Mwanafalsafa Claudius HAULE Ligendayika

Mwanafalsafa Claudius HAULE Ligendayika Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Mwanafalsafa Claudius HAULE Ligendayika, Film/Television studio, Quarters Street Majengo, Songea.

TAMBUA MAANA YA TAFSIRI YA KISHERIA YA KOSA LA UHAINI LILIVYOTAFSIRIWA KWENYE SHERIA ZA TANZANIA NA UMUHIMU WAKE WA KIKA...
17/08/2023

TAMBUA MAANA YA TAFSIRI YA KISHERIA YA KOSA LA UHAINI LILIVYOTAFSIRIWA KWENYE SHERIA ZA TANZANIA NA UMUHIMU WAKE WA KIKATIBA WA KUIREKEBISHA AU KUTOIREKEBISHA.

Kwa kufuata sheria za Tanzania kifungu cha 39 ( 1 ) cha kanuni za adhabu kinahukumu kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya Muungano au popote, kujaribu kumuua Rais, kuanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Muungano, kusababisha, kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kuhusu kifo, kumlemaza, kumzuia, kufungwa kwa Rais.

Kumwondolea Rais heshima na jina la mkuu wa nchi, amiri jeshi mkuu, au kiongozi wa serikali, kupindua serikali iliyo madarakani, kutishia serikali, bunge au mahak**a kwa makosa haya na yale yaliyotajwa hapo juu mtu wa namna hiyo atakuwa ametenda kosa la jinai ambalo ni kosa la uhaini

Kwa kufuata sheria za Tanzania imehalalishwa kuhukumu kifo kwa raia yeyote atakaye wekwa hatiani kwa kosa la uhani kulingana na kifungu cha sheria namba 39 na 40 cha kanuni ya adhabu.

Watanzania tuwe makini kwenye hotuba zetu za kisiasa tunazozielimisha kwenye umma wa watanzania ili zisikiuke sheria za nchi na kusababisha tuhukumiwe kifo kwa kosa la uhaini.

Kupinga makosa yaliyofanyika kwenye mkataba wa bandara siyo kosa la jinai wala siyo kosa la uhaini. Pia kufanya maandamano ya kupinga makosa yaliyofanyika kwenye mkataba wa bandara siyo kosa la jinai wala siyo kosa la uhaini. Hapa inamaanisha kuwa kupinga makosa ya serikali na viongozi wake siyo kosa la uhaini.

Bali kwa mujibu wa kanuni za adhabu ya kifungu cha sheria namba 39 na 40 ni kosa la uhaini kuangusha mamlaka ya urais kinyume cha sheria za nchi na za kikatiba, ni kosa la uhaini kuangusha taasisi ya urais kinyume cha sheria za nchi na za kikatiba, ni kosa la uhaini kuangusha mamlaka ya bunge, ni kosa la uhaini kuangusha mamlaka ya mahak**a, ni kosa la uhaini kuangusha mamlaka ya viongozi wa serikali na pia ni kosa la uhaini kuiondolea heshima serikali na viongozi

Kwa hiyo basi kwa kufuata sheria za Tanzania imebainika kuwa serikali ya Tanzania kamwe haiwezi kuangushwa kwa njia ya maandamano, au kwa njia ya kuikosesha heshima serikali na viongozi wake kwa sababu kufanya hivyo ni kosa la uhaini.

Swali linakuja, je ni aina gani ya ukosoaji dhidi ya makosa ya serikali na viongozi wake ambao hautaikosesha heshima serikali na viongozi wake? Je hatuoni umuhimu wa kurekebisha sheria hiyo inayotafsiri kosa la uhaini na hukumu yake? Naomba majibu yenu.

Kwa maswali na ushauri nipigie 0757559876.

Ni mimi Doctor Claudius Haule Ligendayika

SIRI YA USHINDI WA MAPAMBANO YA AINA YEYOTE YA VITA YA KUDAI HAKI HULAZIMISHA KUWAINGIZA GHAFLA PASIPO KUJIJUA WAPAMBANA...
13/08/2023

SIRI YA USHINDI WA MAPAMBANO YA AINA YEYOTE YA VITA YA KUDAI HAKI HULAZIMISHA KUWAINGIZA GHAFLA PASIPO KUJIJUA WAPAMBANAJI WAKE WA KIVITA KUJIKUTA KWENYE MIKATABA YA VIAPO VYA SIRI VINAVYOWALAZIMISHA KUJIHUKUMU KIFO WENYEWE BILA RIDHAA YAO IKIWA K**A WATASALITI VIAPO VYAO VYA USHINDI WA VITA YA KUDAI HAKI.

