Uvinza FM

Uvinza FM Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Uvinza FM, Radio Station, Nkwaza, Uvinza.

Uvinza FM is registered community radio with a VISION: To be a pioneer agent of positive social participation and income generating behaviour change in Uvinza and elsewhere in Lake Tanganyika Corridor Basin in Kigoma. And a MISSION:
To disseminate social and economic changes information through awareness creation news, drama, entertainment, talk shows discussions and speciality programs in education, health, agriculture, animal husbandry, entrepreneurship, sports and culture orientations.

 : Mkuu wa mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro amewataka wawekezaji kuchangamkia fursa za uwekezaji katika mkoa huo kwani ...
16/10/2025

: Mkuu wa mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro amewataka wawekezaji kuchangamkia fursa za uwekezaji katika mkoa huo kwani uwekezaji ni nguzo muhimu ya kiuchumi na Maendeleo ya nchi kuanzia ngazi ya familia mpaka ngazi ya Taifa

RC Sirro ameyasema hayo wakati alipokutana na kuzungumza na mkufunzi Mkuu na Kaimu Mkuu wa chuo cha Uk**anda na Unadhimu cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kanali Jafari Ramadhan ambaye yuko Kigoma kwa ziara ya ndani

"Uongozi wa mkoa wa Kigoma unaendelea kufanya uchunguzi kuhusu vyamzo ya kiuchumi huku ukirihusu ubunifu na kutumia nguvu kazi iliyopo ili kuongeza kipato kwa wananchi wa Kigoma na kuongeza Pato la Taifa" Balozi Sirro



Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya Mh. Raila Odinga amefariki dunia leo wakati akipatiwa matibabu katika hospitali moja nchi...
15/10/2025

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya Mh. Raila Odinga amefariki dunia leo wakati akipatiwa matibabu katika hospitali moja nchini India kulingana na Duru za kimataifa na familia yake

Kiongozi huyo aliyefariki akiwa na miaka 80 kabla ya kifo chake atakumbukwa kwa kupigania uhuru wa kidemkokrasia, haki za binadamu na mabadiliko ya kitaifa

Kufatia msiba huu Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye kwa sasa ni mgombea nafasi ya Rais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt Samia Suluhu Hassan amesema

"Tumepoteza kiongozi muhimu sana, mwanajumuiya ya Afrika mashariki, mpenda amani na mtafuta suluhu ambaye ushawishi wake na upendo wake haukuww tu ndani ya Kenya bali Afrika mashariki na Afrika kwa ujumla msiba huu ni weti sote" Dkt. Samia
house.kenya

 : Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro akufahi pamoja na wananchi wa wilaya ya M...
15/10/2025

: Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro akufahi pamoja na wananchi wa wilaya ya Muleba mkoani Kagera leo wakisubili kuanza kwa mkutano wa kampeni za mgombea nafasi ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan

 : Katika mwendelezo wa kampeni za siasa Kuelekea uchaguzi Mkuu wa Tanzania katika nafasi za Diwani, Mbunge na Rais wa J...
15/10/2025

: Katika mwendelezo wa kampeni za siasa Kuelekea uchaguzi Mkuu wa Tanzania katika nafasi za Diwani, Mbunge na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa ifikapo Octoba 29 Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kimeendelea kushika kasi kwa kusambaza sera zake na kuomba kura kwa wananchi katika maeneo mbali mbali nchini

Kupitia Mgombea wake nafasi ya Diwani kata ya Itebula wilayani Uvinza Ndg. Boniface Daudi Nkunzumwami amewaahidi wananchi wa kata ya Itebula kuzitatua changamoto zao zilizowakabili kwa muda mlefu zaidi ndani ya siku 100 za mwanzo k**a watamuamini na kumpa ridhaa ya kuwa Diwani wao

Boniface amesema, katika kata ya Itebula kuna changamoto nyingi katika huduma za Afya, Elimu, Miundo mbinu, Maji, Umeme, Kilimo na changamoto za kijiografia katika kuunganisha vitongoji vyote 15 vya kata ya Itebula. Na hayo yote ndio mambo anayokwenda kushughulikia kwa haraka zaidi baada ya kuapishwa rasmi k**a Diwani

Kwa upande wake Katibu - Mwenezi CHAUMMA kata ya Itebula Ndg. Shukuru Kasoro (Profesa) amesema Chama hicho kimejipanga vizuri katika kuitekeleza ilani yake inayolenga kuboresha maisha ya wananchi kwa ujumla kwa kuanza vipaumbele vyake vyenye tija kwa watanzania


 : Ni wananchi wa Katoro mkoani Geita waliohudhuria mkutano wa kampeni wa Mgombea nafasi ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano...
13/10/2025

: Ni wananchi wa Katoro mkoani Geita waliohudhuria mkutano wa kampeni wa Mgombea nafasi ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt Samia Suluhu Hassan leo 13 Octoba

Mgombea nafasi ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan amewakabidhi i...
13/10/2025

