Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Ukurasa rasmi wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda imefanya ziara maalum ya kukagua Miradi ya Maendeleo ya Viwanda katika eneo t...
19/12/2025

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda imefanya ziara maalum ya kukagua Miradi ya Maendeleo ya Viwanda katika eneo tengefu la Uwekezaji wa Viwanda liliopo Dunga Zuze, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusuni Unguja kwa lengo la kuona hatua iliyofikiwa kwa Miradi hiyo.

Aidha ziara iliongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Habiba Hassan Omar ambae aliambatana na Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Viwanda, Dkt. Abdulla R. Abdulla, Katibu Tawala Wilaya ya Kati,Ndugu Hamza Ibrahim Mahmoud, Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kati (OCD), Joram. N. Samson, Afisa wa Idara ya Uhamiaji, na Maafisa kutoka Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda.

Viongozi hao kwa pamoja walitembelea ujenzi wa kiwanda cha nguo (Mama Afrika Textile Company Lilited), kiwanda cha Dawa (Africa Bio Chem Co. Ltd na Kiwanda cha kusarifu chuma, mbao na Aluminiam (Arenist Group (Z) Company Lilited) na kuona hatua iliyofikiwa ya ujenzi huo wa Viwanda.

Ziara hiyo imefanyika leo tarehe 18/12/2025 ikiwa ni hatua ya maandalizi ya uwekaji wa jiwe la msingi kwa Miradi ya Wizara kufuatia maandalizi ya Sherehe za miaka 62 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar

Ikulu habari Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
MKOA WA Kusini Unguja
Zanzibar Fair Competition Commission
Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania

Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Dkt. Habiba Hassan Omar ameongoza kikao baina ya Wakala wa Usa...
16/12/2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Dkt. Habiba Hassan Omar ameongoza kikao baina ya Wakala wa Usajili wa Biashara na Mali Zanzibar (BPRA) na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni Tanzania Bara (BRELA).

Aidha, kikao hicho kilijadili uimarishaji wa mashirikiano baina ya Taasisi hizo katika biashara za Kikanda na Kimataifa, ambapo kimehudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na BiasharaTanzania Bara, Dkt. Hashil A. Talib, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais,Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Ndg. Mzee A. Haji, Wakurugenzi na Menejimenti ya Taasisi ya BPRA na BRELA, pamoja na Wakurugenzi wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda.

Kikao hicho kimefanyika leo tarehe 16/12/2025 katika ukumbi wa Wizara ya Biashara Kinazini, Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar.
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
BRELA Tanzania
Zanzibar Fair Competition Commission
Ikulu habari Zanzibar
Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania

Wizara ya  Biashara na Maendeleo ya Viwanda inatoa pongezi za dhati kwa Dkt. Said Seif Mzee kuteuliwa tena kuwa Naibu Ka...
16/12/2025

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda inatoa pongezi za dhati kwa Dkt. Said Seif Mzee kuteuliwa tena kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
Zanzibar Fair Competition Commission
Ikulu habari Zanzibar
Zanzibar State Trading Corporation - ZSTC

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda imeshiriki katika  kikao cha pamoja na wadau wa sekta ya bandari Zanzibar kuj...
12/12/2025

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda imeshiriki katika kikao cha pamoja na wadau wa sekta ya bandari Zanzibar kujadili mikakati ya kuboresha mpangilio na kuongeza ufanisi wa uendeshaji wa shughuli za bandari (Port Operations) katika Bandari ya Fumba, ambapo kwa upande wa Wizara ameshiriki Afisa Biashara Muandamizi Ndugu Zawadi Zaidu Nyange.

Aidha, Kikao kimeandaliwa na Shirika la bandari Zanzibar (ZPC), kilichoongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari Zanzibar, Ndugu Akif Ali Khamis, pamoja na mambo mengine kilijadili changamoto zinazojitokeza katika utoaji wa huduma na kuweka mikakati ya kuzitafutia ufumbuzi, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

Kikao hicho kimefanyika Disemba 11, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale (Baraza la Wawakilishi la zamani),
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
Shirika La Bandari Zanzibar
Ikulu habari Zanzibar

Wizara ya  Biashara na Maendeleo ya Viwanda inatoa pongezi za dhati kwa uteuzi wa Katibu Mkuu  wa Wizara ya  Biashara na...
24/11/2025

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda inatoa pongezi za dhati kwa uteuzi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Dkt. Habiba Hassan Omar

Hongera sana na karibu Wizarani
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
Zanzibar Fair Competition Commission
Mamlaka BLRA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amemteuwa Dkt. Habiba Hassan Omar kuw...
21/11/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amemteuwa Dkt. Habiba Hassan Omar kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda katika taarifa iliyotolewa Novemba 20. 2025 na Mhandisi Zena A. Said, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi.

