Dizzim Fm

Dizzim Fm Official page for Dizzim fm | Instagram & Twitter | Frequency 93.1 Morogoro |

WAZIRI KOMBO, KABUDI WAKUTANA NA NAIBU WAZIRI MKUU WA MISRI, TANZANIA YAMWAGIWA SIFA.Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikia...
19/12/2025

WAZIRI KOMBO, KABUDI WAKUTANA NA NAIBU WAZIRI MKUU WA MISRI, TANZANIA YAMWAGIWA SIFA.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo na Waziri wa Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Prof. Palamagamba Kabudi wamekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu wa Misri ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Viwanda na Uchukuzi Mhe. Kamel Al-Wazir Disemba 18, 2025 katika Ofisi zake zilizopo kwenye Mji wa Utawala Jijini Cairo nchini Misri.

Katika Mazungumzo yao, Mawaziri hao wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika masuala mbalimbali yakiwemo Uchukuzi, Kilimo pamoja na Viwanda.

Pamoja na ushirikiano mzuri uliopo kati ya mataifa haya mawili, Mhe. Balozi Kombo amemhakikishia Mhe. Naibu Waziri Mkuu Kamel kuendelea kushirikiana na Misri katika Nyanja mbalimbali kwa manufaa ya mataifa yote mawili.

Aidha, kwa upande wake Mhe. Naibu Waziri Mkuu Kamel, amemueleza Mheshimiwa Kombo juu ya nia ya Misri kujenga viwanda vikubwa katika eneo lililopo Kwala Mkoani Pwani, kutokana na sera nzuri za uwekezaji pamoja na maendeleo ya kuimarisha miundombinu thabiti ya kuwezesha kuwekeza katika mazingira mazuri na ya uhakika.


Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imesema inafanya maandalizi ya kusajili watoto wenye umri wa chini ya ...
19/12/2025

Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imesema inafanya maandalizi ya kusajili watoto wenye umri wa chini ya miaka 18 ili kuwapatia namba ya utambulisho wa kipekee (Jamii Namba) itakayotumika tangu kuzaliwa hadi mwisho wa maisha ya mtu.

Ameyasema hayo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, katika Kituo cha Kuchakata Taarifa cha Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), wakati wa ziara yake ya kukagua uzalishaji wa vitambulisho.

Ameongeza kuwa zoezi hilo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Samia Suluhu aliyoyatoa Agosti 10, 2023, na kwamba jumla ya shilingi bilioni 11.3 zimetengwa kwa ajili ya usajili wa watoto.


  Hatua ya awali ya usikilizaji wa kesi 17 za kupinga matokeo ya uchaguzi wa Uwakilishi, zilizofunguliwa na waliokuwa wa...
19/12/2025

Hatua ya awali ya usikilizaji wa kesi 17 za kupinga matokeo ya uchaguzi wa Uwakilishi, zilizofunguliwa na waliokuwa wagombea wa Chama cha ACT WAZALENDO katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, imekamilika katika Mahak**a Kuu ya Zanzibar iliyopo Tunguu.

Mrajisi wa Mahak**a Kuu, Valentine Katema, amesema baada ya taratibu zote za awali kukamilika, ofisi yake itayawasilisha majalada ya kesi hizo kwa Jaji Mkuu wa Zanzibar kwa ajili ya kupangiwa majaji watakaosikiliza mashauri hayo.

Mrajisi Katema ameahirisha kikao cha leo, akieleza kuwa jukumu lake ni kukamilisha hatua za awali kabla ya Jaji Mkuu kuendeleza mchakato wa kisheria unaofuata.

Kesi hizo 17 zinahusu pingamizi dhidi ya matokeo ya uchaguzi wa Uwakilishi, ambapo wagombea wa ACT WAZALENDO wanapinga kutangazwa kwa wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa washindi. Kati ya kesi hizo, tisa zimefunguliwa Unguja na nane Kisiwani Pemba.

Wagombea wote 17 walihudhuria mahak**ani wakisindikizwa na viongozi wa kitaifa wa chama pamoja na wanachama wao. Baada ya utambulisho wa mawakili wa pande zote mbili, Wakili wa waombaji, Suleiman Abdalla, aliomba mahak**a iwawezeshe walalamikiwa kuwasilisha hati za majibu ya majibu, k**a ilivyoahidiwa katika kikao cha awali kilichofanyika tarehe 10 Disemba 2025.

Upande wa walalamikiwa uliomba muda wa kupitia majibu hayo ili kubaini iwapo kuna haja ya kuwasilisha majibu ya ziada.

