TAMU FM

TAMU FM Tamu FM – Vipindi vya kujenga jamii, vijana & amani. Matangazo na ushirikiano: +255 690 000 128 | www.tamufm.com | [email protected]

09/06/2026

*Miradi ya Singapore Tanzania yazalisha ajira 3,000*

Shirikisho la Biashara la Singapore (SBF) limezitaka sekta binafsi za Tanzania na Singapore kutumia ushirikiano wa kisiasa uliopo kuibua fursa za biashara na uwekezaji katika soko la Tanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Makamu Mwenyekiti wa SBF, Mark Lee, amesema lengo ni kugeuza mahusiano mazuri ya kisiasa kuwa matokeo ya kibiashara yenye manufaa kwa pande zote.
Tangu mwaka 1997, Singapore imewekeza miradi 36 nchini Tanzania yenye thamani ya zaidi ya dola milioni 500 na kuzalisha ajira zaidi ya 3,000.
Ujio wa ujumbe wa kampuni 15 kutoka Singapore unatazamwa k**a hatua ya mwanzo kuelekea ushirikiano zaidi katika sekta za miundombinu ya viwanda, usafirishaji na ugavi, biashara ya bidhaa, kilimo, na huduma za teknolojia.
Lee amesisitiza kuwa lengo si kuvuna faida pekee, bali kushirikiana kujenga uchumi wa pande zote.
Ushirikiano huu unatarajiwa kuimarisha nafasi ya Tanzania k**a kitovu cha biashara na uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki, huku Singapore ikileta mtaji, teknolojia na utaalamu wa kisasa.

09/06/2026

*TPSF: Tanzania inakua kwa kasi*
Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) imesema uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, ukichochewa na maboresho ya sera na mazingira bora ya uwekezaji.
Akizungumza katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Singapore, Mwenyekiti wa TPSF, Angelina Ngalula, amesema Tanzania ina fursa nyingi kwa Singapore kuleta mtaji, teknolojia na utaalamu, hususan katika sekta za teknolojia, huduma za kifedha, usafirishaji, ugavi, na nishati.
Angelina amesisitiza kuwa ingawa serikali huweka mazingira rafiki ya biashara, sekta binafsi ndizo zinazopaswa kutumia fursa hizo kuzalisha bidhaa na kukuza uchumi.
Ameongeza kuwa majukwaa ya ushirikiano kati ya serikali, k**a vile tume za pamoja na mabaraza ya biashara, husaidia kuweka mifumo na makubaliano, lakini biashara halisi hutegemea hatua za kampuni binafsi.
Ushirikiano huu unaonekana kuwa na nafasi kubwa ya kuimarisha diplomasia ya uchumi, mkakati wa Tanzania wa kuvutia uwekezaji na teknolojia mpya.
Aidha, sekta binafsi inatajwa kuwa injini ya ukuaji wa uchumi, ikihimiza ubunifu na ushindani wa kimataifa.
Kwa kuzingatia kasi ya ukuaji wa uchumi na mageuzi ya sera, Tanzania inajipanga kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki.

09/06/2026

*TPSF: Tanzania inakua kwa kasi*
Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) imesema uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, ukichochewa na maboresho ya sera na mazingira bora ya uwekezaji.
Akizungumza katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Singapore, Mwenyekiti wa TPSF, Angelina Ngalula, amesema Tanzania ina fursa nyingi kwa Singapore kuleta mtaji, teknolojia na utaalamu, hususan katika sekta za teknolojia, huduma za kifedha, usafirishaji, ugavi, na nishati.
Angelina amesisitiza kuwa ingawa serikali huweka mazingira rafiki ya biashara, sekta binafsi ndizo zinazopaswa kutumia fursa hizo kuzalisha bidhaa na kukuza uchumi.
Ameongeza kuwa majukwaa ya ushirikiano kati ya serikali, k**a vile tume za pamoja na mabaraza ya biashara, husaidia kuweka mifumo na makubaliano, lakini biashara halisi hutegemea hatua za kampuni binafsi.
Ushirikiano huu unaonekana kuwa na nafasi kubwa ya kuimarisha diplomasia ya uchumi, mkakati wa Tanzania wa kuvutia uwekezaji na teknolojia mpya.
Aidha, sekta binafsi inatajwa kuwa injini ya ukuaji wa uchumi, ikihimiza ubunifu na ushindani wa kimataifa.
Kwa kuzingatia kasi ya ukuaji wa uchumi na mageuzi ya sera, Tanzania inajipanga kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki..

