08/12/2026
Shirikisho la Soka la Uholanzi (KNVB) limeripotiwa kuanza mazungumzo na kocha raia wa Hispania, Roberto Martínez, kuhusu uwezekano wa kumteua kuwa kocha mpya wa timu ya taifa.
Kwa mujibu wa De Telegraaf, Martínez amekuwa mmoja wa majina mapya yaliyoibuka katika mchakato wa kutafuta mrithi wa Ronald Koeman, aliyeondoka kwenye nafasi hiyo baada ya Uholanzi kutolewa katika hatua ya 32 bora ya Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Morocco kwa mikwaju ya penalti.
Ripoti zinaeleza kuwa Nigel de Jong, ambaye ni mkurugenzi wa soka wa KNVB, amefanya mazungumzo na Martínez kuhusu uwezekano wa kocha huyo kurejea kwenye kazi ya ukocha wa timu ya taifa.
Martínez mwenye umri wa miaka 53 amewahi kuiongoza Ubelgiji na Ureno, hivyo ana uzoefu mkubwa wa kusimamia timu za taifa katika mashindano makubwa ya kimataifa.
Sponsored by