Walalamikiwa katika kesi hizo ni Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Upande wa serikali uliwakilishwa na jopo la wanasheria likiongozwa na Wanasheria Waandamizi Salim Said, Mbarouk Suleiman Othman, Ali Issa Abdalla na Maulid Ame Mohamed kwa niaba ya ZEC.

Kwa upande wa Pemba, kesi hizo zinatarajiwa kutajwa tena tarehe 23 Disemba 2025 kwa ajili ya kukamilisha taratibu za awali.

Majimbo yanayopinga matokeo Unguja ni pamoja na Nungwi, Kijini, Mkwajuni, Chaani, Tumbatu, Bumbwini, Mtoni, Mwera, Welezo, Mwanakwerekwe, Pangawe, Kiembesamaki, Amani, Chumbuni, Mpendae, Malindi na Makunduchi.

Kwa Pemba ni majimbo ya Kojani, Micheweni, Wawi, Chake Chake, Chonga, Kiwani, Chambani na Mkoani.


Staa mkubwa wa muziki wa Hip Hop nchini Marekani, Wiz Khalifa amehukumiwa na Mahak**a ya Romania kifungo cha miezi tisa ...
19/12/2025

Staa mkubwa wa muziki wa Hip Hop nchini Marekani, Wiz Khalifa amehukumiwa na Mahak**a ya Romania kifungo cha miezi tisa jela kwa kosa la kuvuta bangi jukwaani akiwa anafanya shoo nchini humo.

Rapa huyo ambaye jina lake halisi ni Thomaz Cameron Jibril, alikiri kuvuta bangi wakati wa onyesho lake katika tamasha la Beach, Please! lililofanyika mwaka 2024 katika Mji wa Costinești, Romania.

Hata hivyo, hukumu hiyo ilitolewa bila yeye kuwepo mahak**ani, na haijulikani iwapo Wiz Khalifa yupo nchini Romania, kwani mara ya mwisho alionekana Jumanne akiwa anatumbuiza pamoja na Gunna, California nchini Marekani.

Maafisa wa polisi wa Romania walisema alikuwa na zaidi ya gramu 18 za bangi na alitumia kiasi kingine akiwa jukwaani, jambo ambalo ni kinyume na sheria za Romania.

Wiz Khalifa alisema katika chapisho lake kwenye mtandao wa X siku moja baada ya tukio hilo kuwa hakukusudia kuikosea heshima nchi hiyo na kuomba radhi.


“Napenda kuwambia kwamba mchakato wa mabadiliko ambao ulianza 2017 sasa unakwenda kufikia tamati. Ni kipindi kigumu tume...
19/12/2025

“Napenda kuwambia kwamba mchakato wa mabadiliko ambao ulianza 2017 sasa unakwenda kufikia tamati. Ni kipindi kigumu tumepita ukiacha Ujerumani hakuna sehemu nyingine unatumika hivyo tumeona changamoto ilivyokuwa namna ya kuupitisha. Unaitwa Hybrid. Kusema kwa uwazi ni miaka nane ambayo ilikuwa na changamoto sana.”

“Kikao chetu cha mwisho tulipitisha Katiba ambayo k**a sio leo au kesho itasajiliwa. Hili ni jambo kubwa kwa Simba, miaka nane ilikuwa kupanda na kushuka lakini sasa tunaingia makubaliano ya kujua mwekezaji atafanya nini na wanachama watafanya nini. Kubwa tulikuwa tumesimamisha kutoa kadi na sasa tunaenda kuanza kutoa kadi. Nawahakikishia tunaenda kuwa klabu ya kwanza yenye wanachama wengi sio ndani tu ya Tanzania hata nje.” - Mwenyekiti wa Bodi Simba SC, Crescentius Magori.



19/12/2025

: Serikali imeanza mpango wa kuunganisha kitambulisho cha Taifa na Huduma nyingine za kiserikali ikiwemo Bima ya Afya,Leseni ya udereva na Masuala ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ili kuepusha utitiri wa vitambulisho pale mwananchi anapohitaji huduma mbalimbali.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene akizungumza katika Kikao Kazi cha Tathmini ya Utekelezaji wa Ahadi za siku Mia Moja za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kinachofanyika mkoani Pwani chini ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, Wakuu wa Wilaya na Viongozi wengine wa juu wa ngazi ya mkoa.


Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imewasili Morocco kwa ajili ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025...
19/12/2025

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imewasili Morocco kwa ajili ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025) zinazotarajiwa kuanza Jumapili, Desemba 21.

Stars imewasili ikitokea Cairo, Misri ambako iliweka kambi ya maandalizi kwa takribani wiki mbili na kucheza mechi za kirafiki kwa ajili ya kujiweka sawa na michuano hiyo.

