Dizzim Fm

Dizzim Fm Official page for Dizzim fm | Instagram & Twitter | Frequency 93.1 Morogoro |

13/06/2026

MC DULLAYO ameuwasha moto usiku wa TWENZETU KINOLE na kuifanya Kinole kutikisika kwa burudani ya kiwango cha juu!

12/06/2026

Timu ya Taifa ya Senegal national football team imeendelea kuvutia hisia za mashabiki wa soka kwa mitindo yake ya mavazi ya nje ya uwanja, huku wachezaji wakionyesha ubunifu na umoja katika kila safari yao.

Wachezaji wa Senegal walionekana wakiwa katika mavazi ya kipekee walipowasili mjini Newark kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao wa kwanza wa 2026 FIFA World Cup.

Senegal inatarajiwa kuanza kampeni yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo dhidi ya France national football team utakaochezwa Juni 16, 2026.

Mitindo ya mavazi ya timu hiyo imeendelea kuwa gumzo miongoni mwa mashabiki, wengi wakisifu namna ambavyo Senegal imekuwa ikichanganya soka, utamaduni na fasheni katika matukio yake mbalimbali.

Hawa hapa Dastan Fred Kamala na Ney Kasote leo usiku watakuwepo ndani TWENZETU KINOLE!
12/06/2026

Hawa hapa Dastan Fred Kamala na Ney Kasote leo usiku watakuwepo ndani TWENZETU KINOLE!

MC DULLAYO anashuka Kinole!Ijumaa hii ya tarehe 12 Juni 2026, tukutane Sokoni Goda kwa usiku wa burudani, muziki na fura...
12/06/2026

MC DULLAYO anashuka Kinole!

Ijumaa hii ya tarehe 12 Juni 2026, tukutane Sokoni Goda kwa usiku wa burudani, muziki na furaha ya pamoja.

Kwa Kiingilio cha Tsh 5,000 tu

Kinole na maeneo yote ya jirani, huu ndiyo muda wa kutoka na kujiachia. Weka tarehe, waite marafiki zako na twenzetu Kinole!

📍 Sokoni Goda
🗓️ Ijumaa, 12 Juni 2026

Hizi ni baadhi ya picha za wakazi wa KINOLE wakieleza hisia na matarajio yao kuelekea TWENZETU KINOLE usiku wa leo.Tukut...
12/06/2026

Hizi ni baadhi ya picha za wakazi wa KINOLE wakieleza hisia na matarajio yao kuelekea TWENZETU KINOLE usiku wa leo.

Tukutane pale Sokoni Doga tuifanye kuwa usiku wa kukumbukwa!

12/06/2026

Timu ya taifa ya DR Congo national football team imewasili jijini Houston nchini Marekani na kupokelewa kwa shangwe kubwa na mashabiki wake walioko nchini humo pamoja na wale waliokuwa wakisafiri na timu hiyo.

Baada ya kuwasili, wachezaji walipokea jumbe za makaribisho, bendera na sapoti kutoka kwa mashabiki wa Congo, hali iliyoongeza hamasa kuelekea michuano inayowakabili.

Kilichovutia zaidi ni ubunifu wa mavazi yao, ambapo wachezaji walionekana wamevalia suti za kisasa zilizochanganywa na mguso wa utamaduni wa kale, zikiwa na mapambo ya ngozi ya chui begani pamoja na mabegi maalum yenye muundo wa kipekee.

Mavazi hayo yamezua mijadala mitandaoni, huku mashabiki wengi wakisifia ubunifu huo na kujiuliza k**a DR Congo ndiyo timu iliyoongoza kwa ubunifu wa mitindo ya nje ya uwanja katika mashindano haya.

12/06/2026

Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) imeendelea na kampeni ya kuhamasisha uzalishaji wa zao la pareto kwa wakulima katika Mkoa wa Njombe, ikilenga kuongeza ushiriki wa vijana na wanawake katika kilimo hicho chenye soko la uhakika.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Afisa Kilimo wa COPRA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Edwin Margwe, amesema Tanzania ina mahitaji makubwa ya pareto kutokana na uwepo wa kampuni 11 zinazotumia zao hilo k**a malighafi ya viwandani.

Amesema mahitaji ya pareto nchini yanafikia tani 9,000 kwa mwaka, huku uzalishaji wa sasa ukiwa kati ya tani 2,500 hadi 4,000 pekee, jambo linaloonyesha uwepo wa fursa kubwa kwa wakulima kuongeza uzalishaji.

Margwe ameeleza kuwa zao la pareto ni rahisi kulima kwani halihitaji matumizi makubwa ya mbolea wala viuatilifu, huku likiwa na uwezo wa kumpatia mkulima mapato mazuri kutokana na bei yake kuwa ya kuvutia sokoni.

Wakulima walioshiriki katika kampeni hiyo wameishukuru serikali na COPRA kwa kuwafikishia elimu hiyo, wakisema imewasaidia kutambua fursa za kiuchumi zilizopo katika kilimo cha pareto.

12/06/2026

Diwani wa Kata ya Kinole ameikaribisha kwa furaha timu ya 93.1 Dizzim FM na kuwapongeza kwa kuwaletea wakazi wa Kinole burudani kupitia TWENZETU KINOLE.

Aidha, ameibariki show hiyo na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kufurahia burudani huku wakidumisha amani, upendo na mshik**ano.

Address

Mtawala
Morogoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dizzim Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category