Khidma TV

Khidma TV KHIDMA ONLINE TV, CHANNEL YA KIISLAMU KWA MAWAIDHA ZAIDI TEMBELEA YOUTUBE +255 752 950 350
(1)

16/08/2025

Maajabu ya dua ya bibi huyu ilipelekea ndege kushindwa kuendelea na safari hata gari pia ili dua ya huyu bibi itimie funzo tumuombe Allah tukiwa na imani kua tutajibiwa hakuna zito Mbele ya Allah.

Kisa hi ni cha kweli na kimetokea zama hizi na huyo Daktari amekiandika katika mmoja ya vitabu alivyo viandika.

16/08/2025

Usipomjua alie kupa amri umakini utakua mdogo ila ikimjua kusnzia hapo utaongeza umakini Allah ametupa amri ya kumuabudu yeye pekee na Akajitambulisha yeye ni nani.

16/08/2025

Sheikh Kishki Akitoa Taarifa ya Kuvunjwa Masjid Ihsaan Vetenary Ili Kupisha Ujenzi wa Msikiti mpya.

Rais wa Zanzibar Dr. Hussein Ali Mwinyi Awataka Viongozi wa Dini na Waumini Kuiombea Nchi Amani Haswa Kipindi Hiki Kuele...
15/08/2025

Rais wa Zanzibar Dr. Hussein Ali Mwinyi Awataka Viongozi wa Dini na Waumini Kuiombea Nchi Amani Haswa Kipindi Hiki Kuelekea Uchaguzi Mkuu.

Ameyasema hayo mara baada ya kumalizika kwa swala ya ijumaa Ampapo Rais. Hussein Ali Mwinyi Alijumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika Sala ya Ijumaa pamoja na Dua Maalumu ya kuwaombea Viongozi Wakuu wa Nchi, iliyofanyika katika Msikiti wa Shaafi, Mbuyu Mnene, Mkoa wa Mjini Magharibi leo tarehe 15 Agosti 2025.

Katika salamu alizotoa baada ya swala na dua hiyo, amewasihi wanasiasa kutumia majukwaa ya kisiasa kutangaza sera za vyama vyao kwa wananchi badala ya kueneza siasa za chuki.

Ni vema wanasiasa kuhubiri amani na kueleza namna watakavyowatumikia wananchi baada ya kupata ridhaa ya kuwaongoza, badala ya kutangaza siasa za chuki, matusi na mifarakano ndani ya jamii.

Aidha, nimewasisitiza viongozi wa dini na waumini kuiombea nchi amani, hasa katika kipindi hiki ambacho kimebakia miezi michache kabla ya Uchaguzi Mkuu.

MASJID IHSAAN TEMEKE VETENARY ULIO CHINI YA SHEIKH NURDEEN KISHKI KUVUNJWA KESHO JUMAMOSISheikh Nurdeen Kishki imamu mku...
15/08/2025

MASJID IHSAAN TEMEKE VETENARY ULIO CHINI YA SHEIKH NURDEEN KISHKI KUVUNJWA KESHO JUMAMOSI

Sheikh Nurdeen Kishki imamu mkuu wa Masjid Ihsaan kupitia mimbari ya Vetenary amewatangazia waumini wa msikitio huo maarufu duniani kua msikiti huo utavunjwa kwanzia kesho tarehe 16,08,2025 ili kupisha ujenzi wa msikiti mwengine mpya.

Akiongea Sheikh Kishki amesema msikiti huo umejipatia umaarufu mkubwa Afrika na Duniani kwa ujumla kwani umekua ukipwekea wageni kutoka katika mataifa mbalimbali duniani wageni ambao kila walipo wasili Tanzania walitamani kufika katika msikiti huo, na mara baada ya kufika walishangazwa na udogo wa msikiti huo ambao ulijengwa mwaka 2005 kua na umaarufu mkubwa duniani lakini ni mdogo sana jambo ambalo Sheikh Kishki hakulipa muda na badala yake aliendelea kufanya Daawah ndani ya msikiti huo.

Aidha Sheikh Kishki ameeleza kua kuna wadau walijitokeza kipindi cha nyuma wakitaka kuuvunja msikiti huo na kumjengea msikiti mpya lakini aliwashukuru na kuwambia msikiti huo bado haujafika muda wa kuvunjwa.

