AV MEDIA TZ

AV MEDIA TZ Your number one source of all the Entertainment News, Music, Gossips & an Audiovisual.

Msanii mkongwe wa muziki wa Hip Hop Bongo, Professor Jay amekabidhiwa rasmi tuzo yake ya kimataifa kutoka Hollywood and ...
19/07/2025

Msanii mkongwe wa muziki wa Hip Hop Bongo, Professor Jay amekabidhiwa rasmi tuzo yake ya kimataifa kutoka Hollywood and African Prestigious Awards (HAPAwards), katika ofisi za Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), jijini Dar es Salaam.

Makabidhiano hayo yaliongozwa hapo jana na Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa wa BASATA, Bwana Edward Buganga, aliyemkabidhi tuzo hiyo kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa BASATA, Dkt. Kedmon Mapana.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo, Prof. Jay alieleza furaha yake kwa kutunukiwa heshima hiyo kubwa na kimataifa, huku akiwashukuru mashabiki wake, wadau wa sanaa, na Serikali kupitia BASATA kwa kuendelea kumtambua na kumthamini.

“Kupokea tuzo hii nyumbani, mbele ya wasanii wenzangu na viongozi wa sanaa, ni heshima kubwa sana kwangu. Muziki wetu una thamani, na ninajivunia kupeperusha bendera ya Tanzania kimataifa,” alisema Prof. Jay kwa shukrani.

Kwa upande wake, Bwana Edward Buganga alitumia fursa hiyo kumpongeza Prof. Jay kwa ushindi huo na kuhimiza wasanii wengine kuendelea kufanya kazi kwa weledi na ubunifu ili kuvuka mipaka ya ndani na kufikia mafanikio ya kimataifa.

Mwimbaji wa Bongofleva, Nandy amesema muda sio mrefu atamzalia mume wake Billnass watoto mapacha huku akisisitiza kuwa h...
17/07/2025

Mwimbaji wa Bongofleva, Nandy amesema muda sio mrefu atamzalia mume wake Billnass watoto mapacha huku akisisitiza kuwa hawezi kumuacha kamwe hata iweje!.

Nandy ametoa kauli hiyo wakati akitoa ujumbe kwenda kwa Billnass ambao unazungumzia miaka mitatu ya ndoa yao ambayo imeshajaliwa mtoto mmoja. Swipe left kusoma ujumbe wake.

17/07/2025

Staa wa Nigeria, Wizkid akitest mitambo.

Mwimbaji wa Bongofleva, Diamond Platnumz katikati picha ya pamoja na Rapa wa Marekani, Ja Rule baada ya kukutana nchini ...
13/07/2025

Mwimbaji wa Bongofleva, Diamond Platnumz katikati picha ya pamoja na Rapa wa Marekani, Ja Rule baada ya kukutana nchini humo hivi karibuni.

Diamond, Mkurugenzi Mtendaji wa WCB Wasafi, alikuwepo Marekani kwa ajili ya shughuli zake za kimuziki ambapo pia alipokea tuzo kwa kufikisha subscribers milioni 10 YouTube.

Mwimbaji wa Bongofleva, Marioo amejitangaza kuwa Mfalme wa muziki huo kupitia video ya wimbo mpya, Ha Ha Ha (2025). Je, ...
12/07/2025

Mwimbaji wa Bongofleva, Marioo amejitangaza kuwa Mfalme wa muziki huo kupitia video ya wimbo mpya, Ha Ha Ha (2025).

Je, Marioo anastahili kuwa Mfalme wa Bongofleva?.

Kumbuka, tangu Marioo ametoka kimuziki na wimbo wake, Dar Kugumu (2018), ameshatoa albamu mbili, The Kid You Know (2021) na The Godson (2025).

11/07/2025

Mama mzazi wa mshindi wa Grammy kutokea Nigeria, Burna Boy, Bose Ogulu akichagiza jambo katika mradi wao mpya.

11/07/2025

Staa wa filamu Bongo, Aunty Ezekiel ameomba radhi kwa mashabiki wake na jamii kwa ujumla kufuatia matumizi yake mabaya ya mitandao ya kijamii.

Kauli ya Aunty Ezekiel inakuja baada ya kukutana na Bodi ya Filamu na kupata elimu ya jinsi anapaswa kuitumia mitandao k**a mtu maarufu katika jamii ambayo ndio walaji wa sanaa yake.

Staa wa Paris Saint-Germain (PSG), Achraf Hakimi ameonekana akitamba katika mitaa ya jiji la New York akiwa na mwanamiti...
11/07/2025

Staa wa Paris Saint-Germain (PSG), Achraf Hakimi ameonekana akitamba katika mitaa ya jiji la New York akiwa na mwanamitindo maarufu mwenye asili ya Misri na Morocco, Imaam Hammam.

