Radio farajatz

Radio farajatz Ukurasa rasmi wa Radio Faraja FM Stereo I 91.3 Mhz Shinyanga
https://farajafm.co.tz/



(1)

Radio faraja ni chombo cha habari kinacholenga kutoa elimu na kusaidia jamii kwa nyakati mbalimbali,
Pia kinaendeshwa na kutoa mahudhui ya Dini ya kikristo kutoka dhehebu la Roman Catholic katika Jimbo la shinyanga Mjini, Ngokoro.

jamii

PICHA MBALIMBALI ZA  IBADA YA MASIFU YA JIONI KUTOKA PAROKIA YA FAMILIA TAKATIFU KILULU JIMBO KATOLIKI SHINYANGA .Ibada ...
13/08/2025

PICHA MBALIMBALI ZA IBADA YA MASIFU YA JIONI KUTOKA PAROKIA YA FAMILIA TAKATIFU KILULU JIMBO KATOLIKI SHINYANGA .

Ibada hiyo ni sehemu ya maandalizi ya Misa takatifu ya Upadrisho wa shemasi Pius Nzumbi Elias itakayoongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu hapo kesho tarehe 14.8.2025 .

13/08/2025

LIVE 🛑: IBADA YA MASIFU YA JIONI AMBAYO NI SEHEMU YA MAANDALIZI YA UTOLEWAJI WA DARAJA TAKATIFU LA UPADRE HAPO KESHO KWA SHEMASI PIUS NZUMBI ELIAS WA SHIRIKA LA SMA KUTOKA PAROKIA YA FAMILIA TAKATIFU KILULU JIMBO KATOLIKI SHINYANGA.

Ibada hiyo inaongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu.

Nyota wa zamani wa klabu ya Simba Sadio Kanoute amekamilisha uhamisho wake na kujiunga Azam FC  kuelekea msimu ujao 2025...
11/08/2025

Nyota wa zamani wa klabu ya Simba Sadio Kanoute amekamilisha uhamisho wake na kujiunga Azam FC kuelekea msimu ujao 2025/2026.

Nyota huyo amesaini mkataba wa miaka miwili ✅

HABARI PICHA: Picha za matukio mbalimbali wakati wa Misa takatifu ya  Kipaimara na mapokezi ya Askofu wa Jimbo Katoliki ...
11/08/2025

HABARI PICHA: Picha za matukio mbalimbali wakati wa Misa takatifu ya Kipaimara na mapokezi ya Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu katika Parokia ya Kristo Mchungaji Mwema - Lugulu iliyopo Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu.

Askofu Liberatus Sangu wa Jimbo Katoliki Shinyanga leo ametoa Sakramenti ya Kipaimara kwa Waimarishwa 108 katika misa ta...
11/08/2025

Askofu Liberatus Sangu wa Jimbo Katoliki Shinyanga leo ametoa Sakramenti ya Kipaimara kwa Waimarishwa 108 katika misa takatifu iliyofanyika katika kanisa la Kristo Mchungaji Mwema Parokia ya Lugulu Jimbo Katoliki Shinyanga.

Akihubiri katika Misa hiyo,Askofu Sangu amewataka Waimarishwa hao kuilinda imani Katoliki,kuitunza ,kuitangaza na kuiishi.

Askofu Sangu amesema Wakristo Wakatoliki hawapaswi kuiacha Imani yao ambayo Kristo yuko ndani ya Ekaristi Takatifu.
Katika hatua nyingine Askofu Sangu amewataka Wakristo Wakatoliki kuwa na upendo na kuacha kunufaika kupitia shida za watu.

Wakati huo huo Askofu Sangu amewakumbusha Watanzania kuilinda Amani iliyopo licha ya changamoto zilizopo na kuwataka kujifunza kupitia Mataifa mengine ambayo kuna machafuko yanayosababisha vifo vya watu.

10/08/2025

LIVE 🛑: MISA YA KIPAIMARA KUTOKA PAROKIA YA LUGURU WILAYA YA BARIADI MKOANI SIMIYU.

Misa hiyo inaongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu

UPIMAJI NA MATIBABU YA MOYO MKOANI SHINYANGA.Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiongozwa na Mkurugenz...
09/08/2025

UPIMAJI NA MATIBABU YA MOYO MKOANI SHINYANGA.

Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga (SRRH) watatoa huduma za tiba mkoba zinazojulikana kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services kwa kufanya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga na Mikoa ya jirani.

Upimaji huu utafanyika kwa watoto na watu wazima tarehe 18-22/08/2025 saa 2:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga (SRRH) iliyopo Mwaweza Shinganya mjini.

