28/10/2025
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Nachingwea kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Fadhiri Liwaka, amefunga kampeni zake kwa kishindo leo Oktoba 28, 2025 katika viwanja vya Maulidi, saa chache kabla ya Uchaguzi Mkuu wa kesho.
Akihutubia maelfu ya wananchi, Liwaka ameahidi kushirikiana na wenyeji wa jimbo hilo katika kuharakisha maendeleo, ikiwemo ujenzi wa barabara ya Nachingwea–Masasi kwa kiwango cha lami, kuboresha huduma za maji, afya, elimu na miundombinu ya barabara.
Liwaka ndiye mgombea pekee wa ubunge katika Jimbo la Nachingwea, na ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuhakikisha utekelezaji wa ahadi hizo unafanyika kwa vitendo.