Radio farajatz

Radio farajatz Ukurasa rasmi wa Radio Faraja FM Stereo 91.1 Mhz Shinyanga
https://farajafm.co.tz/


Radio faraja ni chombo cha habari kinacholenga kutoa elimu na kusaidia jamii kwa nyakati mbalimbali,
Pia kinaendeshwa na kutoa mahudhui ya Dini ya kikristo kutoka dhehebu la Roman Catholic katika Jimbo la shinyanga Mjini, Ngokoro.

jamii

30-August-2026 DOMINIKA YA 22 YA MWAKATAFAKARI KATEKESINa Padri Emmanuel GembuyaJimbo Katoliki Bariadi0764545247Somo 1​​...
29/08/2026

30-August-2026

DOMINIKA YA 22 YA MWAKA

TAFAKARI KATEKESI

Na Padri Emmanuel Gembuya

Jimbo Katoliki Bariadi

0764545247

Somo 1​​​​​​

Yer 20:7-9
Ee Bwana, umenihadaa, nami nimehadaika; wewe una nguvu kuliko mimi, ukashinda; nimekuwa kitu cha kuchekesha, mchana kutwa; kila mtu hunidhihaki. Maana kila ninenapo napiga kelele; nalia, Dhuluma na uharibifu! Kwa kuwa neno la Bwana limefanywa shutumu kwangu, na dhihaka, mchana kutwa. Nami nikisema, Sitamtaja wala sitasema tena kwa jina lake; ndipo moyoni mwangu kumekuwamo k**a moto uwakao, uliofungwa ndani ya mifupa yangu, nami nimechoka kwa kustahimili, wala siwezi kujizuia.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 63:1-5, 7-8 (K) 1a
Ee Mungu, Mungu wangu, nitakutafuta mapema,
Nafsi yangu inakuonea kiu.
Mwili wangu wakuonea shauku,
Katika nchi kame na chovu, isiyo na maji.(K)

(K) Ee Bwana, Mungu wangu, nafsi yangu inakuonea kiu.

Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu,
Nizione nguvu zako na utukufu wako.
Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai,
Midomo yangu itakusifu.(K)

Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai,
Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.
Nafsi yangu itakinai k**a kushiba mafuta na vinono,
Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.(K)

Maana Wewe umekuwa msaada wangu,
Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia.
Nafsi yangu imekuandama sana,
Mkono wako wa kuume unanitegemeza.(K)

Somo 2​​​​​​

Rum 12:1-2
Basi ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala msifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Shangilio​​​​​​​

Lk 21:36
Aleluya, aleluya,
Kesheni kila wakati, ili mpate kuokoka,
na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.
Aleluya!

Injili​​​​​​​

Mt 16:21-27
Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka. Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema. Hasha, Bwana, hayo hayatakupata. Akageuka, akamwambia Petro, nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu. Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona. Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake? Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.

MSALABA K**A ALAMA YA USHINDI

Somo la kwanza (Yer 20:7-9) ni kutoka kitabu cha nabii Yeremia. Katika somo hili, Yeremia anamtolea Mwenyezi Mungu manung’uniko na uchungu ambao kazi yake ya unabii imemletea. Anamwambia Mwenyezi Mungu “umenihadaa nami nikahadaika” yaani umenidanganya nami nikadanganyika. Yeremia anaona amedanganyika kwa sababu ahadi ambazo Mungu alimpa alipomwita kuwa nabii zimegeuka kuwa kinyume.

Sasa kila anayemwona anamcheka, neno analotangaza haoni k**a linapenya katika maisha ya watu. Na hata yeye badala ya kupokelewa k**a mjumbe wa Mungu anaonekana kituko machoni mwao. Pamoja na manung’uniko hayo yote, pamoja na kukata tamaa, Yeremia bado anashangazwa na kitu kimoja. Anapoamua kuiacha kazi ya unabii na kupanga kutokuhubiri tena Neno la Mungu, anashindwa.

Hawezi kujinasua kutoka katika utume wa unabii aliokwisha upokea na aliokwisha uanza. Kimwili amekata tamaa lakini bado kwa ndani Neno la Mungu linawaka na linamsukuma aendelee kulitangaza.

