Kilimanjaro Revival Fm

Kilimanjaro Revival Fm Most Credible Christian Radio broadcast from Moshi-Kilimanjaro."Power Of Revival"

Waratibu na wazimamizi wa uchaguzi,wametakiwa kujiepisha na makundi sogozi ya Whatsapp katika kipindi hiki cha uchaguzi ...
17/07/2025

Waratibu na wazimamizi wa uchaguzi,wametakiwa kujiepisha na makundi sogozi ya Whatsapp katika kipindi hiki cha uchaguzi ili kuepuka kutuma taarifa za siri zisizopaswa kutumwa kwa watu wengine.

Tahadhari hiyo imetolewa leo Julai 17,2025 Mjini Moshi,Mkoani Kilimanjaro na Mjumbe wa tume ya uchaguzi Dkt.Zakia Abubakar wakati akifunga semina ya siku tatu kwa waratibu wa uchaguzi wa mikoa,wasimamizi wa uchaguzi,wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo,maafisa uchaguzi na maafisa manunuzi 119 kutoka mkoa wa Kilimanjaro na Tanga.

“Hivi sasa yapo makundi sogozi ya whatsapp ,jitajidini katika kipindi hiki myapunguze ili msije kukosea kutuma taarifa yoyote katika makundi hayo ambayo haikutakiwa kutumwa kwao,kwa kuanza kutoa taarifa za siri ambazo tume haikukupa maelekezo kuzitoa katika utekelezaji wa kazi zako maana yake utakuwa umetenda kosa chini ya sheria ya kanuni za uchaguzi wa Rais,Wabunge na Madiwani za mwaka 2025 na utawajibika kwa kosa hilo” alisema Dkt.Zakia

Aidha amewataka washiriki hao kutafsiri mafunzo hayo kwenye usimamizi wa shughuli za kila siku za masuala ya uchaguzi kwa kuanza na vikao kwa vyama vya siasa,utoaji wa fomu za uteuzi na uteuzi wa wagombea wa nafasi za ubunge na kuhakikisha utoaji wa fomu za uteuzi na uteuzi wenyewe ngazi ya udiwani unafanyika kwa mumujibu wa sheria,kuhitisha na kuratibu k**ati za upangaji wa ratiba za kampeni na kuhitisha k**ati za maadili iwapo kuna changamoto zitajitokeza wakati wa kampeni.

“Katika maeneo mbalimbali tuliyopita wakati wa uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura tuliona changamoto ya kutobandikwa kwa mabango yanayopaswa kubandikwa ili kumuelekeza aliyekuwa anasifa za kuandikishwa na wadau wengine kufika mahali palipo na kituo hivyo tunasisitiza changamoto hiyo isitokee tena katika kipindi hiki cha uchaguzi hivyo mabango,orodha za majina na matangazo zinabandikwa kwa kulingana na kalenda ya utekelezaji wa majukumu ya uchaguzi ili kuepusha malalamiko na ukiukwaji wa masharti na sheria za kanuni za uchaguzi” alisema Dkt.Zakia
Cc ✍️

TAKUKURU Mkoani Kilimanjaro imekusudia kuwachukulia hatu watia nia nafasi ya Ubunge na Madiwani wanaolalamikiwa kufanya ...
17/07/2025

TAKUKURU Mkoani Kilimanjaro imekusudia kuwachukulia hatu watia nia nafasi ya Ubunge na Madiwani wanaolalamikiwa kufanya makosa ya rushwa katika mchakato wa kuelekea uchaguzi Mkuu mwaka huu.

Akizungumza Julai 15,2025 mara baada ya kumaliza semina maalum ya masuala ya kudhibiti na kukataa rushwa kwa watia nia nafasi ya Ubunge kwa majimbo ya uchaguzi Moshi Mjini,Vunjo na Moshi Vijijini, Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Kilimanjaro Musa Chaulo amesema kuwa wamepokea malalamiko kumi na Moja (11).

