Godlisten P Kitomari

Godlisten P Kitomari Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Godlisten P Kitomari, Media/News Company, Nyegezi Mwanza, Mwanza.

Rio Ferdinand kuhusu Benjamin Šeško na safu ya ushambuliaji ya Manchester United:Mchezaji wa zamani wa Manchester United...
30/07/2025

Rio Ferdinand kuhusu Benjamin Šeško na safu ya ushambuliaji ya Manchester United:

Mchezaji wa zamani wa Manchester United Rio Ferdinand amesema hana shaka sana na uwezo wa Benjamin Šeško, lakini amesisitiza kuwa United wanahitaji mshambuliaji mwenye uzoefu mkubwa, si chipukizi mwingine.

Rio amesema:

“Simpingi sana Šeško k**a mchezaji. Ninachosema ni kwamba Manchester United wanahitaji uzoefu mbele ya goli. Tayari wana Højlund, Zirkzee, na Chido — wachezaji vijana, wasio na uzoefu wa kutosha. Wanahitaji mtu ambaye wachezaji wengine wataangalia na kusema: ‘Ndivyo unavyocheza k**a namba 9. Ndivyo unavyofanya kazi hii.’”

Ameongeza kuwa

“Unaponunua mchezaji ambaye hana uzoefu mkubwa, ni hatari nyingine tena. Swali ni: Je, ni hatari inayostahili kuchukuliwa kwa kikosi chenye vijana wengi wasiokuwa na uzoefu?”

Kauli hii ya Rio inasisitiza umuhimu wa kuwa na mchezaji aliyekomaa katika nafasi ya mshambuliaji wa kati, ili kusaidia kuongoza na kuwafundisha vijana k**a Rasmus Højlund na Joshua Zirkzee ambao bado wanajifunza ngazi ya juu ya soka.

Mashabiki wengi wamekubaliana na kauli hiyo, wakisema amekuwa akisema ukweli huo kwa muda mrefu na sasa ni wakati wa klabu kuchukua hatua.

Ishu sio usajili wa Beki mpya Karibu  Rushine De Reuck ishu inakuja ni ubora wa jezi hii na wao wanasema ni jezi ya mazo...
29/07/2025

Ishu sio usajili wa Beki mpya Karibu Rushine De Reuck ishu inakuja ni ubora wa jezi hii na wao wanasema ni jezi ya mazoezi.

Sikumbuki mara ya mwisho ni lini Simba sc wametoa jezi Bora k**a hii ,wajiangalie sana wanaweza jikuta jezi yenyewe ya msimu ujao inakuwa famba.

“Ndani ya Bodi ya Simba kazi yetu ni kuhakikisha brand ya klabu inazidi kupanda siku baada ya siku. Nguvu kubwa ya Simba...
29/07/2025

“Ndani ya Bodi ya Simba kazi yetu ni kuhakikisha brand ya klabu inazidi kupanda siku baada ya siku. Nguvu kubwa ya Simba ni mashabiki wake ambao wanafanya wadhamini waje kuwekeza kwenye klabu yetu. Sisi tunataka Simba izidi kuwa na nguvu ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.”

“Kwa mashabiki wa Simba tuipe ushirikiano ili wapate wanachokihitaji na hata ambapo tutakuja kusaini mkataba mwingine tupate fedha zaidi. Lakini pia waendelee kuipa ushirikiano klabu yao.”- Mjumbe wa Bodi Simba sc , Salim Muhene.

“Tumeingia Simba sababu ni timu kubwa Afrika, ni timu ambayo inajulikana pande zote za bara hili na hilo ndio tunaangali...
29/07/2025

“Tumeingia Simba sababu ni timu kubwa Afrika, ni timu ambayo inajulikana pande zote za bara hili na hilo ndio tunaangalia zaidi kwenye biashara. Tulikuwa tukiifatilia kwa miaka karibu sita lakini sasa imekuwa kweli. Tunafuraha kufanikisha jambo hili.”
“Huu ni zaidi ya ushirikiano na inatakiwa klabu zote zifaidike na jambo hili. Tunashirikiana na timu nyingi kubwa ambazo tunadhamini hivyo uzoefu huo utatusaidia kufanikisha jambo hili.”

