Adventist World Swahili

  • Home
  • Adventist World Swahili

Adventist World Swahili Karibu kwenye ukurasa wa Facebook wa Gazeti la Adventist World Kiswahili. Kujiunga, bonyeza kwenye kiungo hapo juu kulia. Don’t forget to “like” this page

Gazeti la Adventist World Kiswahili lina makala zilizo tafsiriwa. This Page is your connection to the Kiswahili Edition of the Adventist World Magazine. The magazine is delivered digitally for mobile devices on a WhatsApp Channel, free to subscribers in East and Central Africa, and around the world. Note the Sign-up button at the top right of this page. The Kiswahili Adventist World Magazine conta

ins translations of the English articles, plus up to 25% original Kiswahili material. Other devotional material is also available on the WhatsApp Channel, such as the Grace Notes by Bill Knott, Editor in Chief of the Adventist Review Ministries. This material is also easy to share with others, via WhatsApp. Here you will find posts highlighting the latest articles in the magazine. Inbox us if you have any question, or let us know which articles you have enjoyed. We’d love to hear from our subscribers/readers.

Mei 2025 Toleo hili linaangazia “Kanisa Linaposononesha” na sababu zinazomfanya Yesu kututaka tusalie kwenye kanisa Lake...
02/05/2025

Mei 2025

Toleo hili linaangazia “Kanisa Linaposononesha” na sababu zinazomfanya Yesu kututaka tusalie kwenye kanisa Lake, hata inapokuwa vigumu.

Tunaangazia “Kusudi la Mungu kwa Kanisa Lake,” na Ted Wilson anazungumzia “mwaliko” anaotupa Mungu na jinsi tunavyopaswa kuwa “Tayari kwa Dhifa ya Harusi” ili “Kristo anapotupatia vazi Lake la haki, vazi zuri . . . tunatakiwa tu kulikubali na kulivaa.”

"Tukio la hadubini” linaonyesha wakati mwafaka wa Bwana kwa ajili ya kliniki ya Cochabamba, na katika kisa chetu cha Afya na Uzima, tunachunguza ikiwa kweli vikoleza sukari visivyo vya asili ni mbadala wenye afya.

Bofya hapa ili kusoma Toleo la Mei 2025
https://send-it.me/go/AWMei2025

Pata maktaba ya mtandaoni ambapo majarida yote yanahifadhiwa kwenye kiungo kilicho hapo chini.
https://bit.ly/AWSwahiliMagazineLibrary

Imani Inayokua: RebaMaombi na wema barabarani Na Cathlynn Doré LawMakala yetu ya Imani Inayokua inasimulia kisa cha “bib...
25/04/2025

Imani Inayokua: Reba

Maombi na wema barabarani
Na Cathlynn Doré Law

Makala yetu ya Imani Inayokua inasimulia kisa cha “bibi”, ambaye, kwenye ziara zake za kila siku, alikutana na kuingiliana na Reba, mbwa ambaye mbweko wake ulikuwa mbaya zaidi kuliko kung’ata kwake. Kisa maalum kinachofunua nguvu ya imani na uwezo wa Mungu wa kuponya.

Bonyeza hapa ili kuisoma makala hiyo
https://send-it.me/go/AWAprili2025?page=21

Mtazamo wa Kiulimwengu: Mwaliko Mzuri ZaidiKuitikia witoNa Ted N C WilsonTed Wilson anajadili “mwaliko” tuliopewa na Mun...
17/04/2025

Mtazamo wa Kiulimwengu: Mwaliko Mzuri Zaidi

Kuitikia wito
Na Ted N C Wilson

Ted Wilson anajadili “mwaliko” tuliopewa na Mungu kwa kunukuu baadhi ya mialiko maarufu ya Biblia - “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha” (Mt. 11:28). Anaendelea kuelezea kuwa mialiko hiyo kwa kweli ni miwili, na kwamba “Mungu ameweka baraka nyingi kwa ajili ya wale wanaoalika wenzao kujifunza Kwake.” Makala hii pia inataja njia nzuri zaidi ambazo Mungu amewasaidia watu wanapokuwa katika mchakato wa kuwaalika wengine.