Taifa Stars iko Kundi C na itaanza kampeni yake Jumanne, Desemba 23 dhidi ya Nigeria ‘Super Eagles’, ikisaka matokeo chanya ya kihistoria katika michuano hiyo.

Ratiba ya mechi za Stars
Desemba 23: Tanzania vs Nigeria
Desemba 27: Tanzania vs Uganda
Desemba 30: Tanzania vs Tunisia


19/12/2025

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma amesema mgao wa mirabaha ya tozo za hakimiliki za wasanii itatolewa Januari 23, 2026.


19/12/2025
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo, amelaani tabia ya baadhi ya viongozi wa dini kutumia mamlaka na ushawishi...
18/12/2025

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo, amelaani tabia ya baadhi ya viongozi wa dini kutumia mamlaka na ushawishi wao kwa waumini kuhalalisha migogoro na migawanyiko ndani ya mataifa yao.

Leo, ambaye ni Papa wa kwanza kutoka nchini Marekani, ameyasema hayo kupitia ujumbe wa kurasa nne uliotolewa kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Amani Duniani ya Kanisa Katoliki, yanayolenga kusisitiza umuhimu wa kulinda, kuimarisha, na kudumisha amani katika jamii.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Desemba 18, 2025, Papa Leo amesema kumekuwa na baadhi ya viongozi wa dini wanaotumia kigezo cha sera za uzalendo, k**a nyenzo ya kupandikiza chuki miongoni mwa waumini kitendo ambacho amekiita ni kufuru, au dhambi kubwa inayomdharau na kumtukana Mungu.

"Kwa bahati mbaya, imekuwa jambo la kawaida zaidi kuivuta lugha ya imani katika vita vya kisiasa, kubariki utaifa, na kuhalalisha vurugu na mapambano ya silaha kwa jina la dini," amesema Papa.

Amesema waumini lazima wajue kukanusha kikamilifu, mafundisho na maelekezo yote ya viongozi wa dini ambao wamekuwa na tabia hii, ili kuondoa uwezekano wa kutokea kwa migogoro ndani ya Taifa.

DKT. MWIGULU: AMANI NI MSINGI WA MAENDELEOWaziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 18, 2025 amezungumza na wakazi w...
18/12/2025

DKT. MWIGULU: AMANI NI MSINGI WA MAENDELEO

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 18, 2025 amezungumza na wakazi wa Kiwira mkoani Mbeya ambapo yupo kwenye ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya umma na mali za watu binafsi ambazo zimeathirika na vurugu zilizotokea Oktoba 29, 2025.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amewaeleza wananchi hao kuwa kila Mtanzania anapaswa kuilinda amani iliyopo kwani ndio msingi wa maendeleo. “Kila mtanzania anapaswa kuilinda Tanzania”

Amesema kuwa Watanzania wanapaswa kuwa makini na watu wenye nia ovu dhidi ya Tanzania na kuhamasisha vurugu zinazoathiri shughuli za kiuchumi na kijamii.

“Tunaelewa lengo lao ni rasilimali zetu, Tanzania ina rasilimali adhimu barani Afrika na wanajua ili kuzipata ni lazima kuwavuruga watanzania ambao wameungana, hili msikubali amani yetu ndio kila kitu”


Serikali imeeleza kuwa itaendelea kuboresha mazingira kwa wafanyabiashara wa ndani ili kuzifikia fursa za soko la kimata...
18/12/2025

Serikali imeeleza kuwa itaendelea kuboresha mazingira kwa wafanyabiashara wa ndani ili kuzifikia fursa za soko la kimataifa.

‎Akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 18, 2025, Waziri wa Biashara na Viwanda, Judith Kapinga amesema kuwa uchumi unahitaji kuendana na mahitaji ya sasa na ushindani wa kimataifa.

‎Kapinga amesema Dira 2050 inaweka viwanda na uzalishaji k**a msingi wa mabadiliko ya kiuchumi kwa kutambua kwamba Tanzania itafikia kwa urahisi maendeleo ya kudumu.

Ameongeza kuwa thamani ya bidhaa inazalisha ajira, inapunguza uingizaji wa bidhaa nje ya nchi, inavutia uwekezaji.

‎Kapinga amesema katika sekta ya biashara, Dira ya 2050 inasisitiza kuimarisha ushiriki wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa.

‎Amefafanua kuwa takwimu za kibiashara zinaonyesha kuwa thamani ya ujumla ya mauzo ya nje ya bidhaa na huduma nchini imeongezeka kwa zaidi ya asilimia 9.8 kufikia takribani Sh14.72 bilioni kwa mwaka 2024, ikilinganishwa na mwaka 2023.


Address

Mtawala
Morogoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dizzim Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category