Kusini News

Kusini News Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Kusini News, News & Media Website, Songea.
(2)

PATA HABARI NA MAKALA MBALIMBALI ZA KUVUTIA KIDIJITALI KUTOKA KATIKA VIJIJI,HALMSHAURI,WILAYA,MIKOA,KITAIFA NA KIMATAIFA KUPITIA KUSINI MEDIA KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA SIMU 0784765917 BARUAPEPE [email protected]

SAMAKI WA ZIWA NYASA WANAVYOTOWEKA KIMYAKIMYA: Samaki waliowahi kujaza nyavu za wavuvi wa Ziwa Nyasa mkoani Ruvuma  sasa...
03/06/2026

SAMAKI WA ZIWA NYASA WANAVYOTOWEKA KIMYAKIMYA:

Samaki waliowahi kujaza nyavu za wavuvi wa Ziwa Nyasa mkoani Ruvuma sasa wanapotea kwa kasi, wakiacha simulizi za huzuni kwa maelfu ya familia zinazotegemea ziwa hilo kwa chakula na kipato.

Kutoka Lituhi hadi Chiwindi Mwambao mwa ziwa Nyasa, matumizi ya nyavu amabzo hazifai kwa uvuvi endelevu na uvuvi katika maeneo ya mazalia yameendelea kuhatarisha uwepo wa samaki muhimu k**a ningo, mbasa, mbufu, mbelele na vituhi. Utafiti wa SADC unaonesha Ziwa Nyasa lina uwezo wa kuzalisha tani 165,000 za samaki.

“Samaki aina ya Ningo imebaki historia. Zamani tulivua kwa urahisi, leo unaweza kukesha ziwani bila kupata chochote,” anasema Vikta Komba, mkazi wa Kijiji cha Nkali kata yya Liuli . Naye Mary Haule wa Lituhi anasema bei ya samaki imepanda sana kutokana na upungufu mkubwa wa samaki.

Wataalamu wa mazingira wanaonya kuwa uvuvi katika maeneo ya mazalia, hasa Mto Ruhuhu, unavuruga mzunguko wa uzalishaji wa samaki na kuhatarisha mfumo mzima wa ikolojia ya ziwa.

Licha ya Sera ya Taifa ya Mazingira ya 1997 na sheria za uvuvi kupiga marufuku nyavu ndogo na uvuvi kwenye mazalia, utekelezaji wake bado unakabiliwa na changamoto.

Bila hatua madhubuti kuchukuliwa, Ziwa Nyasa linaweza kubaki na simulizi za samaki waliowahi kuwapo badala ya utajiri wa samaki unaolisha na kuinua uchumi wa vizazi vijavyo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa V...
03/06/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Vnukovo, uliopo Jijini Moscow kwa ajili ya Ziara ya Kitaifa, nchini Urusi tarehe 02 Juni, 2026. Ziara hii ina lenga kuimarisha uhusiano wa Kidiplomasia, kisiasa, kiuchumi na kihistoria baina ya Tanzania na Urusi.

SHULE ZA AMALI ZAWASHA TAA YA MAPINDUZI YA UCHUMI RUVUMAAsubuhi moja katika Kijiji cha Utiri, Mbinga, mkoani Ruvuma  sau...
03/06/2026

SHULE ZA AMALI ZAWASHA TAA YA MAPINDUZI YA UCHUMI RUVUMA

Asubuhi moja katika Kijiji cha Utiri, Mbinga, mkoani Ruvuma sauti za nyundo za mafundi zilianza kuandika historia mpya. Leo, eneo hilo linaibuka kuwa kitovu cha matumaini kupitia Shule ya Sekondari Amali Utiri, mradi unaolenga kuzalisha vijana wenye ujuzi wa kujiajiri na kushindana katika soko la ajira la kisasa.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Shule hiyo , Benitho Komba, shule hiyo ilisajiliwa Januari 9, 2026 na imegharimu Sh milioni 740, ambapo zaidi ya Sh milioni 560 zimetolewa kupitia Programu ya Uboreshaji wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP). Shule ina madarasa 8, maabara za sayansi, maabara ya kompyuta, maktaba na nyumba ya mwalimu.

