MAWIO TZ

MAWIO TZ Karibu katika ukurasa huu maalumu wa MAWIO TZ, unaokuhabarisha Taarifa/Habari na Makala mbalimbali ndani na nje ya Tanzania 🇹🇿

Chama Cha wananchi CUF kimezindua ilani ya uchaguzi ndani ya wilaya ya MOROGORO Mjini kwaajili ya kueleza changamoto na ...
12/08/2025

Chama Cha wananchi CUF kimezindua ilani ya uchaguzi ndani ya wilaya ya MOROGORO Mjini kwaajili ya kueleza changamoto na utekelezaji wa majukumu yao wanayopaswa kuyatekeleza huku wakitangaza majina ya wagombea kwa nafasi ya ubunge ngazi ya majimbo na udiwani ngazi ya kata.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Cuf zilizopo manispaa ya Morogoro mwenyekiti wa CUF wilaya ya MOROGORO Rashid Athuman amesema ilani hiyo imebebba zaidi ya mambo 16 yanayopaswa kutekelezwa kiutawala endapo watapata ridhaa ya kuongoza kutoka kwa wananchi.

“Ilani yetu imejikita zaidi katika mambo makuu 16 lakini kwa ucahhche k**a ajira,miundombinu,afya,elimu uwajibikaji nidhamu katika mamlaka za umma na ulinzi na usalama leo naona idadi ya vijana morogoro katika ajira imekuwa ni changamoto kubwa kwahiyo sisi k**a chama cha siasa tumekuja na tiba jinsi gani tunaweza kutatua kero za wananchi katika masuala hayo ya afya,ajira na miundombinu mana barabara zetu zimekuwa mbovu ,lakini ilani yetu imejikita ni namna gani tutafufua viwanda kwenye mji wetu wa Morogoro, tukichukua dhamana hiyo tutafufua viwanda vyote lakini kipaumbele chetu kingine ni kuweka bandari kavu”Amesema

Aidha mwenyekiti wa chama hicho ametumia nafasi hiyo kutangaza majina ya wagombea waliopitishwa na baraza la CUF mkutano mkuu Taifa katika majimbo 6 kwa nafasi za ubunge kwa jimbo la Ulanga,Malinyi,Kilosa,Kilombero,Morogoro Kusini na Morogoro mjini ambapo katika majimbo hayo wawili ni wanawake na 4 ni wanaume huku wakisimamisha wagombea 19 ngazi ya udiwani kati ya kata 29.
Wagombea hao ni Rashid Athumani Gogomelo kwa jimbo la Morogoro mjini ,jimbo la kilosa ni Sailasi Ramadhani Kasaaro ,kilombero Geogre Cosmas Mwaduha,Ulanga ni Dkt Batuli Salehe ,Morogoro kusini hossein Kiva na Malinyi ni Mwajuma

Nae mkurugenzi wa mipango na uchaguzi wilaya ya Morogoro mjini Nasibu Salum Mbogoya amesema wamejiandaa vema kushiriki katika uchaguzi mkuu na wametoa nafasi kwa makundi ya wanawake na vijana kuweza kugombea nafasi mbalimbali.
“Tumejaribu kugusa makundi mbalimbali katika kuandaa wagombea hususani tumegusa makundi ya wananwake

Maelfu Wamlilia Chifu TEDY MWAKAGHILE MWAIKONDELA Watu wengi kutoka sehemu mbalimbali za Kata ya Kambasegela, na Kata za...
10/08/2025

Maelfu Wamlilia Chifu TEDY MWAKAGHILE MWAIKONDELA

Watu wengi kutoka sehemu mbalimbali za Kata ya Kambasegela, na Kata za Jirani ndani ya Halmashauri ya Busokelo, Rungwe Mkoa wa Mbeya wamehudhuria Katika Msiba wa Chifu wa Wanyakusya katik Eneo la Utawala wake la Kambasegela.

Chifu Mkuu wa Unyakyusa Ndugu JOEL MWAKATUMBULA, Serikali pamoja na Wanachi wa kawaida wamejawa na Majonzi na huzuni kubwa baada ya Kifo cha Chifu huyo, ambaye kwa mujibu wa Jamii aliyokua anaiongoza imedai alikua Muhimili Mkubwa katika Jamii na Daraja muhimu kwa Serikali na Wananchi

Aidha Chifu Mkuu wa Unyakyusa Ameeleza Taratibu zilizopo za Namna Mazishi ya Chifu hufanyika akieleza Sababu za kufanya Kuzika Usiku na Si Mchana k**a ilivyo desturi kwa Watu wengine .

