Maguge Media

Maguge Media Maguge Media ni chombo cha habari kinachotoa taarifa zinapotokea, matukio mbalimbali yanayotokea dun

  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Ta...
13/11/2025

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania.✍️

Aliyekuwa Naibu Spika wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Musa Azzan Zungu amechaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Tanzania. Zungu ...
11/11/2025

Aliyekuwa Naibu Spika wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Musa Azzan Zungu amechaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Tanzania.

Zungu ameshinda kwa kupata kura 378 kati ya kura zote 383 zilizopigwa leo Bungeni wakati wa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kwanza wa Bunge la Kumi na Tatu wa Bunge leo Novemba 11, 2025.

  mh.. John Heche na viongozi wengine wa Chadema waliokuwa wamek**atwa wameachiliwa huru muda huu.Jioni hii Jeshi la Pol...
10/11/2025

mh.. John Heche na viongozi wengine wa Chadema waliokuwa wamek**atwa wameachiliwa huru muda huu.

Jioni hii Jeshi la Polisi limewaachia kwa dhamana viongozi wakuu wa Chadema waliokuwa wanawashikilia, viongozi hao ni
Mhe. John Heche (Makamu Mwenyekiti Bara)
Mhe. Amani Golugwa (Naibu Katibu Mkuu Bara)
Mhe. Godbless Lema (Mjumbe wa Kamati Kuu na Mhe. Boniface Jacob (Mwenyekiti Kanda ya Pwani).

Klabu  ya Yanga imemtambulisha kocha wao mpya Pedro Gonçalves.✍️Karibu Jangwani, Kocha wa Sayansi ya Mpira Pedro Gonçalv...
25/10/2025

Klabu ya Yanga imemtambulisha kocha wao mpya Pedro Gonçalves.

✍️Karibu Jangwani, Kocha wa Sayansi ya Mpira Pedro Gonçalves🔰

Kutoka Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa...
24/10/2025

Kutoka Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Tundu Lissu imehairishwa leo, Ijumaa Oktoba 24.2025 hadi Novemba 03.2025.

Kesi hiyo imehairishwa kufuatia ombi la Jamhuri lililowasilishwa Mahak**ani hapo likieleza kuwa, leo ilitakiwa wamlete shahidi wa Nne (4) aanze kutoa ushahidi wake baada ya yule wa Tatu (3) kukamilisha hapo jana, lakini wameshindwa kuleta shahidi hii leo kutokana na kwamba wameshindwa kumsafirisha kwa wakati na mashahidi wanaohitajika wako nje ya Dar es Salaam (wapo mikoani)

Lissu alionekana kupinga vikali hoja hiyo akidai kwamba hiyo ni janjajanja ya Jamhuri kutaka aendelee kukaa gerezani hadi Uchaguzi Mkuu umalizike hivyo kuiomba Mahak**a kuilazimisha Jamhuri kuendelea na kesi leo au Mahak**a impatie dhamana aende nyumbani.

Katika uamuzi wake, Mahak**a kupitia jopo la Mawakili watatu (3) wanaosikiliza kesi hiyo wamesema kesi inayomkabili haina dhamana, na kwamba suala la kuomba hairisho kutokana na changamoto la mashahidi linakubalika kisheria na ikizingatiwa kuwa tangu kesi hiyo ianze hakuna siku ambayo Jamhuri imeshindwa kumleta shahidi.

Hivyo kesi hiyo imehairishwa sasa hadi Novemba 03.2025 ambapo shahidi wa Nne (4) wa Jamhuri ataanza kutoa ushahidi wake.

  : Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, Mahak**a imekubaliana na pingamizi lililokuwa limewekwa mw...
22/10/2025

: Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, Mahak**a imekubaliana na pingamizi lililokuwa limewekwa mwishoni mwa juma lililopita na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Tundu Lissu, katika kesi ya uhaini inayomkabili.

Kupitia pingamizi hilo ambalo Jamhuri ililijibu mwanzoni mwa juma hili, Tundu Lissu ambaye anajitetea mwenyewe kwenye kesi hiyo alipinga Mahak**a kupokea 'Flash Disk' na 'Memory Card' k**a kielelezo kutoka kwa shahidi wa tatu (3) wa Jamhuri Mkaguzi wa Jeshi la Polisi John Kaaya

Pamoja na mambo mengine, Lissu aliieleza Mahak**a kuwa shahidi huyo ambaye amejitambulisha k**a 'Mtaalamu wa Picha' Mahak**ani hapo hana nguvu ya kisheria ya kuwasilisha kielelezo hicho, kutokana na marejeo ya hoja mbalimbali za kisheria na kesi mbalimbali alizowasilisha Mahak**ani hapo

Hata hivyo, jopo la Mawakili wa Serikali lilipinga vikali hoja za Lissu kwa kuieleza Mahak**a kuwa 'Mtaalamu' huyo anakubalika kisheria kwa sababu ni miongoni mwa wataalamu walioko kwenye orodha ya walioteuliwa na Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali, Jamhuri pia alirejea kwenye hoja mbalimbali za kisheria na kesi mbalimbali

Katika uamuzi wake uliotolewa mapema leo, Jumatano Oktoba 22.2025, Mahak**a kupitia kupitia jopo la Majaji watatu (3) wanaosikiliza kesi hiyo wakiongozwa na Jaji Danstan Ndunguru imeeleza kukubaliana na pingamizi la Lissu kwani shahidi huyo hana mamlaka ya kisheria ya kuwasilisha kielelezo hicho Mahak**ani kwakuwa yeye ni 'Mtaalamu Picha za mnato' na si 'Mtaalamu wa Picha jongefu (Video)' k**a inavyohitajika kulingana na kesi hiyo