Takwimu za ILO za mwaka 2023 zinaonesha luwa zaidi ya asilimia 21 ya vijana Afrika wanakabiliwa na changamoto za ajira, huku UNESCO (2024) ikibainisha kuwa ajira nyingi mpya duniani zinahitaji stadi za teknolojia na ubunifu.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga, Amina Sefu, amesema shule mpya ya Bethrehem pia imejengwa kwa zaidi ya Sh milioni 740, hatua iliyopunguza msongamano wa wanafunzi na kuboresha mazingira ya kujifunzia.

Elimu ya vitendo leo, ni uchumi imara kesho.

DKT. RIZIKI ATOA WITO WA KUJENGA FAMILIA IMARAJe, familia zenye mshik**ano zinaweza kuwa msingi wa maendeleo endelevu? H...
02/06/2026

DKT. RIZIKI ATOA WITO WA KUJENGA FAMILIA IMARA

Je, familia zenye mshik**ano zinaweza kuwa msingi wa maendeleo endelevu? Hilo ndilo swali linalopewa majibu kupitia tukio kubwa la Mtoko wa Familia 2026 linalotarajia kufanyika Julai 4, 2026 kwenye ukumbi wa Songea Club, mkoani Ruvuma.

Akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Madaba, wilayani Songea Mkurugenzi Mtendaji wa Rizex for Life Foundation, Dkt. Riziki Suleiman, amesema tukio hilo linalenga kuimarisha amani, umoja, ushirikiano na mshik**ano wa kifamilia na kijamii.

Amesisitiza kuwa familia zenye mahusiano imara huchangia kupunguza migogoro ya kijamii na kuongeza ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo.
Dkt. Riziki amesema Mtoko wa Familia ni zaidi ya burudani; ni jukwaa la kujifunza, kubadilishana uzoefu na kujenga mitandao ya mahusiano yenye tija.

“Tunajenga jamii bora kwa kuanzia na ngazi ya familia imara,” amesisitiza Dkt. Riziki.

Mtoko wa Familia 2026 ni jukwaa muhimu litakalowakutanisha wadau mbalimbali kwa lengo la kuimarisha mshik**ano na mustakabali wa jamii .

WANANCHI TUNDURU WAHIMIZWA KUILINDA AMANI, KUITUNZA MIRADI NA KUWEKEZA ZAIDI KATIKA ELIMUMustakabali wa maendeleo ya Wil...
02/06/2026

WANANCHI TUNDURU WAHIMIZWA KUILINDA AMANI, KUITUNZA MIRADI NA KUWEKEZA ZAIDI KATIKA ELIMU

Mustakabali wa maendeleo ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma unategemea jinsi wananchi wanavyolinda amani, kutunza miradi ya maendeleo na kuwekeza katika elimu ya watoto wao.
Hayo yamesisitizwa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe. Denis Masanja, wakati wa ziara yake katika Kata za Marumba na Mbati.

Akizungumza kwenye mikutano ya hadhara, Mhe. Masanja alisema amani ndiyo nguzo kuu inayowezesha uwekezaji, utoaji wa huduma na ustawi wa jamii, huku akiwataka wananchi kuendelea kuidumisha ili kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Katika sekta ya kilimo, aliwahamasisha wakulima kutumia mfumo wa Stakabadhi Ghalani, akieleza kuwa mfumo huo umeendelea kuwasaidia kupata bei bora na kuongeza ushindani wa mazao sokoni.

Pia alisisitiza umuhimu wa mpango bora wa matumizi ya ardhi ili kupunguza migogoro na kuhakikisha rasilimali hiyo muhimu inanufaisha kizazi cha sasa na kijacho.

