Sports Online

Sports Online Karibu kwenye ulimwengu wa burudani ya michezo! Tunakuletea habari, matokeo, na matukio moto kutoka ndani na nje ya uwanja. Usipitwe na chochote!

Yanga wamekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Zoman Fc,Célestin EcuaKila kitu kimekamilika, Ecua kujiunga na YangaMsimu...
09/07/2025

Yanga wamekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Zoman Fc,Célestin Ecua

Kila kitu kimekamilika, Ecua kujiunga na Yanga
Msimu uliopita Ecua alifunga goli 15 na assists 12 kwenye michuano yote.

Yanga wamezipiku Simba na Azam kwa Ecua

🚨TETESIKlabu ya Simba inataka bilion 1.5 ili kumuuza Jean Ahoua kwa Kaizer Chiefs, kwenye ligi ya Tanzania kocha wa Kaiz...
08/06/2025

🚨TETESI

Klabu ya Simba inataka bilion 1.5 ili kumuuza Jean Ahoua kwa Kaizer Chiefs, kwenye ligi ya Tanzania kocha wa Kaizer Chiefs anawataka wachezaji wawili ambao ni Feisal na Ahoua,

Ikumbukwe Nabi alikuwa nchini kwa wiki moja kabla hajaenda mapumzikoni Brazil

Hili dau waliloweka Simba ni sawa kwa kiwango cha Ahoua au wanapigwa?

🚨Ameandika Ahmed AllyMsipotangaza Uwanja wa mechi, Bodi ya Ligi itatangazaMsipotangaza Viingilio, Bodi ya Ligi itatangaz...
08/06/2025

🚨Ameandika Ahmed Ally

Msipotangaza Uwanja wa mechi, Bodi ya Ligi itatangaza
Msipotangaza Viingilio, Bodi ya Ligi itatangaza na sisi tutanunua

Msipofanya Promotions, Azam Tv watafanya na wameshaaanza kufanya

Msipokodi Uwanja, Bodi ya Ligi itakodi na ila Gharama za Uwanja mtalipa nyie.

Kanuni zinaipa nguvu bodi ya Ligi kufanya yote hata k**a mwenyeji wa mechi anadema demaa

Mashabiki wenu wakisusa, wetu watakuja na tayari Mashabiki wetu zaidi ya Elfu 10 walishanunua Tiketi
Wanetu mmekalia moto... !!!

🚨Ameandika Jemedari SaidHalafu mkiitwa BONGO MOVIE mnataka kurusha ngumi, sinema k**a hizi ni za kizamani sana yani. Hiz...
06/06/2025

🚨Ameandika Jemedari Said

Halafu mkiitwa BONGO MOVIE mnataka kurusha ngumi, sinema k**a hizi ni za kizamani sana yani.

Hizi episode zimeshapitwa na wakati tumeziona huko nyuma sema nyinyi kwakuwa wageni mnadhani mnafanya kitu kipya na cha maana hapa.

Hii ni sawasawa na kujificha kwenye shamba la matembele halafu unadhani huonekani.
Ukicheza na Mbwa utaingia naye Msikitini
BIN KAZUMARI MTIPA (The voice of the voiceless)

🚨UPDATEYanga haiutambui mchezo wa Tarehe 15 June dhidi ya Simba ScYanga wametia ratiba yao ya mwezi June ambapo kwa rati...
02/06/2025

🚨UPDATE

Yanga haiutambui mchezo wa Tarehe 15 June dhidi ya Simba Sc

Yanga wametia ratiba yao ya mwezi June ambapo kwa ratiba hiyo haionyeshi mchezo wao dhidi ya Simba.

🚨TETESITayari viongozi wa Raja Casablanca wameanza mazungumzo ya siri na kocha wa Simba Fadlu Davids, Raja wanaamini uwe...
02/06/2025

🚨TETESI

Tayari viongozi wa Raja Casablanca wameanza mazungumzo ya siri na kocha wa Simba Fadlu Davids, Raja wanaamini uwezo wa Fadlu baada ya kuifikisha klabu ya Simba fainali ya Shirikisho 2024/25

Hii imekuja baada ya Raja kumkosa Saad Ramovic baada ya klabu yake ya sasa kumuongezea mkataba kocha huyo.

Chanzo changu kinasema tayari Fadlu ameonyesha nia ya kujiunga na Raja Casablanca ya Morocco msimu ujao.

Je Simba wapo tayari kumuacha Fadlu msimu ujao?

🚨Fiston Kalala MayeleMshambuliaji wa Kimataifa wa DR Congo, Fiston Kalala Mayele, ameendelea kuandika historia barani Af...
02/06/2025

🚨Fiston Kalala Mayele

Mshambuliaji wa Kimataifa wa DR Congo, Fiston Kalala Mayele, ameendelea kuandika historia barani Afrika baada ya kutwaa tuzo ya mfungaji bora wa michuano ya CAF Champions League 2024/2025, akiwa na klabu ya Pyramids FC ya Misri.

Mayele aling’ara kwenye michuano hiyo kwa kufunga mabao muhimu yaliyoiwezesha Pyramids kufika fainali na hatimaye kutwaa ubingwa dhidi ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, katika mchezo wa kusisimua uliomalizika kwa ushindi wa goli 2-1 nakufanya mchezo kuwa na jumla ya magoli 3-2.

Tangu ajiunge na Pyramids kutoka Young Africans SC ya Tanzania, Mayele ameonyesha kiwango bora na mshik**ano mkubwa na kikosi hicho, akivutia mashabiki wengi kwa uwezo wake wa kufumania nyavu.

Tuzo hii ni ushahidi wa mafanikio yake binafsi, lakini pia ni heshima kwa wachezaji wa Afrika Mashariki wanaoendelea kung’ara katika anga za kimataifa.

