Dizzim Fm

Dizzim Fm Official page for Dizzim fm | Instagram & Twitter | Frequency 93.1 Morogoro |

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye pia ni mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama ...
29/10/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye pia ni mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), leo amepiga kura katika Kituo kilichopo Chamwino Jijini Dodoma.

Baada ya kupiga kura, Dkt. Samia amewataka wananchi wote waliojiandikisha kujitokeza kwa wingi kutekeleza haki yao ya msingi ya kupiga kura kwa amani na utulivu, akisisitiza umuhimu wa kulinda amani wakati na baada ya uchaguzi.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP Alex Mk**a amepiga kura ya kuchagua Rais, Mbunge na Diwani katika kituo cha Jeng...
29/10/2025

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP Alex Mk**a amepiga kura ya kuchagua Rais, Mbunge na Diwani katika kituo cha Jengo la Usindikaji mtaa wa Bima kata ya Kihonda Maghorofani Manispaa ya Morogoro.

Mara baada ya kitimiza haki yake ya kikatiba, amesema mkoani humo zoezi la uchaguzi linaendelea katika hali ya utulivu na amani, akiwasihi wananchi kuendelea kujitokeza kupiga kura katika vituo walivypangiwa.


Mpambe wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Brigedia Jenerali Nyamburi Mashauri, ametimiza haki yake ya kikatiba ...
29/10/2025

Mpambe wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Brigedia Jenerali Nyamburi Mashauri, ametimiza haki yake ya kikatiba kwa kupiga kura katika Kituo cha Chamwino Ikulu, kilichopo Kitongoji cha Sokoine, Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma.

Upigaji kura umefanyika huku hali ya utulivu na usalama ikiripotiwa kuimarika katika vituo vyote vya kupigia kura mkoani Dodoma.


Mgombea mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akishiriki zoezi la kupiga k...
29/10/2025

Mgombea mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akishiriki zoezi la kupiga kura ya kumchagua Rais, Mbunge na Diwani katika mtaa wake, eneo la Kilimani, jijini Dodoma leo tarehe 29, Oktoba 2025.


Jitokezeni kupiga kura hali ya Ulinzi na Usalama ni shwari.Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. M***a Ali M***a leo mapem...
29/10/2025

Jitokezeni kupiga kura hali ya Ulinzi na Usalama ni shwari.

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. M***a Ali M***a leo mapema Oktoba 29, 2025 ametumia haki yake ya kikatiba ya kupiga kura katika kituo alichojiandikisha huku akiwasishi wanamorogoro wenye sifa ya kupiga kura kujitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura.

Akibainisha zaidi amewahakikishia wanamorogoro kuwa hadi kufikia asubuhi ya leo mkoa uko shwari na hakuna taarifa yoyote ya uvunjivu wa amani katika maeneo yote ya mkoa huo hivyo wananchi wawe na amani wakati wanatekeleza jukumu lao la kikatiba la kupiga kura.


28/10/2025

DKT SAMIA: MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA NITAYAPA MKAZO WA PEKEE

Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan amehitimisha kampeni zake, huku akiahidi mapambano dhidi ya rushwa ni miongoni mwa mambo atakayoyapa uzito wa pekee.

Dkt Samia ameeleza hayo leo, Jumanne Oktoba 28, 2025, alipozungumza katika Uwanja wa CCM Kirumba mkoani Mwanza, wakati wa hafla ya kuhitimisha kampeni zake za urais.

Amesema atakapopewa ridhaa ya kuiongoza nchi, atasimamia vita dhidi ya rushwa, licha ya hatua kubwa iliyopigwa na Tanzania katika kudhibiti vitendoi hivyo.

“Kama mnavyojua kwa kiasi fulani Tanzania tumepanda kwenye kutokuendekeza rushwa, tumeachana na mambo ya rushwa na hadhi yetu inapanda polepole kwa hiyo tutaendelea na kazi hiyo,” amesema.

Eneo lingine atakalolipa mkazo wa pekee, amesema ni maridhiano, utawala bora na upatikanaji wa katiba mpya n ahata kulinda mil ana desturi za Mtanzania.

“Maeneo haya yana umuhimu wa pekee katika ustawi wa Taifa na watu wake. Maendeleo jumuishi tunayokusudia hayana budi kuendana na falsafa yetu ya R4,” amesema.

Amesema amedhamiria kwa dhati kuanzisha tume ya upatanishi ili kujenga msingi wa umoja wa kitaifa, huku akitarajia kupewa imani ili kuwalipa uadilifu na ufanisi katika kuitumikia nchi na kustawisha utu wa Mtanzania.