Nabii Yeremia, katika somo la kwanza, analetwa kwetu leo k**a mfano wa namna ya kujikana mwenyewe. Manung’uniko yake, kukata kwake tamaa na hata kufikia hatua ya kutaka kuuacha utume wa unabii ni matokeo ya kutokujitambua k**a mfuasi na mtumishi anayepaswa kujikana. Mtumishi hapaswi kujiweka katika ngazi moja na utume ambao Mungu amemwitia.

Utume ambao Mungu anamwita mtu na kumpatia unazo njia zake na unayo malengo yake ambayo si mara zote yataendana na malengo ya yule aliyeitwa kuufanya. Na tena ni mtumishi anayebeba gharama za utume aliopewa. Gharama hizo anazibeba kwa kujikana, yaani kujisadaka na kwa kukubali atumike ili utume usonge mbele. Yeremia anatuonesha kuwa hata pale sadaka inapokuwa kubwa, mtumishi hapaswi kuukimbia utume alioupokea.

K**a usemavyo msemo maarufu “bora punda afe lakini mzigo ufike”, ni muhimu kutambua kuwa ni utume ulio na kipaumbele kupita maslahi binafsi ya mtumishi.

Somo la pili (Rum 12: 1-2) ni kutoka katika waraka wa Mtume Paulo kwa Warumi. Katika mpangilio wa waraka kwa Warumi, sura hii ya 12 ambayo tunaisoma leo inafungua sehemu ya pili ya waraka, sehemu ambayo Paulo anajielekeza kutoa maonyo na maelekezo mbalimbali kuhusu maisha ya kila siku ya wakristo wa Rumi.

Leo anawaambia “itoleeni miili yenu k**a sadaka hai na takatifu impendezayo Mungu”. Na tena anawaonya wasishawishike kuiga mitindo ya watu wa ulimwengu bali wao k**a wakristo wazigeuze fikra zao, wamuelekee Mungu ili walitambue na kulitenda lililo jema, lililo kamilifu na lile linalofaa.

Paulo anawaandikia maonyo haya akiyatambua fika mazingira ya Roma ya wakati huo. Huu ulikuwa ni mji mkubwa yalipokuwa makao makuu ya dola ya kirumi. Ni mji ulikusanya kila aina ya watu hivi kwamba pamoja na maendeleo uliokuwa nayo, ulijikuta kuwa pia na mmomonyoko mkubwa wa maadili na uchaji.

Mausia ya Paulo yalilenga basi kuwatahadharisa wakristo walioishi katika mji huu ili wasipoteze utambulisho wao wa kuwa wakristo na wasimezwe na mitindo ya wakazi wa mji huo. Somo hili linazungumza nasi pia ambao mazingira ya ulimwengu tunaoishi hayatofautiani sana na ya Roma ya wakati wa Paulo. Mwaliko ni uleule wa kutunza utambulisho wetu ili tusimezwe na mitindo ya sasa ya ulimwengu.

Waraka wa Mtume Paulo kwa Warumi na mafundisho yake juu ya maisha ya kila siku yampasayo mkristo ndiyo ufuasi wenyewe. Kisha kujikana na kisha kujitwika msalaba, mfuasi anaalikwa kuyaweka katika maisha yake ya kawaida ya siku kwa siku yale anayoyaamini na kuyachuchumalia kwa sadaka na matumaini makubwa.

Injili ya Dominika hii ni kutoka kwa mwinjili Mathayo (Mt 16:21-27). Petro ambaye ni kitambo kidogo tu amekiri Yesu kuwa ndiye Kristo na ambaye Kristo mwenyewe amemwita mwamba ambao juu yake atalijenga kanisa lake, sasa anageuka kuitwa shetani.

Tunasikia katika injili ya leo Yesu anamwambia “rudi nyuma yangu shetani maana wewe huyawazi yaliyo ya Mungu bali yaliyo ya wanadamu”. Karibu katika Israeli yote kulikuwa na mambo makubwa mawili yaliyowatatiza watu kumhusu Yesu.

