Maguge Media

Maguge Media Maguge Media ni chombo cha habari kinachotoa taarifa zinapotokea, matukio mbalimbali yanayotokea dun

✍️Bunge Lijalo Litakuwa La Ndugu Jamaa Na Marafiki": Luhaga Mpina
01/08/2025

✍️Bunge Lijalo Litakuwa La Ndugu Jamaa Na Marafiki": Luhaga Mpina

  unaendelea Raia wa Senegal, Alassane Maodo Kanté (siyo Conte), mwenye umri wa miaka 24, kiungo mkabaji… ametua Msimbaz...
30/07/2025

unaendelea Raia wa Senegal, Alassane Maodo Kanté (siyo Conte), mwenye umri wa miaka 24, kiungo mkabaji… ametua Msimbazi, Simba SC, akitokea CA Bizertin ya Tunisia…

Unamjua?

Bi. Juliana Shonza, aliyewahi kuwa Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Songwe, ameongoza kwa idadi ya wingi wa kura za maoni ...
30/07/2025

Bi. Juliana Shonza, aliyewahi kuwa Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Songwe, ameongoza kwa idadi ya wingi wa kura za maoni baada ya kupigiwa kura na wajumbe kwenye uchaguzi wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) mkoani humo.

Akitangaza matokeo hayo Msimamizi wa Uchaguzi huo Bw. Antony Mtaka, amesema Bi. Shonza, amepata jumla ya kura 572, akifuatiwa na Bi. Neema Mwandabila, aliyepata kura 356 ambaye pia amewahi kuwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa huo, huku nafasi ya tatu ikienda kwa Bi. Tully Magilla aliyepata kura 167.

Hakimu Mfawidhi wa Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu, Franco Kiswaga, ameahirisha kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti w...
30/07/2025

Hakimu Mfawidhi wa Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu, Franco Kiswaga, ameahirisha kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, hadi tarehe 13 Agosti 2025, huku akitoa angalizo kwa upande wa Jamhuri kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha Mahak**a Kuu inatoa uamuzi kuhusu maombi ya kulinda mashahidi.

Akiwa mbele ya Mahak**a hiyo, Hakimu Kiswaga amesema amekuwa na utaratibu wa kutoa maamuzi moja kwa moja, lakini safari hii amehitaji muda zaidi kufanya utafiti wa kisheria kutokana na uzito wa hoja za pande zote.

🗣Sasa ninaahirisha kesi hii ili nijipe muda zaidi wa kufafanua utafiti wa kisheria na kuja na maamuzi madogo, kwahiyo leo sitatoa maamuzi madogo, Ninaahirisha mpaka tarehe ijayo, hoja zilizotolewa na pande zote mbili zinahitaji muda wa kutosha, kwasababu pia authorities ambazo zimekuwa cited zimekuwa ni nyingi na zenye kujirudiarudia, mahak**a inahitaji muda”, amesema Hakimu Kiswaga.

Upande wa Jamhuri uliiomba Mahak**a hiyo kusubiri uamuzi wa Mahak**a Kuu kabla ya kuwasilisha hati ya mashtaka au taarifa ya mashtaka dhidi ya Lissu. Wakili wa Serikali Mkuu, Nassor Katuga, alieleza kuwa maombi hayo ya ulinzi kwa mashahidi yaliwasilishwa Mahak**a Kuu na kupewa tarehe ya kusikilizwa Agosti 4, 2025.

Kwa mujibu wa Katuga, maelezo ya mashahidi yanapaswa kuambatana na taarifa ya mashtaka, jambo lililochelewesha mchakato huo kutokana na mashahidi hao kuwa sehemu ya ombi la ulinzi.

Awali, Tundu Lissu alieleza masikitiko yake juu ya mfululizo wa kuahirishwa kwa kesi hiyo, akidai kuwa mawakili wa serikali wanatumia mwanya huo kuendelea kumuweka mahabusu kwasababu isiyo na msingi.

✍️Tunahitaji mabadiliko ya jumla na ya lazima kwa maslahi mapama ya chama na Taifa letu.✍️Kazi yenu imeisha kazi ya Mung...
29/07/2025

✍️Tunahitaji mabadiliko ya jumla na ya lazima kwa maslahi mapama ya chama na Taifa letu.