Jeshi la Polisi limetahadharisha kuwa kuna kikundi cha watu ambao wanaandaa picha mjongeo na taarifa mbalimbali za matuk...
28/10/2025

Jeshi la Polisi limetahadharisha kuwa kuna kikundi cha watu ambao wanaandaa picha mjongeo na taarifa mbalimbali za matukio yaliyotokea siku za nyuma ambayo yalishashughulikiwa, na mengine ya kutunga ili wayasambaze kwenye mitandao ya kijamii yaonekane yametokea kipindi hiki au muda mfupi uliopita.

Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi imetahadharisha kuwa wapo pia walioandaliwa k**a ambavyo baadhi wameshajitokeza kuzungumza na kutoa taarifa zenye tungo tata, zenye kutaka kuleta taharuki pamoja na kukusanya matukio ambayo yalitokea nchi zingine na kuyatengeneza kwa kuyawekea sauti zenye lafudhi ya Kiswahili ili yaonekane yametokea nchini.

“Pia wamepanga kuchukua picha za baadhi ya viongozi na kuyawekea maneno na sauti zenye matamko ya upotoshaji ili ionekane wao ndiyo wanazungumza au wanayatamka wakati si kweli,” imeeleza taarifa ya Polisi.


Zoezi la kura ya mapema limeanza rasmi leo katika visiwa vya Zanzibar ambapo wasimamizi wa uchaguzi, watumishi wa Tume y...
28/10/2025

Zoezi la kura ya mapema limeanza rasmi leo katika visiwa vya Zanzibar ambapo wasimamizi wa uchaguzi, watumishi wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), pamoja na vikosi vya ulinzi na usalama wanashiriki kupiga kura kabla ya siku kuu ya uchaguzi itakayofanyika Oktoba 29.

Zoezi hilo linafanyika kwa mujibu wa sheria na taratibu za uchaguzi ili kuruhusu makundi yenye majukumu maalum siku ya uchaguzi kutekeleza majukumu yao bila kukosa haki ya msingi ya kupiga kura.

Licha ya changamoto ya mvua kunyesha katika maeneo mbalimbali ya Unguja na Pemba, zoezi linaripotiwa kuendelea kwa utulivu na usalama huku ulinzi ukiimarishwa katika vituo vyote.

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar imetoa wito kwa washiriki wa zoezi hilo kuzingatia sheria, maelekezo ya maofisa wasimamizi na kudumisha amani ili kufanikisha hatua hii muhimu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29.


 📰
28/10/2025

📰

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limethibitisha kumshikilia na kumhoji Mfanyabiashara Jenifer Bilikwiza Jov...
27/10/2025

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limethibitisha kumshikilia na kumhoji Mfanyabiashara Jenifer Bilikwiza Jovin maarufu ‘NIFFER’ (26) mkazi Masaki Peninsula Kinondoni kwa tuhuma za kuhamasisha vurugu na kuharibu miundombinu katika maeneo mbalimbali jijini hasa siku za kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025.

Taarifa imeeleza kuwa hatua zaidi za kisheria zinaendelea kuzingatiwa dhidi ya mtuhumiwa.


27/10/2025

Tunavipenda vyama vyote na tunahimiza umoja ndiyo maana majirani wanaokuja ndani ya Chama Cha Mapinduzi wanakaribishwa kwa mikono miwili, hapa wanapata jukwaa la kuzungumza, kushirikiana na kujenga taifa letu pamoja.

Sisi hatuhamasishi fujo wala uhasama. Kiongozi wa CCM anayeonyesha chuki au kutaka vurugu haendani na misingi yetu ya utu, amani na kazi. Chama chetu kinaamini kila MwanaCCM anadhamira ya kujenga, si kuharibu.

Ikiwa unataka kushiriki kujenga taifa, njoo tuungane kujenga nchi na chama chetu kwa heshima na uwazi.


"Sijui kwanini watu mnazungumzia kuhusu maandamano kwa sababu chama ambacho kinaweza kikaleta maandamano ni ACT tu na si...
27/10/2025

"Sijui kwanini watu mnazungumzia kuhusu maandamano kwa sababu chama ambacho kinaweza kikaleta maandamano ni ACT tu na sisi tunashiriki uchaguzi. Kwahiyo, hata sidhani k**a mnapaswa kupoteza rasilimali za umma kuhangaika na hilo jambo." - Zitto Kabwe, Mgombea Ubunge Kigoma Mjini kwenye kikao cha wadau wa uchaguzi mkoani Kigoma


Address

Mtawala
Morogoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dizzim Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category