Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Ukurasa rasmi wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga Kushirikiana na Serikali ya Oman katika uwekezaji wa mazao ya viungo, hayo ...
11/09/2025

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga Kushirikiana na Serikali ya Oman katika uwekezaji wa mazao ya viungo, hayo yemebainishwa katika ujumbe wa wafanyabiashara wa Oman waliopo Zanzibar kwa ziara ya kibiashara na uwekezaji katika Mkutano uliofanyika Ukumbi wa ZURA ambapo Wizara ya Biashara na Maendelep ya Viwanda na Wizara ya nchi,Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, waliratibu ujio huo.

Katika mkutano huo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Mhe. Shariff Ali Sharif, alisema majadiliano ya uwekezaji yanafanyika kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na nchi mbalimbali katika kuchochea ukuwaji wa Uchumi na kuleta Maendeleo endelevu.

Viongozi Mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar akiwemo Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda ndugu. Fatma Mabrouk Khamis, Vingozi wa Sekta Binafsi na wazalishaji walishiriki mkutono huo.
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
Ikulu habari Zanzibar
ZNCC
Baraza BLRC

karibu Zanzibar   katika Ugeni wa Oman, atakuwepo Dr. Salem Al- Junaibi, Mkuu wa ujumbe wa Wafanyabiashara wa Oman. Nyot...
09/09/2025

karibu Zanzibar katika Ugeni wa Oman, atakuwepo Dr. Salem Al- Junaibi, Mkuu wa ujumbe wa Wafanyabiashara wa Oman. Nyote Mnakaribisha Katika Ukumbi wa ZURA saa 4:00 kamili asubuhi.
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
Baraza BLRC
Zanzibar Fair Competition Commission

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti Utoaji wa Leseni Zanzibar (BLRA) Dkt. Halima Jumaane Wagao leo tareh...
19/08/2025

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti Utoaji wa Leseni Zanzibar (BLRA) Dkt. Halima Jumaane Wagao leo tarehe 19/08/2025 ameripoti kazi katika Ofisi za BLRA Malinda Zanzibar ambapo alikutana na wafanyakazi na kujitambulisha, wakati Agosti 18, 2025 alijitambulisha kwa Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Mhe. Omar Said Shaaban katika ofisi za Wizara Kinazini.

Dkt. Halima amekuwa Mkurugenzi mpya wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti utoaji wa Leseni baada ya uteuzi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ulioanza rasmi Agosti 13, 2025.

Aidha, Dkt. Wagao amewataka Wafanyakazi wa Mamlaka hiyo, kufanyakazi k**a sheria ya Utumishi wa Umma ilivyoelekeza na wao wameahidi kutoa mashirikiano ili kufanikisha adhma ya Serikali, katika kikao kilichuhudhuriwa na Wakurugenzi wa ndani, Wakuu wa Vitengo na Maafisa wa Mamlaka hiyo.
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Ikulu habari Zanzibar
Baraza BLRC
Wizara ya Viwanda na Biashara

Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Mhe. Omar Said Shaaban ameongoza kikao cha majadiliano (Breakfast Meeting on ...
14/08/2025

Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Mhe. Omar Said Shaaban ameongoza kikao cha majadiliano (Breakfast Meeting on Seaweed Production) kujadili hali ya uzalishaji kwa Sekta ya Mwani kikao kilichohudhiriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Bi. Fatma M. Khamis, Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Captain Hamad B. Hamad, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Biashara Dkt. Said S. Mzee na Wadau wa Sekta ya Mwani katika Hoteli ya Madinat Al Bahr Chukwani Zanzibar.

Aidha Mhe. Waziri ameelezea kuwa, Mwani ni zao la kimkakati na la Biashara hivyo Wizara kupitia Baraza la Taifa la Biashara (ZNBC) wameandaa vikao maalumu (Breakfast Meeting) kujadili hali ya uzalishaji ambapo leo waliangazia Sekta ya Mwani.