Hata hivyo, Mahak**a imesema, katika mapitio yake imeona kuwa shahidi huyo ni miongoni mwa wataalamu (expert witness) walioteuliwa na DPP na kutangazwa na Gazeti la Serikali (GN-745) ya Desemba 16.2022, lakini kutokana na kile alichokuwa ameomba kuwasilisha Mahak**ani hana nguvu kisheria kutokana na utaalamu wake,

Kwa sasa kesi ya msingi imeanza, hata hivyo ilianza kwa shahidi huyo wa tatu wa Jamhuri Mkaguzi wa Jeshi la Polisi Samwel Elibariki Kaaya kuomba kuwasilisha kielelezo cha taarifa ya uchunguzi ya picha jongefu (video) zilizopo kwenye 'Memory card' na 'Flash Disk', hata hivyo hoja hiyo imewekewa pingamizi jingine na mshtakiwa Tundu Lissu na sasa anawasilisha pingamizi lake Mahak**ani hapo.

Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kanda ya Victoria Ezekia Wenje amekihama Chama Chake Cha Chad...
13/10/2025

Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kanda ya Victoria Ezekia Wenje amekihama Chama Chake Cha Chadema na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo katika Mkutano wa kampeni za Mgombea Urais kupitia CCM Ndugu Dkt.Samia Suluhu Hassan uliofanyika Chato Mjini.

🗣Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linautaarifu umma wa Watanzania kuwa kumejitokeza baadhi ya watu wanaotu...
04/10/2025

🗣Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linautaarifu umma wa Watanzania kuwa kumejitokeza baadhi ya watu wanaotumia mitandao ya kijamii kuweka maudhui yanayochochea kuliingiza Jeshi katika mambo ya siasa.

🗣Aidha, baadhi ya hoja hizo zinatolewa na watu waliopo katika mazingira ya kijeshi, kujinasibisha na Jeshi, walioachishwa Jeshi kwa tabia na mwenendo mbaya pamoja na kujihusisha na siasa na uanaharakati.

🗣Kwa mantiki hiyo, JWTZ linapenda kuutaarifu Umma wa Watanzania kuwa linaendelea kutekeleza majukumu yake kikatiba kwa uaminifu, utii na uhodari kwa kuzingatia kiapo chetu.

Imetolewa na
Kanali Bernard Masala Mlunga
Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

Baba Askofu Dkt. Stephen Munga amefariki duni jana usiku majira ya saa 9:30! . Askofu Stephen  Munga amehudumu k**a Asko...
20/09/2025

Baba Askofu Dkt. Stephen Munga amefariki duni jana usiku majira ya saa 9:30! . Askofu Stephen Munga amehudumu k**a Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (North Eastern Diocese) ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania kuanzia mwaka 2001 mpaka 2020.

Mahak**a Kuu Masjala ndogo ya Dar es Salaam imepanga kutoa uamuzi mdogo kwenye kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa...
18/09/2025

Mahak**a Kuu Masjala ndogo ya Dar es Salaam imepanga kutoa uamuzi mdogo kwenye kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu Jumatatu ya tarehe 22 Septemba 2025, majira ya saa tatu asubuhi.

Uamuzi huo unakuja kufuatia Lissu kuweka mapingamizi yalikuwa yanahusiana na ubovu wa hati ya mash*taka pamoja na maelezo ya mashahidi (witness statement) kuchukuliwa kinyume cha sheria na pia yapo maelezo ya mashahidi ambao mahak**a ilisema utambulisho wao ufichwe wameshindwa kufanya hivyo.

Lissu aliwakilisha mapingamizi hayo mara baada ya kusomewa mashtaka, kufuatia kutupiliwa mbali pingamizi lake la awali juu ya mapungufu ya kisheria yaliokuwa kwenye Committal process, iliyosomwa kwenye Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Mahak**a Kuu Masijala ya Dar es Salaam imeyakataa mapingamizi yaliyowekwa na Mwenyekiti wa Chadema Mheshimiwa  kwenye ke...
15/09/2025

Mahak**a Kuu Masijala ya Dar es Salaam imeyakataa mapingamizi yaliyowekwa na Mwenyekiti wa Chadema Mheshimiwa kwenye kesi ya Uhaini inayomkabili.

Lissu aliweka mapingamizi mahak**ani hapo akipinga namna kesi ya Ukabidhi (Committal) ilivyoendeshwa kwenye mahak**a ya Kisutu.

Baadhi ya mapingamizi aliyoyaweka ni Uhalali wa Mahak**a ya Kisutu kuendesha Committal wakati mtuhumiwa (Mhe. Lissu) alik**atwa wilaya ya Mbinga mkoa wa Ruvuma, Uahirishwaji kiholela wakati wa kesi na uchakachuaji wa nyaraka wakati wa usikilizwaji wa Committal.

Kesi imeahirishwa kwa muda itaendelea saa nane mchana huu.

Kada wa chama cha ACT Wazalendo ambaye aliteuliwa na chama hicho kugombea Urais wa Tanzania, Luhaga Mpina akiwa katika M...
15/09/2025

Kada wa chama cha ACT Wazalendo ambaye aliteuliwa na chama hicho kugombea Urais wa Tanzania, Luhaga Mpina akiwa katika Mahak**a Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam kufuatilia kesi ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Tundu Lissu, leo Jumatatu Septemba 15, 2025.

Address

Mwanza

Telephone

+255768521654

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Maguge Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Maguge Media:

Share