Ameandika Ahmed Ally:"Wakati Fei alipoondoka kwenu kuelekea Azam, mlimtukana sana yeye na hata familia yake, hasa Mama y...
02/06/2025

Ameandika Ahmed Ally:

"Wakati Fei alipoondoka kwenu kuelekea Azam, mlimtukana sana yeye na hata familia yake, hasa Mama yake mzazi. Lakini sasa mkiwa mnaona kijana anaendelea vizuri, mmeanza kujipendekeza kwake.

Fistoo naye alipojiunga na Pyramids, mlitengeneza visa vingi dhidi yake – vingine hadi vya kishirikina – ili kumzuia asicheze tena. Hata pale alipozungumza kupitia Azam TV, mkaamuru mahojiano yafutwe. Sasa hivi amekuwa bingwa wa Afrika, lakini bado mnaonyesha unafiki.

Tuache tabia ya kuwavunjia heshima wachezaji wanapotaka kuondoka. Dunia hii ni ndogo."

---🗣️Ahmed Ally

Ameandika Ahmed Ally afisa habari wa klabu ya Simba Sc💬"Kurwa aliandika barua ya kujilizalizaJana Kamshawishi Doi nae aa...
30/05/2025

Ameandika Ahmed Ally afisa habari wa klabu ya Simba Sc

💬"Kurwa aliandika barua ya kujilizaliza
Jana Kamshawishi Doi nae aandike malalamiko tena aweke na vitisho eti atajitoa kwenye mashindano, Yaani Doi nae anatishia watu, timu ina miezi sita tangu ianzishwe na yenyewe inaitishia mamlaka

Wameona haitoshi sasa wanawatumia Vibaraka wao kwenye Media kuhamasisha mgomo kwa Vilabu vingine
Vibaraka bila hata kupima ukweli wa jambo wanatoa taarifa Vilabu sita vimeandika Malalamiko na hawatocheza mechi zilizobaki bila hata kutaja vilabu husika

Yaani afungwe Doi halafu Azam aandike Malalamiko au afungwe mbadilisha majina kila siku halafu JKT asusie ligi??

Sisi tutaendelea kushinda mechi kadri Allah anavyotujaalia na kadri tunavyokua bora kiwanjani siku husika

Bodi ya Ligi na TFF endeleeni kusimamia haki, msisikilize kelele za Wapagazi wasiokubali kushindwa na kukubali kuwa msimu huu Simba ni bora

Waamuzi msiyumbishwe na kelele za wanaotaka kuwatia presha mharibu kazi yenu, pigeni kazi simamieni sheria za mpira

Hii ni Ubaya Ubwela Phase One, Tutakapoingia Phase Two watu watatembea bila nguo kwa kuchanganyikiwa"

🚨Huyu ni Jean Charles AhouaAmezaliwa 10 Februari 2002 jijini Abidjan, Côte d'IvoireKwa sasa, anacheza k**a kiungo mshamb...
30/05/2025

🚨Huyu ni Jean Charles Ahoua

Amezaliwa 10 Februari 2002 jijini Abidjan, Côte d'Ivoire
Kwa sasa, anacheza k**a kiungo mshambuliaji wa klabu ya Simba S.C. nchini Tanzania, baada ya kusajiliwa kutoka Stella Club d’Abidjan mnamo Julai 2024.

Alitunukiwa tuzo ya Mchezaji Bora wa Msimu (MVP) katika Ligi Kuu ya Côte d'Ivoire kwa msimu wa 2023/24, akifunga mabao 12 na kutoa pasi 9.

Ana sifa ya uwezo wa kufunga mabao kutoka mbali, uchezaji wa timu, na utengenezaji wa nafasi kwa wenzake.

Simba S.C. ilimsajili Ahoua kwa mkataba wa miaka miwili kwa lengo la kujenga timu yenye nguvu kwa muda mrefu. Anatarajiwa kuchangia kwa ubunifu na kasi, pia kujaza pengo lililoachwa na Clatous Chama aliyetimkia Young Africans.

Hadi sasa ligi kuu NBS ameshafunga mabao 15 na pasi za usaidizi (assist) 5

Ameandika mzee wa jambia"Tatizo Lako Leo ulikuja Kucheza Mechi 2. Mechi moja Kwaajili ya Black Stars na nyingine kwaajil...
29/05/2025

Ameandika mzee wa jambia

"Tatizo Lako Leo ulikuja Kucheza Mechi 2. Mechi moja Kwaajili ya Black Stars na nyingine kwaajili ya Malaika wako..

Nafikiri Heri Sasii hakuona tukio la Kuonyesha Dole la Kati Mara 2. Hii namkumbusha akaitazame na aweke kwenye ripoti yake

Hatuhitaji wachezaji wa aina hii Kwenye Ligi na Mpira wetu kwa ujumla. Unajua Mpaka nikajiuliza huyu jamaa mbona K**a Kipa Katoka?

Imagine Mpira upo kwenye tv saa Kumi Watoto wanatazama mtu anafanya ule Ujinga. Very Disappointed
Nilikuwa na Ku rate Juu sana,Lakini ulichofanya leo this is too low brother na Football yetu hatuhitaji mtu K**a wewe.

Hawa wachezaji sometimes jeuri tunawapa sisi wenyewe,tunawalipa mahela Mengi Kuliko uwezo hapo anajiona Didier Drogba or something
Gutted."

:

Nani anamdai Mukwala??Kipindi cha pili kinaendeleaSimba Sc 1-0 Singida BS(⚽Mukwala)
28/05/2025

Nani anamdai Mukwala??

Kipindi cha pili kinaendelea
Simba Sc 1-0 Singida BS
(⚽Mukwala)

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sports Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sports Online:

Share