Radio farajatz

  • Home
  • Radio farajatz

Radio farajatz Ukurasa rasmi wa Radio Faraja FM Stereo I 91.3 Mhz Shinyanga
https://farajafm.co.tz/


Radio faraja ni chombo cha habari kinacholenga kutoa elimu na kusaidia jamii kwa nyakati mbalimbali,
Pia kinaendeshwa na kutoa mahudhui ya Dini ya kikristo kutoka dhehebu la Roman Catholic katika Jimbo la shinyanga Mjini, Ngokoro.

jamii

Licha ya kukuongoza kikosi cha Chelsea kutwaa ubingwa wa  UEFA Conference League na FIFA Club World Cup kwa mwaka 2025 E...
01/01/2026

Licha ya kukuongoza kikosi cha Chelsea kutwaa ubingwa wa UEFA Conference League na FIFA Club World Cup kwa mwaka 2025 Enzo Maresca ameachana rasmi na klabu hiyo akiwa ndiyo kocha mkuu.

Chelsea wanaamini kuwa mabadiliko hayo yatawqsaidia kupambania malengo yao katika mashindano yote manne ikiwemo kufuzu kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya.

01/01/2026

SEHEMU YA PILI: MISA YA MWAKA MPYA NA SHEREHE YA BIKIRA MARIA MAMA WA MUNGU KUTOKA KANISA KUU LA MAMA MWENYE HURUMA NGOKOLO JIMBO KATOLIKI LA SHINYANGA.

Misa hiyo inaadhimishwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu.

01/01/2026

SEHEMU YA KWANZA: MISA YA MWAKA MPYA NA SHEREHE YA BIKIRA MARIA MAMA WA MUNGU KUTOKA KANISA KUU LA MAMA MWENYE HURUMA NGOKOLO JIMBO KATOLIKI LA SHINYANGA.

Misa hiyo inaadhimishwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu.

KARIBU TUMTAKIE HERI YA MWAKA MPYA ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI SHINYANGA, ANDIKA COMMENT YAKO ITASOMWA LIVE NDANI YA RADIO ...
31/12/2025

KARIBU TUMTAKIE HERI YA MWAKA MPYA ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI SHINYANGA, ANDIKA COMMENT YAKO ITASOMWA LIVE NDANI YA RADIO FARAJA FM.

Hongera kwa utume na kazi zote za kichungaji Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu tunakutakia heri ya mwaka mpya 2026 Mwenyezi Mungu aendelee kukulinda na kukupa afya njema ili uendelee kufanya kazi yake hakika wana Shinyanga tunajivunia uwepo wako 💥💝

"TUNDA LA ROHO NI UPENDO"

Radio Faraja FM inakutakia heri ya mwaka mpya 2026 tunakushukuru kwa kutuchagua na kuwa pamoja nasi kwa kipindj chote ch...
31/12/2025

Radio Faraja FM inakutakia heri ya mwaka mpya 2026 tunakushukuru kwa kutuchagua na kuwa pamoja nasi kwa kipindj chote cha mwaka 2025 kwani mchango wako ni mkubwa sana kwetu na kwa jamii nzima hakika "TUIJENGE JAMII KWA PAMOJA "

NB: Tunakuahidi kuendelea kuwa na wewe kila sekunde, dakika,saa,siku,week,mwezi na mwaka mzima wa 2026 tunakupenda mko mno mno 💝💥

31/12/2025

LIVE: MISA YA MKESHA WA MWAKA MPYA INAYOFANYIKA KATIKA KANISA LA MAMA MWENYE HURUMA NGOKOLO JIMBO KATOLIKI SHINYANGA. INAYOONGOZWA NA MHASHAMU ASKOFU LIBERATUS SANGU.

Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu, leo Jumanne tarehe 30.12.2025, amewapa Daraja la Ushemasi J...
30/12/2025

Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu, leo Jumanne tarehe 30.12.2025, amewapa Daraja la Ushemasi Jumla ya Mafrateri 13 wa Jimbo.