Akitoa taarifa rasmi ya kuvunjwa msikiti huo Sheikh Kishki amesema muda ambao Allah alipanga kwaajili ya kuvunjwa msikiti huo umefika na kupisha ujenzi msikiti mpya ambao unatarajiwa kua ni mkubwa kuliko huu wa sasa.

Sheikh Kishki amewaomba radhi waumini wa Masjid Ihsaan kwa usumbufu utakao jitokeza katika kipindi hiki ujenzi ukiwa unaedelea na kuwataka wawe na uvumilivu na wazidishe dua ili ujenze uwe wa haraka na mwepesi.

Aidha Sheikh kishki ametoa Shurkan na kuwaombea dua waliojenga msikitio huo ambao utabomolewa kesho ambao pia ndio watakao jenga msikiti mpya mahala hapo.

Masjid Ihsaan ni msikiti wenye historia na Sheikh Nurdeen Kishki ambapo miaka 30 ya Daawah yake amehudumu katika msikiti huo kwa miaka 20.

15/08/2025

Tusitaraji ushindi na mafanikio katika jamii ya kiislamu ikiwa tutaendeleza makundi baina yetu waislamu tutaendelea kutafunana sisi kwa sisi.

Sheikh Nurdeen Kishki Ataunguruma Katika Khutuba ya Ijumaa Leo Masjid Ihsaan Temeke Vetenary.Mada. Ijue saa ya kupokelew...
15/08/2025

Sheikh Nurdeen Kishki Ataunguruma Katika Khutuba ya Ijumaa Leo Masjid Ihsaan Temeke Vetenary.

Mada. Ijue saa ya kupokelewa dua siku ya ijumaa. mimi nina shauku kujua huo muda ambao dua inapokelewa siku ya leo ijumaa k**a na wewe una shauku ya kujua hakikisha khutuba hi umeisikiliza ili kujua hilo lisaa ndani ya siku ya ijumaa tuna mengi ya kumwambia Mola wetu.

Inshaallah Khutuba hi utaipata katika channel ya YouTube kwa jina la Khidma TV

14/08/2025

Dini ni mfumo ulio wekwa na watu isipokuwa dini ya uislamu ni mfumo ulio wekwa na Allah.

14/08/2025

Mfano mzuri ni kinachoendelea Palestina hivi sasa k**a Israel atafanikiwa kwa taifa la Palestina ndio utakua mwanzo wa taifa lingine la kiislamu si ajabu ikawa ni Saudia na wakailenga Alkaaba tukufu.

Endepo jamii ya kiislamu itarudisha hali ya ummoja wao licha ya tofauti zao basi waislamu hawato kumbwa na mateso popote pale duniani. Leo palestina inaliwa pekeyake na Israel uko wapi ummoja wetu.

14/08/2025

Sema Alhamdullah kuna wengi hawafanyi icho unachofanya wewe mshukuru Mungu.

13/08/2025

Alisaidiwa na tajiri pesa ya kodi ya mwaka mzima lakini mtu huyo hakutoa hata shukran kwa huyo tajiri na alipopewa mawasiliano alikataa na kumwambia nikipatwa na shida tena nitakuja hapa Mungu atamleta mtu mwengine wakuja kunisaidia sina haja ya namba yako.

AMEPATIKANA AMEPATIKANA ALHAMDULILAH Taarifa mpya kutoka kwa baba mzazi wa kijana Yusuf Tunashukur kwa kila dua, fikra, ...
13/08/2025

AMEPATIKANA AMEPATIKANA ALHAMDULILAH

Taarifa mpya kutoka kwa baba mzazi wa kijana Yusuf

Tunashukur kwa kila dua, fikra, na ushauri ulioyotoa kwa kupatikana Mwanangu Yusuf Muhammad Matano.

Shukran kwa jeshi la polisi, Imaan Media, The Islamic Foundation Taasisi ya Al-Firdaus na Tameya, Taasisi ya Jai, Shule ya Mnazi Mmoja na walimu wote, Hospital zote za rufa Mkoa wa Dar es Salaam mwananchi wa mtaa wa jaribu na Shirika la mabasi ya Mwendokasi. Bila kusahau juhudi za ndugu jamaa na marafiki.

Allah atakulipeni kheir. Taarifa rasmi ya kupatikana kijana kutoka kwa baba mzazi Muhammad Matano.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Khidma TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Khidma TV:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share