✍️Kazi yenu imeisha kazi ya Mungu ndio inaanza sasa." Luhaga Mpina

NITAZUNGUMZA NA UMMA 31 JULAI 2025 SAA 2:00 USIKUMungu akipenda Tarehe 31 Julai 2025 siku ya Alhamisi saa 2:00 Usiku nit...
29/07/2025

NITAZUNGUMZA NA UMMA 31 JULAI 2025 SAA 2:00 USIKU

Mungu akipenda Tarehe 31 Julai 2025 siku ya Alhamisi saa 2:00 Usiku nitazungumza na umma na nitashirikisha wanahabari ambao baada ya maelezo yangu awamu ya pili watakuwa na nafasi ya kunihoji maswali mbali mbali kwa kadiri watakavyoona wao inafaa. Mazungumzo haya yatakuwa mubashara (LIVE)

Wanahabari watakaoshiriki ni;-

Deodatus Balile
Mtozi Aloyce Nyanda
Kalvin Raphael (Zungu)

Awamu hii pili bado nitakuwa natoa rai kwa CCM kujirudi na kufanya marekebisho ambayo yatafanya Chama kiende kwenye uchaguzi na Mgombea Mpya na kikiwa kimeijenga imara na madhubuti oganaizesheni ya Chama. Mwaka 2025 ni Mwaka wa kuifanya CCM Mpya.

Kwa kiasi nitatoa sababu za msingi za kufanya mabadiliko ya uongozi Mwaka huu na nitaweka ushahidi.

Mungu akawabariki na kuwalinda watu wote wenye dhamira njema na mustakabali wa sasa na kesho wa Nchi na Taifa letu la Tanzania 🇹🇿 namwomba Mungu pia akawape moyo wa nyama wakuu wetu ili waweke mbele maslahi ya Nchi na Taifa letu na sio Maslahi binafsi.

Wenu,

Ndugu Humphrey H. Polepole

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, imepitisha rasmi majina ya wagombea wa nafasi mbalimba...
29/07/2025

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, imepitisha rasmi majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi, ikiwemo ubunge na uwakilishi kwaajili ya kwenda kupigiwa kura za maoni na wajumbe watakaochagua mgombea mmoja ambaye atasimama kukiwakilisha chama katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba mwaka huu.

Uamuzi huo umetolewa katika kikao maalum kilichofanyika jijini Dodoma, kikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza na wanahabari mkoani Dodoma mara baada ya kikao hicho, Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla amesema majina yaliyopitishwa yanatokana na mchakato wa kina wa kuchambua, kupima sifa na uwezo wa wagombea waliowasilisha nia ya kugombea kupitia tiketi ya CCM.

Katika taarifa rasmi iliyotolewa Jumanne Julai 29, 2025 katika Ofisi za Chama hicho Jijini Dodoma majina haya hayakuwepo kati ya walioteuliwa.

Mrisho Gambo
Olesendeka
Ruhaga mpina
January makamba
Byabato

Baada ya ukimya wa masaa manne hatimaye Chama cha Mapinduzi ( CCM) kimetoa taarifa kuwa kitataja majina ya waliopitishwa...
28/07/2025

Baada ya ukimya wa masaa manne hatimaye Chama cha Mapinduzi ( CCM) kimetoa taarifa kuwa kitataja majina ya waliopitishwa na k**ati kuu ili kupigiwa kura na wajumbe kuwania Ubunge na Ujumbe wa Baraza la wawakilishi majira ya saa tatu na nusu usiku.

Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini wameendelea kumsubiri tangu saa kumi na moja jioni hii leo Katibu wa Mafunzo ,Itikadi na Uenezi wa chama hicho Amos Makalla ili kutoa taarifa ya Kamati Kuu kuhusu majina ya wanachama hao.

Tangazo la chama hicho awali lilisema kuwa kiongozi huyo angeongea na waandishi wa habari majira ya saa kumi na moja jioni.

Hadi kufikia majira ya saa tatu usiku hakukuwa na taarifa zilizotolewa juu ya kinachochelewesha utangazaji wa majina hayo huku ukurasa wa instagram wa Chama hicho ukitoa tarifa za kuendelea kwa Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Jaji Hamidu Mwanga leo tarehe 28 Julai 2025 amekataa kujitoa katika shauri namba 8323/2025 iliyofunguliwa na Bodi ya Wad...
28/07/2025

Jaji Hamidu Mwanga leo tarehe 28 Julai 2025 amekataa kujitoa katika shauri namba 8323/2025 iliyofunguliwa na Bodi ya Wadhamini ya Chama na Kaimu Katibu Mkuu Mhe. ya kumtaka ajitoe katika shauri la msingi namba 8960/2025 kutokana na wao kutokuwa na imani nae kutokana na maamuzi yake ya awali aliyoyafanya katika shauri hilo la msingi.

