Maguge Media

Maguge Media Maguge Media ni chombo cha habari kinachotoa taarifa zinapotokea, matukio mbalimbali yanayotokea dun

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini imetoa onyo la mwisho kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kikita...
13/05/2026

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini imetoa onyo la mwisho kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kikitakiwa kuwasilisha maelezo ya utetezi kwanini usajili wake usisimamishwe kufuatia tuhuma za ukiukwaji wa Sheria ya Vyama vya Siasa.

​Katika barua rasmi ya Mei 7, 2026, yenye kumbukumbu namba HA.322/362/16A/22, Msajili amebainisha kuwa CHADEMA imekuwa ikitumia lugha za kashfa, uchochezi, na dhihaka zinazoweza kuhatarisha usalama wa taifa na utulivu wa nchi kupitia viongozi wake na matamko ya Kamati Kuu.

​Msajili amewasilisha malalamiko dhidi ya kauli za viongozi wa chama hicho, akiwemo Makamu Mwenyekiti (Bara), John Heche, kuhusu mpango wa kuitisha maandamano kushinikiza kuachiwa kwa Tundu Lissu. Msajili amedai kuwa hatua hiyo ni kuingilia uhuru wa Mahak**a na kuchochea uvunjifu wa amani.

​Aidha, barua hiyo imemnukuu Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Korogwe, Oliver Kisaka, akituhumiwa kutoa matamshi yanayohamasisha matumizi ya nguvu k**a njia ya kufikia malengo ya kisiasa, jambo ambalo ni kinyume na Kifungu cha 19(2)(c) cha Sheria ya Vyama vya Siasa.

Hoja nyingine nzito ni tamko la Kamati Kuu ya CHADEMA la Mei 5, 2026, ambalo Msajili amedai lina lugha za kashfa dhidi ya Rais Samia Suluhu Hassan na vyombo vya dola. Msajili amekosoa madai ya chama hicho kuwa Serikali "imetwaa madaraka kwa mabavu" na "mtutu wa bunduki," akisisitiza kuwa kauli hizo ni batili na zinadhalilisha taasisi ya Urais.

​CHADEMA imepewa hadi Mei 20, 2026, saa tisa na nusu alasiri, kuwasilisha utetezi wake. Msajili ameonya kuwa endapo maelezo hayo hayatatosheleza, chama hicho kinaweza kukabiliwa na rungu la sheria ikiwemo kufutwa kwa usajili, kutozwa faini, au kuzuiwa kufanya baadhi ya shughuli za kisiasa kwa mujibu wa Sheria Namba 3 ya Mwaka 2024.

Uongozi wa Klabu ya Young Africans Sports Club umetangaza  kumfuta kazi Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza Pedro Gonçalves....
06/05/2026

Uongozi wa Klabu ya Young Africans Sports Club umetangaza kumfuta kazi Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza Pedro Gonçalves.

Taarifa ya Yangs iliyotolewa jioni hii imesema Uongozi wa Klabu unamshukuru Kocha Pedro Gonçalves kwa mchango wake alioutoa ndani ya klabu yetu na unamtakia kila la kheri katika majukumu yake yajayo.

Katika kipindi hiki kikosi cha Yanga kitakuwa chini ya uongozi wa Kocha Abdihamid Moalin pamoja na Kocha Patrick Mabedi hadi mwisho wa msimu.

Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi ametangaza ongezeko la kima cha chini cha mshahara kutoka TZS 300,000 hadi TZS 500...
01/05/2026

Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi ametangaza ongezeko la kima cha chini cha mshahara kutoka TZS 300,000 hadi TZS 500,000 kwa mwezi.

Dkt. Mwinyi amesema kiwango hicho kipya cha mshahara kitaanza kutumika Januari 2027.

MSEMAJI WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO CAHDEMA Brenda Lupia amesema:🗣 kweli kuwa, Mwenyekiti alifikishwa mahak**an...
30/04/2026

MSEMAJI WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO CAHDEMA Brenda Lupia amesema:

🗣 kweli kuwa, Mwenyekiti alifikishwa mahak**ani kusomewa uamuzi mdogo kufuatia Maombi yake ya kuunganishwa kwenye kesi ya said Issa Mohamed na wenzake wawili dhidi ya Bodi ya wadhamini na Katibu Mkuu wa Chama.

Katika uamuzi wake, Mahak**a kuu imekataa Maombi ya Mhe Lissu kuunganishwa kwenye kesi hiyo.

Mwenyekiti wa Tume iliyoundwa na Rais Dkt. Samia kuchunguza matukio yaliyojitokeza wakati na baada ya uchaguzi mkuu Octo...
23/04/2026

Mwenyekiti wa Tume iliyoundwa na Rais Dkt. Samia kuchunguza matukio yaliyojitokeza wakati na baada ya uchaguzi mkuu October 29, 2025, Jaji Mstaafu Mohamed Chande Othman amesema miongoni mwa vyanzo vya ghasia zilizotokea October 29, 2026 ni pamoja na malalamiko ya Wananchi kudai Katiba mpya, Tume huru ya uchaguzi, utitiri wa kodi na Watu kutekwa na kupotea.

Jaji Mstaafu Chande amesema hayo wakati akiwasilisha ripoti ya Tume hiyo mbele ya Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo April 23,2026 Ikulu Jijini Dar es salaam.