Taarifa Kamili Tumekuwekea YouTube kwenye Channel yetu ya

Matokeo ya Kura za Maoni Jimbo la Rungwe
05/08/2025

Matokeo ya Kura za Maoni Jimbo la Rungwe

Mchakato wa Wagombea Ubunge kutafuta Uungwaji na wajumbe ili Kuchaguliwa kuipeperusha Bendara ya CCM ngazi ya Ubunge wa ...
02/08/2025

Mchakato wa Wagombea Ubunge kutafuta Uungwaji na wajumbe ili Kuchaguliwa kuipeperusha Bendara ya CCM ngazi ya Ubunge wa Busokelo Unaendelea

Pichani ni REHEMA ULIMBOKA akiwaomba Kura wajumbe wa Kata ya Lupata.

Mchakato wa kura za maoni kuwapata wagombea ubunge viti maalumu kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoani Morogoro...
02/08/2025

Mchakato wa kura za maoni kuwapata wagombea ubunge viti maalumu kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoani Morogoro umemalizika, huku wawili kati ya tisa wakiibuka na ushindi
Wawili hao ni Lucy Damas Kombani ambaye ameongoza kwa kupata kura 1,314 kati ya kura halali 1,646 zilizopigwa, akifuatiwa na Sheila Edward Lukuba aliyepata kura 597.

Mkutano huo maalumu wa kura za maoni,umefanyika katika Uwanja wa Jamhuri Morogoro ambapo umehudhuriwa na wajumbe 1,653 kati ya 1,790 kutoka wilaya 8 za kichama kwa mkoa huo, ambapo kura 6 zimeharibika na kufanya kura halali kuwa 1,646.

Akitangaza matokeo ya kura za maoni zilizopigwa na wajumbe hao, Msimamizi wa uchaguzi huo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima amesema zoezi hilo limehusisha wagombea tisa akiwemo Josephine Kupuna aliyepata kura 454, Jane Claude Mihanji 339, Aliyah Awadh Omar 236, Amina Ally Karuma 153, Hajira Said Mwikoko 90, Kulwa Nuhu Kangeta 75 na Rahel Mashishanga 37.

“Niwapongeze wajumbe kwa hatua hii nzuri tuliyofikia baada ya hapa majina yanaenda ngazi za juu kwaajili ya taratibu za mwisho kwa mujibu wa taratibu za chama chetu cha Mapinduzi,” amesema Malima.

Hata hivyo mshindi wa Kura za maoni Lucy Damas Kombani amewashukuru wasimamizi kwa kusimamia upigaji kura wajumbe wote kupiga kura kwa uhuru na haki, huku akiahidi kuunga mkono mipango ya Serikali kwa maslahi mapana ya Watanzania na Taifa kwa ujumla.

Watatu Wateuliwa na CCM kuwa Wagombea na Rasmi Kuipeerusha Bendera ya CCM ngazi ya Ubunge  katika Majimbo yao bila Kupin...
29/07/2025

Watatu Wateuliwa na CCM kuwa Wagombea na Rasmi Kuipeerusha Bendera ya CCM ngazi ya Ubunge katika Majimbo yao bila Kupingwa, na Kufanya kuwa ndio Majimbo Pekee ambayo yamekuwa na Wagombea Wachache zaidi kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025

Wagombea hao ni:

Jimbo la Bukombe 1 - Dotto Mashaka Biteko
Jimbo la Mchinga 1 - Salma Rashid kikwete
Jimbo la Chalinze 1 - Ridhiwani Jakaya Kikwete

Pamoja na Majimbo hayo, Jimbo la Makambako nalo limeingia kwenye Orodha ya kuwa na Wagombea Wachache albapo ni Wagombea wawili tu, bao ni Daniel Chongolo na Deo Sanga

CCM yawateua 10 Kuchuana Ubunge Jimbo la Kongwa Dodoma.Wateule hao ni:(1) Ndugu Yustino NDUGAI(2) Ndugu Balozi. Emmanuel...
29/07/2025

CCM yawateua 10 Kuchuana Ubunge Jimbo la Kongwa Dodoma.

