Uvinza FM

Uvinza FM Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Uvinza FM, Radio Station, Nkwaza, Uvinza.

Uvinza FM is registered community radio with a VISION: To be a pioneer agent of positive social participation and income generating behaviour change in Uvinza and elsewhere in Lake Tanganyika Corridor Basin in Kigoma. And a MISSION:
To disseminate social and economic changes information through awareness creation news, drama, entertainment, talk shows discussions and speciality programs in education, health, agriculture, animal husbandry, entrepreneurship, sports and culture orientations.

03/06/2026

MAKONDA: MSIWABEZE MASHABIKI WALIOKWENDA

MOROCCO

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amewataka Watanzania kuacha kuwabeza mashabiki waliokwenda nchini Morocco kuishangilia Serengeti Boys, akisisitiza kuwa uwepo wao ulikuwa sehemu muhimu ya kuipa timu morali katika hatua ya fainali ya AFCON U-17.

Makonda amesema mashabiki ni mchezaji wa 12 uwanjani kwa kuwa uwepo wao huwapa wachezaji nguvu, hamasa na kujiamini wanapoiwakilisha nchi katika mashindano ya kimataifa.

"Hakuna timu inayokwenda mashindanoni bila mashabiki. Senegal na mataifa mengine yalikuwa na mamia ya mashabiki waliokwenda kuziunga mkono timu zao. Nasi tunapaswa kuthamini wale waliopata nafasi ya kwenda kuiwakilisha Tanzania na kuwapa nguvu vijana wetu," amesema Makonda.

Ameongeza kuwa badala ya kubezana, Watanzania wanapaswa kuendelea kuungana katika kuunga mkono timu za taifa na kuhamasisha ushiriki mkubwa zaidi wa mashabiki katika mashindano yajayo.

Makonda amesema mafanikio ya Serengeti Boys ni mafanikio ya Watanzania wote na kwamba safari ya maendeleo ya soka la Tanzania inaendelea.

📻Tusikilize Uvinza FM kupitia Masafa ya 96.5 Mhz UVINZA | KIGOMA | KASULU | BUHIGWE | KIBONDO | NGURUKA |KATAVI(Mlele) | TABORA(Kaliua&usinge)| Pia Online kupitia:- Radio Tadio, Online Radio Box, Radio Garden, Radio Zeno, Radioly. tafuta UVINZA FM au https://radiotadio.co.tz/uvinzafm/

03/06/2026

Dkt Samia:Ziara yangu Urusi ina umuhimu mkubwa kwa Watanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan amesema ziara yake ya siku tatu nchini Urusi ina umuhimu mkubwa kwa Tanzania na itaimarisha ushirikiano na Taifa hilo.

Dkt Samia ameeleza hayo leo Jumatano Juni 3, 2026 katika Ikulu ya Kremlin muda mfupi baada ya kukaribishwa na mwenyeji wake, Rais Vladimir Putin. Pamoja na mambo mengi ziara ya kiongozi jhuyo inalenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi baina ya mataifa hayo mawili.

Kwenye mazungumzo yake na Rais Putin, Dkt Samia amesema ziara k**a hiyo ya kitaifa mara ya mwisho ilifanywa na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1969.

“Ni historia kwangu mimi kuja Urusi kujadili masuala mbalimbali ya kimaendeleo kwa ajili ya Watanzania. Kwa niaba yangu na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nawasilisha salamu zao za upendo kwa mwaliko huu.”

‘Nataka tujadiliane kuhusu masuala mbalimbali, lakini kabla ya kuendelea mbele ningeipenda kuishukuru Urusi kwa mchango wake wa harakati za kupigania uhuru wa Afrika”

Dkt Samia aliwasili jjini Moscow Juni 2,2026 kufuatia mwaliko wa Rais Putin ambapo akiwa nchini humo, anatarajiwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Peoples’ Friendship.

