03/06/2026
SAMAKI WA ZIWA NYASA WANAVYOTOWEKA KIMYAKIMYA:
Samaki waliowahi kujaza nyavu za wavuvi wa Ziwa Nyasa mkoani Ruvuma sasa wanapotea kwa kasi, wakiacha simulizi za huzuni kwa maelfu ya familia zinazotegemea ziwa hilo kwa chakula na kipato.
Kutoka Lituhi hadi Chiwindi Mwambao mwa ziwa Nyasa, matumizi ya nyavu amabzo hazifai kwa uvuvi endelevu na uvuvi katika maeneo ya mazalia yameendelea kuhatarisha uwepo wa samaki muhimu k**a ningo, mbasa, mbufu, mbelele na vituhi. Utafiti wa SADC unaonesha Ziwa Nyasa lina uwezo wa kuzalisha tani 165,000 za samaki.
“Samaki aina ya Ningo imebaki historia. Zamani tulivua kwa urahisi, leo unaweza kukesha ziwani bila kupata chochote,” anasema Vikta Komba, mkazi wa Kijiji cha Nkali kata yya Liuli . Naye Mary Haule wa Lituhi anasema bei ya samaki imepanda sana kutokana na upungufu mkubwa wa samaki.
Wataalamu wa mazingira wanaonya kuwa uvuvi katika maeneo ya mazalia, hasa Mto Ruhuhu, unavuruga mzunguko wa uzalishaji wa samaki na kuhatarisha mfumo mzima wa ikolojia ya ziwa.
Licha ya Sera ya Taifa ya Mazingira ya 1997 na sheria za uvuvi kupiga marufuku nyavu ndogo na uvuvi kwenye mazalia, utekelezaji wake bado unakabiliwa na changamoto.
Bila hatua madhubuti kuchukuliwa, Ziwa Nyasa linaweza kubaki na simulizi za samaki waliowahi kuwapo badala ya utajiri wa samaki unaolisha na kuinua uchumi wa vizazi vijavyo.