Kusini Yetu Online Tv

Kusini Yetu Online Tv Ukarasa maalum wa habari utakaokuweza kupata taarifa zote zinazotokea ndani na nje ya Tanzania.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bi. Bahati Geuzye amelipongeza shirika lisilo la kiserikali la Door of Hope lililopo Mko...
04/07/2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bi. Bahati Geuzye amelipongeza shirika lisilo la kiserikali la Door of Hope lililopo Mkoani Mtwara, kwa kufanya utatuzi wa mashauri 131 na kufikia wananchi 6,735.

Akizungumza katika kikao cha mrejesho wa shughuli za huduma za msaada wa kisheria mkoani Mtwara, uliotolewa na Vikosi kazi vya Msaada wa kisheria kutoka Wilaya ya Mtwara na Tandahimba kilichofanyika leo Julai 4,2025 katika ukumbi wa Veta Manispaa ya Mtwara Mikindani, Bi Geuzye amewataka waendelee kutoa elimu kwa jamii ili kuisaidia Serikali kupunguza migogoro inayopelekea masuala ya ukatili wa kijinsia.

Aidha Bi Geuzye ametoa rai kwa shirika hilo kuhakikisha wanawafikia wananchi wa maeneo ya wilaya za pembezoni, ili kukuza wigo wa kutoa huduma hizo za msaada wa kisheria ambazo zimekuwa kikwazo kwa wananchi hususan wa vijijini.

Kwa upande wake Betilda Rwakatale ambaye ni Mwanasheria wa shirika la Door of Hope mkoani Mtwara, akizungumza Kwa niaba ya Mkurugenzi wa shirika hilo amesema wamefanikiwa kufikia wananchi hao 6,735 katika kata Saba, tatu kutoka Wilaya ya Mtwara na Nne kutoka wilaya ya Tandahimba, huku migogoro mingi ikihusu masuala ya Ndoa.


Chama cha Mapinduzi- CCM, mkoa wa Mtwara kimesema kuwa jumla ya  wanachama wake 98 wamechukuwa fomu na kurejesha kwa aji...
03/07/2025

Chama cha Mapinduzi- CCM, mkoa wa Mtwara kimesema kuwa jumla ya wanachama wake 98 wamechukuwa fomu na kurejesha kwa ajili ya kugombea nafasi ya ubunge katika majimbo 10 yalipo mkoani humo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu wa Siasa Uenezi na mafunzo wa CCM mkoani hapa Bwn. Juma Hassan Namkoveka kwa Waandishi wa habari amesema kuwa watia nia hao wanaume ni 74 na wanawake 24.

Amefafanua kwamba waliotia nia kugombea ubunge jimbo la Mtwara Mjini ni 12 kati yao Wanaume tisa (9) na Wanawake watatu (3), Mtwara Vijijini waliotinia kugombea ni watu wanane (8) kati yao Wanaume watano (5) na Wanawake watatu (3).

Jimbo la Nanyamba wagombea watano (5) kati yao Wanaume wanne (4) na Mwanamke mmoja, Tandahimba waliotia nia wagombea 16 kati yao Wanaume 14 na Wanawake wawili (2).

Kwa upande wa Jimbo la Newala Mjini waliotia nia ni wagombea saba (7) kati yao Wanaume wanne (4) na Wanawake watatu (3), Newala Vijijini waliochukua fomu 10 kati yao Wanaume wanane (8) na wanawake wawili (2).

Aidha Jimbo la Nanyumbu waliochukua fomu ni watu tisa (9) kati yao Wanaume saba (7) na Wanawake watatu (3), Jimbo la Lulindi waliochukua fomu 12 kati yao Wanawaume tisa (9) na Wanawake watatu (3), Jimbo la Masasi Mji waliochukua fomu ni wanane (8) kati yao Wanaume watano (5) na Wanawake watatu (3).

Kadhalika kwa upande wa Jimbo la Ndanda waliochukua fomu na kurejesha 11 kati yao Wanaume tisa (9) na Wanamake wawili (2).

