Hadithi Za Dhahabu

Hadithi Za Dhahabu hadithi tamu

13/05/2025

MAHESABU

Safari ya chrismass......01Asubuhi tarehe 20 nimeandaa mizigo yangu salama nikaangalia tiketi yangu ipo nikaweka kqenye ...
21/12/2024

Safari ya chrismass......01
Asubuhi tarehe 20 nimeandaa mizigo yangu salama nikaangalia tiketi yangu ipo nikaweka kqenye mkoba kisha nikashika 20,000 nikatazama kwa uchungu ile pesa sababu sikuwa na pesa ya kula njiani bola hiyo pesa niitunze nikifika mwanza nita nunua hata maharage nipeleke nyumbani, basi nikafanya hivyo nikaitunza kisha nikaanza tutembea haraka ili niwahi daradara ambapo nikipanda mia sita mia nne ntapata hata hela ya karanga ili inipoze njaa, nikadimama pale kituoni kwa muda lakini hakukuwa na magari zaidi ya private tu na sikutaka lift 😭😭😭 nimekoma mimi na lift za njiani nimekoma kabisa sizitaki tena aya ikasimama gari moja akashusha kioo uyo kaka akasema vip unaelekea stend twende nikasema hapana namsubiri mume wangu akanipitia kaenda hapo sheri, yule kaka akashuka kwenye gar akatazama huko sheri hakuna gar kisha akanitazama akasema mbona hakuna gari? Mimi nikamwambia kwani vipi kaka ebu fata ya kwako achana na maisha yangu kisha ikasimama daladala nikapanda nikafika stend nikanunua zangu karanga za mia tatu na maji ya mia nikaweka kwenye mkoba nikaingia kwenye gari lililokuwa linaelekea mwanza nikaweka mizigo yangu sawa kisha nika kaaa katika siti yangu nikatuma meseji kwa mama kuwa nimeanza safari , ilikuwa saa kumi na mbili tayari lakini gari halikuanza kuondoka kumbe kuna mtu lina msubiri watu wakaanza kupiga makelele nyie derevaa unatuchelewesha, dereva akasimama akaomba radhi akasema kuna mtu ni mzee na ni mgonjwa sana ndio maana wanamsubiri basi ilipofika saa 12.30 wakaingia waliokuwa wanasubiriwa ambaye ni yule kaka niliyemjibu vibaya kule stend ya daladala pamoja na wenzie na mbibi hivi anaonekana ana miaka mingi sana na pia ni mgonjwa wakamkalisha kisha kila mtu akawa ana angaza siti yake ilipo kiukweli moyoni nilimuomba sana Mungu asiwe ana kaa karibu yangu niliomba sana lakini akatembea akasimama karibu yangu kisha akasema oh hapa ndio D22 ina maana ana kaa na mimi kisha akatoa simu na usb akaweka begi lake juu kisha akaa kaa akanisalimia nikaitikia , safari ikaanza hapo natamani usingizi unichukue tu maana niliyo nayo kichwani ni makubwa sana ,
Davie: naitwa devie wewe unaitwa nan?
Alinitazama na kuniuliza swali hilo nikamtazama nikamwambia naitwa Annah
Davie:okay unafika mwanza kabisa au unaishia njiani?
Anah: nafika mwanza.
Davie: ok kumbe tupo safari moja asa mbona muda ule ulikataa lift?
Anah; kwani lift lazima jaman ?
Davie: dada wewe mbona mkali sana ?
Anah: niache bana sina mood ya kuongea.
Kisha nikachukua mtandio wangu nikajifunika nikapitiwa na usingizi nilipo shtuka ilikuwa saa mbili hivi lakini pembeni yangu hakuwepo uyo davie alikuwepo bibi nikatazama kumbe walibadilishana siti nikamsalimia ila hakuitikia nikasema uenda hajui kiswahili au ana shida ya kuongea nikanyamaza zangu, hapo njaa inanivuluga usiku nililala nimekunywa chai na maandazi ya mia mia mawili, kidogo yule bibi akaletewa kachupa kadogo akamiminiwa chai ya maziwa akapewa na vitumbua kwa njaa niliyokuwa nayo ile harufu ya vitumbua ilinivuluga sana πŸ₯² sikusema kitu ak**aliza kula hapo akaletewa hapo kamfuko kalikuwa na sambusa mimi hapo nimetulia tu nasikilizia harufu huku tumbo linazidi kunisokota sana πŸ₯²πŸ₯²...itaendelea.....

