
19/07/2025
WATANZANIA TUFANYEJE IKIWA MPAKA SASA CCM HAWAPO TAYARI KUFANYA MABADIRIKO YA SHERIA ZA UCHAGUZI BILA CHADEMA NA WATETEZI WA HAKI KUJITOLEA KUMBWAGA DAMU YA WANACHAMA WAKE NA WATETEZI WENGINE WA HAKI AMBAO NAO HAWAPO TAYARI KUIMWAGA DAMU YAO ILI KUPAMBANA DHIDI YA CCM KWA LENGO LA KUWEZESHA KUFANIKISHA SHERIA ZA HAKI ZA UCHAGUZI?
Je CHADEMA na watetezi wengine wa haki wafanyeje ikiwa mpaka sasa CHADEMA imefungiwa kisheria na mahak**a kufanya shughuli za kisiasa huku mwenyekiti wake Tundu Lissu yupo mahabusi wakati kesi yake inafanyiwa usanii wa muendelezo wa kuarishwa kusikilizwa mashauri yake kiwango kwamba upo uwezekano wa kuipitiliza kesi yake mpaka baada ya uchaguzi batili wa kupora mamlaka ya uongozi wa nchi yetu?
Je watanzania mna ushauri wowote kwa CHADEMA kabla ya mabadiriko ya sheria za uchaguzi kubwagwa na serikali ya CCM hivyo kusababisha CHADEMA kutokufanya siasa kwa miaka mitano wakati viongozi wake wakiwa wamefungiwa kuhutubia mikutano ya hadhara ya uchaguzi?
Je watanzania wafanyeje ikiwa k**a bila wanachama wa CHADEMA kukubali kumwaga damu yao iweze kupambana dhidi ya serikali kudai mabadiriko ya sheria za uchaguzi tutaendelea kubuluzwa, kutekwa, KUUWAWA, kufungwa magereza kwa kesi za kusingiziwa
Je watanzania tukubali kuwa sisi ni wapumbavu wa kukubali kuporwa mamlaka ya uongozi na kikundi kidogo kinachotumia vibaya vyombo vya ulinzi na usalama kupora mamlaka uongozi wa ngazi zote za serikali kuanzia baraza la madiwani, bunge, mahak**a na vyombo vya ulinzi na usalama?
Leteni majibu yenu yasugue akili zetu. Mjadala huu unaendelea kwenye group la Jitambue Kifalsafa ambalo unaweza kujiunga kupitia link hiyo chini
https://chat.whatsapp.com/F7CQSSIAKW92S4RzKuQH3S?mode=ac_t
Ni mimi admin wa group k**anda Doctor Claudius Haule Ligendayika Mwenyekiti wa chadema wilaya ya Songea ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la wazee kanda ya kusini.