05/08/2026
RAS RUVUMA AVUTIWA NA UBUNIFU TUNDURU DC, ASISITIZA TEKNOLOJIA NA UONGEZAJI THAMANI KUKUZA UCHUMI
Teknolojia, ubunifu na uongezaji thamani vinaendelea kuwa nguzo za mapinduzi ya kilimo.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Wakili Mary Makondo,ametembelea Banda la Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya.
Akiwa katika banda hilo Bi. Makondo alipokea maelezo kuhusu teknolojia za kisasa na mbinu bora zinazotumiwa na Tunduru DC kuongeza uzalishaji na tija katika sekta za kilimo na mifugo.
Pia alitembelea mabanda ya wajasiriamali na kujionea bidhaa zinazozalishwa na kusindikwa wilayani humo, akipongeza juhudi zao za kuongeza thamani ya mazao na kuchochea uchumi wa ndani.
Ziara hiyo inaakisi dhamira ya Mkoa wa Ruvuma ya kuhamasisha matumizi ya teknolojia, ubunifu na ushiriki wa wadau katika kuimarisha kilimo, mifugo na ujasiriamali, sambamba na kaulimbiu ya Nanenane 2026: “Tambua Soko; Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050.”