Sport vibe

Sport vibe “Habari na burudani zote za michezo – matokeo, habari moto na stori kali kila siku!”

Kikosi cha pamba jiji kinachoanza dhidi ya Yanga
24/09/2025

Kikosi cha pamba jiji kinachoanza dhidi ya Yanga

Kikosi cha Yanga kinachoanza dhidi ya Pamba Jiji🔰💪🏽
24/09/2025

Kikosi cha Yanga kinachoanza dhidi ya Pamba Jiji🔰💪🏽

🚨Siku hii ya Leo Klabu ya Young Africans Sports Club imekabidhiwa Kiasi cha Tzs Mil 15 k**a sehemu ya ahadi iliyotolewa ...
22/09/2025

🚨Siku hii ya Leo Klabu ya Young Africans Sports Club imekabidhiwa Kiasi cha Tzs Mil 15 k**a sehemu ya ahadi iliyotolewa na Raisi Samia (goal la mama) kwa timu zote zinazoshiliki mashindano ya Kimataifa.

Yanga SC imepokea kiasi hicho mala baada ya kumchakaza Willets bao 3.

FOLLOW US 🙏🏻

Picha ni baadhi ya wachezaji wa Fc Barcelona wakiwa wameanza safari ya kuelekea Paris 🇫🇷 kwaajili ya tuzo za Ballon D'or...
22/09/2025

Picha ni baadhi ya wachezaji wa Fc Barcelona wakiwa wameanza safari ya kuelekea Paris 🇫🇷 kwaajili ya tuzo za Ballon D'or zitakazofanyika usiku wa leo Septemba 22, 2025.

🚨Selemani Matola 'Veron' anataraji kuiongoza Club ya Simba SC kwenye Mchezo dhidi ya Fountain Gate utakaochezwa alhamis ...
22/09/2025

🚨Selemani Matola 'Veron' anataraji kuiongoza Club ya Simba SC kwenye Mchezo dhidi ya Fountain Gate utakaochezwa alhamis tarehe 25 Sept 2025 kwenye dimba la Benjamin Mkapa.

☑Selemani Matola ataanza maandalizi kesho jumanne kukinoa kikosi hicho kwenye mazoezi kuelekea kwenye mechi yao ya kwanza kwenye ligi ya NBC PL.

FOLLOW US 🙏🏻

RASMI: Simba Sc imethibitisha kuwa itautumia uwanja wa Benjamin Mkapa 🏟️ katika mechi zao za nyumbani za NBC PL.FOLLOW U...
22/09/2025

RASMI: Simba Sc imethibitisha kuwa itautumia uwanja wa Benjamin Mkapa 🏟️ katika mechi zao za nyumbani za NBC PL.

FOLLOW US

Kocha Mkuu wa Simba SC, Fadlu Davids, ametangaza kuachana na klabu hiyo kuelekea msimu ujao kupitia ukurasa wake rasmi w...
22/09/2025

Kocha Mkuu wa Simba SC, Fadlu Davids, ametangaza kuachana na klabu hiyo kuelekea msimu ujao kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram.

Katika ujumbe wake wa kuaga, Davids amesema:

🗣️ “Ni kwa moyo mzito naiaga Simba SC. Tangu nilipowasili, nilihisi shauku ya klabu hii kubwa na upendo wa mashabiki wake wa ajabu. Pamoja tulipigana, tukasherehekea, na tukaimarika kupitia kila ushindi na kila changamoto. Shukrani zangu za dhati kwa Rais Mo Dewji kwa uongozi wake wa kutia moyo, maono, na msaada wake wa kila mara.”

Kocha huyo pia aliwashukuru wachezaji, benchi la ufundi na mashabiki wa Simba SC kwa mshik**ano na mapokezi makubwa aliyoyapata, akisisitiza kuwa klabu hiyo itaendelea kubaki sehemu ya maisha yake:

🗣️ “Kwa wachezaji: endelea kupigana, kuamini na kuilinda beji kwa heshima. Kwa mashabiki: ninyi ndio mapigo ya moyo wa klabu hii, nyimbo zenu na shauku yenu zitasikika daima katika kumbukumbu yangu. Simba itabaki sehemu yangu siku zote. Asanteni sana, forever Nguvu Moja.” ❤️🦁

FOLLOW US🙏🏻.

🚨BREAKING  Lamine Yammal siku ya Leo anatarajiwa kuondoka Spain na kusafiri kwenda nchini Ufaransa 🇨🇵 Kwa ajili ya kuhud...
21/09/2025

🚨BREAKING

Lamine Yammal siku ya Leo anatarajiwa kuondoka Spain na kusafiri kwenda nchini Ufaransa 🇨🇵 Kwa ajili ya kuhudhuria usiku wa tuzo za Ballon d'Or ambayo itafanyika tarehe 22 Sept 2025(kesho).

