
15/08/2025
Takriban watu 10, wakiwemo wanawake wawili, walifariki na wengine 37 kujeruhiwa wakati basi walimokuwa wakisafiria kugongana na lori lililokuwa limeegeshwa kando ya barabara katika jimbo la mashariki mwa India Magharibi mwa Bengal mapema Ijumaa, askari wa eneo hilo alisema.
Watano kati ya waliojeruhiwa walikuwa katika hali mbaya. Wahasiriwa wote walitoka katika jimbo jirani la Bihar, na walikuwa kwenye hija.
Waliojeruhiwa wamelazwa katika hospitali ya eneo hilo.
"Tunajaribu kufikia familia za wahasiriwa. Walikuwa wa wilaya ya Motihari jimbo la Bihar. Sita kati ya waliofariki wametambuliwa hadi sasa. Basi lililokuwa limebeba mahujaji liligonga lori lilokuwa limeegeshwa kando ya barabara. Hitimisho la kwanzai, inaonekana kwamba dereva wa basi alilala akiendesha, na kusababisha ajali hiyo mbaya," alisema askari huyo.
Picha ya maktaba)