STORY ZA DAZAR

  • Home
  • STORY ZA DAZAR

STORY ZA DAZAR story

05/05/2026

Maisha/life

04/05/2026

Part 2: Muhuni ataki kukatishwa tamaa

04/05/2026

Part 1: Muhuuni ana ndoto kubwana

29/04/2026

𝗠𝗢𝗬𝗢 𝗨𝗦𝗜𝗢𝗖𝗛𝗢𝗞𝗔 𝗞𝗨𝗣𝗘𝗡𝗗𝗔
𝗦𝗘𝗔𝗦𝗢𝗡 𝟭
𝗘𝗣𝗜𝗦𝗢𝗗𝗘 2

10/04/2026

NGUVA (Samaki Mtu)

SEHEMU YA NNE (4)

Mduara wa maji uliokuwa mbele yao uliendelea kuzunguka polepole, kana kwamba ziwa lilikuwa linavuta pumzi ndefu. Uso wa maji ulianza kushuka katikati ya mduara ule, ukifungua k**a shimo linalojimeza lenyewe. Mtumbwi ukatetemeka kidogo, kamba za nyavu zikagongana kwa sauti ya chuma iliyokwaruza masikio.

Patrick alishika makasia kwa nguvu mpaka vifundo vya vidole vyake vikawa vyeupe. “Hii si kawaida… kabisa.”

Prosper alikuwa anavuta pumzi fupi fupi. “Inaonekana k**a… k**a maji yanazama chini.”

Peter alisimama taratibu ndani ya mtumbwi, akijaribu kudumisha mizani. “Nalia, hii ndiyo sehemu uliyosema?”

Nalia hakujibu mara moja. Macho yake yalikuwa yamefungwa nusu, kana kwamba anasikiliza sauti ambayo wao hawawezi kuisikia. Mikono yake ilikuwa juu ya uso wa maji, vidole vyake vikigusa juu juu kana kwamba anazungumza na kitu kisichoonekana.

“Ndiyo,” alisema hatimaye. “Hapa ndipo nilipoondolewa. Na hapa ndipo lazima nirejeshwe.”

Mduara wa maji ulizidi kupanuka. Mawimbi madogo yakaanza kusukumana kuelekea mtumbwi, si kwa nguvu, bali kwa msukumo wa kudhibitiwa. Ilikuwa k**a mkono mkubwa unaosukuma kwa upole lakini kwa mamlaka.

Patrick akapiga kelele bila kujizuia. “Tunarudishwa chini! Hii ni vifo!”

Peter akamkemea kwa sauti kali. “Tuliza! Kaa chini, usiyumbishe mtumbwi!”

Prosper alikaa kimya, macho yake yakitazama maji kwa hofu. Ndani ya mduara ule, aliona kivuli kikubwa kikizunguka chini ya maji—kikubwa kuliko mtumbwi wao, kikitembea kwa umakini wa kiumbe anayejua kila kitu kuhusu mazingira yake.

“Nalia…” Prosper alisema kwa sauti ya kuomba. “Kitu kile ni nini?”

Nalia akafungua macho yake polepole. Macho yale ya kijani yalionekana kung’aa zaidi sasa. “Ni mlinzi wa mpaka,” alisema. “Mmoja wa wakubwa.”

Patrick akashtuka. “Wakubwa wangapi wapo?”

Nalia hakujibu. Kimya chake kilikuwa jibu lenyewe.

Maji yakaanza kuinuka pembeni ya mtumbwi, yakifunika sehemu ya chini ya mbao zake. Mtumbwi haukuzama, lakini ulikuwa umefungwa kwenye nafasi ile—haukuwa unasogea mbele wala nyuma.

Peter alihisi k**a moyo wake unapiga hadi masikioni. “Sasa tunafanya nini?”

Nalia alis

06/04/2026

𝗠𝗢𝗬𝗢 𝗨𝗦𝗜𝗢𝗖𝗛𝗢𝗞𝗔 𝗞𝗨𝗣𝗘𝗡𝗗𝗔
𝗦𝗘𝗔𝗦𝗢𝗡 𝟭
𝗘𝗣𝗜𝗦𝗢𝗗𝗘 1

AAH! SHEMEJI... ACHA!SEHEMU YA 01Aisha alijiona k**a mtu mwenye bahati ya mtende kwa kutongozwa na shemeji yake. Nafsi y...
04/01/2026

AAH! SHEMEJI... ACHA!

SEHEMU YA 01

Aisha alijiona k**a mtu mwenye bahati ya mtende kwa kutongozwa na shemeji yake. Nafsi yake ilikuwa njia panda; aliwaza amkubalie au amkatalie kwa kigezo cha undugu wa shemeji. Hata hivyo, akili yake iligubikwa na taswira ya utajiri wa shemeji yake huku akilinganisha na hali duni aliyokuwa nayo.

