Simulizi za kapazi

Simulizi za kapazi pata simulizi nzuri za kusisimua zinazoteka hisia za watu

hizi ni simulizi zinazolenga maisha halisi ya binadamu kutokana na changamoto anazopitia...SI RUHUSA KUKOPI, KUJIMILIKISHA AMA KUUZA PASINA RIDHAA YANGU MIMI MWENYEWE

Mkinipa fursa nyingine ya kuwatumikia nitamalizia sehemu ilobaki   AKILI
18/02/2025

Mkinipa fursa nyingine ya kuwatumikia nitamalizia sehemu ilobaki


AKILI

Wimbo gani unakujia kichwani ukiwaona hawa jamaa?
30/09/2024

Wimbo gani unakujia kichwani ukiwaona hawa jamaa?

05/04/2021

NDOA IL

Hakika k**a MUNGU akitaka hiwe itakuwa tu wala haitatokea yeyote Wa kuzuia

Ilikuwa mwaka 2014 mwezi wa 12 kijana mwenye umri Wa miaka 25 anaingia kwenye ndoa rasmi ambapo uchumba wao ulidumu kwa miaka kadhaa na bint mrembo tangu wakiwa shule
Maisha ya ndoa yalianza kwa raha na mazuri mengi huku kijana huyo aitwaye Masoud akizidi kung'aa kazini kwakwe alipokuwa ameajiriwa
Siku nazo hazikuganda hatimaye mwaka 2015 mwezi Wa 9 Vijana hao Masoud na mkewe bi Zena wanabarikiwa kupata mtoto Wa kiume
Furaha ya ndoa ilizidi kuongezeka Mara dufu huku baadhi ya ndugu na majirani wakionea wivu ndoa hiyo iliyojaa amani tele,wapo walotaka kabisa kuona wawili hao wakitengana yote kwa sababu ya furaha walokuwa nayo
MUNGU aliwajaalia kwenye biashara pia zikawa zinaenda sawa siku zote lakini maadui walizidi kuongezeka siku hadi siku,walitumia kila njia kuharibu ndoa hiyo hadi kwenda kwa waganga wa kienyeji kuroga,MUNGU naye umpa MTU atakaye vivyo walivyodhamiria ndo ikawa hatimaye Masoud akaanza kuwa na tabia za ajabu japo hakuwa mlevi Wa pombe wala sigara lakini alijikuta anaingia kwenye umalaya kutokana na pepo la ngono alotumiwa na huyo mchawi alomroga

Kadri siku zilivyozidi kwenda akili yake ikazdi kubadilika kiasi kwamba kuchepuka kwake ikawa ni jambo la kawaida
Mkewe aliumia sana kutokana na tabia aliyokuwa nayo Masoud mana hakuwaga hivyo ila tu amebadilika ghafla kwahiyo akawa ajui afanye nini yeye ni kulalama tu kitu ambacho akisaidii....kwa madada zetu pindi ukiona mumeo yupo hivyo hebu Fanya maombi kwa MUNGU wako ata kufunga funga kwaajili yake mana kuna jambo zito lipo ndani yake nguvu ya MUNGU inahitajika sana hapo

Siku moja katika harakati za kuchepuka Masoud alipata mchepuko ambao...........

Hii ni mwanzo tu simulizi kamili itaanza kuruka kesho

Asanteni

UKO WAPI NIKUFATE ANGEL WANGU(MV NYERERE 04)Maneno ya Angel yalinfanya kujiona kwamba mimi ni nani na nini nifanye hapa ...
08/12/2018

UKO WAPI NIKUFATE ANGEL WANGU
(MV NYERERE 04)

Maneno ya Angel yalinfanya kujiona kwamba mimi ni nani na nini nifanye hapa duniani
"Idd, kumbuka kwamba mama ako ni k**a MAMA angu mzazi hivyo nitakuwa pamoja nanyi kwa kila hatua "
Pumzi ndefu nilishusha baada ya maongezi ya kina ndipo Angel akakata simu nami kufikiria yajayo juu ya MAMA angu

