Uvinza FM

Uvinza FM Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Uvinza FM, Radio Station, Nkwaza, Uvinza.

Uvinza FM is registered community radio with a VISION: To be a pioneer agent of positive social participation and income generating behaviour change in Uvinza and elsewhere in Lake Tanganyika Corridor Basin in Kigoma. And a MISSION:
To disseminate social and economic changes information through awareness creation news, drama, entertainment, talk shows discussions and speciality programs in education, health, agriculture, animal husbandry, entrepreneurship, sports and culture orientations.

Tunakukaribisha sana 🙏🏽       #96.5MHz
02/07/2025

Tunakukaribisha sana 🙏🏽




#96.5MHz

Tuungane kumtakia Mzee wetu pendwa  heri ya siku ya mfanano wa kuzaliwa. Tunakutakia maisha marefu yenye afya, furaha na...
06/05/2025

Tuungane kumtakia Mzee wetu pendwa heri ya siku ya mfanano wa kuzaliwa. Tunakutakia maisha marefu yenye afya, furaha na amani , Ubarikiwe sana 🤲🏼

Tunawatakia Heri ya Pasaka kwa wote wanaosheherekea🙏🏽
20/04/2025

Tunawatakia Heri ya Pasaka kwa wote wanaosheherekea🙏🏽

   ✝️
18/04/2025

✝️

Tunawatakia wote wanaosheherekea Eid Mubarak ✨️🌙
30/03/2025

Tunawatakia wote wanaosheherekea Eid Mubarak ✨️🌙

KAMPENI YA UGAWAJI WA VYANDARUA BURE NGAZI YA KAYA YAANZAWizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI imezi...
14/03/2025

KAMPENI YA UGAWAJI WA VYANDARUA BURE NGAZI YA KAYA YAANZA

Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI imezindua kampeni ya ugawaji wa vyandarua kwa kaya bila malipo ili kupambana na ugonjwa wa malaria. Kampeini hii, inayosimamiwa na Mpango wa Taifa wa Udhibiti wa Malaria, inalenga kuhakikisha kila kaya inapata vyandarua ili kulinda wananchi dhidi ya mbu wanaosababisha malaria.

Katika uzinduzi wa mafunzo ya utekelezaji wa kampeni hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Uvinza, Bi. Dinnah Mathamani, Ambae amekuwa mgeni rasmi katika warsha hiyo amesema kuwa vyandarua vipatavyo laki mbili sitini na mbili elfu mia tatu thelathini na saba vitagaiwa katika Wilaya ya Uvinza.

Licha ya mafanikio yaliyopatikana katika kupunguza visa vya malaria, bado kuna changamoto ya baadhi ya wananchi hutumia dawa za malaria bila kufuata maelekezo ya wataalamu wa afya. Hali hii inasababisha usugu wa vimelea vya malaria dhidi ya dawa, jambo linalohatarisha mafanikio yaliyopatikana katika vita dhidi ya ugonjwa huo.

Amesisitiza umuhimu wa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi ya vyandarua. Ameeleza kuwa licha ya jitihada kubwa zinazofanywa, bado changamoto kubwa ni matumizi mabaya ya vyandarua, ambapo baadhi ya watu hutumia kwa shughuli zisizokusudiwa badala ya kujikinga na mbu.

Takwimu za hivi karibuni zinaonesha kuwa malaria bado ni changamoto kubwa ya kiafya duniani, hasa barani Afrika. Kwa mujibu wa ripoti ya WHO ya mwaka 2024, idadi ya wagonjwa wa malaria iliongezeka kwa milioni 11, kutoka wagonjwa milioni 249 mwaka 2022 hadi milioni 263 mwaka 2023. Tanzania pekee ilirekodi wagonjwa takribani 8,555,000. Vifo vilivyotokana na malaria vilipungua kutoka 608,000 mwaka 2022 hadi 597,000 mwaka 2023.