09/12/2024

Im back

19/06/2024

Usiku wa manane ......5
Mzee ally akasema Wacha nitokee nikamkague uyu Mzee ana nini Cha zaidi ndani ?
Akataka kutoka akashindwa aka hangaika sana pale sebureni lakini hakiweza kutoka uwiii akabaki ana duwaaa pale sebureni akasema basi atoke Kwa njia ya kawaida 🀣 akafungua mlango ukagoma kufunguka πŸ˜­πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ ikabidi aende kwenye chumba Cha Betty agonge ili afunguliwe weee alipo gonga mlango hivi alipigwa short Sasa ikawa short kokote atakapo gusa 🀣🀣🀣🀣 Mzee ally alihangaika sana pale sebureni mpaka pakakucha baba Betty akampita tu k**a hamuoni ikabidi Mzee ally apige magoti kumuomba msamaha baba Betty akasema wewe si ndio kiboko ya Kila kitu jaman au sio wewe? Mzee ally huku machozi yakimtoka hapana jaman hapana 😭😭😭mkubwa ni 2we naomba unisamehe niludi kwangu sitawasumbua Tena nakuapia, basi baba Betty akapiga maombi pale ikumbukwe baba Betty ni mwinjilisti katika Moja ya kanisa hapo mjini , akapiga maombi na kumsalisha sala ya Toba Mzee ally Kisha akamruhusu aondoke, Betty alishuhudia hayo yote na kufurahi sana kuona hivyo kuwa baba yake amemuokoa ,
Baada ya chakula Cha jioni Betty na babake Waka kaaa kuongea baba yake aka msihi sana aludi kanisani ndiko wema ulipo na Hawa waganga hawatamsumbua Tena, basi Betty alikubali akaanza kusali akiomba biashara yake iwe nzuri Tena basi akaanza Tena biashara ya chai Kwa mtaji aliyo pewa na babake lakini mambo sivyo alivyo tegemea biashara bado ilikuwa mbaya tu akawaza labda abadili biashara lakini haiwezekani maana Hana mtaji akawaza sana ikabidi ajiunge kikundi Cha maombi akawa anaombea biashara yake ila ikachangamka Tena sana tu na akaanza kuona manufaa ya maombi Yale 😁😁 hapo Sasa akasema alichelewa wapi yeye kuanza kusali Toka kitambo πŸ˜‚, Kuna siku mchungaji aliita wale wafanya biashara wote wake mbele ili awaombee basi beti nae akapita wakaguswa kichwa wakaombewa baadae ukawa wakati wa shuhudia kuna kijana akasema alikuwa ana mdai mtu million 200 na mwaka Sasa na nusu ila baada ya maombi kalipwa pesa zake uyo kijana aliiitwa Emma, baada ya kutoka kanisani Emma alimfuata Betty na kumsalimia wakajitbulisha na kubadilishana namba hapo Betty anawaza zile pesa πŸ˜‹πŸ˜‹....... itaendelea