MWEZI MMOJA BAADAE
Mawasiliano kati ya Idd na Angel yalizidi kushamiri lakini Hakuna ata mmoja aloweza kufungua kinywa chake kumtamkia mwenzake kwamba tayari ana hisia nae za mapenzi
Kijana Idd uzalendo ukawa unamshinda ndipo akaamua kujaribu kurusha sumu yake ingawaje alifikiria sana itakuwaje endapo k**a angel atakataa
"Angel, kwakweli ni kipindi kirefu sana tangu niwe na mawasiliano naww na mengi umenisaidia ila tatizo lipo moyoni mwangu "
'tatizo gani Idd ongea tu usijali '
"Angel, kwanza natanguliza samahani k**a nitakukwaza kwa kile nitakachoenda kukwambia "
'ongea tu Idd kuwa huru '
"Angel, najijua wazi kwamba mimi ni maskini sina hadhi ya kuwa naww lkn ukweli nimekupenda sana, nahitaji huwe mke wangu Angel "
'uuuhfff, Idd kwann umeongea maneno ya kumuudhi muumba wako? Sisi matajiri hatuna tofauti na nyie tena yawezekana nyie mkawa mnaishi sana kwa amani kuliko sisi"
'lakini pia naomba muda nilifanyie kazi ombi lako Idd, sawa? '
Angel aliongea kwa sauti nzuri ingawaje bado inaonesha kwamba hakufurahia maneno yale ya Idd

****
Baada ya mawasiliano ya dakika kadhaa Angel alikata huku uso wa furaha ukianza kumchanua kwani alishagampenda kijana Idd tangu muda
'yes, sasa hapa nachotaka kufanya ni kumtumia pesa ya matumizi ili kumfanya Idd asiweze kuishi kwa taabu tena

****
Ndani ya dakika 13 Simu ya Idd ikaingia ujumbe mfupi wa maandishi huku kijana huyo akiwa biz na jembe kulipalilia shamba lake analolilima mboga mhoga za majani
"hafu hawa wa mtandao bhana unaweza ukakuta meseji ya kudiwa salio nililokopa "
Sasa kwa uchovu wa jua kali la kipindi hiki Idd aliifata simu ile alivofungua tu ujumbe akawa amepata nguvu .

30/09/2018

UKO WAPI NIKUFATE ANGEL WANGU (MV NYERERE) 03

Maswali ya Angel yalifanya nikawa na ujasiri wa kumjibu ndipo nlipomwambia kwa sauti ile ya unyonge
"Angel, baada ya matibabu ya mama angu nilimeletewa bill yake kwakweli ni kiasi ambacho sina kwa harakaharaka...." kabla sijamaliza Angel alidakia
'ni kiasi gani Idd wangu?' Angel aliuliza
"laki na nusu " nilimjibu Angel lkn hakuwa muongeaji sana akaniuliza
"hii namba yako unaitumia kwenye huduma za kifedha " Angel aliuliza
"ndio "
'ok subiri kidogo '

Angel alikata simu yake namimi nikaendelea kubaki pale nimejiinamia
Baada ya dakika mbili nikasikia ujumbe umeingia kwenye simu yangu, sikutaka kuufungua nilijua tu meseji za huo mtandao wanakumbushia deni lao la salio nililokopa

Mara simu ikaita nikapokea na kuiweka sikioni
'Idd, nimekutumia laki tano utamaliza hapo hospital then nyingine itakuwa balance yako mi naingia darasani saahizi ' Naam ni Angel ndo alikuwa mpigaji wa ile simu, kwakweli sikuamini sikio langu mana ni k**a mtu alopigwa kofi la sikio
"Angel unasema....? " wakati nauliza hivo kumbe tayari Angel alikuwa ameshakata simu
Nilifungua ule ujumbe kuna laki tano na kumi kwenye laini yangu ambayo ilikuwa na sh 130 tu

Kwa haraka zaidi nikaenda mapokezi kuulizia kwa wakala

Nilitoa pesa kisha nikaenda kulipia ile bill
Mama hakujua wapi zilitoka zile pesa hivyo baada ya muda doctor alipita kisha mama akaruhusiwa kurudi nyumbani

Ilikuwa jioni muda wa saa 1 giza laanza kutanda nikavuta simu kisha nikampigia angle lkn cm iliita bila kupokelewa, nilirudi k**a mara nne hivi haikupokelewa
Baada ya nusu saa naona Angel akinipigia
'Idd my mume, nisamehe bure tafadhali ' yale maneno ya Angel yalifanya nishindwe kuongea chochote
Ikachukua k**a dakika mbili ndipo nikaongea
"Hallo Angel, asante sana kwa msaada wako cjawah kufikiria kujuana na binadam mwenye moyo k**a wako" maneno yalinitiririka hatari mana sikuwah kumiliki laki tano zidi ya hela ndogondogo
"Usiseme hivo idd lkn mi nape.... "

Itaendelea...