Wadau mbalimbali wa Sekta ya Mwani k**a Kampuni ya C- W**d Cooperation na Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi waliwasilisha mada na wadau kujadili mambo mbalimbali ikiwemo changamoto za kodi na sera pia kupendekeza mambo mbalimbali ili kupata mpango wa nchi katika kukuza uzalishaji wa zao hilo.
Ikulu habari Zanzibar
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
ZNCC
ZNBC Today

aziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Mhe. Omar Said Shaaban ameongoza kikao cha Mjadala (Breakfast Meeting for Zan...
13/08/2025

aziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Mhe. Omar Said Shaaban ameongoza kikao cha Mjadala (Breakfast Meeting for Zanzibar Manufacturing Sector) kilichowakutanisha Wazalishaji wa Sekta ya Viwanda, Sekta za Serikali na Binafsi kwa lengo la kujadili mambo mbali kuhusu uzalishaji katika Hoteli ya Madinatul Bahari, Mbweni Zanzibar.


kikao hicho, kiliendeshwa kwa njia ya majadiliano na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Bi. Fatma M. Khamis na Naibu Katibu Mkuu Dkt. Said Seif Mzee na wadau wa Sekta ya Uzalishaji na kujadili hali halisi ya Sekta ya uzalishaji, Changamoto zinazowakabili hususani upatikanaji wa umeme na ucheleweshwaji wa malighafi bandarini.


Aidha, Mhe. Waziri amesema kuwa, kazi ya Wizara ni kuratibu na kufuatilia utekelezaji ili kurahisisha ufanisi katika uzalishaji na kutatua changamoto zinazowakabili
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
ZNCC
ZNBC Today

Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar, Mhe. Omar Said Shaban, amesema dhamira ya Serikali ya Mapinduzi ya ...
12/08/2025

Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar, Mhe. Omar Said Shaban, amesema dhamira ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni kuhakikisha kazi za wabunifu, watunzi na wasanii wa Zanzibar zinalindwa na kutunzwa kwa mujibu wa sheria za haki miliki.

Amesema hayo leo huko Mbweni, katika Hoteli ya Madinatul Bahari, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili kwa majaji, Mahakimu, Jeshi la Polisi, Wasajili wa COSOZA, ZAECA na wadau wengine wa Sekta hiyo.

Waziri Shaaban alifafanua kuwa Serikali imekuwa ikilipa suala la ulinzi wa kazi bunifu uzito wa kipekee kwa muda mrefu kupitia vikao mbalimbali vya ngazi za Serikali na Mahak**a, ili kuhakikisha wabunifu, Waandishi wa vitabu na wasanii wananufaika ipasavyo na kazi zao, sambamba na kuwekewa ulinzi wa kisheria dhidi ya matumizi mabaya au bila ruhusa.

Aidha, Mhe Waziri alisisitiza kuwa katika uchumi wa sasa, maarifa ya ubunifu ni nyenzo muhimu ya maendeleo, jambo ambalo limewawezesha watu wengi duniani kunufaika kupitia kazi zao bunifu. Hivyo, alihimiza taasisi husika kuzingatia kwa makini suala la kulinda utajiri wa fikra na ubunifu wa Wazanzibari.
Wizara ya Viwanda na Biashara
Ikulu habari Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi  akiwa katika ziara kutembelea Miradi...
12/08/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa katika ziara kutembelea Miradi ya Maendeleo ikiwemo Miradi ya Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda ya kituo cha Biashara cha Dimani (Dimani Exhibition Center) na Mradi wa Zanzibar International Convection Centre (ZICC)

Aidha Mhe Rais akiwa katika kikao maalum ameelezea kuwa Serikali inaendelea kusimamia utekelezaji wa Mradi mkubwa wa Uwanja wa AFCON pamoja na Miundombinu mbalimbali inayojengwa Fumba, hivyo ni muhimu kubaini mapema maeneo yatakayotumika kwa Miradi hiyo.

Ikulu habari Zanzibar
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara

Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Bi. Fatma M. Khamis amewata washiriki wa Mafunzo ya Mpango wa Mat...
06/08/2025

Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Bi. Fatma M. Khamis amewata washiriki wa Mafunzo ya Mpango wa Matumizi ya Ardhi kwenye maeneo ya Viwanda (Eco Industrial Park Master Plan) kuhakikisha wanayafanyia kazi kwa vitendo mafunzo yaliyotolewa na si kubakia kinadharia tu.

Akifunga mafunzo ya siku mbili yaliyoandaliwa na United Nations Industrial Development Organizations (UNIDO) katika Hoteli ya Madinat Al Bahr Zanzibar ambayo yamewashirikisha wadau wa Sekta za Serikali na Binafsi na Washauri Elekezi kutoka Nimeta Consul (T) Company Limited Bi. Fatma amesema ni vyema kuyafanyia kazi ili kuhakikisha wanapoandaa mpango kazi unafuata vigezo muhimu vilivyozungumzwa katika mafunzo hayo katika utekelezaji mzuri.
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Ikulu habari Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
ZNCC

Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Mhe. Omar Said Shaaban akipata maelezo kutoka kwa Wamiliki wa Kiwanda cha kuz...
01/08/2025

Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Mhe. Omar Said Shaaban akipata maelezo kutoka kwa Wamiliki wa Kiwanda cha kuzalisha Mifuko ya Karatasi na Bomba za Maji (Trust Auto Parts) kilichopo Maungani Wilaya ya Magharibi B. wakati Mhe Waziri akiwa ziarani kukagua kiwanda hicho na kusikiliza changamoto zao.

