Uvinza FM

Uvinza FM Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Uvinza FM, Radio Station, Nkwaza, Uvinza.

Uvinza FM is registered community radio with a VISION: To be a pioneer agent of positive social participation and income generating behaviour change in Uvinza and elsewhere in Lake Tanganyika Corridor Basin in Kigoma. And a MISSION:
To disseminate social and economic changes information through awareness creation news, drama, entertainment, talk shows discussions and speciality programs in education, health, agriculture, animal husbandry, entrepreneurship, sports and culture orientations.

14/09/2026

Kiongozi mbio za mwenge asisitiza Matumizi ya nishati safi na upandaji wa miti.

14/09/2026

MWENGE WA UHURU 2026 WAWEKA JIWE LA MSINGI SHULE YA KUTWA LUGUFU SEKONDARI

Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu WAZO MWANG'ONDA ameweka Jiwe la msingi kwenye ujenzi wa shule ya Kutwa ya Sekondari Lugufu ambayo imegarimu zaidi ya shilling million 600.

Shule hiyo imelenga kuwanufaisha wananchi wanaoishi maeneo hayo kuepukana na adha ya umbali mrefu wa kufata shule ambapo walikuwa wanatembea takribani kilomita 10 kupata huduma hiyo.

đź“»Tusikilize Uvinza FM kupitia Masafa ya 96.5 Mhz UVINZA | KIGOMA | KASULU | BUHIGWE | KIBONDO | NGURUKA |KATAVI(Mlele) | TABORA(Kaliua&usinge)| Pia Online kupitia:- Radio Tadio, Online Radio Box, Radio Garden, Radio Zeno, Radioly. tafuta UVINZA FM au https://radiotadio.co.tz/uvinzafm/

14/09/2026

Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mhe. Dinnah Mathamani ameupokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Kigoma Dr. Rashidi ChuaChua katika Uwanja wa Shule ya msingi Mapinduzi uliyopo Kata ya Mlele Halmashauri ya wilaya Uvinza.

Akizungumza mara baada ya kuupokea Mwenge, Mhe. Dinnah Mathamani amesema kuwa Mwenge wa Uhuru utapitia jumla ya miradi sita yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 6.9 katika Halmashauri ya wilaya Uvinza.

Amesema kati ya miradi hiyo, mradi mmoja utawekewa jiwe la msingi, miradi miwili itazinduliwa huku miradi mingine mitatu itambelewa na Mwenge huo.

Aidha, Mhe. Dinnah Mathamani amesema Mwenge wa Uhuru utakimbizwa kwa umbali wa kilomita 181 ukipitia na kuangazia miradi katika sekta za Maji, Elimu, Afya, Maendeleo ya Jamii pamoja na miradi inayolenga kuwawezesha Vijana.

đź“»Tusikilize Uvinza FM kupitia Masafa ya 96.5 Mhz UVINZA | KIGOMA | KASULU | BUHIGWE | KIBONDO | NGURUKA |KATAVI(Mlele) | TABORA(Kaliua&usinge)| Pia Online kupitia:- Radio Tadio, Online Radio Box, Radio Garden, Radio Zeno, Radioly. tafuta UVINZA FM au https://radiotadio.co.tz/uvinzafm/

13/09/2026

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026, Wazo Michael Mwang’onda, amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya maendeleo kwa niaba ya Serikali kufanya kazi kwa uzalendo na kuzingatia viwango vinavyotakiwa ili miradi hiyo iweze kukamilika kwa wakati na kwa ubora unaokusudiwa.

Mwang’onda ametoa kauli hiyo leo wakati wa kukagua na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa Barabara ya Baptist, iliyojengwa kwa kiwango cha lami nyepesi yenye urefu wa kilomita 0.7 katika Kata ya Katubuka, Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Aidha, Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge amewataka wananchi kutunza miundombinu hiyo ya barabara na kuitumia kwa kuzingatia taratibu ili iweze kudumu kwa muda mrefu na kuendelea kuwa na manufaa kwa jamii.

Mradi huo unaotekelezwa na Serikali kwa gharama ya Shilingi 897,287,450 umeelezwa kuwa ni suluhisho la changamoto ya usafiri iliyojitokeza baada ya barabara za Kagashe pamoja na barabara ya Airport hadi Katubuka kuathiriwa na mafuriko na kushindwa kupitika. Barabara ya Baptist ambayo kwa sasa ipo katika hatua ya matengenezo ya mwisho, tayari imeanza kutumika na inatarajiwa kurahisisha usafiri na usafirishaji kwa wakazi wa Kata za Katubuka na Buhanda, pamoja na kuwezesha upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii, ikiwemo Hospitali ya Baptist na Soko la Nazareth.

13/09/2026

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Zainab Katimba, amewataka wananchi wenye changamoto za kisheria kutumia madawati ya msaada wa kisheria yaliyopo katika halmashauri zote za wilaya nchini, ili kupata huduma hizo kwa urahisi.

Akizungumza na wananchi waliojitokeza kushuhudia Mbio za Mwenge wa Uhuru zinazoendelea mkoani Kigoma, Mhe. Katimba amesema Serikali imeweka huduma hizo karibu na wananchi kwa lengo la kuhakikisha kila mmoja anapata haki kwa wakati na bila vikwazo, akiwataka wananchi kutumia fursa hiyo katika kutatua migogoro mbalimbali ya kisheria inayowakabili.

Amesema upatikanaji wa huduma za msaada wa kisheria katika ngazi za halmashauri ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuhakikisha wananchi, hususan wenye changamoto za kupata huduma za kisheria, wanapata haki kwa urahisi. Wito huo unaendana na Kauli Mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2026 isemayo: “Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja, Kuleta Maendeleo.”

13/09/2026

Baada ya kumbeba Mwenge wa Uhuru kwa mara ya kwanza, Vibe la Mh. Babalevo unalipa asilimia ngapi?

Kwa sasa Mwenge uko Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji, eneo ambalo Baba Levo ni Mbunge wa Jimbo hilo

Tupia asilimia yako, Baba Levo leo amekupa vibe la ngapi?đź“»Tusikilize Uvinza FM kupitia Masafa ya 96.5 Mhz UVINZA | KIGOMA | KASULU | BUHIGWE | KIBONDO | NGURUKA |KATAVI(Mlele) | TABORA(Kaliua&usinge)| Pia Online kupitia:- Radio Tadio, Online Radio Box, Radio Garden, Radio Zeno, Radioly. tafuta UVINZA FM au https://radiotadio.co.tz/uvinzafm/

13/09/2026
12/09/2026

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma ameshiriki kikamilifu katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2026 yaliyofanyika leo katika Wilaya ya Kigoma, huku akiwapongeza wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwa kujitokeza kwa wingi na kuonesha uzalendo, mshikamano na utii.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mkuu huyo wa Wilaya ameandika: “Utii, uzalendo na mshikamano! Nawashukuru sana wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma mmetisha kwa mapokezi makubwa ya Mwenge wa Uhuru. ”

12/09/2026
12/09/2026

đź“»Tusikilize Uvinza FM kupitia Masafa ya 96.5 Mhz UVINZA | KIGOMA | KASULU | BUHIGWE | KIBONDO | NGURUKA |KATAVI(Mlele) | TABORA(Kaliua&usinge)| Pia Online kupitia:- Radio Tadio, Online Radio Box, Radio Garden, Radio Zeno, Radioly. tafuta UVINZA FM au https://radiotadio.co.tz/uvinzafm/

Address

Nkwaza
Uvinza
P.OBOX31

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uvinza FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Uvinza FM:

Shortcuts

Share

Category