13/05/2026
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limethibitisha kupatikana kwa sehemu ya kichwa cha marehemu James Rogers Temba, mwanafunzi wa mwaka wa pili wa Chuo cha IFM, kilichokuwa kikitafutwa baada ya mauaji yaliyotokea mwishoni mwa mwezi Aprili mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa ya polisi, sehemu hiyo ya mwili ilipatikana eneo la Kitunda Kibeberu, Ilala jijini Dar es Salaam ikiwa imefukiwa ardhini, kufuatia uchunguzi wa kina ulioendelea tangu tukio hilo liripotiwe rasmi Aprili 30, 2026.
Polisi wamesema jumla ya watuhumiwa watano wanashikiliwa kuhusiana na tukio hilo, akiwemo mganga wa kienyeji anayetambulika kwa jina la Said Ally maarufu “Side”, huku taratibu za kisheria zikiendelea ili hatua zaidi zichukuliwe dhidi ya watuhumiwa hao.