03/06/2026
MAKONDA: MSIWABEZE MASHABIKI WALIOKWENDA
MOROCCO
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amewataka Watanzania kuacha kuwabeza mashabiki waliokwenda nchini Morocco kuishangilia Serengeti Boys, akisisitiza kuwa uwepo wao ulikuwa sehemu muhimu ya kuipa timu morali katika hatua ya fainali ya AFCON U-17.
Makonda amesema mashabiki ni mchezaji wa 12 uwanjani kwa kuwa uwepo wao huwapa wachezaji nguvu, hamasa na kujiamini wanapoiwakilisha nchi katika mashindano ya kimataifa.
"Hakuna timu inayokwenda mashindanoni bila mashabiki. Senegal na mataifa mengine yalikuwa na mamia ya mashabiki waliokwenda kuziunga mkono timu zao. Nasi tunapaswa kuthamini wale waliopata nafasi ya kwenda kuiwakilisha Tanzania na kuwapa nguvu vijana wetu," amesema Makonda.
Ameongeza kuwa badala ya kubezana, Watanzania wanapaswa kuendelea kuungana katika kuunga mkono timu za taifa na kuhamasisha ushiriki mkubwa zaidi wa mashabiki katika mashindano yajayo.
Makonda amesema mafanikio ya Serengeti Boys ni mafanikio ya Watanzania wote na kwamba safari ya maendeleo ya soka la Tanzania inaendelea.
📻Tusikilize Uvinza FM kupitia Masafa ya 96.5 Mhz UVINZA | KIGOMA | KASULU | BUHIGWE | KIBONDO | NGURUKA |KATAVI(Mlele) | TABORA(Kaliua&usinge)| Pia Online kupitia:- Radio Tadio, Online Radio Box, Radio Garden, Radio Zeno, Radioly. tafuta UVINZA FM au https://radiotadio.co.tz/uvinzafm/