05/09/2026
Mwaka 1950, Mwanamama aliyejaa upendo, huruma na kujitolea, alianzisha shirika la kimisionari pale Kalukata India, lilikuwa ni shirika la kuwasaidia wahitaji, Waishio katika mazingira magumu na watu wenye ukata mkubwa.
Mwanamama huyu alijtolea sana katika enzi za uhai wake mpaka pale ambapo alifikia tamati ya uhai wake mnamo September 5, 1997.
Huyu ni Mother Teresa ambae aliachana na mambo yote na kuchagua njia ya utume wa Usister katika kanisa Katoliki Nchini India, na Mwaka 2016, Papa Francis alimtambua Rasmi k**a Mtakatifu wa Kolukata.
Mother Teresa ni mmoja wa watu ninaojifunza kwao kwa maana aliwahi kusema
*"Kupenda kuna maumivu ila unapaswa kupenda kiwango cha kuyavuka hayo maumivu"*
Kutokana na mchango wake kwa jamii ya watu wa Kolukata, Umoja wa Mataifa uliichagua siku ya September 5 kila mwaka kuwa siku maalum ya kutambua mchango wa watu wanaojitolea katika jamii watu wanaofanya matendo ya huruma
Na cha ajabu ni kwamba, wewe ni miongoni mwa watu muhimu wa kukumbukwa kwa matendo yako ya huruma kwa jamii.
Kwa takribani miaka 6 sasa, umekuwa ukishiriki kwa upendo, huruma na kujitolea kuifikia jamii iliyoko kwenye vituo vya kulelea watoto.
Ninajua kuna wakati unafanya kiasi kwamba unakosa hata kakitu nyumbani k**a vile ambavyo @sheddy_brand aliwahi kusema status kwake.
*Kwamba, kila Charity inatukumbusha upendo, pale ambapo umebeba kilo 10 za unga kwenda kuwapelekea wengine ili hali huenda ghetto kwako hauna hata kilo 1 ya unga.*
Kwa niaba ya Umoja wa Mataifa, niwatakie heri katika kumbukizi ya siku ya matendo ya huruma duniani.
Mungu akuhurumie k**a unavyowahurumia wengine, Akustawishe zaidi na zaidi.
*Ni maombi yangu kwamba*
BWANA akubarikie, na kukulinda;
BWANA akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;
BWANA akuinulie uso wake, na kukupa amani.
Ukawe na Maongezeko zaidi na zaidi.
.
Wise
Mratibu