Kutokana na orodha hiyo jimbo la Tandahimba ndio linaoongoza kuwa na wagombea wengi zaidi yakifuatiwa na Mtwara Mjini na Lulindi.



Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC), Daud Msungu, amerejesha rasmi fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge wa...
02/07/2025

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC), Daud Msungu, amerejesha rasmi fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza mara baada ya kurejesha fomu, Msungu amesema ana nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi wa Lindi Mjini kwa uadilifu, uaminifu na kwa kuzingatia Ilani ya CCM.

Mwanasiasa mkongwe na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, Bi. Hawa ...
02/07/2025

Mwanasiasa mkongwe na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, Bi. Hawa Abdulrahman Ghasia, amechukua fomu ya Ubunge katika Jimbo la Mtwara Vijijini, mkoani Mtwara.

Bi. Ghasia amechukua fomu ya kugombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) ikiwa ni sehemu ya mchakato wa chama hicho kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao.

Mtaalamu wa masuala ya Kisheria  na Mkurugenzi wa ofisi ya Mawakili wa Kujitegemea mkoani Lindi Mhe.Zuwena Millanzi, ame...
01/07/2025

Mtaalamu wa masuala ya Kisheria na Mkurugenzi wa ofisi ya Mawakili wa Kujitegemea mkoani Lindi Mhe.Zuwena Millanzi, amechukua fomu ya ubunge viti maalumu kundi la vijana.

Muanzilishi na Mkurugenzi wa Shirika la The Promise For Youth Foundation na mdau wa Maendeleo katika Mipango Miji nchini...
01/07/2025

Muanzilishi na Mkurugenzi wa Shirika la The Promise For Youth Foundation na mdau wa Maendeleo katika Mipango Miji nchini Kijana Isaack Kubilu amechukua fomu ya ubunge jimbo la Mtwara Mjini.

Isaack amechukua fomu hiyo leo Julai Mosi, 2025 ofisi za Chama cha mapinduzi Manispaa ya Mtwara Mikindani.

Amesema dhamira yake ya kuwania nafasi hiyo ni ile shauku iliyopo ndani yake ya kuwaunganisha wananchi wa Mtwara na rasilimali zinazowazunguka.

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Lindi Bi. Tecla Ungele ni miongoni mwa waliochukua fomu  ya kuwania nafasi hiyo ya ubunge...
01/07/2025

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Lindi Bi. Tecla Ungele ni miongoni mwa waliochukua fomu ya kuwania nafasi hiyo ya ubunge viti maalumu Mkoa wa Lindi.

Bi Tecla amekabidhiwa fumo hiyo na Katibu wa umoja wa wanawake Mkoa wa Lindi Katika ofisi za makao makuu ya chama hicho kilichopo Manispaa ya Lindi Mkoani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari Mama Tecla amesema uamuzi wake wa kuchukua fomu na kuomba tena ridhaa ya kuwatumikia Wanalindi ni pamoja na kuwatetea wanawake na watoto wenye nahitaji maalumu Katika Nyanja ya Afya , Elimu na maswala ya uwezeshaji wanawake kiuchumi.

Saidi Buye (32)na nimtoto wa mkulima amechukua fomu ya kuwania ubunge jimbo la Kilwa Kaskazini leo Julai 1,2025.Buye ame...
01/07/2025

Saidi Buye (32)na nimtoto wa mkulima amechukua fomu ya kuwania ubunge jimbo la Kilwa Kaskazini leo Julai 1,2025.

Buye amekabidhiwa fomu hiyo na Katibu wa Chama cha Mapinduzi Kilwa Suraiya Kangusu.

Aidha baada ya kuchukua fomu hiyo Buye amesema kuwa malengo ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge katika jimbo la Kilwa Kaskazini ni kuendelea kumuunga mkono Rais Samia kwani anafanya kazi kubwa kwa wananchi wake.

