22/10/2025
: Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, Mahak**a imekubaliana na pingamizi lililokuwa limewekwa mwishoni mwa juma lililopita na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Tundu Lissu, katika kesi ya uhaini inayomkabili.
Kupitia pingamizi hilo ambalo Jamhuri ililijibu mwanzoni mwa juma hili, Tundu Lissu ambaye anajitetea mwenyewe kwenye kesi hiyo alipinga Mahak**a kupokea 'Flash Disk' na 'Memory Card' k**a kielelezo kutoka kwa shahidi wa tatu (3) wa Jamhuri Mkaguzi wa Jeshi la Polisi John Kaaya
Pamoja na mambo mengine, Lissu aliieleza Mahak**a kuwa shahidi huyo ambaye amejitambulisha k**a 'Mtaalamu wa Picha' Mahak**ani hapo hana nguvu ya kisheria ya kuwasilisha kielelezo hicho, kutokana na marejeo ya hoja mbalimbali za kisheria na kesi mbalimbali alizowasilisha Mahak**ani hapo
Hata hivyo, jopo la Mawakili wa Serikali lilipinga vikali hoja za Lissu kwa kuieleza Mahak**a kuwa 'Mtaalamu' huyo anakubalika kisheria kwa sababu ni miongoni mwa wataalamu walioko kwenye orodha ya walioteuliwa na Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali, Jamhuri pia alirejea kwenye hoja mbalimbali za kisheria na kesi mbalimbali
Katika uamuzi wake uliotolewa mapema leo, Jumatano Oktoba 22.2025, Mahak**a kupitia kupitia jopo la Majaji watatu (3) wanaosikiliza kesi hiyo wakiongozwa na Jaji Danstan Ndunguru imeeleza kukubaliana na pingamizi la Lissu kwani shahidi huyo hana mamlaka ya kisheria ya kuwasilisha kielelezo hicho Mahak**ani kwakuwa yeye ni 'Mtaalamu Picha za mnato' na si 'Mtaalamu wa Picha jongefu (Video)' k**a inavyohitajika kulingana na kesi hiyo
Hata hivyo, Mahak**a imesema, katika mapitio yake imeona kuwa shahidi huyo ni miongoni mwa wataalamu (expert witness) walioteuliwa na DPP na kutangazwa na Gazeti la Serikali (GN-745) ya Desemba 16.2022, lakini kutokana na kile alichokuwa ameomba kuwasilisha Mahak**ani hana nguvu kisheria kutokana na utaalamu wake,
Kwa sasa kesi ya msingi imeanza, hata hivyo ilianza kwa shahidi huyo wa tatu wa Jamhuri Mkaguzi wa Jeshi la Polisi Samwel Elibariki Kaaya kuomba kuwasilisha kielelezo cha taarifa ya uchunguzi ya picha jongefu (video) zilizopo kwenye 'Memory card' na 'Flash Disk', hata hivyo hoja hiyo imewekewa pingamizi jingine na mshtakiwa Tundu Lissu na sasa anawasilisha pingamizi lake Mahak**ani hapo.