Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Ukurasa rasmi wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis amesema Maonesho ya Saba...
08/07/2025

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis amesema Maonesho ya Sabasaba Jijini Dar-es-Salaam ni fursa kwa Wazanzibari kutangaza utamaduni wao, bidhaa za asili, Utalii, fursa za Biashara pamoja na uwekezaji.

Mapema, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Dkt. Said Seif Mzee alimkaribisha Mgeni rasmi katika Siku ya Zanzibar (Zanzibar Day) iliyogusia mila, silka, na utamaduni wa Zanzibar, fursa na mwelekeo wa uwekezaji endelevu na kufungua milango ya biashara.

Aidha, siku ya Zanzibar iliambatana na majadiliano yaliyoangazia fursa mbalimbali zinazopatikana Zanzibar ikiwemo Utalii, Uchumi wa Buluu, Uwekezaji na Biashara

07/07/2025
Rais wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Maoindizi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema  jukwa la Maonesho ya 49 ya ...
07/07/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Maoindizi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema jukwa la Maonesho ya 49 ya Biashara ya kimataifa ya Dar esalam (sabasaba) yamendelea kua dira ya kushirikiana na mataifa mengine ya dunia kwa maslahi ya pamoja.

Ameyasema hayo Leo tarehe 7/7/2025 wakati akifungua Maonesho hayo katika VIwanja vya Sabasaba huku akiipongeza Tanzania kwa kufanya vizuri katika Maonesho ya Japan Expo 2025 na kufafanua kua hali hii inaifanya Tanzania kufanya vizuri kimataifa.

Aidha, Dkt. Mwinyi amewataka watanzania kupenda na kuthamini bidhaa zao, ili kuimarisha biashara na kuchangia ukuwaji wa uchumi.

Pia, ameziagiza Wizara zote mbili za Viwanda na Biashara za SMT na SMZ na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania ( TANTRADE) kuhakikisha elimu ya alama ya biashara inawafikia Wazalishaji, Wafanyabiashara na Wananchi na Mhe. Mwinyi alikabidhi tuzo kwa Makampuni na Taasisi mbalimbali zilizofanya vizuri katika Maonesho hayo.

Ikulu habari Zanzibar ZNCC Deddah Hija Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Wizara ya Viwanda na Biashara

‎Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda inawatakia Kheri katika Skukuu ya Wafanyabiashara (Sabasaba)
07/07/2025

‎Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda inawatakia Kheri katika Skukuu ya Wafanyabiashara (Sabasaba)

06/07/2025

Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Bi. Fatma Mabrouk Khamis akizungumza katika siku ya China katika hafla iliyofanyika ukumbi wa Sabasaba Hall, katika viwanja vya Sabasaba, Jijini Dar es Salaam

Aidha katika hafla hiyo, Bi. Fatma alikuwa Mgeni rasmi, siku iliyoangazia Sekta ya Viwanda,Usafirishaji, Ujenzi, Miundombinu, Teknolojia pamoja na Nishati

Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar  Bi.  Fatma Mabrouk Khamis  akizungumza katika siku y...
06/07/2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Bi. Fatma Mabrouk Khamis akizungumza katika siku ya China (China Day) hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Sabasaba Hall, katika viwanja vya Sabasaba, Jijini Dar es Salaam

Aidha katika hafla hiyo, Bi. Fatma alikuwa Mgeni rasmi, siku iliyoangazia Sekta ya Viwanda,Usafirishaji, Ujenzi, Miundombinu, Teknolojia pamoja na Nishati

Pia, Ujumbe kutoka China umeahidi kudumisha ushirikiano wa Biashara na Tanzania na kupata fursa ya kupiga picha ya pamoja.

Idara ya Habari Maelezo Zanzibar ZNCC Ikulu habari Zanzibar Deddah Hija Baraza BLRC

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amesema usimamizi madhubuti wa viwango vya bidhaa ni ch...
25/06/2025

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amesema usimamizi madhubuti wa viwango vya bidhaa ni chachu katika kukuza biashara na kufungua milango ya bidhaa za Kiafrika kufikia masoko ya kimataifa.

Mhe. Hemed ameyasema hayo, wakati akimuakilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, katika hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa 31 wa Baraza Kuu la Shirika la Viwango Afrika (ARSO) uliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar.

Aidha, alielezea umuhimu wa kuwa na mifumo rafiki ya udhibiti wa viwango kwa kushirikiana na taasisi k**a Shirika la Viwango Tanzania (TBS), ZBS, Umoja wa Viwango Afrika (ARSO) na miundombinu ya ubora ya Bara la Afrika (PAQI).

Kwa upande wake, Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar, Mhe. Omar Said Shaaban, alisema kuwa viwango vya ubora si hiari tena, bali ni msingi wa kuimarisha ushindani wa bidhaa na huduma za Afrika, pamoja na kulinda maslahi ya watumiaji.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa, Ardhi ni rasilimali adi...
24/06/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa, Ardhi ni rasilimali adimu duniani kote, hivyo ni wajibu wetu kuisimamia ipasavyo kwa Maendeleo endelevu ya nchi yakiwemo masula ya Uwekezaji katika Mahoteli, Viwanda, Makaazi, Kilimo, huduma za kijamii na maeneo ya hifadhi ili kuimarisha uchumi endelevu wa nchi.

‎Aidha, ameyasema hayo leo tarehe 24 Juni,2025 katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Ardhi na Makaazi katika Hoteli ya Amaan Complex ambapo Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda imeshiriki katika Maonesho hayo kwa lengo la kutanga kazi na Miradi inayotekelezwa na Wizara ya Biashara ikiwa ni pamoja na Uwekezeji wa eneo la Viwanda Dunga, Chamanangwe kwa upande wa Pemba na eneo la Biashara Dimani, pia Mhe Rais alipahatika kutembelea Banda la Wizara ya Biashara katika hafla hiyo.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Dkt. Said Seif Mzee amefungua Warsha ya siku mbili (2) ya k...
19/06/2025

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Dkt. Said Seif Mzee amefungua Warsha ya siku mbili (2) ya kimkakati ya kuwajengea uwezo Wafanyabiashara na Wasafirishaji wa mazao ya bidhaa za viungo (Spice) yaliyoandaliwa na Baraza la Wasafirishaji Meli Tanzania (Tanzania Shippers Council) kwa kushirikiana na Baraza la Wasafirishaji Meli Zanzibar (Zanzibar Shipper Council) kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ). katika Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa ndege Zanzibar.

Aidha, Dkt Said amesema, lengo la Warsha hii ni kuwajengea uwezo Wafanyabiashara wa bidhaa za viungo kufungua milango ya kibiashara na Masoko ya bidhaa mbalimbali za viungo kutoka Zanzibar kwenda nje ya nchi katika Masoko ya Afrika Mashariki na kanda ya Afrika, pia alifafanua viungo vinavyopatikana Zanzibar ni bidhaa muhimu ya kuuza na kuwapatia wananchi maisha bora.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Baraza la Wasafirishaji Meli Tanzania (TSC) Bi. Josephine Edington amesema ipo haja kwa wazalishaji wa Bidhaa ya Viungo kutoka Zanzibar kulitumia Soko Huru la Afrika (AFCFTA) ili kupata vyeti halisi (certificate of origin) ya soko hilo.

Address

Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda:

Share