30/09/2018

UKO WAPI NIKUFATE ANGEL WANGU (MV NYERERE) 02


Baada ya mazoea ya Muda mrefu angel alitaka kufahamu historia ya maisha yangu hivyo pasina kumficha kitu nikamwambia Yote kuhusu mimi ndipo nayeye aliponieleza historia yake, kwakweli nilitaman sana kuzaliwa kwenye familia k**a yake....


Niligundua kwamba Angel ni mtoto wa pili wa tajiri mmoja wa hapo Mwanza hivyo alikuwa na dada ake ambaye ndo alikuwa wa kwanza kuzaliwa pia Mdogo wake wa kiume ambaye alikuwa wa mwisho kuzaliwa katka familia yao. Angel alikuwa Chuo mwaka wa tatu akisomea masomo ya udaktari kwenye chuo kimoja maarufu sana hapo jijini Mwanza hivyo alitambulika na watu wengi sana hapo chuoni kutakana na umaarufu na utajili wa baba ake

Baada ya mawasiliano ya mara kwa mara kuna siku alinitumia ujumbe mida ya asubuh lakini sikuweza kumjibu kwakuwa sikuwa na salio, alirudia tena mara kadhaa ndipo alipohamua kunipigia baada ya kuona jumbe zake hazijibiwi na sio kawaida kuwa hivyo
Simu yangu iliita kuangalia mpigaji alikuwa ni Angel nilifurahi japo nilikuwa na huzuni kubwa
'habari ya kwako idd? '
"salama tu Angel, umeamkaje? "
'mi nipo poa, mbona ujibu text zangu Idd au umenichoka? '
Kumbuka kipindi hiko bado hatujawa wapenzi hivyo tulikuwa marafiki tu na hatujawahi kuonana uso kwa uso
"hapana Angel nipo hospital mama angu anaumwa amelazwa tangu jana usiku "
'jamani Idd kwann ujanambia au kwakuwa sina msaada kwako, anaumwa nini, vipi amepata matibabu, anaendeleaje??? ' ni maswali aliyouliza Angel kwa wakati mmoja nisijue nianze kujibu lipi kwani sikuwa na furaha ata kidogo mana siunajua tena uchungu wa MAMA
"tiba amepata anaendelea vizuri tu kwani anaweza kutembea sio k**a ilivokuwa jana "
'sasa k**a ni hivyo mbona unahuzuni badala ya kufurahi au kuna tatizo lingine?' angel aliuliza baada ya kusikia sauti yangu haikuwa na furaha
Ukweli nilikuwa sitaki Angel afaham chochote juu ya kile kinachoninyima furaha lakini nikaona wacha tu nimwambie ..... Itaendelea

28/09/2018

UKO WAPI NIKUFATE ANGEL WANGU (MV NYERERE)

Ilikuwa tarehe, siku na mwezi usiosahaulika kwenye kumbukumbuku za Watanzania kwa ujumla pamoja na serikali nzima ikiongozwa na kiongozi mtukufu Mh Rais

Nchi nzima ilifunikwa kwa majonzi huku nyimbo za maombolezo zikiimbwa kila kona ya nchi. BENDERA ya TAIFA ikipepea nusu mlingoti, wachezaji mpira wakivaa vitambaa vyeusi ili kuomboleza kwa pamoja juu ya msiba uliotokea kwenye kivuko cha Mv Nyerere
Rais wetu mtukufu hakuwa nyuma kuomboleza pamoja na wananchi kwa ujumla kwani alitambua vyema kwamba Dunia njia na pia ndo uzalendo wenyewe

IDD ndo jina langu ni mkulima wa mboga mboga mdogo ninayelima ili kupata kipato cha kukidhi mahitaji yangu japo madogomado

Leo hii naandika simulizi hii kwa huzuni kubwa ilonipata kwa kuondokewa na mpenzi wa ndoto yangu aliyefahamika kwa jina la ANGEL