Jaji Mwanga amekataa kuwa, hajawahi kuwa mtumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Zanzibar.

Uchaguzi wa Madiwani wa Viti Maalum kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa Morogoro Mjini limehitimishwa kwa amani...
21/07/2025

Uchaguzi wa Madiwani wa Viti Maalum kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa Morogoro Mjini limehitimishwa kwa amani, huku baadhi ya vigogo maarufu wakianguka na madiwani sita wa zamani wakirejea katika nafasi hizo.

Uchaguzi huo ambao ulianza Julai 20, 2025 kwa zoezi la kupiga kura na kukesha kuhesabu matokeo hadi alfajiri ya siku ya pili, Julai 21, ulimalizika kwa kutangazwa kwa matokeo majina ya saa 12:15 asubuhi.

Idadi ya wagombea 31 ambao majina yao yalipitishwa kugombea nafasi hiyo na idadi ya kura walizopata yametangazwa na msimamizi wa uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa UVCCM Morogoro mjini, Khalid King kwa kuanza na aliyepata kura ndogo hadi aliyepata kura nyingi.

Kwa utaratibu wa CCM, washindi hawatajwi moja kwa moja, bali hutangazwa majina yote ya wagombea na kura walizopata. Katika zoezi hilo ambapo vikao vikiridhia wateuliwa 10 walioongoza ama vinginevyo ndio hupitishwa kugombea.

Mwanahabari wa Uhuru na Mzalendo, Latifa Said Ganzel, aliibuka kinara kwa kupata kura 934.

Waliofuata ni Batuli Kifea (794), Grace Mkumbae (752), Salma Mbandu (698), Imakulata Mhagama (581), Warda Bazia (562), Rahma Maumba (560), Magreth Ndewe (556), Anna Kisimbo (535), na Amina Zihuye (532).
Miongoni mwao, madiwani sita waliokuwa kwenye nafasi hiyo awali wamerejea, akiwemo Latifa, Grace, Salma, Warda, Rahma, na Amina.

Viongozi maarufu waliokuwa wakitetea nafasi zao, akiwemo Hadija Kibati maarufu k**a ‘Mama Nyau’, Zamoyoni Abdallah na Mwanaidi Ngulungu wameanguka kwenye kinyang’anyiro hicho.

Nchini Kenya Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) imeondoa mash*taka ya ugaidi dhidi ya Mwanaharakati Boniface Mwangi, amba...
21/07/2025

Nchini Kenya Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) imeondoa mash*taka ya ugaidi dhidi ya Mwanaharakati Boniface Mwangi, ambapo sasa atakabiliwa na mash*taka ya kumiliki risasi kinyume cha sheria.

Mwangi ambaye ameachiwa kwa dhamana, awali alishtakiwa kwa kusaidia shughuli za kigaidi zinazohusishwa na maandamano ya kupinga serikali yaliyofanyika Juni 25, 2025.

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimetoa taarifa ya kuahirishwa kwa vikao vya chama kitaifa vilivyopangwa kufanyika kati ya Jul...
19/07/2025

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimetoa taarifa ya kuahirishwa kwa vikao vya chama kitaifa vilivyopangwa kufanyika kati ya Julai 18 hadi 19, 2025 mpaka tarehe 26 hadi 28 julai 2025.

Vikao hivyo Vikitanguliwa na kikao cha halimashauri kuu ya ccm na k**ati kuu.

Taarifa hiyo imetolewa Amaos Makalla, akifafanua sababu ya kusogeza mbele zoezi hilo ni kutokana na wagombea kuwa wengi hivyo kuitaji muda wa kutosha.

Ikumbukwe Vikao hivyo vilipangwa kufanyika kwa ajili ya kufanya mchujo wa wagombea watakaokwenda kupigiwa kura za maoni na wanachama wa CCM kwenye majimbo pamoja na kupitisha wagombea wa Ubunge wa Viti Maalum kwa makundi mbalimbali na wagombea wa nafasi za Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa upande wa Zanzibar

Address

Mwanza

Telephone

+255768521654

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Maguge Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Maguge Media:

Share