Uyui FM Radio

Uyui FM Radio 99.3 Tabora | 96.1 Dodoma | 99.1 Manyara| 97.9 Shinyanga | 96.7 Simiyu | 98.1 Katavi | 103.7 Kigoma

Bofya link πŸ‘‡πŸΎ usikilize UFR popote ulipo Duniani.

Kali za kale kipindi kinachokupa nafasi ya kukumbuka miaka ya nyuma, ungana na Baraka Pius kuanzia saa kumi na nusu mpak...
05/09/2026

Kali za kale kipindi kinachokupa nafasi ya kukumbuka miaka ya nyuma, ungana na Baraka Pius kuanzia saa kumi na nusu mpaka saa kumi na mbili na nusu jioni.

πŸ“» Sikiliza Uyui FM Radio popote ulipo duniani, bofya kiungo (link) kwenye bio yetu.

Timu ya Taifa ya Wasichana U15 ya Tanzania imetwaa ubingwa wa CAF African Schools Football Championship, Kanda ya CECAFA...
05/09/2026

Timu ya Taifa ya Wasichana U15 ya Tanzania imetwaa ubingwa wa CAF African Schools Football Championship, Kanda ya CECAFA, baada ya kuifunga Kenya mabao 3-0 katika mchezo wa fainali.

Mabao ya Sarah Msagala, Eva Maiope na Anna Pascal yametosha kuipa Tanzania ushindi huo na kuiwezesha kutwaa taji la michuano hiyo ya shule za soka barani Afrika kwa ukanda wa CECAFA.

Naye, mshambuliaji wa Tanzania, Debora Salala, ametwaa tuzo ya Mchezaji Bora katika kitengo cha wasichana kwenye CAF African Schools Football Championship 2026, Kanda ya CECAFA.

πŸ“» Sikiliza Uyui FM Radio popote ulipo duniani, bofya kiungo (link) kwenye bio yetu.

05/09/2026

Mwigizaji na mtaalam wa masuala ya mapambo ya uso, Jafari Athumani, maarufu k**a JAFARI ATHUMANI , amesema hali ya sanaa haijadorora kwa sababu wasanii wa sasa hawana uwezo, bali changamoto kubwa ni baadhi yao kukosa fursa za kuonesha vipaji vyao.

Akizungumza kwa njia ya simu na UFR kupitia kipindi cha Maisha Mbashara, Jafari amesema mitandao ya kijamii imekuwa ikiwapa baadhi ya watu nafasi katika filamu kutokana na umaarufu wao, huku wasanii wenye vipaji na waliopitia mafunzo wakati mwingine wakikosa fursa ya kuonekana.

Amesema hali hiyo inapaswa kuwafanya wasanii chipukizi kuwekeza zaidi katika elimu ya uigizaji badala ya kutegemea kukariri maandishi pekee, akisisitiza kuwa mwigizaji mzuri anapaswa kuelewa na kuiishi hadithi iliyo kwenye maandishi.

Jafari amewashauri wasanii kusoma na kujifunza taaluma ya uigizaji ili kuongeza uwezo wao, akieleza kuwa mafunzo yanaweza kuwasaidia kuwasilisha wahusika kwa uhalisia zaidi na hatimaye kujenga tasnia ya sanaa yenye ushindani.

πŸ“» Sikiliza Uyui FM Radio popote ulipo duniani, bofya kiungo (link) kwenye bio yetu.

05/09/2026

Muhtasari wa Habari saa 10 jioni leo Septemba 05, 2026 kupitia UFR.

Msomaji: Samir Salum (Samir S. Salum πŸ‡΅πŸ‡Έ )

πŸ“» Sikiliza Uyui FM Radio popote ulipo duniani, bofya kiungo (link) kwenye bio yetu

Kipindi cha SAUTI YA MTAA kipo hewani muda huu na Butungo Andrew (Butungo). Piga kura yako kwa kutaja jina la msanii una...
05/09/2026

Kipindi cha SAUTI YA MTAA kipo hewani muda huu na Butungo Andrew (Butungo). Piga kura yako kwa kutaja jina la msanii unayemkubali zaidi, utasikika ujumbe wako utasikika mbashara hapa UFR.

πŸ“» Sikiliza Uyui FM Radio popote ulipo duniani, bofya kiungo (link) kwenye bio yetu.

05/09/2026

Baadhi ya vijana wamehimizwa kuacha tabia ya kuchagua kazi na badala yake kutumia fursa mbalimbali zilizopo katika kujiajiri, ikiwemo kilimo, ufugaji na shughuli nyingine za uzalishaji.

Akizungumza na UFR kupitia kipindi cha Konekti leo Septemba 5, 2026, Kocha wa Vijana wa Kujitegemea na Mtetezi wa Haki za Wanawake Mkoa wa Tabora, Steven Kimaro, amesema mfumo wa elimu umekuwa ukichangia kuwafanya vijana wengi kulenga ajira badala ya kuwa wabunifu na kuanzisha fursa za ajira.

Kimaro amesema changamoto nyingine ni baadhi ya vijana kutokuwa tayari kujifunza ujuzi mpya, huku akisisitiza kuwa mtaji si fedha pekee, bali maarifa, ujuzi na rasilimali walizonazo vinaweza kuwa msingi wa kuanzisha shughuli za kiuchumi.

Aidha, amewataka vijana kutumia fursa zinazopatikana kupitia mafunzo, ufadhili wa masomo, mikopo na miradi ya kilimo, huku akiwaonya dhidi ya kutegemea betting na forex k**a njia rahisi ya kutafuta utajiri.

πŸ“» Sikiliza Uyui FM Radio popote ulipo duniani, bofya kiungo (link) kwenye bio yetu.

05/09/2026

Habari kwa ufupi saa tano kamili asubuhi leo Septemba 05,2026 kupitia UFR.

Msemaji: Tamali Merikioli (Tamali Begwa )

πŸ“» Sikiliza Uyui FM Radio popote ulipo duniani, bofya kiungo (link) kwenye bio yetu.

KONTENA: M***a Nkoningo (M***a Nkoningo) Sheila Chambuso (chambuso_tz) pamoja SHAPPA THE BEAST πŸ‡ΉπŸ‡Ώ πŸ“» Sikiliza Uyui FM Rad...
05/09/2026

KONTENA: M***a Nkoningo (M***a Nkoningo) Sheila Chambuso (chambuso_tz) pamoja SHAPPA THE BEAST πŸ‡ΉπŸ‡Ώ

πŸ“» Sikiliza Uyui FM Radio popote ulipo duniani, bofya kiungo (link) kwenye bio yetu.

Habari Kuu kwenye magazeti ya leo Jumamosi Septemba 05, 2026.πŸ“» Sikiliza Uyui FM Radio popote ulipo duniani, bofya kiungo...
05/09/2026

Habari Kuu kwenye magazeti ya leo Jumamosi Septemba 05, 2026.

πŸ“» Sikiliza Uyui FM Radio popote ulipo duniani, bofya kiungo (link) kwenye bio yetu.

πŸ“°

Address

Majengo, Ipuli
Tabora
45107

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uyui FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Uyui FM Radio:

Shortcuts

Share