Noni News

Noni News News around the World

  Aug 18, 2025
18/08/2025

Aug 18, 2025

Takriban watu 30 wamefariki dunia na zaidi ya 1000 kujeruhiwa katika ajali za barabarani zilizohusishwa na sherehe kubwa...
16/08/2025

Takriban watu 30 wamefariki dunia na zaidi ya 1000 kujeruhiwa katika ajali za barabarani zilizohusishwa na sherehe kubwa ya Magal ya 131 ya Touba, moja ya hafla muhimu zaidi ya kidini nchini humo
Kulingana na Kamanda Yatma Dièye, mkuu wa Idara ya Habari na masuala ya umma wa Brigade ya zimamoto wa Kitaifa, jumla ya ajali 270 za trafiki zilirekodiwa tangu Jumatatu, Agosti 12, magari mengi yakihusishwa na kusafiri kwenda au kutoka Touba.
Mnamo 2024, karibu watu 700 walikufa katika ajali za barabarani huko Senegal, na 90% ya ajali mbaya zilitokana na makosa ya kibinadamu
Siku ya Ijumaa, Agosti 15, viongozi wa Senegal walitoa wito wa haraka wa kufuata sheria za trafiki. "Hali hii inahitaji kufuatwa kikamilifu kwa kanuni za trafiki," Kamanda Dièye alisisitiza, akisema kuna hitaji la haraka la uhamasishaji wa pamoja na uwajibikaji barabarani huku serikali ya Senegal ikisisitiza lengo lake la kupunguza ajali za barabarani kwa 50% ifikapo mwaka 2030
Zaidi ya watu milioni sita walikusanyika Touba - karibu km 150 kaskazini mwa mji mkuu, Dakar - mapema wiki hii
Hafla kubwa ya Magal ya Touba inaadhimishwa kila mwaka na ‘Mouride brotherhood’, madhehebu la Kiisilamu la Sufi, kwa heshima ya mafundisho na urithi wa mwanzilishi wake, Shaykh Ahmadou Bamba
Hafla hiyo inaadhimisha kuk**atwa kwake na kufukuzwa kwake na viongozi wa kikoloni wa Ufaransa kwenda Gabon mnamo Agosti 12, 1895.

Rais Donald Trump wa Marekani amesema yeye na Putin wamekuwa na mkutano wenye tija na kwamba wamepiga "hatua kubwa"Trump...
16/08/2025

Rais Donald Trump wa Marekani amesema yeye na Putin wamekuwa na mkutano wenye tija na kwamba wamepiga "hatua kubwa"
Trump na Putin walizungumza kwa pamoja jukwaani kwa takriban dakika 10. Wote wawili walionyesha ishara ya mazungumzo mema waliokuwa nayo wakati wa mkutano wao wa faragha, ingawa ulimalizika bila makubaliano madhubuti
Putin alisema "ana nia ya dhati" katika kukomesha mzozo huo, ambao alielezea kuwa "janga".
Lakini alisema Urusi inahitaji "sababu za msingi" za mzozo huo zitatuliwe kwanza - na akaonya Ukraine na Ulaya hazipaswi "kuhujumu" mazungumzo hayo
Putin, pia alielezea mkutano huo k**a "mahali pa kuanzia kwa utatuzi" wa mzozo huku akisema uhusiano wake na Trump ni "imara" - na kukubaliana na madai ya mara kwa mara ya rais wa Marekani kwamba vita haingeanza ikiwa angesalia madarakani baada ya uchaguzi wa 2020
Kwa upande wake, Trump alisema bado kuna mambo ambayo hawajakubaliana na "hakuna makubaliano hadi maafikiano yawepo" na kuongeza kuwa "hatukufikia" tulipotaka ila tumepiga hatua kubwa
Trump alisema "wamekubaliana mambo mengi" lakini "machache" bado yamesalia, akiongeza kuwa "moja ni muhimu zaidi" bila kutaja hasa ni nini
Trump alimalizia kwa kusema "kuna uwezekano mkubwa" ataonana tena na kiongozi wa Urusi hivi karibuni huku Putin akijibu kuwa: "Wakati ujao itakuwa Moscow"

  Aug 16, 2025
16/08/2025

Aug 16, 2025

Viwango vya kubadilishia fedha za kigeni Aug 15, 2025
15/08/2025

Viwango vya kubadilishia fedha za kigeni Aug 15, 2025

  Aug 15, 2025
15/08/2025

Aug 15, 2025

Mke wa Rais Melania Trump ametishia kumshtaki Hunter Biden kwa zaidi ya $1bn baada ya kudai kuwa alitambulishwa kwa mume...
15/08/2025

Mke wa Rais Melania Trump ametishia kumshtaki Hunter Biden kwa zaidi ya $1bn baada ya kudai kuwa alitambulishwa kwa mumewe na mhalifu wa kingono Jeffyer Epstein

Mawakili wanaofanya kazi kwa niaba ya mke wa rais, ambaye aliolewa na Rais wa Marekani Donald Trump mwaka wa 2005, wameelezea madai hayo kuwa ya "uongo, dharau, kashfa na uchochezi".
Biden, ambaye ni mtoto wa Rais wa zamani wa Marekani Joe Biden, alitoa maoni hayo wakati wa mahojiano mapema mwezi huu, ambapo aliukosoa vikali uhusiano wa zamani wa rais huyo na Epstein.