La kwanza lilikuwa ni kukubali kuwa Yesu ndiye Kristo, yaani Yesu ndiye masiha yule aliyetabiriwa na ndiye masiha aliyekuwa akingojewa kwa miaka mingi. La pili lilikuwa ni kukubali kuwa huyu Yesu ni Masiha atakayeteswa, yaani ataudhihirisha umasiha wake na kuwaokoa watu kwa njia ya mateso. Kwa myahudi ilikuwa haiingii akilini kuchora picha ya masiha mteswa. Ilikuwa ni fedheha na kashfa kubwa.
Petro alipomkiri Yesu kuwa ndiye Kristo alivuka kizingiti cha kwanza. Lakini alishindwa kuvuka kizingiti cha pili cha kukubali kuwa itampasa Yesu kuigia katika mateso hadi kuuwawa na siku ya tatu kufufuka.

Yesu anamkaripia na kutumia maneno makali hadi kumuita shetani ili kurekebisha kasoro hiyo waliyokuwa nayo watu kumhusu. Ni hapa tunaona kuwa karipio hili la Yesu kumuita Petro shetani sio lake peke yake. Ni karipio la wote ambao wanamwamini Yesu kuwa ndiye Kristo lakini bado hawataki au hawako tayari kumfuata katika njia ya mateso Kristo huyo wanayemuamini.

Mtume Petro katika Injili analetwa kwetu k**a mfano mintarafu kigezo cha kujitwika msalaba.

Petro kwa kumzuia Yesu asiingie katika mateso na kifo msalabani ni kushindwa kukipokea kigezo cha pili cha ufuasi, yaani kujitwika msalaba. Njia ya msalaba ni njia ngumu na tena yenye mateso na uchungu mwingi. Hakuna ambaye katika hali ya kawaida angaliichagua k**a kungalikuwa na njia nyingine ya kupita.

Yesu anatudhihirishia kwa mara nyingine tena leo kuwa mfuasi hawezi kuikwepa njia ya msalaba bila kugeuka yeye mwenyewe kuwa kikwazo kwa wokovu. Ni katika njia ya msalaba ndipo unapolala wokovu.

Yesu anatualika tuibebe misalaba yetu tumfuate akijua fika kwamba ni misalaba hiyo hiyo ambayo kwa uhalisia ndiyo inayotubeba sisi kutufikisha katika wokovu anaotuitia.

Mwenyezi Mungu na atujalie neema katika juma hili na siku zote za maisha yetu ili tuweze kujikana na kujitwika misalaba yetu ili tumfuate mwanae Yesu Kristo kila siku ya maisha yetu bila kusitasita na bila kizuio.

Ombi;Tuombe neema ya Mungu itusaidie kuibeba misaba yetu kikamilifu tukiifungamanisha na Kristo ili iwe misalaba ya ushindi.

TUMSIFU YESU KRISTO

TAFAKARI KATEKESI

23-August-2026 DOMINIKA YA 21 MWAKA ATAFAKARI KATEKESINa Padri Emmanuel GembuyaJimbo Katoliki Bariadi0764545247Somo 1​​​...
21/08/2026

23-August-2026

DOMINIKA YA 21 MWAKA A

TAFAKARI KATEKESI

Na Padri Emmanuel Gembuya

Jimbo Katoliki Bariadi

0764545247

Somo 1​​​​​​

Isa 22:19-23
Bwana, Bwana wa majeshi, asema hivi: Nami nitakusukuma na kukutoa katika mahali pako, naye atakushusha utoke hapa usimamapo. Na itakuwa katika siku ile nitamwita mtumishi wangu Eliakimu, mwana wa Hilkia; nami nitamvika vazi lako, nitamtia nguvu kwa mshipi wako, nami nitamkabidhi yeye mamlaka yako; naye atakuwa baba kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa nvumba ya Yuda. Na ufunguo wa nvumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga. Nami nitamkaza kanta msumari mahali palipo imara; naye atakuwa kiti cha utukufu kwa nyumba ya baba yake.

WIMBO WA KATIKATI

Zab 138: 1-3, 6, 9 (K) 9
Nitakushukurukwamoyowanguwote,
Mbeleyamiungunitakuimbiazaburi.
Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu

(K) Ee Bwana, fadhili zako ni za milele, Usiziache kazi za mikono yako.

Nitalishukuru jina lako,
Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako,
Kwamaanaumeikuzaahadiyako,
Kulikojinalakolote.
Sikuileniliyokuitaulinitikia,
Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu. (K)

IngawaBwanayukojuu,amwonamnyenyekevu,
Nayeamjuamwenyekujivunatokeambali.
EeBwana,fadhilizakonizamilele;
Usiziache kazi za mikono yako. (K)

Somo la 2​​​​​​

Rum 11:33-36
Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani! Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake? Au ni nani aliyempa yeye kitu kwanza, naye atalipwa tena? Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina.