Tuzo hiyo kubwa kwa wachezaji soka duniani inataraji kutolewa na Mchezaji wa Manchester City Rodri ambaye ndiye mshindi wa mwisho kuchukuwa, akiwa amechukuwa mwaka jana 2024.

Je unaiyona nafasi ya Dogo Lamine Yamal kuondoka na Ballon d'Or ?

FOLLOW PAGE YETU KWA HABARI ZA MICHEZO 🔥

🚨 Breaking News Kwa mujibu wa Micky jr ameripoti kuwa Kocha Fadlu Davids ameondoka Simba SC na kujiunga na Raja  Casabla...
21/09/2025

🚨 Breaking News

Kwa mujibu wa Micky jr ameripoti kuwa Kocha Fadlu Davids ameondoka Simba SC na kujiunga na Raja Casablanca ya Morocco.

Mchezo wa jana wa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Gaborone United ndio ulikuwa wa mwisho kwake akiwa kocha mkuu.

Fadlu, ambaye ameheshimika ndani na nje ya klabu, ameamua kuachana na timu baada ya mambo fulani kutokwenda k**a ilivyopangwa.

Hakusafiri kurejea na kikosi kutoka Botswana, badala yake alielekea Johannesburg kujiandaa na changamoto mpya.

Anaondoka pamoja na makocha wake wanne wa benchi la ufundi msaidizi wake wa kwanza, kocha wa makipa, mchambuzi na mtaalamu wa mazoezi ya mwili (biokineticist).

Kwa sasa, Matola pamoja na Riedoh Berdien ndio watakaokiongoza kikosi cha Simba kuelekea mchezo ujao wa Ligi Kuu dhidi ya Fountain Gate.

TRA UNITED KUBAKI TABORA: Serikali imewathibitishia mashabiki wa soka mkoani Tabora kwamba timu ya TRA United SC (Tabora...
20/09/2025

TRA UNITED KUBAKI TABORA: Serikali imewathibitishia mashabiki wa soka mkoani Tabora kwamba timu ya TRA United SC (Tabora United) haitohama katika mkoa huo k**a tetesi zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Meneja Elimu kwa mlipa kodi, Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, SPA Paul John Walalasi amethibitisha hilo mbele ya k**ati ya usimamizi wa ushindi wa TRA United, katika kikao kilichofanyika ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Tabora.

Amesema TRA imeinunua timu hiyo kutoka kwa wamiliki ikiwa ni sehemu ya kutekeleza malengo iliyokuwa imejiwekea kwamba msimu huu mpya wa ligi 2025/26 TRA iwe na timu ya NBC Premier League.

SPA Walalasi ametamba timu hiyo ya TRA United italeta ushindani mkubwa kwenye ligi msimu huu.

Katibu Tawala mkoa wa Tabora Dkt. John Mboya amesema timu hiyo itaendeshwa kwa ufanisi mkubwa kwa kuwa ipo chini ya Taasisi ya serikali, hivyo mashabiki wanapaswa kuipa ushirikiano ili ipate ushindi.

"Mnyama kafa mara 6 mfululizo, walichofanikiwa leo ni walau kuonyesha wamefungwa lakini Yanga hawakuwa so dominant, ving...
16/09/2025

"Mnyama kafa mara 6 mfululizo, walichofanikiwa leo ni walau kuonyesha wamefungwa lakini Yanga hawakuwa so dominant, vinginevyo wana safari ndefu dhidi ya Yanga na hawa akina KANTE wao, labda wapate wakina DE.REUICK 5 ndo watawafunga Yanga.

Bado Yanga ni imara mbele ya Simba hata k**a siku hiyo hawakutawala mchezo ila wanauwezo wa kushinda, maana yake bado Yanga watatawala ligi tena na ile ahadi ya ubingwa mara 10 mfululizo ISIDHARAULIKE.

Mohamed Mkono Mwamuzi msaidizi namba 1 wa mchezo wa leo ambaye ni FIFA referee AMEWAUA Simba, ile ni OFFSIDE kabisa, hakupaswa kuruhusu lile bao. Pacome alikuwa offside position akaja kufanya obstruction kwa De.REUICK ambaye alikuwa anamkimbiza Max, Kisha akaukuta mpira akafunga, kufanya obstruction ukitoka kwenye offside position ni KOSA na Mkono anajua hilo.

Anaandika Jemedar Saidi BİN KAZUMARI MTIPA.

MAPUMZIKO |  SIMBA SC 0-0 YANGA SC
16/09/2025

MAPUMZIKO |

SIMBA SC 0-0 YANGA SC

Address

Bima

Telephone

+255763605771

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sport vibe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sport vibe:

  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share