"Tumepokea malalamiko kadhaa mpaka sasa na tayari tumefanyia kazi malalamiko 11 ili kufahamu ukweli ndani yake na wapo watia nia ambao tumesha wahoji ambao wanaolalamikiwa kutengenezeana tuhuma ambazo siyo sahihi na majina yao tutayafikisha ndani ya chama chao "alisema Chaulo

Amesema kuwa TAKUKURU imeita watia nia wote wa Ubunge Mkoa wa Kilimanjaro ili kuwapatia mafunzo hayo na baadae watatoa elimu hiyo kwa watiania nafasi ya udiwani ili kuwajengea uelewa wa madhara ya rushwa katika uchaguzi kwa upande wao na kwa Wananchi.

Akizungumza katika mafunzo hayo mtiania Ubunge Jimbo la Moshi Wakili Willehard Kitali ameishauri TAKUKURU kuwataja watiania walio bainika ili waweze kufahamika kwa wananchi na mamlaka nyingine hali itakayo sadia kukomesha vitendo vya rushwa.

"Tunataka kusikia ni akina nani wanaojihusisha vitendo vya rushwa sababu mmekuwa mkieleza kuwabaini walarushwa na wapokeaji ila hatusikii majina yao yakiwekwa wazi"alisema Kitali.

Naye Joseph Mlay mtia nia Jimbo la Vunjo ameshauri baada ya CCM kurudisha majina matatu ya watia nia watakaogombea katika kura za maoni,taasisi hiyo ikutane nao ili kudhibiti vitendo vya rushwa kuelekea uchaguzi mkuu.
Cc ✍️

Waratibu na wasimamizi wa uchaguzi wametakiwa kusimamia viapo,kutunza siri na kujitoa au kutokuwa mwanachama wa chama ch...
15/07/2025

Waratibu na wasimamizi wa uchaguzi wametakiwa kusimamia viapo,kutunza siri na kujitoa au kutokuwa mwanachama wa chama cha siasa katika kipindi chote cha uchaguzi ili kutimiza matakwa na masharti ya tume huru ya uchaguzi.

Akizungumza hii leo Julai 15,2025 Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kuanzia Julai 15 hadi 17 yaliyowakutanisha washiriki 119 kutoka mkoa wa Kilimanjaro na Tanga yakilenga kuwajengea uwezo wa kusimamia uchaguzi mkuu ujao Mjumbe wa tume ya uchaguzi Dkt.Zakia Abubakar amewataka washiriki hao kusimamia viapo na kutunza siri kipindi chote cha uchaguzi ili shughuli ya uchaguzi ifanikiwe k**a ilivyo kusudiwa.

Amesema kuwa waratibu wa uchaguzi wa mikoa,wasimamizi wa uchaguzi,wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo,maafisa uchaguzi na maafisa manunuzi wanapatiwa mafunzo hayo baada ya kuteuliwa kwa mujibu wa sheria na tume ya uchaguzi kuwaridhia kutokana na utendaji wao wa uadilifu ,uzalendo na uchapakazi.

Amewataka wanao simamia uchaguzi kwa mara ya kwanza kujifunza kwa haraka na kupata uzoefu kupitia majadiliano ya Pamoja na wale wazoefu kutumia fursa hiyo kuongeza maarifa mapya na kubadilishana uzoefu na washiriki wengine.

Aidha amewataka kujiepusha kuwa vyanzo vya malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa na wadau wa uchaguzi kwa kuzingatia ipasavyo kanuni,Katiba,sheria na maelekezo mbalimbali yalitotolewa na yatakayo tolewa na tume

“Vishirikisheni vyama vyote vya siasa vyenye usajili kamili katika hatua zote kwa kuzingatia matakwa ya kikatiba,sheria,kanuni na maelekezo mbalimbali ya tume pamoja na wadau wa siasa ambao wanapaswa kushirkishwa kwa mujibu wa tume huru ya uchaguzi.” Alisema Dkt.Zakia

Mafunzo hayo yanaendeshwa nchini kote na Tume huru ya Taifa ya uchaguzi (INEC) yakilenga kuwajengea uwezo waratibu wapya na wazamani namna ya kufanya uchaguzi mkuu wa mwaka kwa njia ya haki na amani kwa ustawi wa Tanzania.