“Endapo nikikubali na dada akigundua, itakuwaje?” alijiuliza moyoni. “Aah! Lakini si amenitongoza mwenyewe? Siwezi kupiga teke fuko la pesa... Potelea mbali.”

Siku iliyofuata, Aisha alikutana na shoga yake kipenzi, Anita. Bila kusita, Aisha alimsimulia Anita kuhusu yaliyojiri kati yake na shemeji yake.

“Shoga yangu, basi ngoja nikupe mkanda kamili.”
Anita alichekelea kwa hamu. “Hapo ndipo ninapokupendea! Tukikutana barazani huchangamka kwa stori. Haya shoga, hebu nipe huo ubuyu.”

Aisha akaanza kuelezea, “Jana usiku wakati tunakula, dada aliwahi kushiba akaenda zake kulala. Sebuleni tukabaki mimi na shemeji tukipata chakula cha usiku. Basi shoga yangu, shemeji si ndio akaanza... ‘Ooh Aisha unajua wewe ni mzuri sana kuliko hata dada yako.’ Mimi nikabaki kucheka tu.

Dakika chache zikapita mara akaanza tena, ‘Aisha, najua wewe ni mtu mzima na unaweza kutunza siri. Mimi nataka uwe mpenzi wangu lakini dada yako asijue.’”

Aisha alivuta pumzi kidogo kisha akaendelea, “Shoga, nilishtuka! Kwani sikutegemea hata siku moja k**a shemeji atakuja kunitamkia maneno k**a yale, ukizingatia jinsi ninavyomheshimu.”

“Shuu! Atabeba mimba huyo!” Anita alidakia kwa mshangao uliochanganyika na furaha ya umbea. “Heshima hiyo weka pembeni, kwani yule ni baba yako mzazi?” Wote kwa pamoja waliangua vicheko vya umbea.

Anita akaendelea kumpa darasa, “Sasa sikiliza shoga yangu nikwambie; maisha ndiyo hayo yanaanza kukunyookea. Ukizingatia shemeji yako alivyo na utajiri, kumuacha ni sawa na kukataa kuolewa na mfalme ili uje kuwa malkia.”

📣🔈🔉SIMULIZI HII HAIJAFIKA MWISHO
K**a Unataka muendelezo, Chagua njia ya kupata muendelezo👇

Tembelea website yetu👉 https://storytz.online/aah-shemeji-acha-01/
Au
ungana nasi WhatsApp 🟢👇 https://whatsapp.com/channel/0029VbB2NaAA2pLGdeJDzo29

MTIKISIKO WA HIRIZISEHEMU YA  5“Huyo mtu kasemaje?” Panga Sakanyoka alimdaka.“Kwamba Mzee Songoro anaishi na mkewe na mw...
27/09/2025

MTIKISIKO WA HIRIZI

SEHEMU YA 5

“Huyo mtu kasemaje?” Panga Sakanyoka alimdaka.

“Kwamba Mzee Songoro anaishi na mkewe na mwanae mmoja tu, ambaye amekuja majuzi kutoka Dar. Anadai kuwa yeye anaishi nyumba ya tatu kutoka kwa Mzee Songoro, na huwa anamwona Shaka kila asubuhi akinawa uso nje ya nyumba hiyo.”

Banda na Panga Sakanyoka walitazamana kisha Banda akasema, “Naona twende. Matokeo yote tutayapata hukohuko. K**a yupo au hata hakulala hapo tutajulia hukohuko.”

Maandalizi yakafanyika chapchap. Askari wengine kumi wenye silaha wakawekwa tayari. Muda mfupi baadaye Land Rover ilikuwa barabarani ikielekea Mtaa wa Mabatini.

Walipoikaribia nyumba hiyo waliteremka na kuanza kupangiana majukumu.

Hawakutaka kuivamia nyumba hiyo mapema kiasi hicho. Ilikuwa ndiyo kwanza inatimu saa 12.20. Bado kijigiza kilitawala anga. Hivyo Panga Sakanyoka aliwapanga wale askari, akawapa majukumu ya kuizingira ile nyumba na kuhakikisha kuwa hakuna mtu atakayetoka.

“Lakini msifanye chochote,” Panga Sakanyoka aliwaambia askari hao. “Kuweni makini, mkihakikisha hatoki mtu humo ndani, na wala isije ikatokea kuwa jamaa yumo ndani na akagundua kuwa tumemzingira! Na kuweni makini kwa huenda ana silaha. K**a ana silaha, akigundua kuwa amezingirwa hataacha kuitumia. ”

ILIKUWA ni kawaida kwa Mzee Songoro kuzinduka usingizini saa 11 alfajiri. Na alfajiri hii, k**a alfajiri nyingine zilizopita pia alizinduka saa 11 lakini hakutoka kitandani. Alibaki amekodoa macho huku akihisi hirizi iliyokuwa kiunoni mwake ikicheza.