Mgombea nafasi ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan amewakabidhi ilani ya chama hicho wagombea Ubunge mbali mbali wa mkoa wa Geita



Kutokea mkoani Geita ambako mgombea nafasi ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)...
13/10/2025

Kutokea mkoani Geita ambako mgombea nafasi ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt Samia Suluhu Hassan anakoendelea na kampeni zake zikiambatana na kuwaomba kura wananchi ifikapo tarehe 29 Octoba mwaka huu ili awese kuiongoza kwa awamu ya pili

Wakati akihitimisha mkutamo wake amemkabidhi ilani ya chama hicho mgombea nafasi ya Ubunge (CCM) Jimbo la Geita Mjini Dkt. Dotto Biteko akayatekeleze yote yaliyopangwa na chama chake ili kutimiza mipango yote kwa muhura wa serikali 2025/2030





UTEKELEZAJI WA ILANI CHINI YA RAIS DKT. SAMIASOKO LA MWANZA – MWANZA | SH. BILIONI 23 | WATU 5,000 KWA SIKUDkt Samia kat...
13/10/2025

UTEKELEZAJI WA ILANI CHINI YA RAIS DKT. SAMIA
SOKO LA MWANZA – MWANZA | SH. BILIONI 23 | WATU 5,000 KWA SIKU

Dkt Samia katika utawala wake amejenga Soko Kubwa la kisasa kwa USD milioni 9.2 sawa na shilingi bilioni 23. Linauwezo wa kuhudumia watu 5,000 kwa siku, sawa na watu 1,825,000 kwa mwaka.

Linajumla ya vizimba 1,400 na linaweza kuhifadhi magari 500 kwa mpigo. Soko hili ni kielelezo cha ukuaji wa uchumi wa mikoa ya kanda ya ziwa chini ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Limeajiri jumla ya wajasiriamali 3,200, ambapo ajira rasmi ni 1,400 na ajira zisizo rasmi ni 1,800, hakika Tanzania ni njema atakaye na aje.




JE? WASICHANA WA TANZANIA WANAPATA NAFASI YA KUONYESHA UONGOZI NA KULETA MABADILIKO KATIKA JAMII ZAO ?Na Ezra MeshackKat...
13/10/2025

JE? WASICHANA WA TANZANIA WANAPATA NAFASI YA KUONYESHA UONGOZI NA KULETA MABADILIKO KATIKA JAMII ZAO ?

Na Ezra Meshack

Katika wiki ya maadhimisho ya Mtoto wa k**e Duniani yaliyoanzishwa rasmi mwaka 2011 kwa lengo la kubaini changamoto zinazowakabili watoto wa k**e na kuwanyima fursa mbali mbali za muhimu katika maisha yao ambazo hufanyika kila mwaka tarehe 11 Octoba kumekuwa na mambo ya kujadili ikiwa ni pamoja na swali liloulizwa hapo juu

Akitoa majibu ya swali hilo Afisa Maendeleo ya Jamii kata ya Uvinza Bi Sharifa Masudi amesema jibu la hilo ni NDIYO tena ndiyo yenye ukubwa na uhakika zaidi kwa kutoa mfano kadhaa ya watoto wa k**e (wanawake) waliofanya, wanaofanya na wanaoendelea kufanya vizuri majukumu yao k**a viongozi, watumishi wa umma, wakuu wa taasisi na wengineo kwa kuonyesha mchango wao na mabadiliko waliyoleta kwa Jamii

"Tunae Rais wa Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan, tunae Dr. Amna Henga Mkurugenzi mtendaji wa LHRC anayepambania haki za wanawake na binadamu kwa ujumla, tunae Mwenyekiti wa Chupukizi wa CCM Taifa CDE Qayllah Bilal, tunae Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mh. Dinah Madhamani, Maafisa Maendeleo, Usitawi, Biashara, waandishi wa habari na kada zingine zote wote kwa pamoja wanaofanya kazi nzuri sana yenye mchango mkubwa na mabadiliko kwa Jamii" Sharifa

Lakini pia, amewasihi wazazi na walezi kuhakikisha wanawalinda watoto wa k**e dhidi ya ukatili wa aina zote bila kuwasahau watoto wa kiume ambao nao pia wamekuwa wakikumbwa na ukatili k**a vile kulawitiwa na kupigwa kupita kiasi yote haya kwa pamoja yataifanya nchi yetu kuwa na watu bora, familia bora, watumishi bora na iongozi bora.

