11/08/2025
Askofu Liberatus Sangu wa Jimbo Katoliki Shinyanga leo ametoa Sakramenti ya Kipaimara kwa Waimarishwa 108 katika misa takatifu iliyofanyika katika kanisa la Kristo Mchungaji Mwema Parokia ya Lugulu Jimbo Katoliki Shinyanga.
Akihubiri katika Misa hiyo,Askofu Sangu amewataka Waimarishwa hao kuilinda imani Katoliki,kuitunza ,kuitangaza na kuiishi.
Askofu Sangu amesema Wakristo Wakatoliki hawapaswi kuiacha Imani yao ambayo Kristo yuko ndani ya Ekaristi Takatifu.
Katika hatua nyingine Askofu Sangu amewataka Wakristo Wakatoliki kuwa na upendo na kuacha kunufaika kupitia shida za watu.
Wakati huo huo Askofu Sangu amewakumbusha Watanzania kuilinda Amani iliyopo licha ya changamoto zilizopo na kuwataka kujifunza kupitia Mataifa mengine ambayo kuna machafuko yanayosababisha vifo vya watu.