Misa ya utolewaji wa Daraja la Ushemasi imefanyika katika kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga, na imehudhuriwa na Mapadre, watawa na waamini kutoka sehemu mbalimbali za ndani na nje ya jimbo.

Askofu sangu amewahimiza waamini kuendelea kuwaombea Mashemasi hao ili Mungu roho Mtakatifu awaongoze katika utume wao.

Aidha, amewataka Mashemasi hao kutambua kuwa, wameacha yote ikiwemo maisha ya ndoa kwa ajili ya kazi ya Mungu, hivyo wakawe walimu waaminifu wa neno la Mungu na kielelezo cha Imani kwa watu.

Mashemasi hao wapya ni Boazi Madundo kutoka Parokia ya Nyalikungu, Charles Mahembo wa Parokia ya Gula, John Mkama wa Parokia ya Buhangija, Joseph Solo wa Parokia ya Maganzo, Nicholaus Masele wa Parokia ya Old Maswa, Nobert Nyabahili wa Parokia ya Malampaka, Paschal Jilala wa Parokia ya Shishiyu na Severino Komanya wa Parokia ya Mwanangi.

Wengine ni Shemasi Simon Masolwa kutoka Parokia ya Shishiyu, Stephen Seso wa Parokia ya Malampaka, Sylvester Masano wa Parokia ya Nyalikungu, Valerian Maziku wa Parokia ya Mipa na Yusto Mrosso wa Parokia ya Mwamapalala.

Askofu Sangu ametangaza kuwapa Daraja takatifu la Upadre Mashemasi wote 13 mnamo Julai 16 mwaka 2026.

30/12/2025

LIVE: MISA YA UTOLEWAJI DARAJA LA USHEMASI KWA MAFRATELI 13 WA JIMBO KATOLIKI LA SHINYANGA
MISA INAONGOZWA NA MHASHAMU ASIKOFU LIBERATUS SANGU

Jumla ya Mafrateri 13 wa Jimbo la Shinyanga, leo wamekiri Imani na kula viapo mbalimbali mbele ya Askofu na Kanisa, ikiw...
29/12/2025

Jumla ya Mafrateri 13 wa Jimbo la Shinyanga, leo wamekiri Imani na kula viapo mbalimbali mbele ya Askofu na Kanisa, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kupewa Daraja la Ushemashi hapo kesho.

Mafrateri hao wamekiri Imani na kula viapo kupitia Ibada ya masifu ya jioni ambayo imefanyika katika kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga.

Ibada hiyo imeongozwa na Askofu wa Jimbo la Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu, ambaye amewataka Mafrateri hao kupitia Daraja la Ushemasi watakalopewa hapo kesho kwenda kumhubiri Kristo na kuwafanya watu wamwongokee Mwenyezi Mungu.

Askofu Sangu amewakumbusha kuwa, kazi ya kuokoa roho za watu kupitia mafundisho watakayoyatoa hawataiweza kuifanya kwa kutegemea nguvu zao wenyewe, bali wakaifanye kwa uchaji na unyenyekevu wakimruhusu Mungu roho Mtakatifu awaongoze katika wajibu huo.

Mafrateri hao ambao watapewa Daraja la Ushemasi hapo kesho ni Boazi Madundo wa Parokia ya Nyalikungu, Charles Mahembo wa Parokia ya Gula, John Mkama wa Parokia ya Buhangija, Joseph Solo wa Parokia ya Maganzo, Nicholaus Masele wa Parokia ya Old Maswa, Nobert Nyabahili wa Parokia ya Malampaka, Paschal Jilala wa Parokia ya Shishiyu na Severino Komanya wa Parokia ya Mwanangi.

Wengine ni Frateri Simon Masolwa wa Parokia ya Shishiyu, Stephen Seso wa Parokia ya Malampaka, Sylvester Masano wa Parokia ya Nyalikungu, Valerian Maziku wa Parokia ya Mipa na Yusto Mrosso wa Parokia ya Mwamapalala.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio farajatz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio farajatz:

  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share