Shangilio​​​​​​

Mt 11:25
Aleluya, aleluya,
Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili. ukawafunulia watoto wachanga.
Aleluya

Injili​​​​​​​

Mt 16:13-20
Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipo, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? Wakasema, Wengine hunena Yohane Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. Akawaa- mbia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia. Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikufunulia hili, bali Baba vangu aliye mbinguni. Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. Ndipo alipowakataza sana wanafunzi wake wasimwambie mtu ye yote ya kwamba yeye ndiye Kristo.

JE, NANYI MWANINENA MIMI KUWA NINANI?

Somo la kwanza (Isa 22:19-23) ni kutoka kitabu cha Isaya. Katika somo hili, Isaya anatoa unabii kwa mtu aliyeitwa Shebna. Huyu alikuwa ni mkuu wa nyumba ya mfalme.

Somo hili linatuletea sehemu pekee ambapo Isaya anatoa unabii kwa mtu binafsi. Mara zote ametoa unabii wake au kwa Israeli nzima au kwa mataifa mengine ya kigeni. Katika unabii huu, Isaya anatabiri kuwa Shebna ataondolewa katika nafasi yake na nafasi hiyo atapewa mtu mwingine.

Anapotoa utabiri huo, Isaya anatumia lugha ya picha ya ufunguo pamoja na maneno ya kufunga na kufungua. Lugha hii ya picha ya ufunguo inamaanisha mamlaka ya kutawala na maneno “kufunga na kufungua” humaanisha mamlaka ya kuhukumu au kutoa hukumu. Na Mungu mwenyewe anapotamka kwa kinywa cha nabii Isaya akisema nitaweka mabegani mwako funguo – au nitakupatia funguo – anajitambulisha kuwa ni yeye anayetoa mamlaka hayo katika himaya ya mfalme.

Tendo hili linakuwa ni kielekezo cha Mungu mwenyewe kuamua kuamua kumpa mwanadamu mamlaka na uwezo wa kutenda kazi juu ya ndugu zake. Tendo hili Kristo atalifanya kwa Petro anapomweka juu ya Kanisa lake. Naye atampa mamlaka ya kutawala na ya kutoa hukumu akimwambia anampatia funguo za kufunga na kufungua.

Katika somo la kwanza Nabii Isaya anatuhimiza kuwa waaminifu katika nyadhifa mbalimbali tulizo na pia Somo hili linatuonya na kutuhimiza kuwa watu waaminifu katika shughuli mbalimbali tunazo pewa na Mungu au na jamii inayotuzunguka na tufanye kazi kwa manufaa ya jamii siyo kwa manufaa ya kwetu binafsi.

Somo la pili (Rum 11: 33-36) ni kutoka katika waraka wa Mtume Paulo kwa Warumi. Katika somo hili, Paulo ahahitimisha mafundisho yake kwa warumi, mafundisho ambayo yalijikita kuelezea wokovu upatikanao kwa njia ya Kristo kwa ajili ya wayahudi na kwa wasio wayahudi. Kwa kweli fundisho hilo ambalo Paulo amekuwa analitoa lilikuwa ni gumu.

Lilikuwa ni gumu kueleweka wa watu kwa sababu ni k**a lililenga kubomoa msingi wa mapokeo yaliyokuwapo lakini pia lilikuwa ni gumu kwake yeye mwenyewe Paulo kulielezea kwa ufasaha na hapa na pale ilimbidi kutumia namna nyingi na tofauti tofauti kuelezea kitu kile kile kimoja.

Mtume Paulo anaonesha ni jinsi gani Mungu alivyo na hekima ambayo akili ya binadamu haiwezi kufahamu chochote juu ya mipango ya Mungu. Hakuna anaye jua nia ya Bwana na vitu vyote vinatoka kwake tena vinarejea kwake maana utukufu una yeye milele.