Kwa upande wake Mchungaji Eliud Rafael Mpinda wa Dayosisi ya Tanganyika Magharibi (D.W.T) Kanisa Anglikana Tanzania Parishi ya Uvinza amesema "watoto wa k**e ni tunu kubwa katika jamii na wanapaswa kupewa kupaumbele k**a ilivyo kwa watoto wa kiume"

Amesema, katika shughuli za kidini watoto wa k**e wanafanya vizuri na kwa uaminifu mkubwa katika nafasi mbali mbali ikiwemo kumwimbia Mungu (kwaya), kuhubiri injiri, uongozi wa makundi, Elimu na kadharika, huku akiwataka watoto wa k**e kuendelea kujitunza



 : WAZAZI WAASWA KUWASIKILIZA WATOTO WA K**E NA KUWAPA NAFASI YA KUFANYA MAAMUZINa Ezra Meshack Kila mwaka tarehe 11 oct...
11/10/2025

: WAZAZI WAASWA KUWASIKILIZA WATOTO WA K**E NA KUWAPA NAFASI YA KUFANYA MAAMUZI

Na Ezra Meshack

Kila mwaka tarehe 11 octoba, Dunia huathimisha siku ya kimataifa ya Mtoto wa k**e (International Day of the Girl Child) siku yenye fursa ya kuangazia haki, usitawi na nguvu ya Mschana katika kila nyanja ya maisha

Siku hii husisitiza kwamba wasichana wana nguvu, uongozi na uwezo wa kuleta mabadiliko hata katika nyakati za changamoto k**a vile majanga, migogoro au hali ngumu ya kijamii ikiwa ni sehemu pia ya kuondoa mitazamo potofu, ukosefu wa nafasi na unyanyasaji wa kijinsia

Katika maadhimisho haya yenye kauli mbiu isemayo "MIMI NI MSICHANA KINARA WA MABADILIKO YA TANZANIA TUITAKAYO 2050" Afisa maendeleo ya jamii kata ya Uvinza Bi. Zainab Kasindi amewataka wazazi kuwaamini watoto wa k**e na kuwapa nafasi ya kufanya maamuzi binafsi kuhusu maisha yao

Bi Zainab amesema "watoto wanatofofautiana uelewa hivyo ni vema kuwajengea uwezo wa kujipambanua tangu wakiwa wadogo ili waweze kuyakabili maisha watakapokuwa watu wazima sambamba na kuwafunza haki na uwajibikaji"

Kwa upande wake pia Afisa maendeleo kata ya Uvinza Bi. Sharifa Masudi akizungumza kupitia Radio Uvinza FM amebainisha changamoto zinazowakabili watoto wa k**e k**a vile kukosa stahiki za msingi, kufanyiwa ukatili, kukosa Elimu, Kubakwa na kunyimwa fursa mbali mbali za muhimu hali inayowafanya wawe nyuma kimaendeleo

Bi Sharifa amesema "Njia pekee ya kuyaondoa makwazo hayo ni jamii kuelimika na kutambua mchango wa mtoto wa k**e katika nyanja mbali mbali za kijamii na kuwaomba wazazi na walezi watenge muda kuzungumza na watoto wa k**e ili kuwajenga na kuwapa nguvu za uthubutu"

Ikumbukwe miongoni kwa sababu zinazopekekea watoto wa k**e kutokufanya vizuri ni pamoja na wao wenyewe kutokuamini na kupokea chanya mafundisho wanayopewa na wazazi, kutokujiamini na kuthubutu ambavyo kwa pamoja vikikomeshwa vitaleta mabadiliko makubwa katika jamii yetu (Bi Sharifa)



🌍✨ Proud Moment for Uvinza FM! ✨🌍We are thrilled to announce that Uvinza FM Radio has officially joined the United Natio...
11/10/2025

🌍✨ Proud Moment for Uvinza FM! ✨🌍

We are thrilled to announce that Uvinza FM Radio has officially joined the United Nations Global Compact Network Tanzania which is the world’s largest corporate sustainability initiative! πŸŽ‰

As a new member, we commit to uphold and advance the Ten Principles of the UN Global Compact in the areas of Human Rights, Labour, Environment, and Anti-Corruption, and to take bold action in support of the Sustainable Development Goals (SDGs).

This milestone marks our deepened dedication to responsible media, ethical leadership, youth empowerment, and community transformation in Uvinza and beyond.

Together with , we are shaping a more sustainable and inclusive future β€” one voice, one story, and one community at a time. πŸ’ͺπŸ“»πŸŒΏ

 : KWA SASA WATOTO WANAANDALIWA KUJITEGEMEA WENYEWE - NDARICHAKONi sehemu ya maneno aliyozungumza mwalimu Mkuu wa shule ...
11/10/2025

: KWA SASA WATOTO WANAANDALIWA KUJITEGEMEA WENYEWE - NDARICHAKO

Ni sehemu ya maneno aliyozungumza mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Nyambutwe Jane Ndarichako katika mahafari ya kuhitimu darasa la saba yaliyofanyila shuleni hapo akieleza msingi mkuu wa Elimu ya msingi

Akibainisha kwamba wakati mwingine wazazi wanaweza wasielewe sana kinachofanyika kwa sababu za mabadiliko ya mitaala ya Elimu ambayo kwa sasa inawaanda Wanafunzi kukabili majukumu na kujitegemea wawapo shuleni na nje ya shule

>>> Ni picha matukio mbali mbali, wanafunzi, wazazi na walezi



Address

Nkwaza
Uvinza
P.OBOX31

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uvinza FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Uvinza FM:

Share

Category