
11/09/2025
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga Kushirikiana na Serikali ya Oman katika uwekezaji wa mazao ya viungo, hayo yemebainishwa katika ujumbe wa wafanyabiashara wa Oman waliopo Zanzibar kwa ziara ya kibiashara na uwekezaji katika Mkutano uliofanyika Ukumbi wa ZURA ambapo Wizara ya Biashara na Maendelep ya Viwanda na Wizara ya nchi,Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, waliratibu ujio huo.
Katika mkutano huo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Mhe. Shariff Ali Sharif, alisema majadiliano ya uwekezaji yanafanyika kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na nchi mbalimbali katika kuchochea ukuwaji wa Uchumi na kuleta Maendeleo endelevu.
Viongozi Mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar akiwemo Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda ndugu. Fatma Mabrouk Khamis, Vingozi wa Sekta Binafsi na wazalishaji walishiriki mkutono huo.
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar
Wizara ya Viwanda na Biashara
Ikulu habari Zanzibar
ZNCC
Baraza BLRC