Kuonekana kwa wawili hawa kumeibua mijadala mbalimbali katika mitandao ya kijamii kuwa huenda wawili hawa wana uhusiano wa wa zaidi ya urafiki wa kawaida

Imaam mwenye umri wa miaka 28, pia alikuwepo katika uwanja wa MetLife, New Jersey hapo Julai 9 Akishuhudia PSG wakiibuka na ushindi wa 4-0 dhidi ya Real Madrid. Kitendo kilichotaffsiriwa kuwa ishara ya kumuunga mkono Hakimi.

Mahusiano ya Hakimi na mwanadada Hiba Abouk yaliyoishia kwa talaka mwaka 2023 yalizua gumzo dunia nzima baada ya Hiba kudai nusu ya Mali za Hakimi na kugundua mali zake zote zinamilikiwa na mama yake.

Staa wa Bongofleva kutokea WCB Wasafi, Diamond Platnumz amefanikiwa kufikisha views bilioni 3 katika mtandao wa YouTube....
23/06/2025

Staa wa Bongofleva kutokea WCB Wasafi, Diamond Platnumz amefanikiwa kufikisha views bilioni 3 katika mtandao wa YouTube.

Kwa matokeo hayo, Diamond anakuwa mwanamuziki wa kwanza Afrika Mashariki na Kati, na wa pili kusini mwa Jangwa la Sahara kufikia mafanikio hayo.

Ikumbukwe mwimbaji wa Nigeria na mshindi wa Grammy, Burna Boy ndiye anaongoza upande wa Sahara ila kazidiwa subscribers na Diamond.

Picha hii imepigwa katika show ya Diamond Platnumz iliyofanyika London, Uingereza wikiendi iliyopita ambapo Staa wa Nige...
19/06/2025

Picha hii imepigwa katika show ya Diamond Platnumz iliyofanyika London, Uingereza wikiendi iliyopita ambapo Staa wa Nigeria, Mr. Flavour naye aliibuka.

Utakumbuka wawili hao tayari wameshirikiana katika nyimbo tatu na zote zimefanya vizuri, mathalani Nana (2015) video yake ina views zaidi ya milioni 100 YouTube.

Mwimbaji wa Bongofleva, Zee Cuty amewekwa chini ya uangalizi maalum wa kimatibabu kutokana na changamoto za afya ya akil...
19/06/2025

Mwimbaji wa Bongofleva, Zee Cuty amewekwa chini ya uangalizi maalum wa kimatibabu kutokana na changamoto za afya ya akili inayomkabili k**a alivyoeleza hivi karibuni.

Taarifa kwa umma kutoka kwa meneja wake ndio imeeleza hayo k**a ifuataavyo.

Kwa heshima kubwa, Familia na manager wa msanii Zee Cute unawataarifu vyombo vya habari, mashabiki, na wadau wote wa tasnia ya muziki kwamba msanii wetu kwa sasa yupo chini ya uangalizi na matibabu maalum kutokana na changamoto za kiafya, hususan zinazohusiana na afya ya akili ambazo amekuwa akikabiliana nazo katika kipindi hiki.

Tunatoa taarifa hii kwa uwazi iii kuendeleza juhudi za kuelimisha na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kulinda na kuenzi afya ya akili, hasa kwa vijana na wasanii ambao mara nyingi hukumbana na mazingira yenye shinikizo kubwa. Ni wajibu wetu k**a jamii kutoa msaada, faraja, na mazingira salama kwa wale wanaopitia changamoto k**a hizi.

Kwa sasa, tunafanya kila jitihada kuhakikisha Zee Cute anapata huduma bora ya afya na mapumziko ya kutosha ili aweze kupona na kurejea katika hali yake ya kawaida akiwa na nguvu mpya ya kuendelea kufanya kazi. Tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa mashabiki, wasanii wenzake, na wadau wote wa muziki walioleta salamu za pole, sala, na maneno ya faraja. Mchango wenu wa kihisia na kimaadili unathaminiwa kwa kiasi kikubwa.

Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote unaoweza kujitokeza katika shughuli za muziki kipindi hiki. Tunashidi kuendelea kuwapatia mashabiki na wadau tariffa rasmi kuhusu maendeleo ya afya ya msanii wetu kupitia kurasa zake halali za mitandao ya kijamii.

Mwisho, Zee Cute anawashukuru mashabiki wake wote kwa upendo, maombi, na kuendelea kuunga mkono kazi zake za muziki. Anaamini kwa pamoja tunaweza kuvuka kipindi hiki kigumu kwa mshik**ano na matumaini.

Asanteni sana.

Imetolewa na:
Manager wa Msanii Zee Cute
Baraka Frank

Staa wa Bongofleva, Diamond Platnumz akikumbatiana na mwenzake wa Nigeria, Tiwa Savage. Hiyo ni baada ya kumalizika kutu...
18/06/2025

Staa wa Bongofleva, Diamond Platnumz akikumbatiana na mwenzake wa Nigeria, Tiwa Savage.

Hiyo ni baada ya kumalizika kutumbuiza pamoja huko London, Uingereza wikiendi iliyopita.

Tazama picha zaidi kwenye comments.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AV MEDIA TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to AV MEDIA TZ:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share