04/06/2024

usiku wa manane.....04
mama Betty huku kakucha sura akasema Mimi siwezi kukubali mwanangu aende kwenye familia hile Kila mtu anaijua Ile familia walivyo wachawi alafu nikamtelekeza mwanangu kule 😭😭😭😭 wee Toka hapa nakwambia Toka yule kijana hakuondoka akaka kaa pale akimgojea baba Betty aludi adi saa mbili usiku baba Betty akafika nae jibu lilikuwa Lile liel Kuwa hawezi kumtoa mwanae katika Ile familia wake watano watoto wengi k**a mbuzi wanao jichunga wenyewe wajukuu Sasa k**a siafuu alafu Betty akaoshi vi na bado isitoshe wale ni wachawi mnoo kutwa kulogana mtoto wa mamdogo kaloga mtoto hapana k**a mnatuua tuuweni lakini Betty hawezi kuolewa na uyo Mzee,
Kisha yule kijana aliye tumwa barua akasema Mimi nimefikisha hapa naiacha hapa siwezi ludi nayo k**a mnaichana ni nyie lakini mie nimefikisha ujumbe.
baba Betty akachukua kiberiti akashika Ile bahasha hapo ndani Kuna laki mbili akaanza kuichoma moto mbele ya yule mtoto wa mganga πŸ˜‚πŸ˜‚ mpaka ikaishilia akamwambia Aya potea ....
usiku wakiwa wamelala baba Betty alibanwa mkojo akaenda chooni alipotoka akamkuta Mzee ally mganga kakaa sebureni.. na wewe Mzee unafanya nn hapa....
nimekuja tuongee kistaarabu tu bila tatizo ...
nimesema hivi sitaki labda uniue....
baba Betty akafunga mlango akasema najua hujapitia mlangoni hivyo pita hukohuko uliko pitia mwanzo lakini mwanangu huwezi kumchukua, akaingia kulala, Mzee ally akamfuata huko huko chumbani lakini Cha kushangaza kule chumbani alishindwa kuingia na uganga wake wote na uchawi wake wote alishindwa kuingiaaa
itaendelea...

