Sport vibe

Sport vibe “Habari na burudani zote za michezo – matokeo, habari moto na stori kali kila siku!”

🦁🔥 RASMI: Simba Day 2025 yaja kwa kishindo!Klabu ya Simba SC imetangaza kuwa Sherehe za Simba Day 2025 zitafanyika Septe...
18/08/2025

🦁🔥 RASMI: Simba Day 2025 yaja kwa kishindo!

Klabu ya Simba SC imetangaza kuwa Sherehe za Simba Day 2025 zitafanyika Septemba 10, 2025 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Siku hii maalumu imekuwa sehemu ya utamaduni wa Wanasimba kila mwaka, ambapo mashabiki hukusanyika kushuhudia:
✨ Utambulisho wa wachezaji wapya kuelekea msimu mpya
✨ Burudani za wasanii wakubwa
✨ Mechi ya kirafiki ya kimataifa kwa heshima ya Simba Day
✨ Sherehe ya rangi nyekundu na nyeupe

Simba Day ni zaidi ya tamasha – ni utambulisho wa jeuri ya Msimbazi, na mwaka huu shangwe zinatarajiwa kuwa kubwa zaidi!

📍 Tarehe: 10/09/2025
📍 Mahali: Benjamin Mkapa Stadium, DSM

🇿🇦 Bafana Bafana nje ya CHAN 2024! 🇿🇦Timu ya Taifa ya Afrika Kusini imetolewa nje ya michuano ya Kombe la Mataifa Afrika...
18/08/2025

🇿🇦 Bafana Bafana nje ya CHAN 2024! 🇿🇦

Timu ya Taifa ya Afrika Kusini imetolewa nje ya michuano ya Kombe la Mataifa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN 2024) baada ya kulazimishwa sare ya kusisimua 3-3 na Uganda The Cranes katika uwanja wa Mandela, Kampala.

Uganda ilimaliza kileleni mwa Kundi C kwa alama 7 baada ya mechi 4, ikifuatwa na Algeria waliomaliza na pointi 6. Timu hizi mbili ndizo zimefuzu hatua ya robo fainali, huku Afrika Kusini na Niger wakibaki nje ya mashindano.

🔹 Matokeo ya jana:
🇺🇬 Uganda 3-3 Afrika Kusini 🇿🇦
⚽ 31’ Ssemugabi
⚽ 88’ Okello (P)
⚽ 90+6’ Torach (P)
⚽ 52’ Mphahlele
⚽ 58’ Kutumela
⚽ 83’ Ndilondlo

🇩🇿 Algeria 0-0 Niger 🇳🇪

📊 Msimamo wa Kundi C (Mechi 4):
1️⃣ Uganda – 7pts
2️⃣ Algeria – 6pts
3️⃣ Afrika Kusini – 5pts
4️⃣ Niger – 2pts

Uganda na Algeria sasa zinaelekea robo fainali, wakati Bafana Bafana wanalazimika kuondoka mapema.

Ameandika AHMED ALLY"Ni wakati sahihi mimi kuingilia kati sakata la Sheikh Walid, kuhakikisha kijana anaenda kutimiza nd...
11/08/2025

Ameandika AHMED ALLY

"Ni wakati sahihi mimi kuingilia kati sakata la Sheikh Walid, kuhakikisha kijana anaenda kutimiza ndoto yake ya kucheza Nje ya Nchi.

Naingilia kati kuhakikisha kijana anauzwa kwa thamani yake halisi na sio Bei za kukurupuka ili kukwamisha Biashara makusudi

Haiwezekani kila mchezaji akitaka kuondoka kwenu ianze vita, Kwa Mayele tulijua bahati mbaya kwa Feisali tukasema haitojirudia tena na sasa kwa Walid hii haikubaliki

Kuzuia mtu asitimize malengo yake ni unyonyaji na unapotaja Bei isiyoendana na uhalisia ni lugha iliyojificha ya kumwambia mtu siuzii bidhaa hii

Hili siwezi kulifumbia macho, Tulimnusuru Mayele, tukamkomboa Fei na sasa ni zamu ya Walid

Kwako Walid wewe endelea kuipigania Tanzania, sisi tutapambana nao na mwisho wa siku tutakukabidhi ushindi Insha Allah"

🚨 Droo ya hatua ya awali (preliminary round) ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa msimu wa 2025/26 imekamilika ambapo wawakili...
09/08/2025

🚨 Droo ya hatua ya awali (preliminary round) ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa msimu wa 2025/26 imekamilika ambapo wawakilishi wa Tanzania kwenye CAFCL, Simba Sc, Yanga Sc na Mlandege Fc wamebaini wapinzani wao kwenye ‘CAFCL Preliminary round’

Mabingwa wa Ligi Kuu bara Yanga Sc wamepangwa dhidi ya vigogo wa Angola, Wiliete Benguela Sc huku watani zao Simba Sc wakikutanishwa na wababe wa Botswana, Gaborone United wakati Mlandege Fc ikipewa Ethiopia Insurance ya Nchini Ethiopia.