Bonyeza hapa ili kusoma makala hiyo
https://send-it.me/go/AWAprili2025?page=13

Fokasi: Mwokozi Atoshelezaye Kuokolewa kwa neema kupitia kwa imaniNa Darius JankiewiczDarius Jankiewicz anaichunguza dha...
13/04/2025

Fokasi: Mwokozi Atoshelezaye
Kuokolewa kwa neema kupitia kwa imani

Na Darius Jankiewicz

Darius Jankiewicz anaichunguza dhana ya wokovu kupitia kwa mada tano zinazohusiana, ambazo zinajumuisha: ufunuo wa tabia ya Mungu; asili ya dhambi ya mwanadamu na utii na utakatifu: tunda la Imani. “Tunapokaa ndani ya Kristo, analeta utii ndani yetu, si ili tuokolewe bali kwa sababu tumeshaokolewa.”

Bonyeza hapa ili kuisoma makala hiyo
https://send-it.me/go/AWAprili2025?page=11

April 2025Katika toleo hili tunaangazia “kuokolewa kwa neema kupitia kwa imani” dhana iliyochunguzwa kwa kina kupitia kw...
11/04/2025

April 2025

Katika toleo hili tunaangazia “kuokolewa kwa neema kupitia kwa imani” dhana iliyochunguzwa kwa kina kupitia kwa mada tano katika makala “Mwokozi Atoshelezaye”. Pia tunajadili dhana ya dhambi na neema katika “Utakatifu na Neema ya Mungu Itakasayo”.

Michael Sokupa anakumbushwa umuhimu wa kutazama nyuma kwenye uongozi wa Mungu katika historia yetu kwenye makala yake “Kugundua Maeneo ya Waanzilishi wa Waadventista wa Sabato huko Kimberley”. Pia tunaangalia umuhimu na utaratibu wa “Kutembea kwa Kuomba” katika makala yetu ya Mtindo wa Maisha, na katika kisa chetu cha Afya na Uzima, tunachunguza jinsi ya “kuzuia kusinyaa kwa tishu ya mifupa kabla hakujaanza”.

Bonyeza hapa ili kusoma Toleo la Aprili 2025
https://send-it.me/go/AWAprili2025

Pata maktaba ya mtandaoni ambapo majarida yote ya AW yanahifadhiwa kwa kubonyeza kiungo kilicho hapo chini.
https://bit.ly/AWSwahiliMagazineLibrary

Mtindo wa Maisha: Kutayarishwa kwa KusudiKujenga msingi wa umilele Na Beth ThomasBeth Thomas anachunguza umuhimu wa msin...
20/03/2025

Mtindo wa Maisha: Kutayarishwa kwa Kusudi
Kujenga msingi wa umilele

Na Beth Thomas

Beth Thomas anachunguza umuhimu wa msingi imara kwa mioyo na akili za vijana kupitia kwa elimu ya Kikristo. “Elimu ya Kikristo ni zaidi ya mafanikio ya kitaaluma; inahusu kuunda mioyo na akili kwa ajili ya umilele.”

Bonyeza hapa ili kusoma makala hiyo
https://send-it.me/go/AWMachi2025?page=16

Mtazamo wa Kiulimwengu: Ukuta wa Moto Mungu anajibu maombi.Na Ted N C Wilson Kundi la vijana wanapojitahidi kufanya mkut...
14/03/2025

Mtazamo wa Kiulimwengu: Ukuta wa Moto
Mungu anajibu maombi.

Na Ted N C Wilson

Kundi la vijana wanapojitahidi kufanya mkutano wa uinjilisti kwenye mji mdogo kwenye pwani ya Tanzania, wanakabiliwa na upinzani mkali. Nguvu ya imani yao na maombi yao ya pamoja yanasababisha ulinzi wa kimuujiza katika hali hatari na zisizojulikana.

Bonyeza hapa ili kuisoma makala hiyo
https://send-it.me/go/AWMachi2025?page=13

Imani Inayokua - “Ujasiri kwa ajili ya Mungu”Hupewa thawabuNa Janice SchmidtJanice Schmidt anasimulia safari yake ya kue...
10/03/2025

Imani Inayokua - “Ujasiri kwa ajili ya Mungu”
Hupewa thawabu

Na Janice Schmidt

Janice Schmidt anasimulia safari yake ya kuenda Ufilipino kufanya kazi ya utume, yakiwemo matunda matamu ya kigeni, wadudu wa ajabu, na bila shaka watu wazuri sana. Janice anasema, “Nimepata shangwe kuu kuwepo mahali ambapo Roho wa Mungu hufanya kazi.”