Serekali imethibitisha uwepo wa shilingi bilioni 488 za kutekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara ya njia nne kutoka...
14/07/2025

Serekali imethibitisha uwepo wa shilingi bilioni 488 za kutekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara ya njia nne kutoka Mailisita Wilaya ya Hai hadi Kiborloni katika Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro,unaotarajiwa kuanza wakati wowote, baada ya serikali kupokea fedha hizo zitakazo kamilisha mradi huo.

Hayo yameelezwa Julai 13, 2025, na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Wilayani Mwanga Mkoani Kilimanjaro katika Ibada ya kuwekwa wakfu na kuingizwa kazini Askofu wa Dayosisi ya Mwanga Dkt.Daniel Mono.

"Barabara hii kutoka Mailisita mpaka Kiborloni, itajengwa njia nne, na kutoka Kiborloni mpaka Holili, itapanuliwa ili iweze kupitika kwa njia mbili, huku kukiwa na nafasi ya kutosha pamoja na ya waenda kwa miguu,kazi hiyo itaanza wakati wowote, na daraja letu kubwa liko pale Kikafu. Barabara hii mpya haitapita kwenye daraja lile tena,itapita daraja jingine ambalo linanyooka linatokea kule mbele (Kwa Sadala) alisema Waziri Mkuu

Aliongeza kusema kuwa, "Barabara ile ya sasa itabaki k**a ilivyo, ili huko mbele, ambaye anataka kupita daraja jipya apite na anayetaka barabara ya zamani apite kila mmoja ataamua mahali pa kupita." Waziri Mkuu Majaliwa.

Itakumbukwa kuwa Machi 3, 2016,Rais wa Tanzania, Hayati Dk. John Magufuli na mwenzake wa Kenya, Rais mstaafu, Uhuru Kenyatta, waliweka jiwe la msingi katika barabara hiyo itakayounganisha Jiji la Arusha na Mji wa Voi, nchini Kenya.

Barabara hiyo kutoka Arusha hadi Taveta inatarajiwa kurahisisha uchukuzi na kuimarisha biashara kati ya mataifa hayo mawili.

Barabara hiyo itakuwa na umbali wa kilomita 234, na ni sehemu ya mradi mkubwa wa barabara inayotoka Arusha na kupitia Holili na Taveta hadi Mwatate.
Cc ✍️

Daktari bingwa wa watoto kutoka Hospitali teule ya Kibosho Wilayani Moshi Mkoani Kilimanjaro,Magreth Joseph Swai (30) am...
14/07/2025

Daktari bingwa wa watoto kutoka Hospitali teule ya Kibosho Wilayani Moshi Mkoani Kilimanjaro,Magreth Joseph Swai (30) ameripotiwa kujiua kwa kujinyonga kwa kutumia waya wa antena.

Akizungumza kuhusu tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro SACP Simon Maigwa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo ameeleza kuwa tukio hilo lilitokea Julai 10,2025 majira ya saa tatu kamili usiku katika makazi yake yaliyopo Longuo Kata ya Longuo,Tarafa ya Moshi Magharibi.

Amesema Marehemu alitumia waya WA antena alioufunga kwenye nondo ya mlango wa chumbani katika nyumba anayoish.

"Chanzo cha tukio hilo ni msongo wa mawazo uliotokana na afya ya akili ambapo Marehemu alifungua waya huo kwenye nondo iliyopo juu ya mlango na kujitundika" alisema SACP Maigwa.