K**a ilivyo urithi wa uchawi ambao urithi wake hupewa mtu bila yeye kujulishwa kuwa atakuwa mchawi lakini atatumbulishwa kwa matendo yake kuwa yeye ni mchawi baada ya hatari ya matendo yake kulazimika kuwa ya siri la sivyo akijulikana kwa matendo yake kutahatarisha kutoweka kwa uhai wake ndivyo inavyopaswa kurithishwa siri ya ushujaa wa upambanaji wa vita ya aina yeyote ya kudai haki.

Ikiwa k**a watanzania wanaona umuhimu wa kuhitaji kujikomboa kutoka kwenye serikali yao wanayoituhumu k**a ina ushahidi wa uwepo wa viongozi wezi, majambazi na wala rushwa ambao wanahatarisha usalama wa taifa, wanaangamiza uchumi wa taifa na kuuza nchi yao basi zoezi lao muhimu la kwanza ni kutambua namna ya kuwatofautisha raia wa haki na wasio wa haki ili wale wa haki wawatumbukizwe kwenye vita ya kudai haki bila tahadhari ya wao wenyewe kujijuwa kuwa wanatumbukizwa kwenye vita vya kudai haki ambayo ghafla wanawaingiza kwenye viapo vinavyopinga usaliti wao utakao walazimisha kujihukumu kifo wao wenyewe bila kupenda ikiwa k**a watasaliti viapo vyao.

Mfumo huu wa vita ya kudai haki kamwe hauwezi kushindwa kwa sababu wapiganaji wake wa kudai haki kamwe hawawezi kukata tamaa na kamwe hawawezi kutoa siri ya mapambano ya kivita. Mapambano ya kivita ya kudai haki kamwe hayawezi kuwa kwenye mfumo wa uwanaharakati wa kuuza sura za kujipatia umaarufu wa kisiasa ambao mara nyingi hauwezi kushinda vita za kudai haki kwa sababu unatoa siri za mbinu za mapambano na pia taarifa zake zisizo za siri kwa umma za namna ya kuendesha mapambano yake ya vita ya kudai haki husababisha kujulikana kwake kulazimika kuwekewa vikwazo dhidi ya ushindi wake wa vita hiyo.

Kwa wale walioelimika elimu ya ujasusi wanaelewa nini ninachoelimisha leo kwenye umma wa watanzania waliopo kwenye mitandao ya kijamii. Uwanaharakati wa vita ya kudai haki una idadi kubwa ya mashabiki wake ambao hawana uwezo wa kulikomboa taifa kutoka kwenye serikali ya wezi, majambazi na wala rushwa kwa sababu hawajaingizwa kwenye viapo vinavyowafunga wenyewe kwenye kujihukumu kifo wenyewe ikiwa k**a watasaliti viapo vyao wakiwa k**a viongozi au wafuasi au mashabiki.

Siasa za vita ya kudai haki nchini Tanzania zipo changa sana kwa sababu hazijaunda masharti ya viapo vya vifungo vya utekelezaji vinavyowawajibisha watekelezaji wake iwapo watasaliti viapo vyao. Je kiongozi gani hapa Tanzania alijiwajibishwa kujihukumu kifo chake mwenyewe kwa kosa la kusaliti viapo vyake vya vita ya kudai haki? Hivi mnanielewa kweli? K**a mnanielewa basi mnajua sababu ya nchi zingine zilizofanikiwa kupata utawala wa haki k**a vile China, Urusi, Korea ya Kasikazini na kungineko.

Mkiona wanasiasa wenye msimamo mkali k**a sisi tumekaa kimya mjuwe tupo kazini huku tukiwa kwenye viapo vya siri vinavyotulazimisha kujihukumu kifo sisi wenyewe ikiwa k**a tutasaliti viapo vyetu.

Ni mimi Doctor Claudius Haule Ligendayika wa Songea.

Address

Quarters Street Majengo
Songea

Telephone

+255757559876

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwanafalsafa Claudius HAULE Ligendayika posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mwanafalsafa Claudius HAULE Ligendayika:

Share