JamiiTalk

JamiiTalk Media Ya Habari kwa Kiswahili

Shirika la Umeme nchini (TANESCO) limetoa taarifa ya kuwepo kwa hitilafu ya dharura katika sehemu ya mfumo wa Gridi ya T...
19/04/2026

Shirika la Umeme nchini (TANESCO) limetoa taarifa ya kuwepo kwa hitilafu ya dharura katika sehemu ya mfumo wa Gridi ya Taifa, hali iliyosababisha kukatika kwa huduma ya umeme katika baadhi ya Mikoa nchini.

Mikoa iliyoathirika ni pamoja na Dodoma, Njombe, Mbeya, Simiyu, Ruvuma, Geita, Shinyanga, Mara, Mwanza, Tabora, Songwe, Kilimanjaro, Arusha, Iringa pamoja na maeneo ya jirani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma TANESCO, hitilafu hiyo imetokea saa 11:38 jioni na kusababisha kukosekana kwa umeme katika maeneo hayo kwa muda.

Aidha shirika hilo limeomba radhi kwa usumbufu uliosababishwa na kukatika kwa umeme na linawaomba wateja kuwa wavumilivu wakati jitihada za kurejesha huduma hiyo zikiendelea.

JamiiTalk Inakutakia Sikukuu njema ya Pasaka (Happy Easter)
05/04/2026

JamiiTalk Inakutakia Sikukuu njema ya Pasaka (Happy Easter)

JamiiTalk Celebrating 4 years of success
22/03/2026

JamiiTalk Celebrating 4 years of success

15/03/2026

Discover. Connect. Grow
This is more than a network, this is your digital community. Join JamiiTalk today.

Happy International Women's Day (IWD)
08/03/2026

Happy International Women's Day (IWD)

Mambo machache kuhusu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.1. Jina lake halisi ni nani? Kuna watu wanadhani Mwadhama ni jin...
22/02/2026

Mambo machache kuhusu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.

1. Jina lake halisi ni nani? Kuna watu wanadhani Mwadhama ni jina lake? Wengine wanadhani Polycarp ni cheo chake. Jina lake ni Polycarp Pengo. Kardinali ni cheo cha Kanisa, na Mwadhama ni kivumishi cha sifa, k**a ambavyo Maaskofu huitwa Mhashamu au Mbunge kuitwa Mheshimiwa.

2. Kwanini neno Kardinali lipo katikati ya majina yake na sio mwanzoni? Kwanini hakuitwa Kardinali Polycarp Pengo, akaitwa Polycarp Kardinali Pengo? Kanisa Katoliki lina utaratibu wa majina. Utaratibu huo huitwa modus titulorum ama style of titulature kwa kingereza. Kwa Makardinali wote, neno Kardinali hukaa katikati ya majina yao. Ndiyo maana Kardinali mpya anaitwa Protase Kardinali Rugambwa. Hata Papa Leo XIV kabla ya kuwa Papa aliitwa Robert Kardinali Prevost.

3. Kardinali Pengo ni miongoni mwa Maaskofu wachache kutoka Tanzania waliowekwa wakfu na Papa mwenyewe. Alipoteuliwa kuwa Askofu wa Nachingwea, aliitwa Vatican na kuwekwa wakfu na Papa John Paul II January 6, mwaka 1984 katika Basilika Kuu la Mtakatifu Petro.

4. Watu wengi wanashangaa kumbe Pengo alikuwa msomi wa kiwango cha PhD? Mbona alikuwa hajiiti Dr? Jibu ni kwamba katika Kanisa Katoliki, vyeo vya kitaaluma havipewi kipaumbele kuliko vyeo vya kiroho. Kuna doctrine ya unyenyekevu (humility) ambayo inasisitiza watawa wasijikweze kwa vyeo vya kisomi, bali wajitambulishe kwa nafasi zao za kiroho (Askofu, Kardinali, Padre etc).

Kardinali Pengo alikuwa na PhD ya Moral Theology kutoka Chuo Kikuu kinachoheshimika sana duniani cha Lateran, lakini maisha yake yote hakuwahi kujiita Dokta. Na hata pale TEC karibu Maaskofu wote ni PhD lakini huwezi kusikia wakijiita Dokta. Ni kwa sababu ya doctrine of humility.

5. Kwanini hakuzikwa kijijini kwao Mwazye, Kalambo? Ukiwa Mkleri utazikwa kwa utaratibu wa Kanisa. Mkleri ni mtu aliyepokea sakramenti ya daraja Takatifu. Hata hivyo angeweza kuzikwa Jimbo Katoliki Lindi au Tunduru-Masasi alipokuwa Askofu wa kwanza wa jimbo hilo. Lakini alishajiandalia kaburi lake kule Pugu. Na alichagua Pugu kwa sababu maisha yake ya utume yamekua zaidi Dar kuliko mahali pengine. Na pia alitamani kuzikwa pamoja na Wamisionari wa kale waliozikwa Pugu.!

Katika pitapita  Mtandaoni tukakutana na kitabu cha PAULO EVARIST KOBA kiitwacho UNATUMIAJE BANDO LAKO-1Good thing kweny...
05/02/2026

Katika pitapita Mtandaoni tukakutana na kitabu cha PAULO EVARIST KOBA kiitwacho UNATUMIAJE BANDO LAKO-1
Good thing kwenye kitabu hicho imetumika k**a mfano.
Shukurani kwa

02/02/2026

Introducing JamiiTalk

Siku ya Elimu Duniani | Happy International Day of Education
23/01/2026

Siku ya Elimu Duniani | Happy International Day of Education

31/12/2025
JamiiTalk wishes you Merry Christmas
24/12/2025

JamiiTalk wishes you Merry Christmas

Address

JamiiTalk

3020

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when JamiiTalk posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share