“Nina furaha kwa ushirikiano huu lakini tutafanya kazi kuangalia namna gani ya kufanikisha ushirikiano na vilabu vingine vikubwa ambavyo tunashirikiana navyo.”- Mkuu wa Udhamini wa BetWay Afrika, Jason Shield.

“Mkataba ambao tumeingia unakwenda kuleta mapinduzi kwenye mchezo wa soka hapa Tanzania na unakwenda kuongezea nguvu dha...
29/07/2025

“Mkataba ambao tumeingia unakwenda kuleta mapinduzi kwenye mchezo wa soka hapa Tanzania na unakwenda kuongezea nguvu dhamira ya Simba kuwa klabu namba moja barani Afrika.”

“Udhamini huu ambao thamani yake ni Bilioni 20 kwa miaka mitatu, unaonyesha namna Simba imedhamiria kuleta mabadiliko ya kuwa klabu kubwa.” - CEO Zubeda Sakuru.

Simba sc  yapata Mdhamini mpya Betway kwa mkataba wa miama Mitatu wenye Thamani ya Shilingi Billion 20 Awali Simba iliku...
29/07/2025

Simba sc yapata Mdhamini mpya Betway kwa mkataba wa miama Mitatu wenye Thamani ya Shilingi Billion 20

Awali Simba ilikuwa na mdhamini M.bet ambaye alisaini mkataba wa miaka mitano wenye Thamani ya Billion 26 .

Kisasi kimelipwa na wadada wa England kwaajili ya kaka zao
28/07/2025

Kisasi kimelipwa na wadada wa England kwaajili ya kaka zao

Kocha Sarina Wiegman aweka rekodi pekee ya kushinda euro ya wanawake mara 3 mfululizo.2017 🏆 -Uholanzi 2022🏆 - England 2...
28/07/2025

Kocha Sarina Wiegman aweka rekodi pekee ya kushinda euro ya wanawake mara 3 mfululizo.

2017 🏆 -Uholanzi
2022🏆 - England
2025 🏆 -England

Timu ya Taifa ya wanawake ya England inaendelea kulipa heshima Taifa lao ..Wametetea taji lao la Euro na wamelipa kisasi...
28/07/2025

Timu ya Taifa ya wanawake ya England inaendelea kulipa heshima Taifa lao ..

Wametetea taji lao la Euro na wamelipa kisasi dhidi ya Spain baada ya kufungwa fainal ya kombe la Dunia la wanawake 2023.

Happy birthday my uncle..Mungu akupe afya njema siku zote ..
25/07/2025

Happy birthday my uncle..Mungu akupe afya njema siku zote ..

TRIPLE H ASEMA BILA HULK MIEREKA ISINGEKUWEPOMkurugenzi wa Uundaji wa Vipindi wa WWE, Triple H, amemuaga nguli wa mielek...
24/07/2025

TRIPLE H ASEMA BILA HULK MIEREKA ISINGEKUWEPO

Mkurugenzi wa Uundaji wa Vipindi wa WWE, Triple H, amemuaga nguli wa mieleka Terry “Hulk Hogan” Bollea kwa maneno mazito na ya heshima akimtaja k**a shujaa wa kipekee aliyebadilisha tasnia ya mieleka duniani.

Katika ujumbe wake, Triple H amesema: “WWE isingekuwa hapa ilipo leo bila wahusika wa kipekee waliopambana ulingoni … na hakuna aliyeonekana mkubwa k**a Hulk Hogan.

Hakuna aliyefanana na huenda asijirudie mwingine k**a yeye.”

Triple H alihitimisha kwa kupeleka salamu za rambirambi kwa familia, marafiki na mashabiki wa Hogan aliyefariki leo Alhamisi, akiwa na umri wa miaka 71.

Address

Nyegezi Mwanza
Mwanza
199169

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Godlisten P Kitomari posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Godlisten P Kitomari:

Share