30/05/2024

Usiku wa manane .... 03
Palipo kucha mganga akamuomba asiondoke akae apo hapo Kwa siku tatu Betty alikubali na ukumbuke hapo chakula mganga πŸ˜‚ anakula k**a kawaida 🀣🀣🀣🀣basi baada ya siku kuisha Betty akaludi biashara yake ikiwa ya kawaida sana sio k**a ilichangamka kiviile hapana, akawa ana shangaa vipi mbona maokoto hayaji k**a alivyokuwa anatalajia akaludi Kwa mganga mganga akamwambia Kuna dawa ya kuwekewa siku Saba oooh Betty akasema ujinga huuu basi wakajibishana pale mganga πŸ˜‚ akamfanya bubu hapo hapo Betty na akamwambia nilikuwa nakutamani sana Toka unasoma shule na Mimi ndio nilikutia Giza usipate ajira selikalini Wala kwenye kampuni ili ubaki hapa hapa na ukitaka kupona na kuwa salama ni Bora ukubali uwe mke wangu wa sita upo dada? 😭😭😭😭😭 Betty alilia sana hata hakiweza kusema mdomo unafunguka lakini maneno hayatoki alikuwa analia Kwa uchungu tu basi ikabidi akubali 😱😱😱😱 huku moyoni akiwa ana sikitika sana inakuwaje hivi jaman yaani awe mke wa kibabu kizeee uwiii 😭😭😭😭alilia, yule mganga akamfumbua mdomo akasema chumba chako nishakuandalia utalala na Mimi mpaka hizo siku Saba na hao marafiki zako watakuja kwako na watakushangilia zaidi ya zamani, basi Betty akakubali 😒😒😒 aka kaa pale mpaka siku ya Saba kweli alipo ludi nyumbani marafiki zake walimshangilia sana na walimpenda mnooo lakini hakuwa na furaha Tena na hayo maisha aliumia moyoni hapo usoni alitabasamu akaenda Kwa mama yake akamwambia kuwa anataka kuolewa, mama yake akamwambia mwanangu ni jambo jema lakini kwann usisimame kwanza kibiashara mpaka hata mwakani ndio uolewe? Betty alilia sana huku akimwambia mama yake hapana mama Mimi nimepata mwanaume anayenipenda kweli nataka kuolewa we mwambie baba jumatano wanakuja kuleta barua ya uchumba, mamayake akauliza kwani uyo kijana ni nan? Ni WA hapa mtaani au?
Betty alimtazama mama yake kwa uchungu asijue amwambie vipi ila alilia sana 😭😭😭😭😭 machozi ya uchungu yalimtoka sana, mara mlangoni ikasikika odiii mama Betty akamkaribisha alikuwa ni bi zubeda .
Mama Betty; karibu mama karibu ndani
Bi zubeda: hata sihitaji karibu Yako uyo mtoto wako Betty upo?
Mama Betty; ndio yupo ndani
Bi zubeda akaingia ndani Kwa fujo akafika akamkaba nguo Betty.
' wewe ndio unajifanya mtamu sana kuliko Wana wake wote tulio olewa na mume wangu sio?' ... Betty hakujibu kitu mama Betty akapata jawabu kuwa mwanae anaolewa na Mzee uwiii alipigwa mwanoooo wa hatari ,
Mama Betty; mwanangu umekosea nn wewe jaman ?
Betty; mama ngoja nikuelezee
Bi zubeda; hakuna Cha kuelezea hapa Sasa nakupa siku tatu uachane na mume wangu tuo olewa tumetosha Mimi k**a bi mkubwa naongea wewe ni k**a mjukuu wangu huwezi kuwa mke mwenzangu Sasa k**a unataka kushindana na Mimi endelea kuja kulala Kwa mume wangu...
Mama Betty akazimia hapo hapo maana hakuamini maneno ya bi zubeda πŸ™ŒπŸ™Œ majirani wamejaa dirishani maana sauti ya bi zubeda ilikuwa juu sana, Kisha bi zubeda akaondoka Kwa mbwembwe na tambo , majirani wakaingia ndani kumsaidia mama Betty huduma ili akae sawa hapo Betty analia tu Hana la kufanya...
Sasa mtaa mzima unajua k**a Betty anatoka kimapenzi na Mzee ally mganga maalufu Kwa Ile kata 😱😱😱ni aibu Kila mja anaongea lake mara ukute na mtaji kautoa uko Kwa mganga na wengine ooh Betty apikiagi mwiko anapikia mkono wa mtoto 😭😭😭😭alilia akafungua kibanda maana wateja walimkimbia, akaludisha na chumba alichokuwa amepanga akakusanya vitu vyake akaludi nyumbani kuishi Kwa mama yake,
Wiki ikapia Betty atoki kutembea anaona aibu Kwa maneno yalivyo zagaa, basi siku Moja akaja kijana wa kwanza wa familia ya Mzee ally mganga anaitwa salumu akafika akamsalimia mama Betty lengo ilikuwa kuja kuleta barua ya uchumba wa baba yake, mama Betty akagoma kuipokea akasema hapana msubiri babake aje Mimi sipokei hii laana ...... itaendelea