Ndugu wanafamilia ya Mungu, sisi sote tunatakiwa kuwa na imani thabiti kwa Mungu na kumkiri kuwa yeye ndiye muumba wa vitu vyote. Tusiwe na mioyo migumu k**a wayahudi wenzetu waliomkataa Kristo k**a ni Mkombozi wetu. Mungu anajifunua kwetu kwa njia ya kutukomboa katika utumwa wa dhambi kuanzia kwa wayahudi na baadaye kwa mataifa mengine kwa kuhubiriwa habari njema ya wokovu.

Injili ya dominika hii ni kutoka kwa mwinjili Mathayo (Mt 16:13-20. Katika injili ya leo Petro anamkiri Yesu kuwa ndiye “Kristo mwana wa Mungu aliye hai”. Petro anafanya ungamo hili la imani pale Yesu anapowageukia wanafunzi na kuwauliza “na ninyi mwanisema mimi kuwa ni nani”? Ilikuwa ni muhimu kabisa kuwa baada ya kumwelezea Yesu mwono wa watu juu yake, wao nao waoneshe mwono wao juu yake.

Ungamo hili la imani ambalo Petro analifanya, Yesu anamwambia si matokeo ya ubinadamu wake bali ni matokeo ya ufunuo kutoka kwa Mungu. Hili linatuonesha kuwa imani ni zawadi kutoka kwa Mungu. Ni paji linalotoka juu ambalo ni Mungu pekee anaweza kuwajalia watu wake kwa ufunuo.

Mwanadamu yeye huipokea tu zawadi hii pale anapofungua moyo wake na kuifungua akili yake kuangazwa na ufunuo huu.

Ndugu zangu wapendwa katika Kristo maswali haya yanatuhusu sana katika maisha tunayoyaishi nyakati zetu hizi. Kila mmoja wetu ajiulize nafsini mwake.Wanafunzi wakamjibu wakisema, wengi hunena u Eliya, wengine u Yohana mbatizaji, Yeremia na wengine mmoja wa manabii.

Ndugu zangu wapendwa katika kristo licha ya majibu hayo yalliyotolewa na wanafunzi Yesu hakukomea hapo, akawauliza na wao wenyewe, nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Petro mmojawapo wa wale wanafunzi akajibu swali hilo, Wewe ndiye Kristo, mwana wa Mungu aliye hai.Kutokana na jibu hili Yesu ana mkabidhi Petro madaraka ya kuliongoza kanisa yaani taifa la Mungu kwa uaminifu, kwa imani thabiti, kwa upendo thabiti na matumaini ya kweli.

Ndugu zangu wakristo tujiulize wenyewe katika mazingira yetu, watu tunaoishi nao huko mitaani wana sema Kristo ni nani? au sisi wenyewe tunasema mwana wa Adamu ni nani? kwa wale tunaoishi nao, mimi na wewe Kristo ni nani kwetu? au na sisi tunaungana na wayahudi waliotoa majibu tofauti tofauti kwa sababu walikosa imani kuwa Yesu ni mwana wa Mungu hasa kwasababu waliishinaye na mama yake na ndugu zake walikuwa wanawafahamu. Hivyo ipo hatari ya kuwalaumu wayahudi kumbe na sisi wenyewe hatumjui Kristo ni nani katika maisha yetu ya hapa duniani.

Wapendwa, kusudi tuweze kumfahamu vizuri mwana wa Adamu turejee katika jibu la mtume Petro; aliye kiri wazi kabisa kuwa wewe ndiwe Kristo mwana wa Mungu aliye hai. Ndugu zangu kwa ubatizo wetu tumemkiri Yesu Kristo kuwa ndiye dira ya maisha yetu hapa duniani na huko mbinguni hivyo tunalazimika kumtangaza kwa watu wote kuwa yeye ndiye Mwokozi.

Kristo leo anampa madaraka mtume Petro ya ufalme wa mbinguni na duniani kwamba atakalolifunga duniani litakuwa limefungwa na huko mbinguni na atakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa na mbinguni.

Ndungu zangu wapendwa katika Kristo, katika Kanisa Katoliki tuna viongozi mbalimbali wanaoliongoza kanisa hili aliloachiwa mtume Petro. Viongozi hao ni maaskofu, mapadre na mashemasi. Viongozi hawa wamepewa mamlaka ya kuliongoza kanisa.

Pia tukumbuke kuwa kila mmoja wetu ni kiongozi katika viongozi kwa kumtangaza Kristo kwa maneno na matendo yetu hivyo tuwajibike inavyotakiwa na Mungu. Si kukwepa wajibu huo.

