Mara Online Plus

Mara Online Plus Pata Taarifa zote za ukweli na uhakika Habari, Michezo, Burudani pamoja na Makala.

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis, amefariki dunia leo April 21,2025 kwenye Jumatatu ya Pasaka akiwa na ...
21/04/2025

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis, amefariki dunia leo April 21,2025 kwenye Jumatatu ya Pasaka akiwa na umri wa miaka 88 ambapo Vatican imethibitisha na kusema Papa amefia kwenye makazi yake Vatican na taarifa zaidi kuhusu kifo chake zitatolewa.

Papa ambaye alizaliwa mwaka 1936 hivi karibuni amepitia changamoto ya upumuaji hadi kuhitaji mashine ya kusaidia kupumua na amekuwa akikabiliwa na matatizo ya kiafya ikiwemo maambukizi ya mapafu(nimonia) hadi kupelekea kulazwa kwa wiki kadhaa kabla ya baadaye afya yake kuimarika.

"Tunajua kwamba Simba makao makuu yapo Msimbazi lakini tunakwenda kujenga ofisi za kisasa. Lakini pia kila mwaka tutatoa...
16/04/2025

"Tunajua kwamba Simba makao makuu yapo Msimbazi lakini tunakwenda kujenga ofisi za kisasa. Lakini pia kila mwaka tutatoa Tsh. 100 milioni ya kusaidia kukuza soka la vijana. Kila mwaka pia tutachangia Tsh. 100 milioni kuchangilia pre season. Pia tumeahidi kujenga kituo maalumu cha matibabu ya wachezaji. Kila mwaka pia tutashiriki bega bega katika Simba Day, tutachangia Tsh. 100 milioni kila mwaka."- Mkurugenzi wa Jayrutty Investment Company Limited, CPA Joseph Rwegasira.

Jambo ambalo linanyika hii leo ni jambo ambalo tumelitamani kwa muda mrefu lakini leo limekamilika.”“Timu ya vijana inaf...
16/04/2025

Jambo ambalo linanyika hii leo ni jambo ambalo tumelitamani kwa muda mrefu lakini leo limekamilika.”

“Timu ya vijana inafanya mazoezi kwenye uwanja wa kukodi, timu ya wanawake inafanya mazoezi kwenye uwanja wa kukodi ni senior team peke yake ndio inafanya mazoezi Mo Simba Arena, Bunju. Wanaokodisha waanze kutafuta wateja wengine. Inakuja ndinga mpya, ipo timu wanayo lakini yao itakuwa ya zamani, yetu itakuwa mpya zaidi.”

“Wakati tunaipongeza kampuni ya Jayrutty, tuipongeze pia kamati ya tenda na Bodi ya Wakurugenzi kwa kuwa na mawazo ya kuichagua Jayrutty. Wangekuwa ni viongozi wanaojali maslahi yao wangechangua yeyote lakini sababu wameweka maslahi ya Simba mbele wamemchagua Jayrutty na kumpa mkataba wa miaka mitano ili afanye kile alichokusudia ili Simba izidi kwenda kimataifa.”

“Moja ya ahadi ni kujenga ofisi mpya, watu wa menejimenti ya Simba muanze kushangilia. Mimi mkijenga ofisi mpya naomba unijengee ofisi ya peke yangu. Lakini pia tunajengewa ofisi ya media ni jambo la kupongeza. Kwa sasa tunaongoza mitandao yote ya kijamii na hapo bado hatujajengewa studio. Kwasasa mpinzani wetu ni Al Ahly na Zamalek lakini kwa studio hii tunakwenda kuwapita.”- Semaji Ahmed Ally.

Kampuni ya JAYRUTTY Investment baada ya kusaini mkataba wa miaka mitano na Simba SC, JAYRUTTY wao wameingia mkataba na k...
16/04/2025

Kampuni ya JAYRUTTY Investment baada ya kusaini mkataba wa miaka mitano na Simba SC, JAYRUTTY wao wameingia mkataba na kampuni ya vifaa vya michezo Duniani Diadora.

Mkataba wa JAYRUTTY na Diadora ni kwa ajili ya kufanya production ya jezi na vifaa vyote vya Simba Sports Club.

Mzabuni Mpya wa Jezi za Simba SC Joseph Samson Kupitia Kampuni ya Jayrutty Investment Amehidi Kununua Basi JIPYA Aina ya...
16/04/2025

Mzabuni Mpya wa Jezi za Simba SC Joseph Samson Kupitia Kampuni ya Jayrutty Investment Amehidi Kununua Basi JIPYA Aina ya Irrizar na Ameahidi Kwamba Tutaliona Muda si mrefu.

Klabu ya  rasmi imeingia mkataba wa Uzabuni na kampuni ya Jayrutty Investiment Limited wa Sh.Bl.38,120,400,000 kWa muda ...
16/04/2025

Klabu ya rasmi imeingia mkataba wa Uzabuni na kampuni ya Jayrutty Investiment Limited wa Sh.Bl.38,120,400,000 kWa muda wa Miaka Mitano.

MSHAMBULIAJI WA GABON BOUPENDZA AFARIKI DUNIAMshambuliaji wa kimataifa wa Gabon, Aaron Boupendza (28) amefariki dunia ba...
16/04/2025

MSHAMBULIAJI WA GABON BOUPENDZA AFARIKI DUNIA

Mshambuliaji wa kimataifa wa Gabon, Aaron Boupendza (28) amefariki dunia baada ya kuripotiwa kuanguka kutoka ghorofa ya 11 ya jengo la ghorofa nchini China

Mamlaka za eneo hilo zimeanzisha uchunguzi, huku ripoti zikieleza kuwa kuna uwezekano mchezaji huyo kujiua.