Watakaogundulika kuwa na matatizo ya moyo watafanyiwa uchunguzi zaidi na kupatiwa matibabu hapo hapo au kupewa rufaa ya kuja kutibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Upanga jijini Dar es Salaam. Tunawaomba wananchi mjitokeze kwa wingi kupima afya zenu kujua k**a mna matatizo ya moyo ili kuanza matibabu mapema k**a mtu atakayegundulika kuwa mgonjwa.

Kwa taarifa zaidi wasiliana kwa simu namba 0756568291 Dkt. Luzila John Mganga Mfawidhi na 0688665508 George Mganga Afisa Habari.

B“Afya ya Moyo Wako ni Jukumu Letu”.

Timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imetinga hatua ya robo fainali katika michuano ya CHAN baada ya ushindi wa goli ...
09/08/2025

Timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imetinga hatua ya robo fainali katika michuano ya CHAN baada ya ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Madagascar.

Ushindi huo unakuwa wa tatu katika michezo mitatu waliyocheza ndani ya michuano ya CHAN ambapo mchezo wa kwanza walishinda goli 2-0 dhidi ya Burkina Faso na mchezo wa pili walishinda goli 1-0 dhidi ya Mauritania.

Hadi hivi sasa Taifa Stars wamefanikiwa kufunga hatua ya robo fainali kwani bado ni vinar wa kundi B.

1️⃣ Tanzania - 9 pts
2️⃣ Mauritania - 4 pts
3️⃣ Burkina Faso- 3 pts
4️⃣ Madagascar - 1 pts
5️⃣ Central African Republic - 0 pts

Mechi ya mwisho : Tanzania vs Central African Republic ✅

09/08/2025

TAZAMA VIDEO YA ASKOFU SANGU AKIWAPONGEZA WANAWAKE WAKATOLIKI TANZANIA (WAWATA) JIMBO KATOLIKI SHINYANGA BAADA YA WANAKABIDHI VITU MBALIMBALI KATIKA SEMINARI YA MTAKATIFU ALOYSIUS GONZAGA SHANWA.

Aakofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu amewashukuru Wanawake Wakakatoliki Tanzania (WAWATA) Jimbo Katoliki Shinyanga kwa kutembelea katika Seminari ndogo ya Mtakatifu Aloysius Gonzaga iliyopo Shanwa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu na kutoa vitu mbalimbali ikiwemo gunia 28 za mahindi ikiwa ni sehemu ya kutekeleza wajibu wa mama kwa mtoto (kunyonyesha) katika malezi na makuzi ya mtoto.

09/08/2025

TAZAMA VIDEO YA WANAWAKE WAKATOLIKI TANZANIA (WAWATA) JIMBO KATOLIKI SHINYANGA WAKIWA WANAKABIDHI VITU MBALIMBALI KATIKA SEMINARI YA MTAKATIFU ALOYSIUS GONZAGA SHANWA.

Wanawake Wakakatoliki Tanzania (WAWATA) Jimbo Katoliki Shinyanga wametembelea katika Seminari ndogo ya Mtakatifu Aloysius Gonzaga iliyopo Shanwa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu na kutoa vitu mbalimbali ikiwemo gunia 28 za mahindi ikiwa ni sehemu ya kutekeleza wajibu wa mama kwa mtoto (kunyonyesha) katika malezi na makuzi ya mtoto.

HABARI PICHA : Wanawake Wakakatoliki Tanzania (WAWATA) Jimbo Katoliki Shinyanga wakiwa katika picha za pamoja baada ya k...
09/08/2025

HABARI PICHA : Wanawake Wakakatoliki Tanzania (WAWATA) Jimbo Katoliki Shinyanga wakiwa katika picha za pamoja baada ya kutembelea katika Seminari ndogo ya Mtakatifu Aloysius Ngonzaga iliyopo Shanwa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu na kutoa vitu mbalimbali ikiwemo gunia 28 za mahindi ikiwa ni sehemu ya kutekeleza wajibu wa mama kwa mtoto (kunyonyesha) katika malezi na makuzi ya mtoto.

09/08/2025

LIVE 🛑 : MISA YA KUTEKELEZA WAJIBU WA MAMA KWA MTOTO (KUNYONYESHA) KATIKA MAKUZI NA MALEZI KWA WASEMINARI WANAOSOMA KATIKA SEMINARI NDOGO YA MTAKATIFU ALOYSIUS NGONZAGA ILIYOPO SHANWA WILAYA YA MASWA MKOANI SIMIYU.

Misa hiyo inaongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu ambapo Wanawake Wakakatoliki Tanzania (WAWATA) Jimbo la Shinyanga wametembelea katika Seminari hiyo.

Address

Shinyanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio farajatz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio farajatz:

Share

Category