Kwa upande wa elimu, DC Masanja aliwataka wazazi na walezi kuhakikisha watoto wote wa umri wa kwenda shule wanapata elimu, akibainisha kuwa elimu ni kichocheo kikubwa cha kupunguza umaskini na kuongeza maendeleo ya jamii.

KAMPUNI  YA AVIV TANZANIA YATOA KOMPYUTA YA MILIONI 2.5 KWA OFISI YA MKUU  WA MKOA WA RUVUMA kampuni ya kahawa ya AVIV T...
02/06/2026

KAMPUNI YA AVIV TANZANIA YATOA KOMPYUTA YA MILIONI 2.5 KWA OFISI YA MKUU WA MKOA WA RUVUMA

kampuni ya kahawa ya AVIV Tanzania Limited imekabidhi kompyuta ya kisasa aina ya HP 13th Generation yenye thamani ya Sh milioni 2.5 kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.

Kompyuta hiyo imekabidhiwa ikiwa imeambatana na vifaa muhimu vya matumizi ikiwemo monitor, mouse, keyboard, HDMI cable na power cable.
Kompyuta hiyo imekabidhiwa kwa Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Ndugu Jumanne Mwankhoo

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, mwakilishi wa AVIV Tanzania Limited alisema kampuni hiyo inaamini teknolojia ni nguzo muhimu katika kuharakisha maendeleo na kuboresha huduma kwa jamii.

Hatua ya AVIV Tanzania Limited inaonesha jinsi sekta binafsi inavyoendelea kushirikiana na serikali katika kuimarisha mazingira ya kazi na kuharakisha safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa kidijitali.

KIWANDA CHA BILIONI TATU KINAVYOBADILI MAISHA YA VIJANA RUVUMA, AJIRA 60 ZA KUDUMU ZATOKEAKijiji cha Lipokela wilayani  ...
02/06/2026

KIWANDA CHA BILIONI TATU KINAVYOBADILI MAISHA YA VIJANA RUVUMA, AJIRA 60 ZA KUDUMU ZATOKEA

Kijiji cha Lipokela wilayani Songea mkoani Ruvuma leo kimegeuka kitovu cha ajira na uchumi baada ya uzinduzi wa kiwanda cha kisasa cha kusaga kokoto cha kampuni ya OVANS CONSTRUCTION LTD chenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni tatu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Mhandisi Valence Urio amesema Mradi huo uliozinduliwa umezalisha ajira zaidi ya 100 za muda wakati wa ujenzi na ajira 60 za kudumu kwa vijana na wanawake wa Ruvuma.

Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mheshimiwa Kapenjama Ndile, alisema kiwanda hicho kitapunguza utegemezi wa kokoto kutoka Chalinze mkaoni Pwani na kushusha gharama za miradi ya ujenzi Kusini mwa Tanzania.

Kiwanda hicho kinazalisha aina tisa za kokoto zinazotumika kwenye barabara, majengo na miradi mingine ya maendeleo.

Miongoni mwa wanufaika wa kiwanda hicho ni Mwanga Stanley aliyesema ajira hiyo imemwezesha kununua kiwanja, huku Klaudia Komba akieleza kuwa sasa ana uwezo wa kugharamia elimu ya mtoto wake.

Kiwanda hicho kinaibuka k**a mfano halisi wa jinsi uwekezaji wa ndani unavyoweza kuchochea ajira, kuongeza mapato ya wananchi na kuimarisha uchumi wa Ruvuma.

MAFUNZO YA  LISHE NA MASOKO KUFUNGUA MILANGO YA AJIRA KWA VIJANA WA RUVUMA Wakati maelfu ya vijana nchini wakikabiliwa n...
02/06/2026

MAFUNZO YA LISHE NA MASOKO KUFUNGUA MILANGO YA AJIRA KWA VIJANA WA RUVUMA

Wakati maelfu ya vijana nchini wakikabiliwa na changamoto ya ajira, zaidi ya vijana 250 wa Ruvuma tayari wameanza kunufaika na mapinduzi ya kilimo-biashara kupitia mradi wa YEFFA.