Angel ni binti ambaye tulifahamiana kuipitia mtandao wa kijamii maarufu wa facebook, aliniomba urafiki pasina kinyongo nikamkubalia
Angel hakuacha ku like ata post yangu moja vivohivyo nikafanya kwenye post zake

Angel ni binti mzuri kimuonekano wala wazazi wake hawakukosea kumpa jina la Angel

Tulifahamiana k**a miezi sita ilopita hivyo ule ukaribu ukaanza kuzaa ukaribu zaidi hatimaye tukaanza kuchat inbox

Mazoea yalizidi mipaka mwisho wa siku tukaanza kupeana namba za simu

Muda mwingi wa asubuhi ilikuwa ni desturi yake kunipigia kunijulia hali vivohivyo mchana kwani Muda huo huwa nakuwa shambani nikilima kisha jioni naporudi ndo tunachat

Baada ya mazoea ya Muda mrefu angel alitaka kufahamu historia ya maisha yangu hivyo pasina kumficha kitu nikamwambia Yote kuhusu mimi ndipo nayeye aliponieleza historia yake
Kwakweli nilitaman sana ningezaliwa kwenye familia k**a ya akina Angel mana......

Hii simulizi si ya kweli, ni maneno yaliyotungwa na mwandishi ili kunogesha simulizi yetu
Toa maoni yako kwenye mapungufu kwani Wewe ndo judge wa simulizi zangu

Mpo tayari niachie muendelezo....???

03/04/2018

KIKAO CHA MAGAIDI 02

Idd alipatwa na mshtuko mkubwa ulopelekea kuanguka kwenye kiti alichokalia.
Hakuwa na jinsi tararibu alizisogelea zile gari huku akiwa na hofu kubwa moyoni mwake

Dereva alokuwa kwenye gari la thamani zaidi aliteremka kisha kuzunguuka upande wa kushoto kufungua mlango, ulionekana mguu wa k**e ulojaa sawasawa ukikanyaga ardhi ya mahali hapo kwa madaha sana

Mpaka wakati huo Idd hakujua huo ugeni ni wa nini na nan aliyeshuka kwenye gari ilo la thamani sana akiangaza macho yake huku na kule kana kwamba bado anashangaa hali ya Mazingira yalivyo mabaya kwenye nyumba ya bwana malhotra haliyakuwa kwa Mazingira ya kwetu hiyo nyumba ndo ya thamani na hakuna hata mwenye theruthi ya kujenga nyumba k**a hiyo

"Karibu binti yangu karibu tena nyumban " alikuwa bwana malhotra alikuwa anatoka ndani kuja kumpokea binti yake na hadi wakati huo bado huyo Idd bado ajamfahamu jina lake
"Daddy, miss you so much my lovely " binti alikuwa anamkimbilia baba ake huku akiwa anaongea Lugha ya kiingereza

Kwa muonekano tu binti anaonekana ni msomi sana tena elimu yake ameipatia kwenye shule kubwa huko nchi za ulaya

"namimi pia binti yangu " mzee malhotra alijibu kwa furaha sana wakiwa bado wamekumbatiana
"daddy, where is a get man? " binti alimuuliza baba ake lakini baba alinyoosha kidole kuelekea kwa Idd ishara ya jibu kwa mwanaye
"we mpumbavu kwanini muda mwingi tulikaa getini pasipo kuja kufungua geti " binti wa mzee malhotra aliongea kwa ukali kuonesha kwamba amechukia kwa kitendo hicho
"nisamehe Dada " Idd aliongea kwa sauti ilojaa upole na unyenyekevu
"unaniita mimi Dada,?Hivi una Dada k**a mimi masikini mkubwa wewe " binti wa mzee malhotra alionekana mwenye dharau zilizobalehe mana hakuogopa kuongea maneno ya shombo mbele ya baba ake mzazi
" Sanji mwanangu, kumbuka yule binamu k**a wewe binti yangu kwanini uongee maneno mabaya kiasi hicho " mzee malhotra aliongea
Sasa hapa ndo tunapata kujua jina la binti huyo kwamba anaitwa SANJI

Inaendelea
Usisahau

07/03/2018

Habari ya mwaka jana ndugu zangu wapendwa,poleni kwa kukosa simulizi zetu kwa muda lakini yote hii ni kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wangu
Ndugu zangu nahitaji maoni yenu, tuendelee na au ?

