Elia Migongo

Elia Migongo Huu ni ukurasa unaomilikiwa na mtu binafsi kwa ajili ya kupashana habari katika nyanja tofauti tofau

30/07/2025

Vita ya Hadhi

Rais William Ruto ametangaza kuvunjiliwa mbali kwa baraza lake la mawaziri, katika hotuba yake Alhamis hii, amesisitiza ...
11/07/2024

Rais William Ruto ametangaza kuvunjiliwa mbali kwa baraza lake la mawaziri, katika hotuba yake Alhamis hii, amesisitiza kuwa katika kipindi cha kuundwa upya baraza, huduma za kiserikali hazitayumba.

Kwa takribani majuma matatu sasa, serikali ya Rais Ruto inakabiliwa na ukosoaji mkali kutoka kwa kundi la vijana, maarufu k**a Gen Z, walioanza harakati zao kwa kupinga muswaada wa fedha, ambao licha ya kupitishwa na bunge, baadae Rais alikataa kuuitia saini.

Waziri mkuu ambaye pia ni waziri wa masuala ya kigeni Bwana Musalia Mudavadi, na Makamu wa Rais Rigathi Gachagua, wamesalia katika nyadhifa zao.

Hongera sana Da Tee for being awarded k**a mtangazaji bora anayeongoza mapambano dhidi ya ukatili 2024... Am happy to be...
09/06/2024

Hongera sana Da Tee for being awarded k**a mtangazaji bora anayeongoza mapambano dhidi ya ukatili 2024... Am happy to be part of your journey kwenye taaluma ya utangazaji... Hongera sana na Mungu akujaalie mema mbeleni

Because there is BETRAYAL IN THE CITY, I WILL MARRY WHEN I WANT, THIS TIME TOMORROW, because THE BEAUTIFUL ONES ARE NOT ...
07/06/2024

Because there is BETRAYAL IN THE CITY, I WILL MARRY WHEN I WANT, THIS TIME TOMORROW, because THE BEAUTIFUL ONES ARE NOT YET BORN...

So far so good, nowadays it is easy to find THREE SUITORS ONE HUSBAND, and when you open windows while hiding your ears will be blessed with THE SONG OF LAWINO

🤣🤣🤣

BARAKA ZA MUNGU ZIAMBATANE NANYI NYAKATI ZOTE!!! mr and mrs
23/05/2024

BARAKA ZA MUNGU ZIAMBATANE NANYI NYAKATI ZOTE!!! mr and mrs

NEEMA YA MUNGU IKO JUU YA KILA MTU, ILA ANAYEIFAIDI NI MWENYE BIDII NA JUHUDI...Tuzungumze kidogo kuhusu neema; kwa lugh...
18/04/2024

NEEMA YA MUNGU IKO JUU YA KILA MTU, ILA ANAYEIFAIDI NI MWENYE BIDII NA JUHUDI...

Tuzungumze kidogo kuhusu neema; kwa lugha rahisi sana, neema ni upendeleo, kustahilishwa, unaweza kupata kitu usichostahili kwa kuwa tuu neema iko juu yako imekufunika... Kwenye neema sheria huwa haifuatwi...

Na Mwl Migongo E.N.D

Kwa wasomaji wa biblia wanaweza tofautisha enzi za agano la kale, sheria ilifuatwa, ilikuwa ukitenda dhambi ni pale pale, unawakumbuka enzi za Nuhu, Sodoma na gomora, ni baadhi ya mifano michache ya hasira ya Mungu kwa watenda dhambi...
Unakumbuka hata hadithi ya Anania na mkewe Safira, walipodanganya kuhusu sadaka, waliposemeshwa kuhusu uongo wao wakaanguka wakafa?

Sasa ili uelewe kwamba neema inafanyaje kazi, jiulize mara ngapi umefanya k**a Anania, au yale ya sodoma na gomora, siku hizi si mpaka wanadai haki mahak**ani na wapo hadi makanisani na wengine wanaongoza...