Akizungumza mjini Songea, Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi. Mary Makondo, alisema zaidi ya asilimia 85 ya wakazi wa mkoa huo wanategemea kilimo, hivyo vijana wanapaswa kutumia teknolojia, kuongeza thamani ya mazao na kuingia kwenye masoko yenye ushindani.

Kwa mujibu wa Benki ya Dunia na FAO, sekta ya kilimo inaajiri zaidi ya asilimia 65 ya Watanzania. Hata hivyo, ukosefu wa mitaji, teknolojia na masoko umekuwa kikwazo kikubwa kwa vijana wengi.

Alisema kilimo cha kisasa ni biashara inayoweza kuzalisha ajira, kuongeza kipato na kuboresha lishe ya jamii.

Kupitia mradi wa YEFFA unaotekelezwa na GAIN Tanzania, AGRA na Mastercard Foundation, vijana 100 Songea wamepata mafunzo ya kuongeza thamani ya mazao, huku vijana 45 Mbinga wakithibitishwa kuwa wazalishaji wa mbegu bora.

Ruvuma inaonesha kuwa vijana wakipewa maarifa, teknolojia na masoko, kilimo kinaweza kuwa injini mpya ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

WALIMU WAPYA NYASA WATAHADHARISHWA MAADILI, WELEDI NA AMANI Katika kipindi ambacho mitandao ya kijamii imekuwa na ushawi...
02/06/2026

WALIMU WAPYA NYASA WATAHADHARISHWA MAADILI, WELEDI NA AMANI

Katika kipindi ambacho mitandao ya kijamii imekuwa na ushawishi mkubwa kwa jamii, walimu wapya wa Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma wamepewa ujumbe wa uadilifu, weledi na kulinda amani kuwa ni msingi wa mafanikio yao kazini.

Akifungua mafunzo elekezi kwa walimu wa shule za msingi na sekondari walioajiriwa kati ya Februari na Mei 2026 katika Shule ya Sekondari Lovund, Katibu Tawala wa Wilaya ya Nyasa, Bw. Salum Ismail, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, aliwataka walimu hao kuwa mfano bora kwa wanafunzi na jamii.

Bw. Ismail alisema tafiti nyingi za elimu zinaonesha kuwa walimu wenye maadili na nidhamu bora huchangia kwa kiasi kikubwa kuongeza ufaulu wa wanafunzi na kujenga mazingira salama ya kujifunzia. Aliwasisitiza kutekeleza majukumu yao kwa kujituma, kusimamia nidhamu, kuzingatia mavazi yenye staha na kutumia mitandao ya kijamii kwa uwajibikaji.

Pia aliwataka kuwa mabalozi wa amani katika maeneo yao ya kazi kwa kushirikiana na jamii badala ya kuwa chanzo cha migogoro.

Mafunzo hayo yanalenga kuwajengea walimu wapya msingi imara wa taaluma na kuwaandaa kuzalisha matokeo chanya katika sekta ya elimu.

02/06/2026

TAKUKURU RUVUMA YAREJESHA MILIONI 9 ZA MRADI WA UVIKO-19
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Ruvuma imefanikiwa kurejesha kiasi cha Shilingi 9,072,126 serikalini baada ya kubaini matumizi mabaya ya fedha za mradi wa UVIKO-19 katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa.
Akitoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2026, Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma, Bw. Arterio Kawonga, amesema TAKUKURU Wilaya ya Nyasa ilikamilisha uchunguzi wa tuhuma za uhujumu uchumi na kuwafikisha watuhumiwa mahak**ani.

Address

Songea

Telephone

+255784765917

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kusini News posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kusini News:

Share