Aidha, Mhe. Omar aliambatana na Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Bi. Fatma M. Khamis na Maafisa wa Wizara na alisema uzalishaji wa Mifuko na Bomba za Maji ni bidhaa muhimu, hivyo Serikali kupitia Wizara ya Biashara itahakikisha inatatua changamoto ambapo Wamilikib walielezea ucheleweshwaji wa Malighafi (Raw Materials) Bandarani.

Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Ikulu habari Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara

Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Bi. Fatma M. Khamis amesema, siku ya mwani   imeweza kuwaunganish...
24/07/2025

Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Bi. Fatma M. Khamis amesema, siku ya mwani imeweza kuwaunganisha watu wote kwenye mnyororo wa thamani kwa Taasisi za Serikali na Binafsi, wakulima, wasarifu, wanunuzi, watafiti na wadau mbalimbali na Serikali kwa ujumla ili kuimarisha mnyororo mzima wa thamani.

Ameyasema hayo, katika kilele cha Maadhimisho ya kumi (10) ya siku ya Mwani Zanzibar yenye kauli mbiu Imarisha mnyororo wa thamani kwa kuboresha Sakta ya mwani, hafla iliyofanyika katika Hoteli ya Golden Tulip uwanja wa ndege na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa Sekta ya Mwani.

Aidha Bi. Fatma alisema Serikali inafahamu Sekta ya Mwani inakabiliwa na changamoto hasa utekelezaji wa sera maalum ya kilimo cha mwani na usarifu hivyo, Serikal ya Awamu ya nane inayoongozwa na Rais Dkt. Husein Ali Mwenyi inafanya jitihada kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima na wasarifu wa mwani ikiwa yote hayo ndio vipaombele vya Serikali.

Maadhimisho hayo, yaliambatana na majadiliano ya pamoja kati ya wadau wa Sekta binafsi na Serikali(Public Private Dialogue) kwa lengo la kujadili sera, changamoto, fursa na mikakati katika kuendeleza mnyororo wa thamani wa zao la mwani hapa Zanzibar.
Idara ya Habari Maelezo ZanzibarWizara ya Viwanda na Biashara
ZNCC

22/07/2025

Maonesho ya 49 ya Biashara ya kimataifa ya Dar esalam (sabasaba) 2025
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
Zanzibar State Trading Corporation - ZSTC

Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Mhe. Omar Said Shaaban amewataka vijana wa Tanzania kuchangamkia fursa na maf...
19/07/2025

Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Mhe. Omar Said Shaaban amewataka vijana wa Tanzania kuchangamkia fursa na mafunzo yatolewayo na Chuo Kikuu cha Kilimo cha China (China Agricultural University) katika mradii mkubwa kwa Bara la Afrika na kutanabahisha mradi huu utawasaidia vijana hasa kutoka vijijini wanao jishughulisha na kilimo na bidhaa za mazao katika kupata elimu ya ujasiriamali ili kuengeza maarifa, katika mradi unaotekelezwa kwa miaka mitatu (3) na nafasi 170 zimeshatangazwa

Aidha, Mhe. Omar ameyasema hayo, katika hafla ya kufunga mpango wa maendeleo ya wajasiriamali vijana wa vijijini kwa Tanzania na Uganda na uzinduzi wa Mpango wa kimataifa wa vijana kwa Wajasiriamali wa vijijini katika Hoteli ya Serena Zanzibar na kufafanua dhamira ya Serikali ni kuhakikisha mafunzo yatolewayo yanaendana na dira ya Taifa

Nae, Balozi mdogo wa China Zanzibar Consul General H.E. Li Qianghua alisema, nchi ya China itaendelea kuunga mkono maendelea ya Zanzibar, ambapo Mhe. Waziri na Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Bi. Fatma M. Khamis na Uongozi wa Chuo Kikuu cha kilimo China kwa pamoja waliwatunuku zawadi za vyeti vya ushindi vijana walioshiriki mafunzo ya ujasiriamali nchini china.

Address

46 BARABARA YA MALAWI, GHOROFA 1 And 5
Zanzibar
S.L.P601,[email protected]

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda:

Share