Uvinza FM

Uvinza FM Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Uvinza FM, Radio Station, Nkwaza, Uvinza.

Uvinza FM is registered community radio with a VISION: To be a pioneer agent of positive social participation and income generating behaviour change in Uvinza and elsewhere in Lake Tanganyika Corridor Basin in Kigoma. And a MISSION:
To disseminate social and economic changes information through awareness creation news, drama, entertainment, talk shows discussions and speciality programs in education, health, agriculture, animal husbandry, entrepreneurship, sports and culture orientations.

 : Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Maw...
24/12/2025

: Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, amewatakiwa watanzania wote Heri ya Christmas

"Tusherehekee sikukuu hii kwa Amani, upendo ma UTULIVU tukidumisha mshik**ano wa kitaifa"




24/12/2025

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi SACP S. Jongo, amawatakia wanageita heri ya Christmas na Mwaka mpya, huku akiwahikikishia usalama kwamba hakuna maandamano wala vurugu mkoani Geita, wahakikishe wanawalinda watoto wasiache watembee peke yao

24/12/2025

: Na Ezra Lonka

Kufatia changamoto ya wazazi kutoa adhabu kali kwa watoto na baadhi ya adhabu hizo kupekea vifo kwa watoto na kusababisha madhara makubwa ya kimaendeleo kwa jamiii na Taifa

Afisa Maendeleo ya Jamii Mratibu Dawati la Maendeleo ya Mtoto kutoka Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma Bi Sharifa Masudi amewataka wazazi na walezi kutotumia adhabu ya kipigo kizito kwa watoto wanapofanya makosa mbali mbali ya kimaadili katika familia

Ametoa wito huo leo terehe 24 Desemba 2025 akizungumza na Uvinza FM Bi Sharifa amesema, unaweza kumuadhibu mtoto kwa namna nyepesi hata kwa kumpa kazi ya kufanya ambayo ataifanya k**a adhabu wakati huo huo akijifunza na kazi za kijamii ili kumjengea uwezo katika makuzi yake

"Wazazi tusiache kuzungumza na watoto, kwamba mwanangu mimi pamoja na hali duni hii lakini sijawahi kuchukua kitu cha mtu wala kuiba, kwa hiyo katika maisha yako hakikisha hauchukii vitu vya watu ili kumjenga mtoto asishiriki matengo mabaya" Sharifa

Aidha, amewakumbusha wazazi wote na walezi kwamba kipigo hakijawahi kuwa njia sahihi ya kurekebisha tabia za mtoto, k**a mzazi au mlezi usikatae unapopewa taarifa za mtoto kuhusu uharifu, zichunguze, ongea na mtoto wako, timiza wajibu wako kwa kumlea mtoto kwa maadili mema ya kitanzania



24/12/2025

: Na Ezra Lonka

Afisa TAKUKURU wilaya ya Uvinza Ndg. Ibrahim Mtangoo amewataka wananchi wa Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma kushiriki Katika miradi ya maendeleo, kushiriki Katika Kutengeneza bajeti na kusimamia kwa uwazi na ukweli miradi hiyo ili kuhakikisha lengo la serikali linatekelezeka

Ametoa wito huo akizungumza na Uvinza FM leo tarehe 24 Desemba 2025, ambapo amesema Rushwa imekuwa ikikwamisha maendeleo na Kutengeneza migogoro katika jamiii katika sekta mbali mbali

Mtangoo amesema, katika miradi mbali mbali vitendo vya Rushwa vimekuwa vikifanyika na watu hawatoi taarifa jambo linalokwamisha maendeleo na kusababisha serikali kuongeza pesa baada ya pesa za awali kutokutumika vizuri au kubadhirishwa

Aidha, amewaasa wananchi kuwa msitari wa mbele kukemea vitendo vya Rushwa na kutoa taarifa kwa mamlaka husika pindi mtu anapoona vitendo au viashiria vya Rushwa

Kwa upande mwingine, Afisa Mtangoo, amewataka wananchi kupiga namba: 0738 150 109 ofisi ya TAKUKURU wilaya ya Uvinza, kutoka taarifa kuhusu vitendo na Rushwa, pia unaweza kupiga namba 113 makao makuu ya TAKUKURU Dodoma bure
tz

24/12/2025

: Afisa TAKUKURU Wilaya ya Uvinza Ndg. Ibrahim Mtangoo
tz

24/12/2025

: Afisa TAKUKURU Wilaya ya Uvinza Ndg. Ibrahim Mtangoo
tz

24/12/2025

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Katibu Tawala mkoa wa Kigoma Mh. Hassan Rugwa amewatakia wanakigoma na Watanzania wote kwa ujumla Heri ya Christmas na mwaka, sambamba na kuwahakikishia usalama Kuelekea sikukuu



24/12/2025

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi SACP Filemon Makungu amewatikia wanakigoma Heri ya Christmas na mwaka mpya na kuwakumbusha kutii sheria bila shuruti
tanzania

23/12/2025

Christmas and Happy New Yeah: na Ezra Meshack

23/12/2025

: Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana Mh. Joel Arthur Nanauka, akizungumza na waandishi wa Habari Desemba 23 Jijini Dar Es Salaam kuhusu mipango ya Serikali kwa maendeleo ya vijana

23/12/2025

: Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana Mh. Joel Arthur Nanauka, akizungumza na waandishi wa Habari Desemba 23 Jijini Dar Es Salaam kuhusu mipango ya Serikali kwa maendeleo ya vijana


Address

Nkwaza
Uvinza
P.OBOX31

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uvinza FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Uvinza FM:

Share

Category