22/11/2017

KIKAO CHA MAGAIDI 01

Katika harakati za kutafuta maisha kijana IDD aliamua kuenda popote pale ilimradi tu asikie kaz ipo na malipo yapo
Ilikuwa kijiji cha MAPOKEO kipatikanacho wilaya ya MVOMERO kijana idd alipata kazi ya ulinzi katika jumba moja kubwa linalomilikiwa na bwana MALHOTRA ambaye ni muindi aliyekuja kufanya maisha yake kijijin hapo
Idd aliendelea hadi ikafika miezi kumi huku kaz zake zikiwa za nje tu yan tangu afike hapo ajawah kupata ruhusa ya kuingia ndan ya mjengo huo zidi ya kuzunguka nje tu ya nyumba hyo

Siku moja idd alipewa habari kwamba kuna ugen hvo afanye mazngira yote ya nje ya nyumba kuwa safi basi idd hakuwa na hiyana mana ndo kazi yake ilompeleka hapo hana budi kuitumikia ingawaje wahindi wanajua kutuma bwana yan utafanya kaz ata ulalapo unakuwa hoi lkn wao hawajal kitu kwako.
Ilikuwa mida ya mchana kuna magari mawili ya kifahari yaliingia lakn idd alipitiwa na usingz hvo hakusikia k**a kuna gari zinapiga honi huko nje kwo kashtuka gari zipo ndani ya geti ilo

Itaendelea
Likes plz!

20/11/2017

SITAKUSAHAU REVOCUTA 32


Hali ya maumiv yalizidi kuupamba moyo wa idd huku akimuangalia mpenz wake akiwa anaondoka,kila mmoja alikuwa anakuwa anamuangalia mwenzake huku akibubujisha machoz...Ndugu msomaji hakuna kitu kibaya k**a yule umpendae kuondoka kipnd ambacho mapenz ndo yapo motomoto

Hawakuweza ata kupata nafasi ya kuagana mana mzee huyo alikuja na gari hvo moja kwa moja wakaondoka huku kijana idd akiwa bado yupo shule anaangalia vile wanavondoka .....

SIMULIZI HII NI YA KWELI KABISA NA MAJINA YA WAHUSIKA NI YA KWELI LAKIN KUNA MENGINE YAMEONGEZEWA ILI KUNOGESHA SIMULIZI HII

Kaa mkao wa kula kusubiri simulizi ijayo ambayo itakufanya uburudike na kujifunza pia kupitia simulizi za kapazi

NARUHUSU KUKOSOLEWA MANA MIMI NI BINADAM YAWEZEKANA KUNA SEHEM NKAWA NIMEFANYA KUKUKWAZA AU NIMEKOSEA KIUANDISHI

Pia asanteni sana wasomaji wangu na wale ambao mmeniruhusu kutumia majina yenu na kwa muda wenu kwa kunfanya nik**aliza simulizi hii

MWISHO WA SESSON 1


20/11/2017

SITAKUSAHAU REVOCUTA 31

Kitendo cha idd kuona ile chupi alovaa bidada revocuta mara nyoka wake akaanza kusumbua kule alipofichwa
"revo kwann lakn,hafu mbona muda wa shule huu"
"hapana idd mi nataka mwenzio mana sijui tutaonana tena" revo aliongea kwa saut ya puani
"najua revo wangu lakn naomba twende shule kwanza hafu tukirud tutafanya" idd alikuwa anamchombeza revo ili akubali waende shule mana muda wa kufika shule ndo ulishafika

Hatimaye revo kalainika kwenda shule baada ya kupewa denda tamu kutoka kwa kijana idd

Mida k**a saa nne baba ake revo mzee lebba alifika shulen hapo wakat huo idd akiwa kwa mbal anamuona yule mzee,kwakwel kisicho riziki hakiliki ndo ilivokuwa mana baada ya muda revo aliitwa stuf ya waalim jwaajil ya kuagwa kisha akawa anatoka huku akifuta machozi.Dalili hzo zilimfanya idd kutambua kilichotokea huko ndan kwamba revo sasa si mwanafunz wa MELELA SEC hali ilopelekea ata yeye kulia kwa uchungu sana,waliagana kwa ishara mana kila mmoja akawa anaogopa ujio wa mzee huyo
....

Address

MOROGORO
Morogoro

Telephone

+255752541979

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Simulizi za kapazi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category