Amesema pia kutokana na umri alionao amewiwa kugombea ili kuwatumikia wananchi wa Kilwa Kaskazini, kuchochea maendeleo yanayoweza kupatikana katika maeneo ya Kilwa.

"Nitahakikisha nashirikiana na wananchi kwani Kilwa kuna rasilimali nyingi sana,nanikifanya hivyo Kilwa Kaskazini itasonga mbele zaidi"amesema Buye.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara linamshikilia Victor Fransis Thomas (39), mkulima na mkazi wa Kitongoji cha Kadudu, Kijij...
01/07/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara linamshikilia Victor Fransis Thomas (39), mkulima na mkazi wa Kitongoji cha Kadudu, Kijiji cha Lupaso, Wilaya ya Masasi kwa tuhuma za mauaji ya mchungaji wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), Thomas Rajabu Nkasimonga (58), ambaye pia ni mkazi wa kijiji hicho.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara SACP ISSA Suleiman, tukio hilo lilitokea Juni 27, mwaka huu majira ya saa kumi na mbili jioni katika Mtaa wa Misheni, Kijiji cha Lupaso.

Taarifa zinaeleza kuwa siku ya tukio, mtuhumiwa akiwa na baadhi ya ndugu zake alifika kanisani kwa ajili ya kupata huduma ya maombi ya kiroho kutokana na changamoto za kiafya zinazodaiwa kumkabili.

Hata hivyo, baada ya muda mrefu wa maombi, mtuhumiwa alionekana kuchoka, ndipo ndugu zake wakamrejesha nyumbani kwa ajili ya kupumzika na kuendelea na maombi baadaye.

Hali ilibadilika ghafla baada ya mtuhumiwa kufika nyumbani ambapo alitoroka kwa kutumia pikipiki na kurejea akiwa na panga. Alimkimbiza mchungaji huyo na kumshambulia kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake, hali iliyosababisha kifo chake kutokana na majeraha aliyoyapata.

Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa kina kuhusu tukio hili, na mara utakapokamilika, mtuhumiwa atafikishwa mahak**ani kujibu mash*taka yanayomkabili.

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Kata ya Ndoro Katika Kata ya Ndoro halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani Lindi amechuk...
30/06/2025

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Kata ya Ndoro Katika Kata ya Ndoro halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani Lindi amechukua fomu ya kuogombea Ubunge wa viti maalumu Mkoani humo.

Sharifa Mselem amekuwa ni miongoni mwa wanawake waliochangamkia fursa ya kutumia haki ya kikatiba ya kuchaguliwa ambapo mapema Leo juni 30, 2025 amefika Katika ofisi za chama cha mapinduzi CCM Mkoa wa Lindi kwa ajili ya kuchukua fomu.

30/06/2025


Kada maarufu wa Chama cha Mapinduzi wilayani Masasi na Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya ulinzi ya Respect Security Solu...
30/06/2025

Kada maarufu wa Chama cha Mapinduzi wilayani Masasi na Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya ulinzi ya Respect Security Solutions Company limited, Bwn. Faraji Buriani Nandala leo Juni 30, 2025 amechukua fomu ya ubunge wa jimbo la Ndanda.

Hii ni mara ya pili kwa kada huyo kuomba nafasi hiyo ya ubunge jimbo la Ndanda baada ya kufanya hivyo mwaka 2020 na kuwa mshindi wa pili kati ya watia nia 16 waliojitokeza.

"Huu ni muendelezo wa safari niliyo ianza rasmi mwaka 2020 safari ya matumaini, safari ya kwenda kuwatumikia wananchi wa jimbo la Ndanda nina imani wajumbe wa mkutano mkuu wa jimbo watanipokea na kunikopesha imani yao, k**a walivyofanya mwaka 2020 cha msingi waniombee jina langu lirudi niwe miongoni mwa majina matatu yatakayo pitishwa na vikao vya uchujaji vya chama" amesema.

Address

1050
Mtwara

Telephone

+255682907172

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kusini Yetu Online Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kusini Yetu Online Tv:

Share