09/06/2026

*Miaka 45 ya Tanzania na Singapore katika uchumi na diplomasia*
Tanzania na Singapore ni marafiki wa muda mrefu na mwaka huu wanasherehekea miaka 45 ya uhusiano wa kidiplomasia.

Uhusiano huu si wa kihistoria pekee, bali pia umejikita katika ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo ya kijamii.

Kwa sasa, Singapore imewekeza miradi 36 nchini Tanzania yenye thamani ya Dola milioni 535.13 za Marekani na imezalisha ajira 3,228 kwa Watanzania. Sekta zinazoguswa ni kilimo, usafirishaji, ujenzi, na rasilimali za asili.

Ziara ya siku tatu ya Rais wa Singapore, Tharman Shanmugaratnam, kwa mwaliko wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, inalenga kuimarisha zaidi maeneo ya ushirikiano.

Wakuu hao watajadili biashara na uwekezaji, maendeleo ya bandari na usafirishaji, uchumi wa kidijitali, elimu na mafunzo ya ujuzi, utalii, miundombinu, teknolojia na ubunifu, pamoja na maendeleo endelevu.

Uhusiano huu unatarajiwa kuendelea kuimarika, na kuleta fursa zaidi za uwekezaji, ajira, na maendeleo ya miundombinu. Kwa Watanzania, hii ni nafasi ya kushiriki katika uchumi wa kidijitali na kujiweka katika ramani ya kimataifa.

09/06/2026

*Rais Samia ampokea mgeni wake kutoka Singapore*
Rais wa Singapore, Tharman Shanmugaratnam, amewasili Ikulu ya Dar es Salaam na kupokelewa kwa heshima na mwenyeji wake, Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Mapokezi hayo yaliambatana na gwaride la heshima na mizinga 21 iliyopigwa, ikiwa ni ishara ya saluti kwa kiongozi huyo wa ngazi ya juu wa Singapore.

Ziara hiyo ni ya kihistoria na ya kwanza kufanywa na Rais wa Singapore nchini tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo, mwaka 1980.

Historia nyingine inayoandikwa katika ziara hiyo ni kwamba, inafanyika wakati ambao Tanzania na Singapore zinaadhimisha miaka 45 ya uhusiano wa kidiplomasia.

Rais Shanmugaratnam, anafanya ziara hiyo kwa siku tatu kuanzia Juni 8 hadi 10, mwaka huu. Ziara hiyo, inaendana na mkakati wa Tanzania wa kuimarisha diplomasia ya uchumi, ili kuvutia uwekezaji, teknolojia, masoko na utaalamu.

Katika ziara hiyo, maeneo kadhaa ya ushirikiano yatajadiliwa, ambayo ni biashara na uwekezaji, maendeleo ya bandari na usafirishaji, uchumi wa kidijitali, elimu na mafunzo ya ujuzi, utalii, miundombinu, teknolojia na ubunifu na maendeleo endelevu.

Mapokezi hayo, yamefanyika leo, Jumanne Juni 9, 2026, Ikulu jijini Dar es Salaam.

05/06/2026

*Putin: Tanzania ni kiungo muhimu kati ya Afrika Mashariki na masoko ya dunia*

Rais wa Urusi, Vladimir Putin, ameitaja Tanzania kuwa lango muhimu linalounganisha Afrika Mashariki na masoko ya dunia, akisisitiza kuwa nafasi ya nchi hiyo inaendelea kuwa ya kimkakati katika mfumo mpya wa uchumi wa dunia.

