09/06/2026
*Miradi ya Singapore Tanzania yazalisha ajira 3,000*
Shirikisho la Biashara la Singapore (SBF) limezitaka sekta binafsi za Tanzania na Singapore kutumia ushirikiano wa kisiasa uliopo kuibua fursa za biashara na uwekezaji katika soko la Tanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Makamu Mwenyekiti wa SBF, Mark Lee, amesema lengo ni kugeuza mahusiano mazuri ya kisiasa kuwa matokeo ya kibiashara yenye manufaa kwa pande zote.
Tangu mwaka 1997, Singapore imewekeza miradi 36 nchini Tanzania yenye thamani ya zaidi ya dola milioni 500 na kuzalisha ajira zaidi ya 3,000.
Ujio wa ujumbe wa kampuni 15 kutoka Singapore unatazamwa k**a hatua ya mwanzo kuelekea ushirikiano zaidi katika sekta za miundombinu ya viwanda, usafirishaji na ugavi, biashara ya bidhaa, kilimo, na huduma za teknolojia.
Lee amesisitiza kuwa lengo si kuvuna faida pekee, bali kushirikiana kujenga uchumi wa pande zote.
Ushirikiano huu unatarajiwa kuimarisha nafasi ya Tanzania k**a kitovu cha biashara na uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki, huku Singapore ikileta mtaji, teknolojia na utaalamu wa kisasa.