18/12/2022
NINI MAANA, MATUMIZI NA MALENGO YA BIOTECHNOLOGY YAANI KWA KISWAHILI INAYOPASWA KUITWA UHANDISI WA VIINI HAI VYA KIBAOLOJIA.
Kuna fikra potofu za baadhi ya wataalamu wa afya za ukwezaji wa kutishia utata wa ujuaji, matumizi na malengo ya sayansi ya afya ya biotechnology yaani uhandisi wa viini hai vya kibaolojia kana kwamba ni elimu ya kisayansi yenye upekee wa kutisha ujuaji wake unaolazimisha washiriki wa matumizi ya elimu hiyo ya biotechnology kulazimika kuhitimu kiwango cha chuo kikuu kitu ambacho siyo kweli.
Nikiwa mtaalamu wa phytomedical science, biotechnology, electronic engineering na celestial engineering leo nitaelimisha maana ya biotechnology, matumizi yake na malengo yake kisha mtagundua ukweli kuwa wengi wenu mmetumia maarifa ya elimu ya biotechnology kwa kiwango cha uhitimu wa elimu ya chuo kikuu bila kujijua.
Biotechnology ni sayansi ya kiteknolojia ya uhandisi wa namna ya kushirikisha maarifa mbalimbali ya sayansi za kiteknolojia zenye uwezo wa kufanikisha ugunduzi wa viini hai vya kimolekuli vya kibaolojia, chembe hai za viumbe hai, vifurushi vya kibaolojia vya virutubisho lishe, kinga na dawa kwa malengo ya uzalishaji wa vifurushi vya kibaolojia vya virutubisho lishe vya afya ya binadamu, vifurushi kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali na vifurushi dawa za kuponyesha magonjwa ya wanyama na mimea pamoja na uzibiti wa mapambano dhidi ya chembe hai za vijidudu vya uzalishaji wa magonjwa mbalimbali ya wanyama na mimea.
Biotechnology inafanikishwa matumizi na malengo yake kwa kushirikisha sayansi za kiteknolojia za uhandisi mbalimbali k**a zifuatazo;
1) Molecular biology yaani sayansi ya uhandisi wa kibaolojia wa viini hai vya kimolekuli inayolazimisha matumizi ya teknolojia za mashine za blenda, mashine za kusanga unga, matumizi ya kemikali za reagents zenye malengo ya utenganishaji wa chembe hai, molekuli na vifurushi vya kibaolojia vya virutubisho lishe na vifurushi kinga na dawa.
2) Cellular biology yaani sayansi ya uhandisi wa chembe hai za viumbe hai yenye malengo ya kujua chembe hai za viumbe hai mbalimbali, utofauti na uhusiano wa chembe hai hizo na namna zinavyowezekana kutumika kwa manufaa ya viumbe uhai mbalimbali vya wanyama na mimea. Pia Cellular biology hulazimisha matumizi ya teknolojia za mashine za blenda, kemikali za reagents na darubini.
3) Genetics ni sayansi ya afya ya kibaolojia inayohusu maarifa ya utambuzi wa RNA, DNA, vinasaba( genes ), utofauti wa vinasaba ( genes), uhusiano wa vinasaba unaosababisha utofautisha na ufananaji wa vinasaba na mwisho ni urithishaji wa vinasaba.
4) Genomics ni sayansi ya afya inayohusu utambuzi, matumizi na malengo ya ujumla wa DNA ya aina ya kiumbe yeyote husika ambaye DNA yake inamiliki ukamilifu wa vinasaba ( genes) vyake, maumbile ya vinasaba vyake, utendaji wa vinasaba vyake, historia ya mabadiriko ya vinasaba vyake na marekebisho ya vinasaba . Wengi hupotosha Genomics kwa kuifanya kuwa genetics japo kwa kiwango fulani kuna uhusiano kwa sababu genetics ni chimbuko lililozalisha Genomics.
4) Genetic engineering au gene editing yaani sayansi ya uhandisi wa marekebisho ya vinasaba yenye maarifa ya kulazimisha matumizi ya teknolojia za uhandisi wa matumizi ya vifaa vya mashine za umeme, mashine za elekronic, darubini na reagents kwa lengo la kutenganisha, kuunganisha na kurekebisha vinasaba. Genetic engineering ndiyo iliyo kiini cha teknolojia ya uhandisi wa CRISPR CAS 9 yenye uwezo wa kupandikiza sifa na vitendo vya vinasaba kutoka kwenye aina yeyote ya kiumbe hai kwenda kwa aina yeyote ya kiumbe hai ikiwa pamoja na matumizi ya vinasaba hivyo kuviwezesha kuwa dawa za uponyaji wa magonjwa ya wanyama na mimea au kuwa vyanzo vya viangamizi vya uzalishaji wa magonjwa mbalimbali yenye lengo la kuangamiza aina yeyote ya kiumbe akiwemo aina ya rangi yeyote ya binadamu, iwe ya kiafrika, kiasia au kizungu yaani kiyuropa.
