ALII TV

ALII TV Alii TV ni channel ya YouTube tunapost video mbalimbali zikiwemo nyimbo mpya vichekesho muvi Kali zilizotafsiriwa kwa kiswahili tunaomba u subscribe

ALII TV YOUTUBE CHANNEL __KWA NYIMBO MPYA MUVI KALI ZILIZO TAFSIRIWA VICHEKESHO habari mbalimbali na matukio vinapatikana kwenye channel yetu

17/03/2020
Serikali ya Tanzania imetangaza kuwa, tayari imechukua hatua kadhaa za tahadhari ili kukabiliana na maambukizi ya Virusi...
16/03/2020

Serikali ya Tanzania imetangaza kuwa, tayari imechukua hatua kadhaa za tahadhari ili kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona na kwamba kwa sasa nchi iko salama.

Kauli hiyo ya serikali imetolewa jijini Dodoma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt Hassan Abbasi wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari.

Amesema kuwa, serikali inaendelea kufanya jitihada mbalimbali kuhakikisha virusi hivyo vya corona sio tu haviingii nchini, lakini pia kuzuia kusambaa kwa maambukizi endapo vitaingia.

“Zipo hatua zinazochukuliwa ndani ya taasisi na wizara moja moja, lakini pia zipo hatua za kitaifa za kukabiliana na virusi hivyo, na hivyo naomba kuwatoa hofu Watanzania kuhusu Corona” amesema Dkt. Abbasi.

Njia muhimu za kujinga na virusi vya Corona

Aidha ametaja miongoni mwa hatua hizo kuwa ni ile ya serikali kuandaa utaratibu maalumu katika maeneo ya viwanja vya ndege na maeneo ya mipakani, ambapo watu hawapimwi homa ya corona bali joto la mwili ili kuangalia endapo joto limezidi kiwango cha kawaida cha binadamu.

Wakati nchini Tanzania hali ya mambo ikiwa hivyo, Serikali ya Rwanda imethibitisha kesi nyingine nne za maambukizi ya virusi vya Corona na kufanya idadi ya kesi hizo kufikia tano.

Nchi Kenya pia, jana kulithibitishwa kesi mbili mpya za virusi vya Corona katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

Rais Kenyatta ameagiza kufungwa kwa shule zote za kutwa nchini humo kuanzia leo Jumatatu, huku shule za bweni zikipewa hadi Jumatano kutekeleza agizo hilo. Aidha Vyuo Vikuu na taasisi za elimu za juu nchini humo zimetakiwa kufungwa kufikia Ijumaa ijayo

15/03/2020

:Mtu mmoja amefariki dunia papo hapo na wengine saba kujeruhiwa baada ya magari mawili ya abiria kugongana katika eneo la njia panda ya Runzewe, Biharamulo na Bwanga wilayani Chato mkoani Geita. ALII TV

 :Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amefunga shule zote nchini humo kutokana na kuongezeka kwa watu wawili ambao wamepatikana...
15/03/2020

:Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amefunga shule zote nchini humo kutokana na kuongezeka kwa watu wawili ambao wamepatikana na virusi vya Corona nchini humo.

Watu hao wawili walikuwa wametangamana na mgonjwa wa kwanza aliyepatikana na virusi hivyo. ALII TV

 :Serikali ya Tanzania yasema mpaka sasa hakuna mgonjwa wa Corona, yawataka wananchi kupuuza taarifa zinazosambazwa kati...
15/03/2020

:Serikali ya Tanzania yasema mpaka sasa hakuna mgonjwa wa Corona, yawataka wananchi kupuuza taarifa zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii.Soma zaidi->https://bit.ly/2IPqj8U. ALII TV

 :Mvua kubwa zimenyesha tena na kulizoa daraja la Muda la Kiegeya na kulikata upya kalavati katika barabara kuu ya Morog...
15/03/2020

:Mvua kubwa zimenyesha tena na kulizoa daraja la Muda la Kiegeya na kulikata upya kalavati katika barabara kuu ya Morogoro Dodoma eneo la Mkange Kiegeya.

"Ndugu zangu Watanzania mnapoomba corona isiingie Tanzania, msiishie hapo tu tafadhali!, kwenye maombi yenu ongezeni na ...
15/03/2020

"Ndugu zangu Watanzania mnapoomba corona isiingie Tanzania, msiishie hapo tu tafadhali!, kwenye maombi yenu ongezeni na kuwaombea Watanzania walioko Mataifa mbalimbali Duniani nao wasipatwe na Corona!! 🙏, sijui K**a na-Make sense lakini!!🤷‍♂️"-Msanii Roma Mkatoliki ambae yupo Marekani kwa sasa

(Wanawake watano na Mwanaume mmoja) baada ya ukaguzi mmoja alikutwa na homa, kikohozi na mwili kuchoka” - Waziri wa Afya...
15/03/2020

(Wanawake watano na Mwanaume mmoja) baada ya ukaguzi mmoja alikutwa na homa, kikohozi na mwili kuchoka” - Waziri wa Afya Ummy Mwalimu • •

“Wasafiri wote sita walitengwa katika Hospitali ya Mawenzi na kuchukuliwa sampuli zao ambazo zilipelekwa maabara DSM, uchunguzi umebaini wote hawana maambukizi, msafiri aliekutwa na joto kali amebainika kuwa na mafua ya kawaida, wote wameruhusiwa kuendelea na shughuli zao”-UMMY •


“Ninawatoa hofu Wananchi kuwa hadi sasa Tanzania haina mgonjwa mwenye maambukizi ya virusi vya corona, ninapenda kuendelea kuwataka Wananchi wachukue tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huu, pia natoa rai kwa Watu kutosambaza taarifa ambazo hazijathibitishwa na Serikali”- Waziri Ummy
.

Rwanda imethibitisha kuwa na mgonjwa wa kwanza mwenye virusi vya corona, mgonjwa huyo ni Raia wa India ambae ameingia Rw...
14/03/2020

Rwanda imethibitisha kuwa na mgonjwa wa kwanza mwenye virusi vya corona, mgonjwa huyo ni Raia wa India ambae ameingia Rwanda March 08, 2020 akitokea Mumbai, India, Rwanda inakuwa Nchi ya pili Afrika Mashariki kuwa na maambukizi ya corona baada ya Kenya.
TV.
Like
Comments
Share

WANGAPI MNAMJUA HUYU DADA
14/03/2020

WANGAPI MNAMJUA HUYU DADA

Address

Kilombero
Morogoro
MMBAGA11

Telephone

+255714400547

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ALII TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category