Boupendza alikokuwa akiichezea Zhejiang FC.

Michuano ya Kombe la Muungano itaanza kutimua vumbi Jumatano Aprili 23, 2025 katika dimba la Amaan Zanzibar. Ni wababe w...
16/04/2025

Michuano ya Kombe la Muungano itaanza kutimua vumbi Jumatano Aprili 23, 2025 katika dimba la Amaan Zanzibar.

Ni wababe wa PBZ Premier League dhidi ya wababe wa NBC Premier League.

Ratiba ya mechi:

Jumatano, April 23, 2025
JKU 🆚 Singida Black Stars (Saa 10:15 Jioni)

Alhamisi, April 24, 2025
Zimamoto 🆚 Coastal Union (Saa 8:15 Mchana)
KMKM SC 🆚 Azam FC (Saa 10:15 Jioni)

Ijumaa, April 25, 2025
KVZ FC 🆚 Yanga SC (Saa 2:15 Usiku)

Wizara ya TAMISEMI imesema kupitia ubia kati ya Serikali na Sekta binafsi (PPP) imefanikisha hatua ya kihistoria ya kusa...
16/04/2025

Wizara ya TAMISEMI imesema kupitia ubia kati ya Serikali na Sekta binafsi (PPP) imefanikisha hatua ya kihistoria ya kusaini mikataba na watoa huduma watatu wa uendeshaji wa awamu ya pili ya mabasi yaendayo haraka ambapo imesema mabasi hayo yatapunguza foleni za Dar es salaam na kuharakisha uchumi.

Akiongea leo April 16,2025 Bungeni Jijini Dodoma wakati wa hotuba yake kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2025/2026, Waziri wa TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa amesema “Kwa muda mrefu Watu wa Jiji la Dar es salaam wamekuwa wakisubiri, wengine kwa matumaini, wengine kwa mashaka lakini wote kwa kiu ya mabadiliko, leo kwa mara ya kwanza tunasema, subira yao haikuwa ya bure, kupitia ubia kati ya Serikali na Sekta binafsi (PPP), tumefanikisha hatua ya kihistoria kusaini mikataba na watoa huduma watatu wa uendeshaji wa awamu ya pili ya mabasi yaendayo haraka”

“Hili ni tukio la mwanzo wa zama mpya siyo tena hadithi ya ahadi zisizotekelezwa, bali ya huduma bora zinazoonekana na kuguswa ‘Great things take time’, Wanafalsafa wanasema, ‘Mambo makubwa yanahitaji muda’ hatua hii si tu ununuzi wa huduma, bali ni ununuzi wa matumaini mapya kwa wakazi wa Jiji letu, hatutaki kurudia makosa ya jana, bali tunajenga mfumo imara, unaozingatia ubora, ufanisi na heshima kwa muda na maisha ya abiria”

“Hope is being able to see that there is light despite all the darkness’ – Desmond Tutu, kwa miaka mingi Wananchi wamepitia usumbufu, foleni zisizokwisha na huduma zisizoeleweka lakimi, tunasema kwa sauti ya matumaini, nuru inaanza kuonekana, mabasi haya hayatakuwa tu magari ya kusafirisha Watu, yatakuwa magari ya kusukuma uchumi, kuunganisha fursa na kupunguza mzigo wa maisha ya kila siku, ‘Progress is not in enhancing what is, but in advancing toward what will be’ – Khalil Gibran.

“Mradi huu unaonesha jinsi tunavyotoka kwenye kilichozoeleka foleni, ajali, uchakavu na kuelekea kwenye kile kinachowezekana, usafiri wa kisasa, wa heshima, wa watu wote, tunajenga mfumo wa usafiri wa umma ambao utaweka heshima kwa abiria, uwajibikaji kwa watoa huduma na thamani kwa kila senti inayowekezwa”

“Sisi ni Real Madrid tunaamini inawezekana”“Tukiwa kwenye Bus,London,tulianza kuamini inawezekana kupindua meza”“Kesho t...
15/04/2025

“Sisi ni Real Madrid tunaamini inawezekana”

“Tukiwa kwenye Bus,London,tulianza kuamini inawezekana kupindua meza”

“Kesho tunaingia na mawazo ya kupindua meza,hii inawezekana kwa sababu ya historia ya klabu,na pia tunaamini timu inaweza kufanya vitu maalumu”

“Neno pekee linalotumika kwa sasa kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ni “Remontada” (Comeback)”

🗣️ Jude Bellingham

Wananchi, Young Africans Sc wameifuata JKT Tanzania kwenye nusu fainali ya kombe la Shirikisho la CRDB (FA Cup) kufuatia...
15/04/2025

Wananchi, Young Africans Sc wameifuata JKT Tanzania kwenye nusu fainali ya kombe la Shirikisho la CRDB (FA Cup) kufuatia ushindi mnono wa 8-1 dhidi ya Stand United katika dimba la KMC Complex kwenye mchezo wa robo fainali.

Yanga Sc 8-1 Stand United
⚽ 16’ Aziz Ki
⚽ 20’ Kibabage
⚽ 32’ Chama
⚽ 39’ Chama
⚽ 51' Aziz Ki
⚽ 60' Aziz Ki
⚽ 63' Aziz Ki
⚽ 87' Musonda
⚽ 49' Msenda

MAPUMZIKO |   HT: Yanga SC 4-0 Stand UnitedStephane Aziz Ki 16'Nickson Kibabage 20'Clatous Chama 32', 41
15/04/2025

MAPUMZIKO |

HT: Yanga SC 4-0 Stand United
Stephane Aziz Ki 16'
Nickson Kibabage 20'
Clatous Chama 32', 41

Address

Musoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mara Online Plus posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mara Online Plus:

Share