Donald Trump alikuwa rafiki wa Epstein, lakini amesema wawili hao walitofautiana mwanzoni mwa miaka ya 2000 kwasababu mfadhili huyo alikuwa amewawinda kiharamu wafanyakazi waliokuwa wakifanya kazi kwenye saluni na urembo (spa) katika klabu ya gofu ya Trump ya Florida.

Barua kutoka kwa mawakili wa mke wa rais na iliyotumwa kwa wakili wa Hunter Biden inamtaka abatilishe madai hayo na kuomba radhi, au atachukuliwa hatua za kisheria kwa "fidia ya zaidi ya $1bn".

Inasema kuwa mke wa rais amepata "madhara makubwa ya kifedha na sifa" kwa sababu ya madai aliyorudia.
Pia inamtuhumu mtoto huyo mdogo wa kiume wa Biden kwa kuwa na "historia kubwa ya kufanya biashara kwa majina ya wengine"

Shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) limepiga marufuku watu kuingia viwanjani na vifaa vyenye viashiria vya kisiasa...
15/08/2025

Shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) limepiga marufuku watu kuingia viwanjani na vifaa vyenye viashiria vya kisiasa, dini au vile vinavyokinzana na wadhamini rasmi wa mashindano ya timu za za Taifa kwa wachezaji wa ligi za ndani ya nchi.

Afisa wa ulinzi na usalama wa kitaifa wa fainali hizo za Afrika kutoka Tanzania, Mratibu wa Polisi (SP) Hashim Abdallah amewataka mashabiki wa soka na watanzania kwa ujumla wanapoingia uwanjani kutazama mechi za fainali hizo kutoingia na nguo au vifaa vingine k**a bendera zenye maandishi au alama zenye viashiria vya kiasiasa, dini, au hata vinavyo kinzana na wadhamini rasmi wa mashindano husika.

“Mtu yeyote anayevaa T-shirt ambayo inakinzana na wadhamini wa CAF, mfano ana jezi imeandikwa matangazo yoyote jezi za kidini viashiria vya kisiasa na kidini na mambo mengine hawataruhusiwa uwanjani watavuliwa hizo nguo, na watakwenda kubadilisha au kuigeuza ili mradi lile tangazo lisiweze kuonekana”
Siku za hivi karibuni Tanzania ilipigwa faini ya dola za kimarekani 10,000 kutokana na vitendo vya uvunjifu wa usalama k**a ilivyoanishwa kwenye kifungu cha 82 na 83 cha kanuni za usalama za CAF.

Kanuni za FIFA zinakataza watu kuangia uwanjani na vifaa vyovyote vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani. Hii si kwa mashabiki tu hata wachezaji wakati mwingine hupigwa faini kwa kuingia na vitu hivyo au kujichora maandishi kwenye nguo zao ambayo yanakinzana na kanuni.

Viongozi wa Ulaya wana matumaini baada ya kuwasiliana na Trump kabla ya mkutano wa kilele wa PutinViongozi wa Ulaya wame...
15/08/2025

Viongozi wa Ulaya wana matumaini baada ya kuwasiliana na Trump kabla ya mkutano wa kilele wa Putin

Viongozi wa Ulaya wameonekana kuwa na matumaini makubwa baada ya kufanya mkutano wa kawaida na Donald Trump siku ya Jumatano, siku mbili kabla ya kukutana na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin huko Alaska kujadili kumaliza vita nchini Ukraine.

Trump aliripotiwa kuwaambia viongozi hao wa Ulaya kwamba lengo lake la mkutano huo ni kupata usitishaji wa mapigano kati ya Moscow na Kyiv.
Pia alikubali kwamba masuala yoyote ya kimaeneo yanapaswa kuamuliwa kwa kuhusika kwa Volodymyr Zelensky, na kwamba dhamana ya usalama inapaswa kuwa sehemu ya mpango huo, kwa mujibu wa Emmanuel Macron wa Ufaransa.

Kuzungumza na Trump kumempa Zelensky fursa ya "kufafanua nia yake" na kuipa Ulaya nafasi ya "kueleza matarajio yetu," Macron alisema.

Trump na Makamu wa Rais JD Vance walizungumza na viongozi wa Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Finland na Poland pamoja na mkuu wa Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen na mkuu wa Nato Mark Rutte.

Ulaya imetengwa katika mkutano wa kilele ulioandaliwa kwa haraka huko Alaska na simu yao Jumatano ilikuwa jaribio la mwisho la kuweka masilahi ya Ukraine na usalama wa bara hilo mbele ya mawazo ya Trump.

Mpiganaji wa PARECO huko Nyamilima, Kivu Kaskazini, mwaka wa 2008.Marekani imeliwekea vikwazo kundi lenye silaha nchini ...
15/08/2025

Mpiganaji wa PARECO huko Nyamilima, Kivu Kaskazini, mwaka wa 2008.