📻Tusikilize Uvinza FM kupitia Masafa ya 96.5 Mhz UVINZA | KIGOMA | KASULU | BUHIGWE | KIBONDO | NGURUKA |KATAVI(Mlele) | TABORA(Kaliua&usinge)| Pia Online kupitia:- Radio Tadio, Online Radio Box, Radio Garden, Radio Zeno, Radioly. tafuta UVINZA FM au https://radiotadio.co.tz/uvinzafm/

03/06/2026

Rais Samia alivyopokewa na Rais Putin Ikulu ya Kremlin

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokutana na Rais wa Urusi katika Ikulu ya Kremlin Jijini Moscow, Urusi leo Jumatano Juni 03, 2026.

Dk. Samia yuko nchini Urusi kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Rais Putin, katika ziara inayolenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi pamoja na kukuza ushirikiano katika sekta za uwekezaji na biashara.

📻Tusikilize Uvinza FM kupitia Masafa ya 96.5 Mhz UVINZA | KIGOMA | KASULU | BUHIGWE | KIBONDO | NGURUKA |KATAVI(Mlele) | TABORA(Kaliua&usinge)| Pia Online kupitia:- Radio Tadio, Online Radio Box, Radio Garden, Radio Zeno, Radioly. tafuta UVINZA FM au https://radiotadio.co.tz/uvinzafm/

03/06/2026
02/06/2026

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam akiwa katika Big screen na wananchi.

02/06/2026

Fainali AFCON U17 ilivyotoa fursa ya mtoko, furaha kwa wananchi Dar

Imekuwa k**a mtoko wa sikukuu kwa familia mbalimbali jijini Dar es Salaam, baada ya Serikali kuandaa maeneo maalumu kwa wananchi kuangalia mechi ya fainali ya mataifa bingwa Afrika kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 17.

Katika maeneo mbalimbali ya Jiji hilo, Televisheni kubwa zimefungwa mitaani kutoa nafasi kwa wananchi kuangalia mechi hiyo ya fainali inayoihusisha timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17 ya Tanzania 'Serengeti Boys' dhidi ya Senegal.

Mbali na wananchi katika maeneo hayo, viongozi mbalimbali wa Serikali ngazi za Mikoa na Wilaya, wameshuhudiwa wakikusanyika sambamba na wananchi kufuatilia mechi hiyo, inayoiweka Tanzania katika ramani ya soka duniani.

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, alitoa ndege maalumu kuwabeba wachezaji na mashabiki kwa ajili ya kwenda kuishabikia timu hiyo ya vijana.

Hata hivyo, Dkt Samia pia alitoa Sh. milioni 500 k**a motisha kwa vijana hao, baada ya kufanikiwa kuingia hatua ya fainali ya michuano hiyo

Amani na utulivu umetawaka katika maeneo hayo, wananchi wakifuatilia mechi hiyo.

02/06/2026

Wananchi wamsifu Dkt Samia kwa uwekezaji kwenye michezo

Hatua ya Timu ya Taifa kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 kucheza fainali ya Mataifa Bingwa Afrika (AFCON U17), imewaibua wananchi, walioyahusisha mafanikio hayo na uwekezaji uliofanywa na Dkt Samia Suluhu Hassan katika michezo.

Wananchi hao wameeleza hayo leo, Jumanne Juni 2, 2026 walipofika katika maeneo mbalimbali kulikofungwa skrini kubwa kushuhudia mechi ya fainali kati ya Serengeti Boys dhidi ya Senegal

02/06/2026

Simai: Kuna Yuda Serikalini anakwamisha maendeleo

Mwandishi Wetu

Mbunge kupitia Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Simai Mohamed Said, amesema ndani ya Serikali kuna viongozi wanaomsaliti Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na kukwamisha maendeleo ya nchi.

Simai, ameijenga hoja yake hiyo akiwafananisha viongozi wasaliti na Yuda, huku akiwasihi waache kutumia majina ya viongozi wastaafu na kufanya siasa za 2030 mapema, jambo alilosema linalochonganisha na kuharibu utulivu.