Wateule hao ni:
(1) Ndugu Yustino NDUGAI
(2) Ndugu Balozi. Emmanuel David Mwaluko Luhembe MBENNAH
(3) Ndugu Ngaya David MAZANDA
(4) Ndugu Deus Gracewell SEIF
(5) Ndugu Philip Eliud CHIWANGA
(6) Ndugu Paschal Joseph MAHINYILA
(7) Ndugu Dkt. Simon Saulo NGATUNGA
(8) Ndugu Dkt. Samora Stanley MSHANG’A
(9) Ndugu Isaya Mngurumi MOSES
(10) Ndugu Elias John MDAO

Sambba na hilo yafuatayo ni Majimbo yenye Wagombea zaidi ya 8 (
Majimbo 14):

Ilemela 9
Arumeru mashariki 8
Temeke 8
Kibamba 8
Kawe 8
Kinondoni 8
Dodoma mjini 8
Mwanga 8
Kilombero 8
Morogoro kusini 8
Mvomero 8
Itwangi 8
Bukene 8
Lushoto 8
Kiembe samaki 8
Handeni vijijini 8
Dimani 8
Kiembe samaki 8

Wabunge 7 wa awamu iliyoishia mwaka huu 2025, Majina yao yamekatwa na hawatakua Miongoni mwa wale  watakaochuana Kusaka ...
29/07/2025

Wabunge 7 wa awamu iliyoishia mwaka huu 2025, Majina yao yamekatwa na hawatakua Miongoni mwa wale watakaochuana Kusaka Kura ya Maoni ili Kuipeerusha Bendera ya CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 katika Majimbo yao.

Na hawa ndio VIGOGO WA CCM WALIOACHWA KWENYE MCHUJO huo:

1: Luhaga Mpina - Jimbo la kisesa
2: January Makamba - Jimbo la Bumbuli
3: Josephat Gwajima - Jimbo la Kawe
4: Mrisho Gambo - Jimbo la Arusha Mjini
5: Christopher Olesendeka- Simanjiro
6: Anjelina Mabula - Ilemela
7: Seif Gulamali- Manonga

Na Wengine waliokatwa ni:

Pauline Gekul- Babati Mjini.
Lengai Olesabaya - Arumeru Magharibi
Stephen Byabato - Bukoba Mjini

Wagombea watano Kuchuana ndani ya CCM Kumpata Mgombea Mmoja atakaye peperusha Bendera ya CCM Jimbo la Busokelo kwenye Uc...
29/07/2025

Wagombea watano Kuchuana ndani ya CCM Kumpata Mgombea Mmoja atakaye peperusha Bendera ya CCM Jimbo la Busokelo kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025

Mkuu wa wilaya ya Kusini Unguja Othman Masudi amesisitiza kuendelea kudumisha na kuilinda tunu ya muungano ilioachwa na ...
26/07/2025

Mkuu wa wilaya ya Kusini Unguja Othman Masudi amesisitiza kuendelea kudumisha na kuilinda tunu ya muungano ilioachwa na waasisi wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Aman Karume pamoja na kuendelea kuimarisha amani na utulivu kuelekea uchaguzi mkuu.

Ameyasema hayo katika mapokezi ya Jukwaa la walimu wazalendo kutoka mikoa 7 ya Tanzania bara waliowasili visiwani Zanzibar kwa ziara ya kikazi ya siku 3 itakayoangazia kubadilishana uzoefu,kutembelea maeneo ya kihistoria pamoja na miradi ya kimkakati inayotekelezwa na serikali chini ya Dr.Hussein Ally Mwinyi.
Aidha ameongeza kuwa Zanzibar katika sekta ya utalii inachangia pato la serikali kwa asilimia 30 kupitia utalii wa ndani hivyo kufanyika kwa ziara hiyo ni ishara ya muamko wa kufanya utalii wa ndani bila ya kutegemea wageni.

Hata hivyo katibu mtendaji wa taasisi ya Vijana nguvukazi kutoka kizimkazi Abuusuphian Yakuti Juma pamoja na mratibu wa jukwaa la walimu wazalendo kutoka Morogoro Mwl Kassimu Mandwanga wamesema ziara hiyo ina lengo la kuendeleza mahusiano mazuri yaliyopo baina ya walimu kutoka mikoa ya Tanzania bara na Zanzibar,kukuza utalii, kudumisha muungano na kuhamasisha dhana ya kushiriki uchaguzi.
Katika ziara hiyo ya Muungano kupitia Jukwaa la walimu wazalendo wanatarajia kutembelea maeneo mbalimbali ya kihistoria katika mikoa ya Mjini Unguja,Kaskazini Unguja na Kusini Unguja,kuzuru kaburi la hayati Ally Hassan Mwinyi,mradi wa bandari,na kutembelea maeneo ya kasa.

Walimu hao ni kutoka mikoa ya Morogoro,Tanga,Pwani,Dar es salaam,Shinyanga,Mbeya na Kigoma ambapo wametembelea Zanzibar kwa mualiko rasmi wa Taasisi ya Vijana nguvu kutoka Kizimkazi mkoa wa Kusini Unguja.

Address


Telephone

+255676506998

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MAWIO TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MAWIO TZ:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share