake wa UWT kuendelea kueneza mazuri yanayofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Ametaja juhudi mbalimbali zinazotekelezwa na serikali yake katika maendeleo ya nchi, huku akisisitiza kuwa njia bora ya kutoa shukrani ni kumchagua kwa kura nyingi za ndiyo katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.

https://youtube.com/?si=NtML_ZLmkY0aQa_H
04/02/2025

https://youtube.com/?si=NtML_ZLmkY0aQa_H

TAI MEDIA is a media outlet aimed at informing and educating the community while changing perspectives in all areas of economic social political technology and cultural life.

NANE WADAKWA TUKIO LA KILUVYA.Na Mwandishi Wetu.Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar limesema linawashikilia Watu 8 kwa tuhu...
04/12/2024

NANE WADAKWA TUKIO LA KILUVYA.

Na Mwandishi Wetu.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar limesema linawashikilia Watu 8 kwa tuhuma za tukio la Novemba 11, 2024 eneo la Kiluvya ambapo Watu kadhaa walifanya jaribio la kumteka Mfanyabiashara, Deogratius Tarimo, Mkazi wa Kibaha - Pwani

Kamanda Kanda Maalum ya Polisi, Muliro J. Muliro - SACP amesema Watuhumiwa wamekamatwa kwa nyakati tofauti katika Mikoa ya Dar, Songea Ruvuma na eneo la Mbingu Mlimba Morogoro, pia wamekamata gari aina ya Toyota Raum waliyoitumia wakati wa tukio ikiwa na namba T 237 EGE ambayo si halisi, ambapo uchunguzi umebaini namba halisi ni T237 ECF

Amewataja waliokamatwa kuwa ni Bato Bahati Tweve (umri Miaka 32 – Bondia), Yusuph Abdallah (32), Fredrick Juma (31), Nelson Elimusa Msela (24 - Dereva Tax), Benk Daniel Mwakalebela ‘Tall’ (40), Thomas Ephraim Mwakagile ‘Baba Mage’ (45), Anitha Alfred Temba (27) na Isack Mwaifani (Bondia)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akizungumza jambo na Rais wa Marekani Mhe. Joe...
04/12/2024

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akizungumza jambo na Rais wa Marekani Mhe. Joe Biden kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Marekani, Kongo na Zambia kuhusu Ushoroba wa Lobito (Lobito Corridor), ambapo Tanzania ni mgeni mwalikwa katika Mkutano huo unaofanyika katika Mji wa Lobito nchini Angola tarehe 04 Desemba 2024.

RAIS SAMIA AHITIMISHA ZIARA YAKE YA KIKAZI MKOANI ARUSHA.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu ...
01/12/2024

RAIS SAMIA AHITIMISHA ZIARA YAKE YA KIKAZI MKOANI ARUSHA.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali pamoja na wananchi wa Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro Mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi kwenye mkoa wa Arusha leo Jumapili Disemba 01, 2024. Rais Samia pamoja na shughuli nyingine, alikuwa Mkoani Arusha kwenye maadhimisho ya miaka 25 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyowakutanisha Marais na Wawakilishi wao kutoka nchi zote nane za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na wale wa kimila wa jamii ya Kimasai (Malaigwanani) wanaoishi Ngorongoro na maen...
01/12/2024

Viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na wale wa kimila wa jamii ya Kimasai (Malaigwanani) wanaoishi Ngorongoro na maeneo jirani wakiwa kwenye kikao na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Ikulu ndogo ya Arusha tarehe 01 Desemba, 2024.

CHADEMA MBEYA YAWAFUNDA WATIA NIA YA KUGOMBEA NAFASI YA WENYEVITI WA MITAA JIJI LA MBEYA
05/11/2024

CHADEMA MBEYA YAWAFUNDA WATIA NIA YA KUGOMBEA NAFASI YA WENYEVITI WA MITAA JIJI LA MBEYA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge Jimbo wa Jimbo la Mbeya Mjini na Rais wa Umoja wa...
20/10/2024

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge Jimbo wa Jimbo la Mbeya Mjini na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani(IPU) Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo Oktoba 20,2024 amejiandikisha kwenye Orodha ya wapiga Kura kwaajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Dkt. Tulia amejiandikisha katika kituo cha Uzunguni A Kata ya Sisimba Mbeya Mjini na amewataka Wananchi ambao hawajajiandikisha kutumia Muda uliobaki kujiandikisha ili waweze kutumia haki yao ya Msingi ya kuwachagua Viongozi wanaowataka Kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Address

Mbeya
124

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BOMBA Fm RADIO 104.1 Mhz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share