01/03/2024
.
βπ»Timu mbili ambazo kipindi cha kwanza kila mmoja alikuwa anaona njia sahihi ya kupita ni katikati ya uwanja na wote wawili wakafunga njia za ndani : Al Ahly bila mpira wakiwa 4-4-1-1 wakati Yanga bila mpira wanakuwa 4-1-4-1 , wote wakiwa compact sana na kukubali kuacha space pembeni tu .
βπ»Kipindi hiko hiko cha kwanza Al Ahly upande wao wa mashambulizi ni kushoto kwao : Maaloul na El Shahat wakati Yanga ilionekana sana nao upande wa kushoto Pacome na Lomalisa . Lakini kwanini kipindi cha kwanza njia zao hazikufanikiwa sana ?
1: Musonda alikuwa na kazi ya kurudi nyuma dhidi ya Maaloul ( mara chache sana alisinzia ) lakini mara nyingi alifanikiwa na ndio maana Al Ahly hawakutengeneza sana nafasi
2: Yanga wao licha ya Lomalisa kuwa na space upande wa kushoto shida walikuwa wanachelewa kushambulia kwa idadi kubwa ya wachezaji kwenye eneo la Al Ahly
βπ»Kipindi cha pili Al Ahly ndio walionekana kupata suluhisho zaidi jinsi gani ya kuifungua Yanga
1: Rotations ya fullbacks na wingers wao pembeni ya uwanja , kivipi na ilisaidia nini ?
2: Pale ambapo Maaloul ana overlap basi El Shahat anaingia ndani kwenye halfspace , na El Shahat akibaki pembeni basi Maaloul anafanya runs kwa ndani sawa sawa na upande wa Percy Tau na Tawfik .... faida yake ?
3: Moja , Kupata space katikati ya mstari wa ulinzi na kiungo wa Yanga , Mbili kuharibu muundo wa ulinzi wa Yanga kwenye eneo lao la pili ulinzi ( kiungo ) na tatu kutengeneza idadi ya wachezaji wengi pembeni ya uwanja ( overloads )
βπ»Nafikiri baada ya goli moja pale mechi ikabadilika ikawa k**a ya mpira wa kikapu , timu zote zikaacha spaces za kutosha katika mistari yao maana yake nani atakuwa mfanisi kutumia hizo spaces ?
NOTE
1: Diarra kuna saves anafanya zinaonekana nyepesi lakini positioning yake ni nzuri
2: Abdelmonem ni kitasa aisee , nguvu , kasi , akiwa na mali mguuni utulivu wa hali ya juu
3: Leo unaona kabisa kuna energy fulani ilikosekana kwa Al Ahly kwenye kiungo kwasababu ya Dieng kukosekan