TAMU FM

TAMU FM TAMU FM
TAMU TV
TAMU MEDIA
C.E.O Mr_Honest

02/12/2025

Rais Samia: Vurugu zililenga kuipindua nchi

Rais Samia Suluhu Hassan amesema vurugu za Oktoba 29, zilipangwa, kugharimiwa na kuratibiwa na watu kutoka nje wakishirikiana na wa ndani, kwa lengo la kupindua nchi.

“Lile lilikuwa ni jambo la kupangwa na vurugu zile zilidhamiria makubwa. Vurugu zile ni mradi wenye nia ovu wenye wafadhili, wash*tiri na watekelezaji,” amesema.

Amesema vurugu hizo zilizoratibiwa na watu kutoka ndani na nje ya nchi, kati yao wapo wanaojulikana na wasiojulikana, hivyo Serikali inawatafuta ili kuwajua.

Ametaja baadhi ya sababu za kutaka kuipindua nchi, ni ushindani wa Tanzania kibiashara na utajiri mkubwa wa rasilimali, ikiwemo madini adimu.

Pamoja na hayo, Rais Samia amesema wapo walioingia kwa kufuata mkumbo kwa ahadi ya maisha mazuri baadaye.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo, Jumanne Desemba 2, 2025 katika hotuba yake kwa Taifa, wakati wa kikao chake na wazee wa Jiji la Dar es Salaam.

02/12/2025

Rais Samia: Nyinyi ni nani? Msitupangie!
Rais Samia Suluhu Hasana amesema Tanzania ni nchi huru haitakubali kupangiwa namna ya kufanya mambo yake na mataifa mengine kwa kisingizio cha misaada au kitu kingine chochote kile, badala yake itaamua mambo yake kadiri ya mahitaji ya watu wake.
Akiongea na wazee wa Dar es Salaam, Desemba 02, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere Rais Samia alisema baadhi ya mataifa wamekuwa wakiunga mkono madai yasiyokuwa na msingi ya baadahi ya vyama vya siasa kwa malengo ya kuivuruga nchi.
Alisema baadhi vya vyama vya siasa vilijitoa vyenyewe kwenye Uchaguzi Mkuu, kwa kuogopa kushindwa na sasa wanatafuta visingizio kwa kusaidiwa na kufadhiliwa na watu wa nje.
“Katika ile aibu ya kuepuka kushindwa uchaguzi wanaweka visingizio. Visingizio vyote hivi vinaungwa mkono na nje (mataifa ya nje) hawana hata aibu, nje huko wanakaa wanasema Tanzania ifanye moja, ifanye mbili, ifanye tatu, halafu ndiyo itakuwa hivi, who are you?,” alihoji Rais Samia.
“Niwaulize ndugu zangu, kwao hayatokei? Tumenyanyua sauti kusema ya kwao? Wanadhania bado wao ni wakoloni kwetu? Kitu gani? ni fedha chache wanzotugawia, na fedha yenyewe sasa haipo, tunafanya biashara ili wao wapate na sisi tupate ndipo tunaposimamia.”
Alisema Tanzania ni k**a mwanake mzuri ambaye anapiganiwa na wanaume wawili na kwamba siasa ya kutofungamana na upande wowote ambayo haibagua mtu wa kushirikiana naye ndiyo inayowasumbua kwa kuwa kila mtu anavuta upande wake.
Aliwataka watanzania kutambua kuwa nchi ina utajiri mwingi wa rasilimali na hizo zimekuwa chanzo cha chokochoko za mataifa ya nje na hivyo kuwataka kushik**ana, kuwa imara na kulilinda taifa lao.

02/12/2025

Dkt Samia: Nguvu tulioitumia imeendana na vurugu zilizotokea

Rais Samia Suluhu Hassan amesema nguvu iliyotumika na Serikali kudhibiti vurugu, iliendana na ukubwa wa tukio lenyewe na kwamba ameapa kuilinda nchi, mipaka yake na usalama wa raia wake.

Ilivyofanywa na Serikali siku hiyo, amesema ndivyo inavyofanyika katika mataifa mbalimbali kunapotokea tukio la vurugu zinazotishia usalama wa raia na Taifa kwa ujumla.