Hiyo ndio nguvu ya neema si k**a Mungu haelewi, au haoni, hapana anaheshimu kanuni za ulimwengu wa roho, hasa baada ya kuiachilia damu ya Yesu ili itukinge na hasira zake pale tunapomkosea... Maana Yesu alitolewa ili awe upatanisho kwaajili yetu na Mungu, kazi zingine tunaitumia tu kwa umakini na kwa kibali na lazime uwe makini tofauti na hapo mmmhhh (kasome maandiko)

SASA ni hivi neema pamoja na kuw aimeachiliwa, ila inahitaji juhudi ili kuifurahia hiyo neema, ukizembea inakupita na utapoteza kila kitu kilichokusudiwa...

Usipoonesha bidii / juhudi hata Mungu hatakuwa na furaha nawe, wacha tutazame mfano huu wa kuzaliwa kwa PERESI na ZERA, hawa walikuwa mapacha, na saa ya kuzaliwa Zera, alipata neema ya kutokeza wa kwanza, maana yake huyu ndiye Kulwa, na Peresi alipaswa awe Doto...

Kilichotokea ni uzembe wa Zera kutoka tumboni mwa Tamari maana tayari aliwekwa na alama ya uzaliwa wa kwanza; Peresi akaona wacha atie bidii (nguvu) huenda mambo yakabadilika, na kweli akafanikiwa... SOMA kitabu cha Mwanzo 38... au wacha nikusaidie hapa...

Mwanzo 38 27 Wakati wa kujifungua kwake Tamari ulipofika, ikafahamika kuwa alikuwa na mimba ya mapacha. 28Basi, alipopata uchungu wa kuzaa pacha mmojawapo alitoa mkono nje, naye mkunga akaufunga kwa u*i mwekundu, akisema, “Huyu ndiye aliyezaliwa kwanza.” 29 Lakini huyo mtoto alipourudisha mkono wake ndani, ndugu yake akazaliwa wa kwanza. Mkunga akasema, “Mbona wewe umepita kwa nguvu?” Kwa hiyo akaitwa Peresi. 30Baadaye ndugu yake akazaliwa akiwa na ule u*i mwekundu mkononi, naye akaitwa Zera...

Sasa tazama madhara ya uzembe wa Zera ulivyomgharimu, thamani yake mbele za Mungu ikapotea, yaani kwa uzembe tuu wa kutoka saa ya kuzaliwa, thamani yake ikawa sifuri kuliko hata ya Rahabu yule kahaba, (kasome maandiko)...

Inapokuja suala la Yesu kuja duniani, unamuona Rahabu (kahaba mstaafu) na humuoni Zera, ila unamuona mzee wa spidi Peresi... Soma kitabu cha ukoo wa Yesu, kwa mtumishi Mathayo
Mathayo 1: 1 Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu. 2 Ibrahimu alimzaa Isaka; Isaka akamzaa Yakobo; Yakobo akamzaa Yuda na ndugu zake; 3 Yuda akamzaa Peresi na Zera kwa Tamari; Peresi akamzaa Esromu; Esromu akamzaa Aramu; 4 Aramu akamzaa Aminadabu 5 Salmoni akamzaa Boazi kwa Rahabu; Boazi akamzaa Obedi kwa Ruthu; Obedi akamzaa Yese;

Hapo Zera kaishia kuoneshwa tuu alizaliwa, na bila shaka alizaa, ila nani anajali kusimulia habari za zake, kuna pahala aliyumba kuitumia neema, ila mkak**avu Peresi na kahaba Rahabu; NEEMA INATUHITAJI BIDII NA JUHUDI ILI KUFAIDIKA NA MEMA YANAYOAMBATANA NA NEEMA ILIYO JUU YETU...