5) Phytopharmacology ni sayansi ya afya ya uhandisi wa utenganishaji, uunganishaji na urekebishaji wa viini hai vya vifurushi vya kibaolojia vya mimea vilivyolengwa kuwa virutubisho lishe vya ujenzi wa afya bora, vifurushi dawa za kinga na uponyaji wa magonjwa yote mbalimbali ya wanyama na mimea. Phytopharmacology ni msingi wa mwanzo wa uhandisi wa synthetic pharmacology ujulikanayo kuwa pharmaceutical engineering au pharmaceutical technology ambayo huzalisha madawa ya kifamasia( pharmaceutical drugs)
6) Micro biology ni sayansi ya afya ya uhandisi wa utambuzi wa viini hai vya kibaolojia vidogo kabisa vya mwisho kwa ukubwa wake ambavyo hulazimisha kushirikisha uhandisi wa cellular biology, molecular biology, genomics na genetics
7) Biological celestial engineering ni uhandisi wa utambuzi wa namna ya kujua maarifa ya nguvu za mvutano wa umeme wa sumaku wa vitu vya anga vya mwezi, sayari na nyota zinavyoathiri muundo na utendaji wa viini hai vya kibaolojia. Elimu hii ndiyo inayowezesha utabibu wa kuponyesha ugonjwa wa kifafa na baadhi ya magonjwa ya utaahira na ya ukichaa.
Kwa hiyo wewe k**a mtabibu ukiwa na maarifa ya phytopharmacology ujuwe una elimu ya uhandisi wa biotechnology. Pia usitishike na msamiati huo wa phytopharmacology kiwango kwamba ukajiona hauhus**i kivitendo kwenye utaalamu wa uhandisi huo wa phytopharmacology. Phytopharmacology ni msamiati unaotokana na maneno mawili yaani phyto yenye maana ya mimea na pharmacology yenye maana ya utenganishaji, uunganishaji na urekebishaji wa vifurushi dawa vya kinga na uponywaji wa magonjwa ya wanyama na mimea.
Hivyo basi wengi wenu hapa mmekuwa wahandisi wa biotechnology na phytopharmacology bila kujijua kwa kufanikiwa kutenganisha vifurushi dawa kwa kutumia reagents za kemikali za kibaolojia za ethanol, mafuta ya petroli, vinegar yaani s**i, mafuta ya kula na kazalika.
Pia wengi wenu hapa mmekuwa wahandisi wa Genetics na Genomics bila kujua kwa kufanikisha kufanya marekebisho ya vinasaba vya wanyama na mimea japo katika hali ya kawaida sana lakini mlifanikiwa kupandikiza vinasaba kutoka kwenye species ya kiumbe hai mmoja tofauti kwenda kwenye species kingine tofauti ambacho kimefanana kwenye genus ya aina moja. Mfano wale ambao walilima mahindi ya aina mbili tofauti za species ambazo zipo kwenye aina moja ya genus lakini mkaamua kukata maua dume yote yenye mbegu dume ya species ya aina moja na kuacha maua dume yote yenye mbegu dume ya aina ya pili ya species na hatimaye kufanikiwa kuzalisha mbegu ya chotara yaani hybrid watakuwa wamethibitika kuwa wahandisi wa Genomics na Genetics. Hapa msifanye complecations. Naomba tuelekezane vizuri ili tuelimishane.
Ni ukweli usiopingika kuwa karibu sisi sito tuliopo hapa hatuna maarifa ya vitendo ya uhandisi wa genetic engineering or gene editing technology lakini upo uwezekano wa wachache wetu wenye elimu ya nadharia ya Genetic engineering nikiwemo na mimi mwenyewe mwandishi wa mada hii. Ukweli ni kwamba uhandisi wa teknolojia ya CRISPR CAS 9 Bado haijaelimishwa kwa vitendo kwenye vyuo vikuu vyote vya Afrika kusini mwa jangwa la Sahara.
Ni aibu ya kisomi kupotosha ukweli kuwa eti watabibu wetu hawana elimu ya uhandisi wa molecular biology wakati dawa za watabibu hao wa tiba asili zimetengenezwa kwa kutambua utenganishaji wake kwa kiwango cha kimolekuli za kibaolojia zenye vifurushi dawa za kinga na uponywaji wa magonjwa mbalimbali ya wanyama na mimea.