Mbunge huyo, ameeleza hayo bungeni jijini Dodoma leo, Jumanne Juni 2, 2026 alipochangia hoja katika mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Fedha kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Amesema Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, anaongoza Serikali yake na Watanzania kwa upendo na mshik**ano, lakini kufanikiwa kwa Taifa wakati mwingine kuna watu wanaotembea kinyume.

“Leo nambatiza mmoja aliyekuwepo ndani ya Serikali, ni Yuda. Nasema hivyo kwanini, sisi tunataka maendeleo ya nchi yetu, kosa la mama (Dkt Samia) ni wapi? Kwa sababu ya kumuamini mtu kumbe ni Yuda,” amehoji.

Amesisitiza kiongozi huyo msaliti ameibuka hadi katika nyumba za ibada akitafuta huruma za watu na kutumia majina ya viongozi wastaafu ilimradi aonyeshe anapendwa.

Amesema tayari ameshawaumiza wengi, wengine walikuwa mbele na sasa wako nyuma, wako wafanyabiashara, watendaji ndani ya Serikali, wengine walikatwakatwa na wameathirika na wana msongo wa mawazo.

“Lakini Yuda tumeanza kumuona anaibuka katika nyumba za ibada kutafuta huruma ya wananchi na makundi mbalimbali, lakini nataka niseme, wabunge wenzangu na Serikali tuamkeni.

Amesema waliompenda hayati Magufuli wanajulikana na hadi sasa wapo, hivyo kiongozi huyo aliyefariki dunia Machi 21, 2021 aachwe apumzike kwa amani kwa kuwa alifanya kazi nzuri.

Ametaka ujengwe uchumi imara, mawaziri wasimame vema, washauri wa Rais Dkt Samia waifanye kazi yao vizuri bila kuathiriwa na huyo aliyemwita Yuda.

📻Tusikilize Uvinza FM kupitia Masafa ya 96.5 Mhz UVINZA | KIGOMA | KASULU | BUHIGWE | KIBONDO | NGURUKA |KATAVI(Mlele) | TABORA(Kaliua&usinge)| Pia Online kupitia:- Radio Tadio, Online Radio Box, Radio Garden, Radio Zeno, Radioly. tafuta UVINZA FM au https://radiotadio.co.tz/uvinzafm/

31/05/2026

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Magharibi, , amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimepoteza dira na malengo ya msingi yaliyopelekea kuanzishwa kwake, akidai kuwa kimeshindwa kuwainua wananchi kiuchumi kupitia sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, biashara na ajira.

Matata ametoa kauli hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Kasulu mkoani Kigoma, uliowakutanisha wananchi pamoja na viongozi mbalimbali wa CHADEMA kutoka wilaya tofauti za mkoa huo.

Katika hotuba yake, amesema wakulima bado wanakabiliwa na changamoto kubwa za upatikanaji wa masoko, pembejeo na bei zisizo na tija, huku wafanyakazi na wafanyabiashara wadogo wakidaiwa kuendelea kuathirika na mazingira magumu ya uchumi.

Aidha, amewataka wananchi kuendelea kushiriki katika mijadala ya kisiasa na kufanya maamuzi yatakayochochea maendeleo pamoja na uwajibikaji wa viongozi kwa manufaa ya taifa.

📻Tusikilize Uvinza FM kupitia Masafa ya 96.5 Mhz UVINZA | KIGOMA | KASULU | BUHIGWE | KIBONDO | NGURUKA |KATAVI(Mlele) | TABORA(Kaliua&usinge)| Pia Online kupitia:- Radio Tadio, Online Radio Box, Radio Garden, Radio Zeno, Radioly. tafuta UVINZA FM au https://radiotadio.co.tz/uvinzafm/

Address

Nkwaza
Uvinza
P.OBOX31

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uvinza FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Uvinza FM:

Share

Category