RPC Maigwa ameongeza kuwa marehemu alianza kuugua ugonjwa wa afya ya akili akiwa katika mafunzo kwa vitendo k**a Daktari maalum wa watoto wa miaka minne iliyopita.

Taarifa hizi zinakuja wakati ambapo Mfanyabiashara anaye fanya kazi zake Moshi na Dodoma mkazi wa Msufini Wilayani Moshi Ronald Malisa (35) naye akiripotiwa kujinyonga Julai 10,2025 kwa shuka chooni kwake ambapo Jeshi la Polisi lilieleza chanzo ni msongo wa mawazo uliosababishwa na tatizo la afya ya akili miezi nane baada ya kufunga ndoa yake,ambapo mazishi yake yanatarajiwa kufanyika Julai 15,2025.
Cc ✍️

BREAKING: Humphery Polepole Balozi na Mkuu wa Kituo Cha Uwakilishi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Havana -Cuba pamo...
13/07/2025

BREAKING: Humphery Polepole Balozi na Mkuu wa Kituo Cha Uwakilishi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Havana -Cuba pamoja na uwakilishi wa eneo la Karibe, Amerika ya Kati na nchi rafiki za Colombia, Venezuela na Guyana ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo kutokana na kile alichodai kuwa hawezi kuendelea kuwa sehemu ya uongozi usiohamasika na utii wa misingi ya katiba ya nchi na chama, haki, maadili, utu na uwajibikaji kwa wananchi.

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐔𝐅𝐔𝐀𝐓𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐊𝐀 𝐌𝐈𝐓𝐀𝐍𝐃𝐀𝐎 𝐘𝐄𝐓𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐀𝐌𝐈𝐈

@ Kilimanjaro revival fm

Kocha Mbwana Makata amejiunga na Klabu ya Polisi Tanzania kwa mkataba wa miaka miwili.Makata ametambulishwa leo Julai 9,...
09/07/2025

Kocha Mbwana Makata amejiunga na Klabu ya Polisi Tanzania kwa mkataba wa miaka miwili.

Makata ametambulishwa leo Julai 9, 2025 Jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Timu hiyo Kamishna wa Polisi Jamii CP Faustine Shilogile.

Kocha Makata ana historia na Polisi Tanzania kwa kuwa ndiye aliyekuwa Mwalimu Mkuu wakati inapanda kucheza Ligi Kuu msimu wa 2018/2019.

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐔𝐅𝐔𝐀𝐓𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐊𝐀 𝐌𝐈𝐓𝐀𝐍𝐃𝐀𝐎 𝐘𝐄𝐓𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐀𝐌𝐈𝐈

@ Kilimanjaro revival fm

Alianza soka lake 2012 akiwa Azam FC ambapo alionesha uwezo mkubwa hadi kuwa kipa namba moja wa timu hiyo na kuisaidia k...
09/07/2025

Alianza soka lake 2012 akiwa Azam FC ambapo alionesha uwezo mkubwa hadi kuwa kipa namba moja wa timu hiyo na kuisaidia kutwaa ubingwa wa ligi kuu 2014.

Mwaka 2017 alijiunga na Simba SC na kuleta mafanikio makubwa kwa timu hiyo, ikiwemo kushinda mataji manne ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Mwaka 2023 alipata majeraha ya nyonga, yaliyomuweka nje kwa muda mrefu.

July 2025, anajiunga tena na Azam FC k**a mchezaji huru, amesaini mkataba hadi 2028.

Kila la kheri Tanzania One, Aishi Manula.

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐔𝐅𝐔𝐀𝐓𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐊𝐀 𝐌𝐈𝐓𝐀𝐍𝐃𝐀𝐎 𝐘𝐄𝐓𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐀𝐌𝐈𝐈

Kilimanjarorevivalfm

📻 SIKILIZA KILIMANJARO REVIVAL RADIO
95.9 KILIMANJARO, ARUSHA, TANGA, MANYARA


Address

Mapumulo

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kilimanjaro Revival Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kilimanjaro Revival Fm:

Share