
08/07/2025
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis amesema Maonesho ya Sabasaba Jijini Dar-es-Salaam ni fursa kwa Wazanzibari kutangaza utamaduni wao, bidhaa za asili, Utalii, fursa za Biashara pamoja na uwekezaji.
Mapema, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Dkt. Said Seif Mzee alimkaribisha Mgeni rasmi katika Siku ya Zanzibar (Zanzibar Day) iliyogusia mila, silka, na utamaduni wa Zanzibar, fursa na mwelekeo wa uwekezaji endelevu na kufungua milango ya biashara.
Aidha, siku ya Zanzibar iliambatana na majadiliano yaliyoangazia fursa mbalimbali zinazopatikana Zanzibar ikiwemo Utalii, Uchumi wa Buluu, Uwekezaji na Biashara