Rais Samia ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam leo, Jumanne Desemba 2, 2025 alipozungumza katika kikao chake na wazee wa jiji hilo.

“Sasa tunapoambiwa kwamba tulitumia nguvu kubwa sana kwenye tukio lile, nguvu ndogo ilikuwa ni ipi? Ilikuwa tuwaangalie waandamanaji waliojiandaa kufanya mapinduzi mpaka wafanikiwe? Hapo patakuwa pana dola kweli, dola haipo hivyo,” amesema.

Rais Samia amesema jambo k**a hilo, limeshuhudiwa pia katika maeneo mengine mengi, panapotokea vurugu k**a hizo, Serikali hutumia nguvu kubwa kudhibiti.

02/12/2025

*Dkt Samia: Viongozi wa dini, kaeni kwenye mstari wenu*

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi wa dini kuacha kujivika majoho ya kuendesha nchi kwa utashi wao binafsi, bali Tanzania itaongozwa kwa Katiba.
Ameeleza kuwa Tanzania haitendeshwa kwa madhehebu ya dini bali kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais Dkt Samia ameeleza hayo leo, Jumanne Disemba 2, 2025 akihutubia Taifa katika mkutano wa Rais Samia Suluhu Hassan na wazee wa Jiji la Dar es Salaam.
“Ubora wa dini upo mioyoni mwetu, hakuna overriding hapa...Kwamba mimi dini yangu, nitaoveriding Tanzania, nikilitoa ndio hilohilo...,”
“Toka nimekaa matamko nane yametolewa na TEC, lakini ukienda chini wenyewe kwa wenyewe wanapingana, matamko hayafanyi kazi vizuri,”
Amesema Tanzania ni nchi ya umoja, mshik**ano ndio ngao, akiwataka Watanzania kutokubali kuvurugana kwa misingi ya dini na kisiasa, hata k**a aliyeopo madarakani haumpendi.
“Kama haumpendi anayeongoza mvumilie tu...mioyo yote imeumb

02/12/2025

*Dkt Samia: Vijana walioingia barabarani, walitumwa na kuimbishwa mambo yasiyowahusu*

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan, amesema vijana waliongia barabarani Oktoba 29, 2025 walitumwa kufanya mambo yasiyowahusu na sio sababu ya ugumu wa maisha k**a wanavyodai.
Mkuu huyo wa nchi, amefafanua kuwa vijana hao waliingia njia na kuimbishwa wimbo wasioujua, wanadai haki, je haki gani?
“Ebu avutwe tu kijana aambiwe anadai haki je haki gani? Hiyo haki hawakuweza kuitafuta kwa njia nyingine hadi kuingia barabarani kufanya vurugu... kuchomwa vituo...,” amesema Dkt Samia.
Rais Dkt Samia ameeleza hayo leo, Jumanne Desemba 2, 2025 akihutubia Taifa katika mkutano wa Rais Samia Suluhu Hassan na wazee wa Jiji la Dar es Salaam.
“Ningekuwa na uwezo ningebeba vijana wa Kitanzania nikawapeleka nchi tofauti hapa Afrika, pamoja na majirani zetu wakaone ugumu wa maisha uliokuwepo, halafu wasema Tanzania ni mahali pema,”
“Hawana sababu, ugumu wa maisha kwa raha zake anaingia njia kuimba huo ugumu wa maisha? Mwenye ugumu wa maisha anaingaika kutafuta chakula chake, hawa wengine hawakuwa na ugumu wa maisha walikuwa na sababu zao,”
Dkt Samia amewataka vijana wa Kitanzania kutomezeshwa mambo na wao wakayameza badala ya kuyachuja.

02/12/2025
Jaji Chande: Tutafanya uchunguzi huru na kamilifuTume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani baada ya Uchaguzi, im...
01/12/2025

Jaji Chande: Tutafanya uchunguzi huru na kamilifu

Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani baada ya Uchaguzi, imesema itafanya kazi yake kwa weledi na kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu yeyote na kwa viwango kwa sababu kazi yao inatazamwa na watu wengi wa ndani na nje yan chi.

