UMG Digital

UMG Digital Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from UMG Digital, Media/News Company, .

Mwenyekiti na Mwanzilishi wa , Bi Asma Ali Hassan Mwinyi (), amekabidhi sanda kwa ajili ya maiti wasio na ndugu katika H...
14/07/2025

Mwenyekiti na Mwanzilishi wa , Bi Asma Ali Hassan Mwinyi (), amekabidhi sanda kwa ajili ya maiti wasio na ndugu katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kupitia Taasisi ya JAI – taasisi inayohudumia na kuzika maiti zisizo na ndugu au waliotelekezwa.

Kupitia mchango huu, AMF inaendeleza dhamira yake ya kuhudumia watu wote – hata wale waliotangulia mbele ya haki pasipo kuwa na wa kuwazika. Bi Asma ametoa wito kwa Watanzania wote kuchangia kwa uwezo wao, kwani kumstiri mwenzako ni ibada yenye thawabu kubwa.

Mhe.  Baada ya  Miaka 32 amerudi kutembelea Shule aliyosoma Darasa la kwanza hadi la tatu.Kusema kweli wanafunzi saivi h...
12/07/2025

Mhe. Baada ya Miaka 32 amerudi kutembelea Shule aliyosoma Darasa la kwanza hadi la tatu.

Kusema kweli wanafunzi saivi hawakalii mabox na mabao napia nimefarajika kuona watoto wenye uthubutu wa kuwa na ndoto kubwa la kutujengea Taifa Bora lijalo, Pia Mhe. Toufiq Turky amekula na kupeana Motisha na kuwashukuru kuwa Mlezi wao na ahadi yao kwa Mhe Toufiq kuwa itakuwa shule yenye viwango vikubwa Visiwani Zanzibar

Mhe Toufiq Turky akimaliza kwa kusema kabla hamjanishambulia niwaambie kuwa shule hio haimo kwenye Jimbo langu wala sikuenda kumpigia siasa yeyote ila nilienda k**a mwamfunzi wa Kajificheni


Mtangazaji wa Tv na Content Creator pia ni Manager wa Wasanii Nchini Abdul Malick Anania Sangura  Ametia nia ya Kuomba R...
08/07/2025

Mtangazaji wa Tv na Content Creator pia ni Manager wa Wasanii Nchini Abdul Malick Anania Sangura Ametia nia ya Kuomba Ridhaa ya Kugombea nafasi ya Katibu Mkuu kupitia Chama cha Muziki wa Dansi Tanzania (Chamudata)

Anania Junior ni Mtoto wa Promoter Mkongwe wa Muziki wa Dansi Africa Mashariki Marehemu Anania Sangura ambae alifungua Milango ya Soko la Kimataifa la Muziki wa Dansi nchini kwa kuwaleta Wanamuziki Nyota kutoka Congo DRC akiwemo Pepe Kalle, Sam Mangwana, Madiluu, Mayaula, Soukous Stars, Awilo Longomba nk. Pia Anania Sangura alikuwa Nyota wa zamani wa Soka wa Simba na Yanga katika Miaka 1984

Aidha Anania Junior ameshawahi kuwa Manager wa Wasanii kupitia THT mwaka 2017. Aidha Mwaka 2019 - 2020 amewahi kuwa Msaidi wa Meya wa Jiji la Dar Es Salaam (PR) Mhe. Abdallah Mtinika, pia amefanya kazi na Wasanii mbali mbali k**a Ali Choki, Christian Bella, Papii Kocha, Tukuyu Sound Claudia Bakisa kutoka Congo DRC pia Mwaka 2022 aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano na Mitandao ya Kijamii Town Classic Band.

Mhe. Fahad Gulamhafiz Mkuadam ametia nia na kuchukua fomu ya kuomba ridhaa Chama cha Mapinduzi CCM  kugombea ubunge jimb...
04/07/2025

Mhe. Fahad Gulamhafiz Mkuadam ametia nia na kuchukua fomu ya kuomba ridhaa Chama cha Mapinduzi CCM kugombea ubunge jimbo la Shinyanga Mjini .misfit

Fahad Gulamhafiz Mukadam anatambulika kwa asili yake ya kisiasa akiwa mtoto wa mwanasiasa mkongwe na Meya mstaafu wa Manispaa ya Shinyanga, Mzee Gulamhafiz Mukadam.

Mbali na msingi huo wa kifamilia, Fahad ni mwekezaji, kiongozi wa biashara, na mtaalamu wa masoko na teknolojia. Ameanzisha na kuongoza kampuni kadhaa zikiwemo Octopus International, Koikoi Pro na Brands & Stories Ltd, sambamba na kutoa ushauri wa kimkakati kwa kampuni binafsi.