Kinachotakiwa kuwaelimisha watabibu wa tiba asili na mbadala ni kuwaelewesha kuwa viwango vya maarifa wanayotumia kutengenezea dawa zao za kinga na uponywaji wa magonjwa mbalimbali ya wanyama na mimea wanatumia maarifa ya uhandisi wa aina mbalimbali pasipo wao wenyewe kujua kuwa wana elimu za aina mbalimbali za uhandisi zinazoshirikishwa kufanikisha utengenezaji wa dawa zao zikihusisha uhandisi wa molecular biology, cellular biology, genomics na genetics
Haina maana ya kueleza kiwango changu cha uhandisi wa biotechnology lakini nimefanikishwa kuwezeshwa kuelimishwa biotechnology kwa vitendo kwa ushirikishwaji wa mkufunzi wangu aliyenielimisha kwa vitendo nikiwa nje ya nchi. Nawaomba watabibu wenzangu wa tiba asili na mbadala msitishike na misamiati iliyokuwa kwenye uhandisi wa biotechnology wakati wengi wenu wenu mmetekeleza kwa vitendo aina zake mbalimbali za uhandisi wa biotechnology. Kinachowafanya muonekane hamjui ni utofauti tu wa matumizi ya lugha za kiteknolojia ambazo Kiingreza kina misamiati yake na kiswahili kina misamiati yake ijapokuwa misamiati hiyo haijakua kiasi cha kuiwakilisha kuwa misamiati sahihi ya kisayansi ya lugha ya kiswahili
Ni kashfa kuwaambia eti watabibu wetu wa tiba asili na mbadala hawana elimu ya cellular biology kwa sababu tu hawana darubini za kuwawezesha kuona chembe hai. Lakini unawezaje kupotosha ukweli kuwa watabibu wetu hawana uhandisi wa cellular biology wakati dawa zao nyingi ni cellular tea yaani ni chai ya chembe hai? Hapa cha msingi ni kuwafumbua macho watabibu wetu kuwa wanachohudumia chai zao za chembe hai zinazokutwa kwenye utabibu wenye mafanikio ya uponyaji wa magonjwa mbalimbali basi wajuwe wana viwango vikubwa vya uhandisi wa cellular biology ambavyo vinapaswa kueliweshwa maana yake kwa vitendo wavifanyavyo kwenye utabibu wao.
Mimi nikiwa kwenye ushirikiano na mhandisi wa biotechnology kutoka uingereza tulifanikiwa kutembelea kitabibu nchi tano za kiafrika ambazo zilimshangaza mwingereza huyo kuona uwezo wa kiafrika wa kutumia uhandisi wao wa kiasili wa biotechnology ambao hautambuliki kwao kuwa ni biotechnology ambao unaowawezesha kutengeneza dawa zao za kuponyesha magonjwa mbalimbali ya wanyama na mimea.
Umefika wakati serikali za kiafrika zinawajibika kuwaelimisha watabibu wetu waweze kutambua viwango vya elimu zao za kitabibu zikihusisha kwenye uwezo wao wa utambuzi wa maarifa ya uhandisi wa biotechnology, molecular biology, cellular biology, Genomics na Genetics huku wakilengwa kuboresha ubora wa ufanisi wa aina hizo za uhandisi wa biotechnology, molecular biology, cellular biology genomics na genetics
Kwa vile nimebahitika kuwa na elimu ya uhandisi wa electronic engineering nitalazimika siku moja kuelimishwa namna ya utengenezaji wa vifaa mbalimbali vinavyotumika kwenye biotechnology ili kuwawezesha watabibu wetu waweze kutengeneza vipimo vya kupima viwango vya acid na alkali za dawa wanazotengeza kwa lengo la kuepuka kutengeneza dawa zenye sumu zinazouwa figo, ini, mapafu na moyo pamoja na kusababisha vidonda vya tumbo.
Siku za mbeleni nitalazimika kuwaelimisha watabibu wenzangu namna ya kutenganisha DNA kutoka kwenye tishu za aina zozote za mimea na wanyama ili watabibu wetu wakielewa wawe na ujasiri wa kutotishwa eti hawana elimu ya uhandisi wa Genomics inayowawezesha kujua kiwango cha umeme wa kibaolojia wa DNA ya species ya aina moja ya genus na kuuhusisha umeme wake wa kibaolojia dhidi ya RNA za virus au DNA za virus au DNA ya fungus au DNA ya aina yeyote ya mmea na mnyama.
Nitalazimika kuwafundisha kwa vitendo namna ya kuvitengeneza vifaa na mashine za aina mbalimbali za biotechnology nikiwa k**a mtaalamu wa electronic engineering ili kila mmoja wetu awezeshwe kutengeneza vifurushi dawa vya tiba asili na mbadala kwa lengo la kufanikisha uponyaji wa magonjwa mbalimbali ya wanyama na mimea.
Maamuzi haya nimeyafanya baada ya kuona watabibu wetu wa tiba asili na mbadala wanadhalilisha hasa na wale waliokuwa kwenye ajira rasmi zinazotambulika kiserikali.
Kwa maswali zaidi kuhusu mada hii niliyoiwasilishwa kwenu na matatizo ya magonjwa yote sugu nipigie 0757559876
Ni mimi Doctor Claudius Haule Ligendayika wa Songea.