17/03/2026
WATU WAWILI WAFA MAJI NA WANNE WAJERUHIWA KWA RADI MOROGORO.
MOROGORO.
Jeshi la polisi mkoani Morogoro limetoa taarifa ya watu wawili Kufa maji na wengine wanne kujeruhiwa Kwa kupigwa na radi.
Akizungumza na wanahabari Jana March 16 2026, Kamanda wa polisi mkoani Morogoro SACP Alex Mk**a amewataja waliopoteza maisha ni Hamisi Waziri mwenye umri wa miaka 45 mkulima na mkazi wa Kisaye Morogoro pamoja na Nyerere Kidagati mwenye umri wa miaka 50 mfugaji na mkazi wa Mkonowamara wilaya ya Morogoro walikufa maji walipokuwa wakijaribu kuvuka kwenye maji ambapo maji yaliwazidi Nguvu na kuwasomba hatimaye kusababisha vifo vyao.
Matukio hayo yametokea Mnamo March 14 2026, katika kata ya Tegetero na Mkambarani Wilaya ya Morogoro.