Marekani imeliwekea vikwazo kundi lenye silaha nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo linalofanya kazi na serikali ya Kinshasa, chama cha ushirika cha uchimbaji madini nchini humo, na makampuni mawili ya Hong Kong, ikiywatuhumu kuchangia ukosefu wa usalama nchini DRC na uchimbaji madini kinyume cha sheria.

Wizara ya fedha ya Marekani inasema inalenga moja ya makundi yanayofanya kazi na serikali ya DRC, PARECO-FF (Coalition des Patriotes Résistants Congolais-Force de Frappe), ikilishutumu kwa "kuendesha miradi haramu ya uchimbaji madini na ushuru huko Rubaya".

Kundi hilo, linaloundwa zaidi na Wahutu kutoka DRC, lilidhibiti migodi katika eneo la Rubaya - ambayo ina madini ya thamani muhimu kwa sekta ya teknolojia, ikiwa ni pamoja na simu za mkononi -kuanzia mwaka 2022 hadi mapema 2024, kulingana na Marekani.

John K. Hurley, Naibu Waziri wa fedha wa Marekani, alisema kuwa "madini ya migogoro yanaua raia wa Congo, kuchochea rushwa, na kukvuruga biashara halali za kuwekeza nchini DRC."

"Wizara ya fedha haitasita kuchukua hatua dhidi ya mashirika ambayo yanainyima Marekani na marafiki zetu kupata madini ya thamani ambayo ni muhimu kwa usalama wa taifa letu," alisema.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema anahisi yuko kwenye "ujumbe wa kihistoria na kiroho," na "anajitolea sa...
15/08/2025

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema anahisi yuko kwenye "ujumbe wa kihistoria na kiroho," na "anajitolea sana" kwa maono ya Israeli makubwa, ambayo yanajumuisha maeneo ya Palestina, "na labda pia sehemu za Jordan na Misri," kulingana na The Times of Israel.

Gazeti hilo liliripoti kwamba Sharon Gal, mhojiwaji wa idhaa ya Israel i24, ambaye kwa muda mfupi alikuwa mwanachama wa mrengo wa kulia wa Knesset, alimpa Netanyahu hirizi katika mfumo wa "ramani ya Nchi ya Ahadi." Alipoulizwa jinsi alivyojitambulisha na "maono" haya ya Israeli makubwa, Netanyahu alijibu, "Hakika."

Neno "Israeli Kubwa" lilitumika baada ya Vita vya Siku Sita mnamo Juni 1967, ambavyo pia vilijulikana k**a "Naksa," kurejelea Israeli na maeneo iliyokuwa inayamiliki wakati huo, ambayo ni pamoja na Jerusalem Mashariki, Ukingo wa Magharibi, Ukanda wa Gaza, Rasi ya Sinai, na Milima ya Golan.

Gazeti la Israel lilibainisha kuwa "baadhi ya Wazayuni wa awali walitumia maneno haya ku husiana na Israel ya sasa, Gaza, Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na Jordan."

Wakati wa mahojiano hayo , Netanyahu aliulizwa jinsi alivyohisi alikuwa kwenye harakati kwa niaba ya watu wa Kiyahudi. Alijibu, "Mimi niko kwenye ujumbe wa kizazi. Kuna vizazi vya Wayahudi ambavyo vimeota kuja hapa, na vizazi vya Wayahudi vitakuja baada yetu.

Tel aliingia k**a kiungo mbadala katika dakika ya 79Tottenham wamesema "wamechukizwa" na unyanyasaji wa kibaguzi aliopok...
15/08/2025

Tel aliingia k**a kiungo mbadala katika dakika ya 79

Tottenham wamesema "wamechukizwa" na unyanyasaji wa kibaguzi aliopokea mshambuliaji Mathys Tel kufuatia kushindwa kwao na Paris St-Germain kwenye michuano ya Uefa Super Cup.

Klabu hiyo, ambayo ilishindwa kwa mikwaju ya penalti 4-3 baada ya kuongoza kwa mabao mawili kwa moja, ilisema watu waliotuma ujumbe wa matusi kwa Tel kwenye mitandao ya kijamii "si chochote ila waoga".
Tel, 20, aliingia k**a mchezaji wa akiba katika dakika ya 79 na alikuwa mmoja wa wachezaji wawili wa Spurs ambao walishindwa kufunga bao kwenye mikwaju ya penalti.

"Mathys alionyesha ujasiri wa kusonga mbele , lakini wale wanaomnyanyasa si chochote ila waoga - wanaojificha nyuma ya majina ya watumiaji na wasifu ambao haukujulikana kudhihirisha maoni yao ya kuchukiza," Tottenham ilisema.
"Tutashirikiana na mamlaka na mitandao ya kijamii kuchukua hatua kali iwezekanavyo dhidi ya mtu yeyote ambaye tunaweza kumtambua.
"Tunasimama na wewe, Mathys."

Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Noni News posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share