13/05/2026
siku moja mvua ilikuwa inanyesha sana abiria wakiwa kwenye gari huku safari inaendelea ila kila mara ladi ilipiga mbele ya gari abiria waliogopa sana huku dereva ajui cha kufanya kila akienda mbele ladi inapiga tena walifika sehemu kuna mti mkubwa dereva akasema kila mmoja wetu atakuwa anashuka na kwenda kushika mti ule na kurudi kwenye gari!
abiria walianza mmoja mmoja anashuka anashika mti na kurudi kwenye gari ilipofikia zamu ya bibi mmoja aligoma kushusha kwenye gari lile kuwa yeye huwaamini ushirikina na yeye sio mshirikina abiria pamoja na dereva walimtukana sana yule bibi kuwa ni mchawi anaroga gari walimsukuma yule bibi mpaka nje na kufunga milango ya gari wanafunga tu mlango gari likawaka moto kumbe lile gari muda mrefu lingewaka ila nguvu ya imani ya bibi yule ndo ilikuwa inazuia lile jambo lisitokee