🗣Tume imebainisha vyanzo vitano na vichocheo nane vilivyosababisha kilichotokea October 29, ghasia hizo zimetokana na changamoto mbalimbali ambazo zimekuwepo kwenye Jamii kwa muda mrefu bila kutatulia, yapo masuala ya kisiasa yanayohusisha Katiba mpya, madai ya maboresho ya uchaguzi na Tume huru ya uchaguzi, pili utitiri wa tozo na kodi na mfumo usio rafiki wa utozaji na ukusanyaji, maisha magumu kwa Watanzania, rushwa, ubadhilifu wa mali za umma na utekaji na upoteaji wa Watu”

Mahak**a ya Rufani Kanda ya Dodoma, Aprili 15, 2026 imetengua maamuzi ya Mahak**a Kuu yaliyokizuia Chama cha Demokrasia ...
15/04/2026

Mahak**a ya Rufani Kanda ya Dodoma, Aprili 15, 2026 imetengua maamuzi ya Mahak**a Kuu yaliyokizuia Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( ) kufanya shughuli za Siasa nchini, kufuatia kesi iliyofunguliwa na Said Issa Mohamed (aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar), Maulidah Anna Komu na Ahmed Rashid Khamis dhidi ya chama hicho.

Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Rugemeleza Nshala amesema taarifa zaidi kuhusu hatua hiyo itatolewa baadaye Saa 9:00 Alasiri.

🗣Nadhani tunaweza kumnyongwa Besigye ifikapo mwezi ujao. Tusipomnyongwa, tutampiga risasi na kumuua. 🗣Hiyo itakuwa siku ...
10/04/2026

🗣Nadhani tunaweza kumnyongwa Besigye ifikapo mwezi ujao. Tusipomnyongwa, tutampiga risasi na kumuua.

🗣Hiyo itakuwa siku nzuri kwa Uganda." Muhoozi Kainerugaba, mkuu wa majeshi wa Uganda

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetarifu umma kuwa leo, tarehe 10 Aprili 2026, Makamu Mwenyekiti wa chama,...
10/04/2026

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetarifu umma kuwa leo, tarehe 10 Aprili 2026, Makamu Mwenyekiti wa chama, Mheshimiwa John Heche, ameongoza jopo la viongozi wa chama katika kikao na ujumbe maalum wa Mjumbe wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Rais mstaafu wa Malawi, Dkt. Lazarus Chakwera, ambao wapo nchini kwa ajili ya kufuatilia matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu yaliyoripotiwa kutokea tarehe 29 Oktoba, ambapo wananchi wengi walipoteza maisha.

Walioambatana na Mhe. John Heche
ni Katibu Mkuu Mhe. John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Bara Mhe. Amani Golugwa, Mwanasheria Mkuu wa Chama Mhe. Rugemeleza Nshala, Mwenyekiti wa Bazecha Taifa Mhe. Susan Lyimo na rafiki wa Chadema Mhe. Jenerali Twaha Ulimwengu

Katika kikao hicho, Dkt. Chakwera amepokea taarifa ya msimamo wa Kamati Kuu ya CHADEMA. Aidha, amepewa maelezo ya kina kuhusu matukio yaliyotokea kabla na baada ya tarehe 29 Oktoba, ikiwemo kuk**atwa kwa Mwenyekiti wa chama, Mheshimiwa Tundu Lissu, pamoja na wimbi kubwa la utekaji, mauaji ya raia, na kuzuiwa kwa shughuli halali za kisiasa za chama.

Vilevile, Dkt. Chakwera amepokea ombi rasmi kutoka CHADEMA la kuruhusiwa kwenda kumuona Mheshimiwa Tundu Lissu akiwa gerezani, ili kujionea hali halisi na kupata taarifa za moja kwa moja.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesimamisha uchaguzi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) ...
10/04/2026

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesimamisha uchaguzi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) uliokuwa ufanyike Aprili 12, 2026 pamoja na kuusimamisha uongozi wa sasa, kufuatia malalamiko ya baadhi ya wagombea kuenguliwa na kukosekana kwa uwazi na haki katika mchakato huo.

Ili kuruhusu uchunguzi huru, Waziri Makonda ameteua k**ati ya uongozi wa muda itakayoongozwa na Ismail Aden Rage k**a Mwenyekiti, huku akitangaza pia kuundwa kwa k**ati ya uchunguzi itakayoshirikisha taasisi mbalimbali ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Jeshi la Polisi na Msajili wa Vyama vya Michezo.

Makonda amesisitiza kuwa hatua hiyo inalenga kurejesha uadilifu, uwazi na imani katika uongozi wa michezo nchini bila kuingilia uhuru wa vyama vya michezo, huku Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan ikiendelea kuimarisha maendeleo ya sekta hiyo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa bei za mafuta nchini bado ziko chin...
08/04/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa bei za mafuta nchini bado ziko chini ikilinganishwa na nchi jirani, licha ya baadhi ya nchi kupunguza kodi.

Akizungumza leo Aprili 08, 2026 mara baada ya uapisho wa viongozi wateule katika Ikulu ya Chamwino, Rais Samia alisema:

🗣Hapa kwetu Tanzania bei za mafuta ziko chini ukilinganisha na majirani zetu wote waliotuzunguka. Pamoja na kupunguza kwao kodi kwenye mafuta, lakini bado ukilinganisha na bei ya mafuta hapa kwetu, bado bei yetu iko chini kuliko wengine."

Akitolea mfano nchi ya marekani amesema lita moja ni dola 800 ambapo hii leo yameshuka mpaka dola 600.

Rais aliongeza kuwa hali hiyo inaonyesha jitihada za serikali kuhakikisha mafuta yanapatikana kwa bei nafuu kwa wananchi, huku akihimiza matumizi makini ya rasilimali za taifa.

Address

Mwanza

Telephone

+255768521654

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Maguge Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Maguge Media:

Share