Akiongea na waandishi wa habari jinni Dar es Salaam Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji mstaafu Mohamed Othman Chande, amesema tume hiyo itafanya kazi yake kwa uhuru. Akieleza kuwa hata kabla ya kuanza kazi wao wenyewe wamejiangalia na kutathmini watanzania wanataka nini.

“Tumebaini watu wanataka uchunguzi kamilifu, usifanyike nusunusu, wanataka uwazi kwenye kazi na k**a utachukuliwa ushahidi uwe utakaotumika sio ambao hauwezi kutumika,” alieleza Jajic Chande.

Alisema kuwa yako mambo sita ambayo watayafanyia kazi kuwa ni pamoja na kuchuguza na kubaini chanzo halisi cha yaliyotokea, malengo yaliyokusudiwa na waliopanga kutekeleza vitendo hivyo, madhara yaliyojitokeza ikiwemo vifo, majeruhi, uharibifu wa mali na hasara za kiuchumi zilizojitokeza.

Masuala mengine ni kuangalia mazingira na hatua mbali mbali zilizochukuliwa na serikali na vyombo vyake, kupendekeza maeneo yahayohitaji kuimarishwa zaidi kuongeza uwajibikaji wa viongozi na raia ili kulinda usalama na utawala bora, utawala wa sheria, haki za binadamu na mfumo madhubuti wa majadiliano ya kisiasa na kijamii hadi kufikia maridhiano na kuhakikisha vurugu hizi hazijirudii tena.

Aliogeza kuwa katika hadidu hizo za rejea wamepewa nafasi ya kuchunguza jambo lolote ambalo tume itaona kuwa ni muhimu na linaendana na majkumu ya tume na kwamba wakiona jambo la iana hiyo hawatahitaji kibali cha mtu kulifanyia kazi.

Amesema tume k**a hizo huwa na mwenendo wa kimahak**a kwani mtu anapotoa ushahidi anaapa ili baadaye utumike.

Pia, amesema tume hizo huwa huru kuandaa taratibu zake na hazifuati ufundi k**a ilivyo katika mahak**a na ina mamlaka ya kutoa wito.

“Pamoja na tume kuomba ushirikiano, lakini ina mamlaka ya kushurutisha ushirikiano, lakini sisi hatwendi huko,” amesema Jaji Chande.

Katika ujtekelezaji wa shughuli zao, amesema watatumia njia za mapitio ya uchambuzi wa nyaraka mbalimbali, mahojiano ya ana kwa ana na kwa njia ya mt

Mabalozi wasisitiza dhamira ya kuimarisha ushirikiano na Tanzania*Mabalozi wanaowakilisha mataifa na taasisi za kimataif...
28/11/2025

Mabalozi wasisitiza dhamira ya kuimarisha ushirikiano na Tanzania*

Mabalozi wanaowakilisha mataifa na taasisi za kimataifa nchini, wamethibitisha kwa kauli moja dhamira yao ya kuendeleza ushirikiano na Serikali ya Tanzania katika nyanja mbalimbali zikiwemo za kiuchumi.

Hayo yamejiri leo, Ijumaa Novemba 28, 2025 katika Mkutano wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo na Jumuiya ya Wanadiplomasia wanaowakilisha mataifa na taasisi mbalimbali nchini.

Wanadiplomasia hao, wamesema wanaiona Tanzania k**a mshirika muhimu, imara na wa kuaminika katika diplomasia ya kikanda na kimataifa.

Pia, wamesema wametambua juhudi zinazofanywa na Serikali kurejesha umoja wa Taifa baada ya matukio ya Oktoba 29, na wametoa pongezi kwa hatua zinazoendelea kuchukuliwa ili kuimarisha amani, utawala bora na ustahimilivu wa kitaifa.

Akizungumza katika mkutano huo, Balozi Kombo amewahakikishia mabalozi hao kuwa, Tanzania itaendeleza ushirikiano wa manufaa kwa pande zote.

Ametumia fursa hiyo kuwapa taarifa kuhusu mwenendo wa uchaguzi mkuu, matukio yaliyojitokeza baadaye na hatua ambazo Serikali imechukua ikiwemo kulinda maisha na mali za wananchi, kurejesha utulivu na kuendeleza huduma za kijamii na uchumi bila kusuasua

.

Address

Zanzibar
Zanzibar City
71800

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAMU FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category