Anaelezwa kuwa na uzoefu katika masoko ya kidijitali, tafiti za soko, na ushawishi kupitia mitandao ya kijamii. Jina lake limeendelea kusemwa zaidi baada ya kuchukua fomu ya CCM, na baadhi ya wanachama wanamtazama k**a sura mpya inayobeba nguvu ya kizazi kipya chenye maono ya kisasa na weledi wa kiuchumi.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema "Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) una viwango ya Kimataifa kutokana na kufanya k...
04/07/2025

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema "Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) una viwango ya Kimataifa kutokana na kufanya kazi kwa weledi na kwa kuzingatia viwango bora vya kimataifa".

"Hii imethibitika kuwa WCF inatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia viwango vya ubora vya Kimataifa na ndio sababu mataifa jirani wamekuwa wakivutiwa kuja kujifunza tumefikia hatua hii, ni mbinu zipi tumezifanya. Endeleeni  kupokea wageni muwaambie ili Tanzania tuendelee kuwa kinara kwenye eneo hili la fidia kwa wafanyakazi," amesema Waziri Mkuu Majaliwa

Ameyasema hayo  katika maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) mkoani Dar es Salaam

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameeleza pia  moja ya mafanikio ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ndani ya kipindi cha miaka 10 ni kuongeza aina za mafao yanayotolewa na mfuko huo kutoka fao moja hadi kufikia mafao saba.

 
"Mafao hayo saba ni fao la matibabu, fao la ulemavu wa muda mfupi, fao la ulemavu wa kudumu, pensheni kwa wategemezi, fao la msaidizi wa mgonjwa, fao la utengemano ambalo baadae nitalizindua pamoja na fao la msaada wa mazishi," amesema Waziri Mkuu Majaliwa

 
Ametaja mafanikio mengine kuwa ni kuongezeka kwa viwango vya fidia vilivyokuwa vinatolewa na sekta zote za umma na sekta binafsi akieleza kuwa ni ishara ya kuimarika kwa mfuko na dhamira ya Serikali katika kulinda maslahi ya wafanyakazi wake.



Mheshimiwa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya WCF, akiongozwa na Mkurugenzi Mku...
04/07/2025

Mheshimiwa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya WCF, akiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa WCF Dk. John Mduma kutembelea maonyesho ya historia ya Mfuko.

Maonyesho haya yanaonesha safari ya miaka 10 ya WCF katika kutoa fidia stahiki kwa wakati kwa wafanyakazi wa Tanzania. Kuanzia hatua za mwanzo, mafanikio, hadi dira ya miaka ijayo historia hii ni ushahidi wa dhamira ya kweli kwa mfanyakazi.


William Mathew Makufwe leo jumanne 01 Julai, 2025 amerejesha fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (...
01/07/2025

William Mathew Makufwe leo jumanne 01 Julai, 2025 amerejesha fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanganyika Mkoani Katavi katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Ikumbukwe Ndugu. William Mathew Makufwe aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Mtendaji wa Halmashauri za Handeni, Makete na Kaliua akitumikia katika utumishi wa umma.

Mtia niyo huyo amefika mapema katika ofisi ya chama hicho iliyoko Kijiji cha Majalila Wilaya ya Tanganyika na kukabidhi fomu mbele ya Katibu wa CCM Wilaya ya Tanganyika, Adelaida Machenchewa.

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara,Exaud Kigahe, Amechukua Fomu ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwanua u...
01/07/2025

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara,Exaud Kigahe, Amechukua Fomu ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwanua ubunge katika jimbo la Mufindi Kaskazini mkoani Iringa.

30/06/2025
30/06/2025
Mwenyekiti wa Chama Cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA), mfanyabiashara maarufu, na kada mwaminifu wa Chama Cha Mapi...
29/06/2025

Mwenyekiti wa Chama Cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA), mfanyabiashara maarufu, na kada mwaminifu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Elias Stephen Lukumay, leo tarehe 29 Juni 2025, amechukua rasmi fomu ya kuwania Ubunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, Mkoa wa Arusha.

Aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Viti 15 Tanzania Bara 2017 - 2022 na Mjumbe wa Tume ya Uhakiki wa Mali ...
29/06/2025

Aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Viti 15 Tanzania Bara 2017 - 2022 na Mjumbe wa Tume ya Uhakiki wa Mali za CCM (Tume ya Makinikia ya CCM) Ndugu William Sarakikya amerudisha fomu ya kuomba kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM Jimbo la Arumeru Mashariki, Halmashauri ya Meru, Mkoani Arusha kupitia Chama cha Mapinduzi leo tarehe 29.06.2025 kwa Katibu wa CCM wa Wilaya ya Meru Ndugu Rehema Nzunye.

Alipoulizwa nini matarajio na mipango yake? Alisema "wakati ukifika nitasema, lakini kwa sasa ni wakati wa kufuata maelekezo ya Chama na kuacha Vikao vya maoni, mapendekezo na uteuzi vifanye kazi zake."

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UMG Digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UMG Digital:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share