Akizungumza Juni 5 katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg (SPIEF) 2026, Putin amesema Tanzania ina nafasi inayofanana na ile ya Uzbekistan katika Asia ya Kati, kwa kuwa ni kiungo muhimu kinachounganisha uchumi wa kikanda na vituo vikubwa vya biashara duniani.

"Tanzania ina nafasi k**a hiyo katika Afrika Mashariki," amesema Putin wakati akizungumzia nchi ambazo nafasi zao za kijiografia na uhusiano wao wa kiuchumi zinazozifanya kuwa madaraja muhimu yanayounganisha maeneo mbalimbali ya dunia.

Ameeleza mataifa yanayoweza kuoanisha maendeleo yao ya ndani na mahusiano imara na vituo vipya vya ukuaji wa uchumi duniani yanazidi kuwa na umuhimu mkubwa kadiri mifumo ya biashara ya kimataifa inavyoendelea kubadilika.

Putin pia amegusia kile alichokitaja kuwa ni mabadiliko yanayoendelea katika mfumo wa biashara ya dunia, akisema biashara ya kimataifa inajiondoa katika misingi yake ya awali iliyowekwa chini ya Shirika la Biashara Duniani (WTO).

Kauli hizo zinakuja wakati Tanzania ikiendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika miundombinu ya usafirishaji, maendeleo ya bandari na kuimarisha mtandao wa biashara wa kikanda, hatua zinazozidi kuimarisha nafasi yake k**a lango kuu la biashara kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati.

05/06/2026

*Dkt Samia ataja siri Tanzania kuvutia uwekezaji, biashara*
Rais wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan ameeleza Tanzania ilivyojipanga katika uwekezaji na kuwavutia watu wa nje kuja kufanya biashara nchini.
Dkt Samia amesema kuanzia mwaka 2021 hadi sasa Tanzania imevutia miradi mingi hatua inayowezesha Taifa kuwa imara katika uchumi wake.
Ameeleza hayo leo, Ijumaa Juni 5, 2026 alipozungumza katika Jukwaa la 29 la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg (SPIEF 2026) nchini Urusi, alikokwenda kwa ziara ya siku tatu ya kikazi.
“Jambo jingine Tanzania ipo katikakati ya korido ya uchumi ya Afrika Mashariki, Afrika ya Kati na Bandari ya Dar es Salaam ndio inayohudumia mataifa mengine. Hatua hii peke yake inafanya Tanzania ivutie vitu vingi ndani ya nchi,”
“Kwa hiyo katika ile Kanda Tanzania ni kitovu muhimu na uchumi wake unakuwa kwa uimara kamwe hatutakosea hatua,” amesema mkuu huyo wa nchi.
Alipoulizwa anawezaje kuhimili uchumi na wakati yeye ni Rais mwanamke Dkt Samia amejibu “uchumi hautegemei jinsia ya mtu, bali unavyosimamia mipango ya nchi, iwe mwanaume au mwanamke unatakiwa uwe mikakati ya kuhimili uchumi, ndicho kinachotakiwa,”.

05/06/2026

*Dkt Samia aitangaza Tanzania katika jukwaa la dunia*

Rais Dk Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuiweka Tanzania kwenye ramani ya uchumi wa dunia, baada ya kushiriki Jukwaa la 29 la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg nchini Urusi.

Jukwaa hilo limewakutanisha zaidi ya washiriki 24,000 kutoka zaidi ya nchi 140, wakiwemo wakuu wa nchi, wawekezaji na viongozi wa makampuni makubwa duniani.

Kupitia ushiriki huo, Tanzania imepata fursa ya kutangaza vivutio vyake vya uwekezaji katika sekta za madini, nishati, utalii, kilimo na usafirishaji.

Hatua hiyo inaendelea kuimarisha nafasi ya Tanzania k**a kitovu cha biashara na uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki.

05/06/2026

Fun time

05/06/2026

Address

Zanzibar
Zanzibar City
71800

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAMU FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category