Ndugu zangu k**a wewe ni padre, shemasi , askofu ,mtawa au mlei wajibika katika nafasi yako uliyopewa na na Kristo katika maisha yako. Shika amri za Mungu na kuziishi na kuwasaidia watu katika shida mbalimbali zinazo tukabili katika mazingira tunayoishi.

Ndugu wanafamilia ya Mungu, Yesu leo anawauliza mitume wake maswali mawili kwa makusudi kabisa. Tukirejea katika historia ya mji wa Kaisaria Filipi, ni sehemu iliyosifika sana kuwa na mahekalu mengi ya miungu ya uongo na hata jina la mji huo linatokana na hekalu lililojengwa ili kumuabudu huyo Kaisari wa kirumi Filipo.

Hivyo tunaweza kusema ni mji wa kipagani. Na hata mahali ambapo Yesu alipowauliza maswali yale kulikuwa na jiwe kubwa ambalo watu wa mji ule baadhi ya wakazi wake walikuwa wanaliabudu jiwe kuwa ni Mungu. Ni katika mazingira tatanishi ya kipagani haya ambapo Kristo anawauliza maswali wanafunzi wake kusudi aone nao wanamwitaje?

Tukirudi katika maisha yetu ya kila siku mimi na wewe tunamtambua Kristo kuwa ni nani? Hii ni changamoto kwetu sote hasa katika kumfuasa Kristo katika ulimwengu huu uliolewa na mambo ya utandawazi, kumsahau na kumkana Mungu.
wapendwa, leo tuna himizwa kuwa wafuasi wa kweli katika kumkiri Kristo hata katika mazingira magumu ambapo wengi wetu wanaya ogopa .

ombi; waaminifu katika kazi ya Bwana ya kuhubiri neno lake kwa watu wote bila ubaguzi wowote ule k**a Kristo alivyofanya na alivyotuagiza.

TUMSIFU YESU KRISTO

TAFAKARI KATEKESI

HABARI PICHA Picha za Matukio mbalimbali katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara kutoka Parokia ya Bikira Maria M...
16/08/2026

HABARI PICHA
Picha za Matukio mbalimbali katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara kutoka Parokia ya Bikira Maria Malikia wa Afrika.

Misa hiyo imeongozwa na Mhashamu Liberatusi Sangu Wa Jimbo Katoliki la Shinyanga ambapo jumla ya waimalishwa 155.

16/08/2026

LIVE ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU YA KIPAIMARA KWA WAIMALISHWA 155 KUTOKA PAROKIA YA BIKIRA MARIA MALKIA WA AFRIKA INAYOONGOZWA NA MHASHAMU ASKOFU LIBERATUSI TK SANGU WA JIMBO KATOLIKI SHINYANGA

14/08/2026

MSAFARA WA MATEMBEZI YA SANAMU LA MAMA BIKIRA MARIA KITAIFA UKIWA UMEWASILI JIMBO LA GEITA.

Tayali makabidhiano yameshafanyika kwa ajili ya kuendelea na matembezi hayo katika Jimbo la Geita.

08/08/2026

Msafara wa matembezi ya Mama Bikra Maria ukitoka parokia ya Old Shinyanga ukielekea Kanisa Katoliki La Maria Mama wa Mungu Nindo

08/08/2026

LIVE MSAFARA WA MATEMBEZI YA MAMA BIKRA MARIA UMEWASILI PAROKIA YA OLD SHINYANGA KATIKA KANISA LA WATAKATIFU PETRO NA PAUL MITUME

08/08/2026

LIVE:Msafara wa Matembezi ya Mama Bikra Maria ukiwa umewasili Kanisa la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Malampaka

08/08/2026

Mkuu wa Msafara wa Matembezi ya Bikira Maria na Raisi wa Utume wa Fatma Ulimwenguni Atilio Joseph Mvewange kutoka Jimbo Katoliki Jombe Akizungumzia Histolia fupi kuhusu Msafara wa Matembezi ya Bikra Maria

07/08/2026

KARDINALI KAMBANDA ATOA WITO KWA WANAHABARI WAKATOLIKI KUWA KICHOCHEO CHA AMANI NA UMOJA

Address

Shinyanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio farajatz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio farajatz:

Shortcuts

Share

Category