Yasome matukio yake yote hapa . . .
https://send-it.me/go/AWFebruari2025?page=19

Fokasi: Msamaha na haki ya MunguImani na matendo, ujumbe na utume Na Jerome SkinnerKwenye makala yetu ya Fokasi, tunataz...
07/03/2025

Fokasi: Msamaha na haki ya Mungu
Imani na matendo, ujumbe na utume

Na Jerome Skinner

Kwenye makala yetu ya Fokasi, tunatazama jinsi “Mungu mwenye maarifa yote anajua namna, wakati, na kiwango cha kutoa haki katika mchakato wa msamaha”. Tunaichunguza dhana ambayo wakati mwingine ni yenye changamoto ya kuwasamehe waliotukosea na pia tunaangalia umuhimu wa kukubali makosa yetu kabla ya kuwahukumu wengine. Tunajifunza kuwa “Msamaha wa Mungu hautegemei sifa au ustahili wa mwenye kosa au aliyekosewa. Msamaha Wake unategemea tu tabia Yake ya upendo, haki, neema na rehema (Zab. 34:6, 7; Dan. 9:18; Mal. 3:6).”

Bonyeza hapa ili kusoma makala hiyo
https://send-it.me/go/AWMachi2025?page=11

Makala Maalum - “Mungu Hufanya Kazi Usiku” Kisa cha Sharath Babu NakkaNa Pratap Gopala Rao Sharath Babu Nakka anapopotez...
03/03/2025

Makala Maalum - “Mungu Hufanya Kazi Usiku”
Kisa cha Sharath Babu Nakka

Na Pratap Gopala Rao

Sharath Babu Nakka anapopoteza uwezo wake wa kuona ghafla akiwa mtoto, karibu baba yake apoteze tumaini. Lakini kupitia kustahimili na imani, familia yao iliweza kuvumilia changamoto na ikaibuka na kisa cha kuhimiza cha kushiriki.

Bonyeza hapa ili kusoma makala.
https://send-it.me/go/AWFebruari2025?page=15

Machi 2025 Katika toleo hili tunaangazia msamaha na haki ya Mungu. Katika makala yetu ya Fokasi, tunatazama jinsi “Mungu...
28/02/2025

Machi 2025

Katika toleo hili tunaangazia msamaha na haki ya Mungu. Katika makala yetu ya Fokasi, tunatazama jinsi “Mungu mwenye maarifa yote anajua namna, wakati, na kiwango cha kutoa haki katika mchakato wa msamaha”.

Katika “Ukuta wa Moto”, kikundi cha vijana wanafanya mkutano wa uinjilisti kwenye pwani ya Tanzania. Nguvu ya maombi yao ya pamoja inafanya wapate ulinzi wa kimuujiza kwenye hali hatari. Tunaangazia umuhimu wa elimu ya Kikristo kwenye makala yetu ya Mtindo wa Maisha “Kutayarishwa kwa Kusudi”. Katika kisa chetu cha Afya na Uzima, tunachunguza matokeo ya umuhimu wa shukrani kwenye afya yetu. Na kwa hilo, tunawashukuru nyote mliojiandikisha, kwa imani yenu inayoendelea na kujitolea kwenu.

Bonyeza hapa ili kulisoma Toleo la Machi 2025
https://send-it.me/go/AWMachi2025

Pata maktaba ya mtandaoni ambako majarida yote ya AW yanahifadhiwa kwa kubonyeza kiungo kilicho hapo chini.
https://bit.ly/AWSwahiliMagazineLibrary

Fokasi: Dada Yangu Mpendwa Barua ya Mwisho ya Ellen WhiteNa Tim PoirierKatika “Dada Yangu Mpendwa,” Tim Poirier anauchun...
26/02/2025

Fokasi: Dada Yangu Mpendwa
Barua ya Mwisho ya Ellen White

Na Tim Poirier

Katika “Dada Yangu Mpendwa,” Tim Poirier anauchunguza ujumbe wa tumaini ambao Ellen White aliuzungumzia katika barua yake ya mwisho. Anatoa muhtasari wa hoja zake kuu za kuhimiza. Ellen White aliandika “Usizungumzie kutostahili kwako na mapungufu yako. Wakati unahisi kana kwamba huzuni inakufunika, mtazame Yesu na useme, Yu hai ili kuniombea.” Barua yake ina ujumbe wa kutia moyo ambao unaweza kuwafaa wote wanaoisoma.

Bonyeza hapa ili kuisoma makala hiyo.
https://send-it.me/go/AWFebruari2025?page=11

Address

MD

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Adventist World Swahili posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Adventist World Swahili:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share