Eth. Insurance 🇪🇹 🆚 Mlandege (Znz)
Gaborone Utd 🇧🇼 🆚 🇹🇿 Simba Sc
Wiliete Benguela 🇦🇴 🆚 🇹🇿 Yanga Sc

Droo ya Kombe la Shirikisho barani AfricaEl Merriekh Bentiu 🇸🇸 vs 🇹🇿Azam FcRayon Sports 🇬🇦vs 🇹🇿Singida Black starsAs Por...
09/08/2025

Droo ya Kombe la Shirikisho barani Africa

El Merriekh Bentiu 🇸🇸 vs 🇹🇿Azam Fc

Rayon Sports 🇬🇦vs 🇹🇿Singida Black stars

As Port🇩🇯 vs KMKM( znz)

Unazani timu za Tanzania zinaweza kutoboa ?

🚨 Klabu ya Manchester United imethibitisha kumsajili mshambuliaji Benjamin Šeško kwa ada ya uhamisho ya jumla ya pauni m...
09/08/2025

🚨 Klabu ya Manchester United imethibitisha kumsajili mshambuliaji Benjamin Šeško kwa ada ya uhamisho ya jumla ya pauni milioni 73.67 pamoja na nyongeza akitokea RB Leipzig ya Ujerumani.

Šeško 22, raia wa Slovenia amesaini mkataba wa miaka mitano utakaombakisha klabuni hapo mpaka Juni 2030.

🚨: Klabu ya Azam Fc imemtambulisha Anicet Kiazayidi 🇨🇩 kuwa kocha msaidizi wa kikosi hicho chini na Ibenge
09/08/2025

🚨: Klabu ya Azam Fc imemtambulisha Anicet Kiazayidi 🇨🇩 kuwa kocha msaidizi wa kikosi hicho chini na Ibenge

"Klabu bingwa Ulaya inaweza kuwa michuano migumu lakini niamini mimi, Chelsea wana kila sifa inayowafanya waweze kuwa ma...
09/08/2025

"Klabu bingwa Ulaya inaweza kuwa michuano migumu lakini niamini mimi, Chelsea wana kila sifa inayowafanya waweze kuwa mabingwa. Baada ya kubeba FIFA Club World Cup, ile hali ya ushindi ipo ndani ya DNA zao na huo ujasiri wanaweza kwenda nao mpaka kuwa mabingwa."

🗣 Jose Mourinho

Dakika ya 22' Chelsea wapo mbele goli moja dhidi ya Bayern Leverkusen goli limefungwa na Estevao ukipenda muite Messinho
08/08/2025

Dakika ya 22' Chelsea wapo mbele goli moja dhidi ya Bayern Leverkusen goli limefungwa na Estevao ukipenda muite Messinho

Kikosi cha Chelsea kinachoanza dhidi ya Bayern Leverkusen
08/08/2025

Kikosi cha Chelsea kinachoanza dhidi ya Bayern Leverkusen

🚨: Huwenda klabu ya Azam Fc inaweza kumtambulisha muda wowote kuanzia sasa Anicet Kiazmak 🇨🇩 kuwa kocha msahidizi wa kik...
08/08/2025

🚨: Huwenda klabu ya Azam Fc inaweza kumtambulisha muda wowote kuanzia sasa Anicet Kiazmak 🇨🇩 kuwa kocha msahidizi wa kikosi hicho chini ya mwamba Florentine Ibenge.

Mazungumzo kati ya Azam Fc na Kocha Anicet kiazmak yamefikia sehemu nzuri kuna nafasi kubwa ya kocha huyo wa zamani wa klabu ya Tabora United akajiunga na azam fc kuelekea msimu ujao.

🚨 klabu ya Police FC ya Rwanda imethibitisha kukamilisha usajili wa mshambuliaji Emmanuel Okwi Kwa mkataba wa miaka miwi...
08/08/2025

🚨 klabu ya Police FC ya Rwanda imethibitisha kukamilisha usajili wa mshambuliaji Emmanuel Okwi Kwa mkataba wa miaka miwili.

Address

Bima

Telephone

+255763605771

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sport vibe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sport vibe:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share