Kucheza kwa hirizi hiyo, kwake ilikuwa ni ishara kuwa kuna tukio kubwa mbele yake. Na wazo lililomjia kichwani ni kumhusu mwanawe, Shaka. Tangu Shaka arejee kutoka Dar, amekuwa mtu wa kutoka mara kwa mara, na majuzi aligundua kuwa alikuwa na pesa nyingi....

Hapa kuna toleo lililofupishwa likiwa na link zote zikiwa wazi na zinazoonekana vizuri ili wateja waweze kubofya moja kwa moja:

📚 HII SEHEMU YA 5 HAIJAFIKA MWISHO

K**a Unataka muendelezo!, Chagua njia moja wapo hapo chini kupata muendelezo👇

1️⃣ KUJIUNGA NA CHANNEL YA WHATSAPP

Wiki – Tsh 1,500
💳 Lipa Hapa👇
checkout.flutterwave.com/v3/hosted/pay/flwlnk-01k5cqt80rnj30f86yef3ha4fm

Mwezi – Tsh 3,500
💳 Lipa Hapa👇
checkout.flutterwave.com/v3/hosted/pay/flwlnk-01k5crhh1d3rq2ndppfdns5abd

📩 Baada ya malipo tuma Screenshot WhatsApp:
👉 wa.me/qr/XEAQUXEYQNCEB1
(Utaunganishwa moja kwa moja kwenye channel)

2️⃣ KUPATA FULL STORY

Story Ndefu (zaidi ya sehemu 5) – Tsh 5,000
💳 Lipa Hapa👇
checkout.flutterwave.com/v3/hosted/pay/flwlnk-01k5crtykcegbzp53e256hgc9f

Story Fupi (sehemu 5 Tu) – Tsh 3,000
💳 Lipa Hapa👇
checkout.flutterwave.com/v3/hosted/pay/flwlnk-01k5cs1qfyyb4x6mxb43k7zhf8

Story 1 Kamili – Tsh 1,000
💳 Lipa Hapa👇
checkout.flutterwave.com/v3/hosted/pay/flwlnk-01k5nyry49y4vygfzthxjwzn9f

📩 Baada ya malipo tuma Screenshot WhatsApp:
👉 wa.me/qr/XEAQUXEYQNCEB1
(Simulizi kamili litakufikia moja kwa moja WhatsApp)

🙏 Asante kwa kuchagua huduma zetu – Tafadhali wasiliana nasi ukiwa huko tayari kulipia.

MTIKISIKO WA HIRIZISEHEMU YA 3“N’na maana kuwa Shaka hakutoroka. Aliruhusiwa kuondoka!”“Aliruhusiwa? Aliruhusiwa na nani...
15/09/2025

MTIKISIKO WA HIRIZI

SEHEMU YA 3

“N’na maana kuwa Shaka hakutoroka. Aliruhusiwa kuondoka!”

“Aliruhusiwa? Aliruhusiwa na nani?”

“Hilo ni jambo lingine. Lakini mimi binafsi hainiingii akilini kuwa Shaka alitoroka. Atatoroka vipi chini ya ulinzi, akiwa ni mtu mwenye rekodi mbaya sana anayepaswa kuchungwa k**a mtu yeyote anavyoichunga mboni ya jicho lake?”

Inspekta Banda aliguna.

“Unasikia afande,” Kessy aliendelea. “Shaka alihukumiwa jela akiwa ni mtu hatari, jambazi sugu ambaye vyombo vyote vya dola vinamtambua. Pale Keko wanamjua vizuri Shaka. Walimpokea wakiwa wanamjua vizuri. Kwa vyovyote, walipaswa kumchunga vilivyo.”

“Lakini nadhani hujaisahau ripoti ya kutoweka kwake pale gerezani,” Banda alisema. “Shaka aliondoka katika mazingira ya kutatanisha…”

“Kutatanisha vipi afande wakati inasemekana kuwa yule askari aliyekuwa na kundi la wafungwa alibaki ameduwaa tu wakati Shaka akiondoka taratibu?” Kessy alikuwa king’ang’anizi.

“Kwa hiyo unataka kusema kwamba kulikuwa na njama za kumtorosha?”

“Ndivyo picha inavyojionyesha.”

“Ok, lakini hilo silo jambo linalotuhusu kwa sasa,” Banda alisema. “Twende kwanza Magomeni. Ni huko tutakapopata la kufanya.”

Walipofika Magomeni na kuwahoji Mado na Temba wakapata picha ya matumaini. Wakatoka.

“Anaweza kuwa yeye?” Kessy alimuuliza Banda wakati akiondoka hapo kituoni.