Nae Afisa Mtendaji wa Mpango wa Taifa wa Udhibiti wa Malaria, Winfred Mwafongo, amesema kampeni hii inalenga kupunguza maambukizi ya malaria kwa kuhakikisha kila familia inapata kinga bora. Ameeleza kuwa vyandarua vinavyotolewa ni muhimu vitumike ipasavyo ili kufanikisha malengo ya kampeni.

Pia ameongeza na kusema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizopo katika nafasi sita za juu kwa nchi zenye maambukizi ya ugonjwa wa malaria hivyo Wananchi wanatakiwa kushiriki kikamilifu.

Uvinza Fm inakutakia kheri ya siku yako ya kuzaliwa Linda Dismas, mtangazaji wa Uvinza Fm.
12/03/2025

Uvinza Fm inakutakia kheri ya siku yako ya kuzaliwa Linda Dismas, mtangazaji wa Uvinza Fm.

“Uvinza FM inawatakia wanawake wote furaha na mafanikio tele katika Siku ya Wanawake Duniani! 💐 Tufurahie pamoja, tukumb...
08/03/2025

“Uvinza FM inawatakia wanawake wote furaha na mafanikio tele katika Siku ya Wanawake Duniani! 💐 Tufurahie pamoja, tukumbuke na kuenzi mchango wa wanawake kila siku. ”

Ikiwa ni kilele cha siku kuu ya Wanawake Duniani leo tarehe 8 Marchi, 2025 Wananchi mkoani Kigoma wamehimizwa kutumia fu...
08/03/2025

Ikiwa ni kilele cha siku kuu ya Wanawake Duniani leo tarehe 8 Marchi, 2025 Wananchi mkoani Kigoma wamehimizwa kutumia furusa zinazotolewa na serikali kujikwamua kiuchumi

Hayo yamethibitishwa na Afisa mtendajo kata ya Uvinza Bw. Edward Amos Nkanga na baadhi ya Wanawake wa wilaya ya Uvinza waliokuwa wakizungumza na Uvinza FM radio ambapo walimaliza kwa kuiimba kauli mbiu ya mwaka huu “WANAWAKE NA WASICHANA: TUIMALISHE HAKI, USAWA NA UWEZESHWAJI”

Hakika imekuwa siku ya furaha sana kwa watanzania wote kuungana na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika jitihada za kumuinua mwanamke na msichana kumfanya ajiamini na kutenda kwa weredi hasa katika shughuli za kiuchumi

Siku ya jana tulipata nafasi, kutembelea Chuo cha Ujjiji Broadcast Academy, k**a sehemu ya kujenga mahusiano imara na ku...
06/03/2025

Siku ya jana tulipata nafasi, kutembelea Chuo cha Ujjiji Broadcast Academy, k**a sehemu ya kujenga mahusiano imara na kufanya ushirikiano wa kudumu na jamii yetu. K**a tunaamini katika nguvu ya habari na mawasiliano kuleta mabadiliko chanya! Tunayo furaha kushirikiana na vyuo k**a hivi ili kuimarisha ufanisi na maendeleo ya kijamii. ”

Uvinza Fm Radio Tunawatakia Heri yaJumatano ya Majivu na siku 40 za   kwa wakristo wote Wanaoanza Mfungo Siku ya Leo🙏🏾
05/03/2025

Uvinza Fm Radio Tunawatakia Heri ya
Jumatano ya Majivu na siku 40 za kwa wakristo wote Wanaoanza Mfungo Siku ya Leo🙏🏾

Tunawatakia kila la heri wasikilizaji wetu wanaofunga katika Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan 🤲🏼       ✨️
01/03/2025

Tunawatakia kila la heri wasikilizaji wetu wanaofunga katika Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan 🤲🏼 ✨️

Address

Nkwaza
Uvinza
P.OBOX31

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uvinza FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Uvinza FM:

Share

Category