Aidha Kabla ya uteuzi huo, Dkt. Habiba alikuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi. Uongozi na wafanyakazi wote wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda wanampongeza kwa uteuzi huo.
Wizara ya Viwanda na Biashara
Ikulu habari Zanzibar
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Zanzibar State Trading Corporation - ZSTC
Mamlaka BLRA
Zanzibar Fair Competition Commission
Bongo5.com

Hongera Mhe. Judith S. Kapinga Waziri wa Viwanda na Biashara  na   Mhe.  Patrobas P. Katambi  Naibu Waziri wa Viwanda na...
18/11/2025

Hongera Mhe. Judith S. Kapinga Waziri wa Viwanda na Biashara na Mhe. Patrobas P. Katambi Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara kwa kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuiongoza Wizara ya Viwanda na Biashara.
Wizara ya Viwanda na Biashara
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
ZNCC
Zanzibar Fair Competition Commission
Zanzibar State Trading Corporation - ZSTC

Hongera Dkt Hussein Ali Mwinyi kwa kuchaguliwa tena kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
06/11/2025

Hongera Dkt Hussein Ali Mwinyi kwa kuchaguliwa tena kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda  imesaini Mkataba na Kampuni ya Maxbit iliopo Zanzibar ili kuandaa mfumo kami...
21/10/2025

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda imesaini Mkataba na Kampuni ya Maxbit iliopo Zanzibar ili kuandaa mfumo kamilishi utakao simamia taratibu za ulipaji leseni, tozo na kodi za upangaji na malipo mbali mbali wa Wizara ya Biashara na Maendelo ya Viwanda.

Kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mkataba huo, umesainiwa na Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Bi. Fatma Mabrouk Khamis na upande wa Kampuni, saini imewekwa na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Maxbit Bw. Yasser Rashad.

Aidha, Bi. Fatma amesema Wizara inatarajia kuwa na mfumo kamili unaosimamia taratibu zote za utoaji vibali na leseni pia kuweza kufanya 'integration' na mfumo wa Wizara wakusajili Viwanda vilivyopo, hivyo makubaliano hayo yataleta mageuzi chanya kwenye Sekta ya Biashara ikiwa ndio dhamira mahususi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi anavyozitaka Wizara na Taasisi kujiendesha kidijitali zaidi.
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Ikulu habari Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
ZNCC

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda inatoa mkono wa pole kwa ndugu na Familia kwa kifo cha msanii maarufu wa fila...
17/10/2025

Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda inatoa mkono wa pole kwa ndugu na Familia kwa kifo cha msanii maarufu wa filamu na muimbaji wa Qaswaida Subira Nassor.
Innallilahi wainna ilaihi rajiuni
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Ikulu habari Zanzibar

16/10/2025
NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar, Dkt. Said Seif Mzee, amesema utekelezaji wa mradi...
16/10/2025

NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar, Dkt. Said Seif Mzee, amesema utekelezaji wa mradi wa uongezaji thamani katika mazao ya kimkakati kwa ajili ya masoko ya ndani na nje ya nchi (MARKUP II), utaongeza ukuaji wa mnyororo wa thamani katika uzalishaji na kuchochea ongezeko la ajira.

Dkt. Mzee ameyasema hayo jijini Dodoma Oktoba 15,2025 wakati akifungua Mkutano wa tatu wa Taifa wa kamati ya Makatibu Wakuu wa Mradi wa MARKUP II, ulioandaliwa kwa lengo la kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kwa awamu ya miaka minne (2023–2027) kwa kushirikiana na Kituo cha Biashara cha Kimataifa (ITC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

“Utekelezaji wa awamu ya pili ya mradi wa MARKUP ni matokeo ya mafanikio yaliyopatikana katika awamu ya kwanza (MARKUP I), ambayo licha ya mafanikio, pia yalibaini changamoto zilizotumika kuboresha utekelezaji wa awamu hii,” amesema Dkt.Said.

Aidha amesema mradi huo unahusisha fursa za masoko na uwezo wa kuyafikia masoko ya bidhaa za Tanzania nje ya nchi, hasa kwa sekta ya viwanda vidogo vinavyotoa mchango mkubwa katika ajira na uchumi wa nchi wanachama wa EAC.

“Kama tulivyokubaliana katika mkutano wetu wa Februari 2025 jijini Dodoma, awamu hii imelenga kuimarisha uongezaji thamani katika mazao ya kahawa, ngozi, parachichi, viungo vya chakula na vinywaji, pamoja na masuala ya vifungashio,” ameongeza.

Hata hivyo Dkt.Mzee amesema, kupitia mkutano huo, wajumbe wamepokea taarifa kuhusu maandalizi ya mkutano wa makatibu wakuu wa kikanda utakaofanyika Bunjumbura, Burundi kuanzia Novemba 3–5, 2025, ambapo maazimio ya mkutano wa Dodoma yatakuwa msingi wa majadiliano hayo.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi wa Market Access Upgrade Programme (MARKUP II) kutoka ITC, Bw. Safari Fungo, amesema, mradi huo unatekelezwa katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ambazo ni Tanzania, Burundi, Kenya, Uganda, Rwanda na Sudan Kusini.

Aidha amefafanua lengo la mradi huo ni kuongeza mnyororo wa thamani wa mazao mbalimbali katika nchi wanachama wa EAC, ambapo kwa upande wa Tanzania, umejikita katika mazao ya kahawa, bidhaa za ngozi na vifungashio.
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Ikulu habari Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
ZNCC

Address

46 BARABARA YA MALAWI, GHOROFA 1 And 5
Zanzibar
S.L.P601,[email protected]

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda:

Share