“Ndiye,” sauti ya Inspekta Banda ilikuwa kavu. “Niliepuka kusema hivyo mbele ya wale vijana ili kuepusha usumbufu ambao wangetupa. Kwa vyovyote wangetaka kujua watazipataje milioni zao kumi.”

Kicheko kikamtoka Kessy. Akauliza, “ Wana ndoto za milioni kumi kabla hata mtuhumiwa hajapatikana?”

Inspekta Banda hakujibu.

SHAKA alitambua fika kuwa alipaswa kuwa makini dhidi ya askari, hivyo alipoingia ndani ya treni, alikwenda moja kwa moja kwenye behewa la vinywaji na vyakula. Huko aliketi na kuagiza chupa ya maji lita moja. Akatulia kitini akinywa taratibu.

Hadi treni ilipofika kituo cha Saranda hali ilikuwa shwari. Kituoni hapo akashuka na kuagiza kuku na viazi mbatata kisha akarudi behewani. Akiwa na miwani yake mieusi usoni, miwani ambayo hakuwa tayari kuitoa bila ya sababu muhimu, huku kofia ikiwa imeganda kichwani pake, Shaka alianza kukifakamia chakula hicho kwa pupa na baada ya dakika chache tu zoezi hilo likawa limehitimishwa.

Akaingiza mkono mfukoni na kutoa noti zilizokuwamo. Alipozihesabu, akafarijika. Zilikuwa ni pesa za kumtosha kiasi. Kwa kiwango hicho hakuiona sababu ya kumfanya ashindwe kunywa bia mbili, tatu katika kuiliwaza akili yake k**a alivyoamini. Saa moja baadaye koo likawa limeshateremsha bia mbili. Akaongeza ya tatu.

Hadi treni ilipokuwa inaingia Tabora, bia tano zilikuwa zimeshatua tumboni mwake na kuichangamsha akili yake. Naam, kwa kiasi fulani alijihisi kuwa timamu kisaikolojia huku pia akijali kuwa makini katika maongezi na mtu yeyote.

Kwa jumla hakutaka kuzoeana na yeyote kwa kiwango kikubwa, na hilo alilifanya kwa kuwa hakumwamini yeyote kwa kipindi hicho.

Aliendelea kukaa humo katika behewa la vinywaji na maakuli hadi saa 7 usiku. Na wakati huduma ilipositishwa na wateja kutakiwa kuondoka, yeye alimwita mmoja wa wahudumu wa behewa hilo na kunong’ona naye pembeni. Muda mfupi baadaye kijana huyo alikuwa na shilingi 5,000 kibindoni.

“Us’konde mwanangu,” Shaka aliambiwa. “Pumzika humu hadi kunakucha. Na k**a unataka bia unaweza kuendelea kuagiza.”

Alichohitaji Shaka siyo kuendelea kukaa humo ili anywe bia, hapana. Shida yake ilikuwa ni kupata nafasi ya kulaza mbavu hadi kunakucha. K**a angekuwa na pesa za kutakata asingesita kuonana na TT na kumpa nauli ya chumba cha daraja la kwanza. Baada ya hapo angemtafuta ‘mrembo’, kati ya ‘warembo’ wengi wanaozagaa-zagaa ndani ya mabehewa, na ‘mrembo’ huyo angeifanya safari kuwa fupi kuliko ilivyo.

ASUBUHI ya siku iliyofuata treni iliingia Kigoma mjini. Na k**a alivyokuwa makini safarini, hata pale stesheni Shaka hakupachukulia kwa uzito wa kawaida. Alijua fika kuwa askari nchi nzima watakuwa na taarifa kuhusu yeye, hivyo watakuwa wakimsaka k**a gaidi au haini.

Hadhari ikapewa kipaumbele. Akatulia behewani akiwaacha wenye haraka zao wateremke, yeye akawa miongoni mwa wachache wa mwisho. Na alipoteremka alikwenda moja kwa moja kukodi teksi moja kati ya nyingi zilizokuwa zimefurika mbele ya jengo la kituo hicho........

HII SEHEMU YA PILI HAIJAFIKA MWISHO K**A UNAITAJI MWENDELEZO WA SEHEMU HII YA PILI TUTAFUTE :-

1) whatsapp tukuunge kwenye channel ya FULL STORY Bonyeza link hii👉👇
wa.me/qr/XEAQUXEYQNCEB1 TUKUUNGE KWENYE CHANNEL YETU

2) Jiunge na channel yetu ya bure kwa kubonyeza link hii 👉 whatsapp.com/channel/0029VbB2NaAA2pLGdeJDzo29

3) Tufollow kwenye page yetu ya clubzila kwa kubonyeza link hii 👉 clubzila.com/STORY?ref=11084 upate simulizi kali

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when STORY ZA DAZAR posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share