28/08/2026
Kiungo wa Uganda, Khalid Aucho, ametambulishwa akiwa ndani ya jezi ya Sidama Bunna FC ya Ethiopia baada ya kujiunga na klabu hiyo akitokea Singida Black Stars.
Aucho amesajiliwa kuongeza nguvu na uzoefu katika kikosi cha Sidama Bunna, hasa kutokana na klabu hiyo kushiriki kwa mara ya kwanza katika CAF Champions League.
Usajili huo unatarajiwa kuongeza uzoefu katika kikosi cha Sidama Bunna kuelekea changamoto za mashindano ya ndani na kimataifa.