Angalia usije laghaika na neema unayoiona juu yako, na ukabaki kutazama wengine ambao hawana neema hiyo kwa sasa, mwisho wa siku utawaona mahala ambapo utaishia tuu huyu kafikaje hapo, au ndio kuanza kujihesabia idadi ya uliowaombea wakapona wakati jirani yako anafanya ukahaba, au anasinzia kanisani saa ya ibada.

Migongo End

03/01/2024

Ni kabila gani wanakula nyama mbichi?

BWANA MUNGU AKUANGAZIE NURU YA USO WAKE, UBARIKIWE UINGIAPO NA KILA UTOKAPO 2024, UBARIKIWE SHAMBANI, UBARIKIWE MJINI......
31/12/2023

BWANA MUNGU AKUANGAZIE NURU YA USO WAKE, UBARIKIWE UINGIAPO NA KILA UTOKAPO 2024, UBARIKIWE SHAMBANI, UBARIKIWE MJINI...

Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itakuhifadhi moyo wako na nia yako katika Kristo Yesu.

Heri ya Mwaka mpya 2024, neema, kibali na juhudi vizidi sana kwako.

Acha nuru iangaze, ametutangulia mbele, anapigana na adui zetu, ameandaa meza mbele ya watesi wetu... TUTASHINDA, YEYE MUNGU akitupigania na sisi tukinyamaza kimya!!!

  Dec 20 2023
20/12/2023

Dec 20 2023

LIBERIA: Wakati matokeo yakiwa yamepatikana kutoka kwa zaidi ya asilimia 85 ya vituo vya kupigia kura katika duru ya pil...
17/11/2023

LIBERIA: Wakati matokeo yakiwa yamepatikana kutoka kwa zaidi ya asilimia 85 ya vituo vya kupigia kura katika duru ya pili ya uchagu*i nchini Liberia, mgombea wa upinzani Joseph Boakai yuko mbele kidogo ya Rais George Weah.

Bwana Boakai kufikia sasa ana asilimia 50.6 ya kura, huku Bw Weah akiwa na asilimia 49.4, tume ya uchagu*i inasema.

Wawili hao walitenganishwa kwa zaidi ya kura 7,000 katika duru ya kwanza mwezi Oktoba, na kusababisha duru ya pili ya Jumanne.

Nyota wa zamani wa kimataifa wa kandanda, Bw Weah, (miaka 57), anawania muhula wa pili.

12/11/2023

Barabara ya Morogoro eneo la jangwani imefungwa kutokana na maji kujaa barabarani

11/11/2023

WAWEKEZAJI KUNUFAISHA WANASHERIA WA TANZANIA: Serikali imesema wakati wawekezaji kutoka nje wakimiminika kuja kuwekeza hapa nchini, ni wakati wa taasisi za kifedha na sekta ya sheria kuhakikisha wanatumia fursa hizo kikamilifu na sio kuwaachia wanataaluma k**a zao kutoka nje kunufaika na uwekezaji unaokuja kufanywa hapa nchini.

Waziri wa katiba na sheria Balozi Pindi Chana ameyasema hayo kwa wanasheria wakati wa mkutano na taasisi za Sheria na wanasheria binafsi kutoka mkoa wa dar es salaam, mkutano uliandaliwa na benki ya NMB huku lengo likiwa kufahamiana nao kwa karibu lakini pia kuwashukuru kwa kazi kubwa wanayofanya ndani ya taaluma yao ambayo imekuwa na mchango mkubwa katika uwekezaji unaendelea kufanyika nchini kuwa wa utulivu na mafanikio makubwa.

Balozi Chana amesema serikali imeweka utaratibu ambao unawalinda wanasheria wa hapa nchini katika kuhakikisha kuwa wananufaika na wawekezaji wanaokuja kuwekeza toka nje ya nchi, na kwa takwimu alizonazo hadi sasa nchi inazaidi ya mawakili elfu kumi na moja.

Address

307
Mwamza

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Elia Migongo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share