06/10/2026
MPANGO WA JESHI LA POLISI DHIDI YA CHADEMA‼️
K**a mtakumbuka siku kadhaa zilizopita ilisambaa taarifa kuhusu Jeshi la Polisi kuvamia nyumbani kwa Yoramu Mbyela (Huyu kwenye picha) ambae ni mfanyabiashara anaeuza vifaa vya CHADEMA ikiwemo matisheti, bendera, madera, kombati, n.k
Polisi wakiwa na gari aina ya FUSO walivamia nyumbani kwake, wakamlazimisha mke wa Mbyela afungue duka, kisha wakabeba na kuondoka na mzigo wote wa vifaa vya CHADEMA ambao waliukuta dukani kwake.
Mke wa Mbyela pamoja na Wakili wao wamefuatilia huo mzigo wao, Polisi wakarudisha baadhi ya vitu lakin mzigo mkubwa wakakataa kurudisha mpaka leo bado wamebaki nao.
Sasa nimejulishwa kwamba Jeshi la Polisi wamebaki na huo mzigo kwasababu wanampango wa kuutumia kufanikisha mpango wao dhidi ya CHADEMA hii ni kutokana na hofu waliyonayo kuhusu Maandamano ya 7/7 yani Julai 7, 2026.
Wamepanga kuwavalisha nguo za CHADEMA watu wao ambao ni Green guard, UVCCM na baadhi ya migambo kisha watawapeleka huko porini ambapo badae Polisi watajifanya kwamba wamevamia eneo hilo baada ya kupata taarifa kutoka kwa Wananchi kwamba waliona kuna kundi la watu ambao hawajui ni akina nan.
Baada ya Polisi kuvamia eneo hilo watautangazia umma kwamba Vijana wa CHADEMA wamek**atwa huko porini wakiwa wanapewa mafunzo ya kijeshi kwa ajili ya Maandamano ya Julai 7 ili Msajili apate sababu ya kuingilia kati aseme kwamba CHADEMA imevuja sheria ya vyama vya Siasa maana Sheria ya Vyama vya Siasa ilipiga marufuku vikundi vya ulinzi na mafunzo ya kijeshi mwisho wa siku CHAMA kinaweza kufutwa.
Lakin pia Jeshi la Polisi litakuwa linawavalisha UVCCM hizo nguo za CHADEMA kisha wanawatuma kwenye mikutano ya hadhara ya CHADEMA kufanya fujo ili ionekane CHADEMA wanagombana wao kwa wao.
Sasa ni muhimu sana Wanachama wenzangu mnapoenda kwenda Mikutano, hakikisha unamtambua mtu ambae umekaaa nae jirani ukiona kuna mtu/watu huwaelewi toa taarifa kwa Viongozi wa CHAMA, hawa wahuni wakivamia mikutano yetu inatakiwa muwape HAKI YAO YA KIKATIBA.