Njiwa Media

Njiwa Media Njiwa Media ni ukurasa unaomilikiwa na Kanisa la Moravian Tanzania-JK.

TANZIA.Katibu Mkuu wa Kanisa la Moravian Tanzania, Jimbo la Kusini, kwa niaba ya Halmashauri Kuu ya Jimbo, anatangaza kw...
03/08/2025

TANZIA.

Katibu Mkuu wa Kanisa la Moravian Tanzania, Jimbo la Kusini, kwa niaba ya Halmashauri Kuu ya Jimbo, anatangaza kwa masikitiko makubwa kifo cha mfanyakazi wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini, Ndugu Furaha Baraka Kamwela.

Ndugu Kamwela amefariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Marehemu alikuwa mfanyakazi wa Kanisa katika Idara ya Fedha KMT-JK na Mazishi yanatarajiwa kufanyika Iwambi, Mbeya, siku ya Jumanne tarehe 5 Agosti 2025.

"Mungu ampumzishe kwa amani. Amen."

Imetolewa na:
Mch. Stephen Mwaipopo
Katibu Mkuu – Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini

Njiwa Media tutaendelea kukuletea taarifa zaidi kuhusiana na msiba huu.

TANGAZO.
01/08/2025

TANGAZO.

31/07/2025

"Na wengine akina Mama mnacheka na Wanaume wengine barabarani huko, lakini Mume wako hucheki nae....." Baba Askofu Conrad S. Nguvumali.

30/07/2025

Jambo kubwa na lenye baraka tele kwako kutoka Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Ushirika wa Mahenge Kiwira.

SHIRIKI LEO ILI UVUNE BARAKA HIZI

30/07/2025

"Wengine mnatunza watoto wasio wenu, mnatunza watoto wa wanaume wenzenu kupitia hawara zenu...." - Baba Askofu Conrad S. Nguvumali.

29/07/2025

"Kuna Wababa wengine wako hapa hawajali familia zao, wanakula kitimoto na mishkaki barabarani lakini nyumbani wameacha chainizi na mchicha…." - Baba Askofu Nguvumali

TANZIA: MZEE DAUDI WALUGANO MWANJA AFARIKI DUNIANjiwa Media tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mzee Da...
26/07/2025

TANZIA: MZEE DAUDI WALUGANO MWANJA AFARIKI DUNIA

Njiwa Media tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mzee Daudi Walugano Mwanja, ambaye ni Baba Mkwe wa Askofu Kenan Salim Panja wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini (KMT-JK).

Mzee Daudi Mwanja hakuwa tu mkwe wa Baba Askofu Panja, bali pia ni mzazi wa Mchungaji George Mwanja anayehudumu katika Ushirika wa Katumba, Jimbo la Kusini.

Taarifa za awali kuhusu msiba huu zimetolewa na mmoja wa wanafamilia wa karibu, na kwa jitihada za kumpata Makamu Mwenyekiti KMT-JK, Mch. Jair Sengo zimefanyika, ambapo amethibitisha kutokea msiba huu na kwamba Ibada ya mazishi itafanyika siku ya Jumatatu 28/07/2025 huko Kijiji cha Ibungu Wilaya ya Ileje.

Njiwa Media inaendelea kufuatilia kwa karibu taarifa za msiba huu, na itakuwa ikikuletea habari zaidi kadri zitakavyopatikana.

Apumzike kwa Amani Mzee wetu Daudi Mwanja. Amina.

KANISA LA MORAVIAN TANZANIA JIMBO LA KUSINI LAMUAGA MCH. JOHANNES KLEMM KWA HESHIMA KUBWA.Rungwe, Tanzania.Kanisa la Mor...
22/07/2025

KANISA LA MORAVIAN TANZANIA JIMBO LA KUSINI LAMUAGA MCH. JOHANNES KLEMM KWA HESHIMA KUBWA.

Rungwe, Tanzania.
Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini limemuaga rasmi aliyekuwa Team Leader Africa na Program Manager Tanzania wa Shirika la Mission 21 lenye makao yake makuu nchini Uswisi, Mchungaji Johannes Klemm.

Hafla hiyo imefanyika katika viunga vya Butusyo Guest House, yaliyopo Makao Makuu ya Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini – Rungwe Mission, chini ya uratibu wa Kamati Tendaji ya Jimbo hilo.

Tukio hilo limehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya za Kanisa la Moravian Tanzania pamoja na wakuu wa Idara na Taasisi zake, ikiwa ni ishara ya kuthamini mchango mkubwa uliotolewa na Mch. Klemm katika kipindi chote alichohudumu nchini Tanzania.

Shirika la Mission 21 limekuwa mshirika muhimu wa maendeleo katika Jimbo la Kusini, likifadhiri miradi mbalimbali ya kijamii hususan katika sekta ya elimu na afya.

Wakizungumza katika hafla hiyo, viongozi wa Jimbo wamemshukuru Mch. Klemm kwa moyo wake wa kujitoa, ushirikiano wa karibu, na uongozi wenye maono. Wamesisitiza kuwa mchango wake utaendelea kudumu katika historia ya maendeleo ya Kanisa na jamii kwa ujumla.

Hafla hiyo pia imehudhuriwa na Mratibu wa Miradi ya Mission 21 nchini Tanzania, Bi. Adrianne Sweetman, pamoja na msaidizi wake, Ndugu Isaack Eliakimu.

Address

Rungwe Mission
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Njiwa Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Njiwa Media:

Share