29/05/2024

Usiku wa manane......02
Basi bhana Betty mambo yakamnyookea akaanza kuuza na chai hapo hapo akatengeneza ka kibanda kazuri ka mabanzi ya mbao akaweka chai akawa anapika na chapati weee nan hakumjua Betty hicho kipindi akajiunga michezo mitatu Kila shughuli za mitaano yumo full kujiachia k**a una shughuli Yako lazima umualike usipowalika unanuniwa na gang lake walikuwa wanajiita watoto wazuri, hii gang ilikuwa balaa k**a una bifu na mtu wanaliunga wanakuchangia utachambwa na ukileta mdomo utapigwa k**a mwizi πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚, na wakishikwa na polisi Betty anatoa hela wanaachiwa kifupi Betty ndio alikuwa don wao na wao k**a machawa ...
Sasa mama jirani nae kwenye uchawi sio kidogo sababu biashara ilimharibikia kabisa wateja hawaji hata Betty akimaliza chakula chote bado hawakanyagi kwake weee ikabidi asafiri aende Tanga Kwa shangazi yake sababu mambo yalikuwa sio mambo huku michezo ana daiwa huku vikoba bado kausha damu akaona ata dhalilika Bora ajiongeze akasafiri k**a siku tatu hivi alipo ludi akaludi na Hali mpya Kwanza Lile gang la watoto wazuri wakawa wanapenda kwake ana wapa chai na vitafunwa bure wakaamia kwake mpaka mwantumu 😱 Betty alikuwa hajui ila siku Moja ana shangaa mtaa wa nyuma Kuna shughuli duh mbona naskia vigoma nan tena kumbe Kuna shughuli pambee tu huko ikabidi aende kuangalia kuona mashoga zake wooote wapo huko na pia Wana Cheka na mwasimu wake 😒😒Betty aliduwaaa nini hiki mpaka bff mwantumu nae yupo huko πŸ₯ΊπŸ₯ΊπŸ₯Ίkhe akaludi nyumbani Kwa hasira akapigwa mahesabu yake huko ndani pesa ikawa haitoshi akiangalia chakula kimeisha lakini pesa haionekani looooh chumaulete Gani uyu Tena kaingia humu 😒😒😒uwiiii basi akaludi usiku ule Kwa mganga akamwelezea Kila kitu Sasa mganga akawambia uyo mama wa jilani mama Amina kachukua nywere zako yaani uzuri wako,kupendwa kwako na nyota Yako vyote kachukua. 😱😱😱Eeh Sasa itakuwaje, mganga akamwambia kwanza inabidi nikuoshe dawa alafu dawa nyingine nikuwekee huko Kwa k. Basi betty akakubali mganga akatayarisha dawa ikiwa ni saa sita za usiku akamtoa nje Betty akaingia kwenye beseni akaanza kusuguliwa na madawa mwili mzima mpaka nywere akasuuzwa ikachukuliwa dawa nyingine akasuguliwa Tena ak**aliza akaambiwa hii hautajikausha maji yaache yakauke yenyewe, akasimama pale ndani mpaka aka kauka kisha mganga akachukia dawa nyingine akachanganya na mafuta ya N**i akaanza kumpaka Kisha aka mwambia haya utakuwa unajipata usoni tu akaitikia ndio... Mganga akamwambia Sasa subiri ifike saaa Tisa na nusu ndio nikuwekee dawa....
Ilipofikoa saa Tisa na nusu mganga akapaka dawa yenye rangi ya blue katika uumie wake Kisha aka mlaza Betty ili amuwekee, Betty akashtuka akasema hapana jaman siwezi, yule babu akamwambia Binti unataka mafanikio au hutaki? 😒😒😒Ikabidi tu akubali huku anaumia maana Betty alikuwa haijawahi kukutana na mwanaume kimwili.......
πŸƒπŸƒπŸƒπŸƒ Itaendelea

28/05/2024

usiku wa manane .......01
Alikuwa anaitwa Betty ndio kahitimu chuo ngazi ya diploma. Katika mambo ya account eeh kazi nazo hola na kale ka bwana aliko kuwaga Nako chuo Nako kamemchunia akituma sms azijibiwi 😒😒😒 ni huzuni πŸ«’πŸ˜†πŸ˜† Aya batty wa watu akaanzisha kuuza vitumbua pale kibarazani kwao ili apate mia mbili mia tatu, Mungu ni mwema wateja wakawa Wana jaa balaa πŸ‘πŸ‘ lakini Sasa kitu Cha kusikitisha sana jirani yake naye akaanzisha hiyo hiyo biashara ya vitumbua Tena yeye anajaza sukari ndiiii k**a vile haitaji faida Kila mtu alikuwa ana sifia vile vitumbua vya mama imma na kufanya biashara ya Betty kudolola,
Siku Moja akiwa anatoka kusaga Michele akili ikiwa imechoka maana vitumbua vina lala tu havina soko akili imechoka sana yupo njiani na mawazo tele πŸ₯²πŸ₯²akakutana na mwantumu wanasalimiana
Mwantumu; shoga nakuona biashara inakukondesha tu ndugu yangu
Betty; we acha tu asiee hii challenge ya mama jilani sio poa.
Mwantumu; usijali jioni uje nikupe maujanja.
Betty; ujanja upi Tena?
Mwantumu; we njoo nyumbani hapa mjini ni unjanja ndugu .
Basi wakaagana jioni ilipofikoa Betty alitamani sana kujua mwantumu ana kipi Cha kumsaidia akaenda mpaka kwao mwantumu, akamkuta mwantumu yupo tayari kabisa Kwa safari Betty akauliza tunaenda wapi mwantumu akamwambia sio mbali sana ni huku nyuma tu, basi wakaongozana wakavuka balabala ya kwanza na ya pili na ya tatu Naya nne wakakatiza vichocholo vingi sana kiasi Betty alisahau alipo tokea...
Wakafika Kwa Mzee majuaji ni mganga wa kienyeji wakaeleza shida zao wakapewa dawa ya kuchanganya kwenye uji wa vitumbua pamoja na kuoga Kisha wakaludi, Betty akafanya k**a alivyo ambiwa kesho yake watu Waka jaa Tena kwenye kigenge chake mambo yakawa bam bamπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Itaendelea......

My dream girlfriend mermaid......01Nikiwa usingizini bado nahangaika sioni njia ya kupokea niliangaika sana nikamuita ma...
17/03/2024

My dream girlfriend mermaid......01
Nikiwa usingizini bado nahangaika sioni njia ya kupokea niliangaika sana nikamuita mama lakini hakuitikia nikajikuta nakimbia sana pumzi inaisha njaa Kali sana nikaishiwa nguvu nipo sehemu ambayo siielewi hata kidogo Kuna Barbara ya vumbi ambayo Haina mwisho najaribu kujisogeza mbele mara naona mtu Kwa mbali nikamuomba anisaidie lakini uyo mtu k**a aniskii kabisa nika mwita Tena weee jaamaa lakini alionesha hata Hana ushirikiano nikashindwa Sasa nikalala lakini usingizi hauji, nikatoka kwenye ndoto najaribu kufumbua macho lakini siwezi naskia mama yupo nyumba ya nyumba anaongea lakini siwezi najaribu kumuita lakini mdomo haufunguki nikajisemea au ndio nimekufa nikaogopa sana, Sasa kwann siamki ?....... Hata mikono siwezi kuitikisa na hema tu niliogopa sana aisee .... Mara mrango ukagongwa alikuwa ni Anna nilisikia saiti yake lakini siwezi kutoka siwezi kufumbua macho mara mama akaja na funguo akafungua na kuja kunishika ndipo nikawa k**a nimepatia uzima nahema sana siamini k**a nimetoka katika jinamizi lile .......
Nikamkumbatia mama sana nikasema nimeota ndoto ya ajabu naona k**a nakufa mama naomba unisamehe sana najua Jana nilikutukana sana mama yangu nisamehe sana... Huku machozi yakinitoka sana kiukweli sikuwa mtoto mzuri Kwa wazazi wangu nilikuwa na kiburi na siku ya Jana usiku nililudi mapema sana lakini sikutaka kuongea na mtu na niliposemeshwa niliwakaripia sana na kumtukana sana mama baba akakasilika na kusema k**a najiona nimekuwa mkubwa basi nitoke hapo nyumbani kwake kidogo nipigane na baba lakini mama aliingilia kati na hapo ndipo baba akagoma nisile chakula Cha pale nyumbani kwani najiona mkubwa sana, mama akanifichia chakula na kuniletea chumbani nilichukua sahani na kumtupia nayo usoni Kisha nikafunga mlango nikalala....
Muda huo nilimtazama mama Ile asubuhi na kugundua usoni Kwa mama kaumia sana kapasuka mpaka karibu na jicho......
Itaendelea.....

Tagg watu watatu nilete story
06/03/2024

Tagg watu watatu nilete story

Address

Mapumulo

Telephone

+255754816149

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hadithi Za Dhahabu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Hadithi Za Dhahabu:

Share