
12/07/2025
🛑 : Kagame ampokea raïs mstaafu wa Kenya kujadili kuhusu amani mashariki mwa DRC
Raïs wa Rwanda, Paul Kagame alimpokea raïs wa mstaafu wa Kenya Uhuru Kenyatta jioni ya hiyo Ijumaa Julai 11, 2025 katika kijiji cha Urugwiro ambapo inasemekana kuwa mazungumzo yao yalilenga kujadili kuhusu vita vinavyoendelea mashariki mwa DRC.
Katika kikao chao, mazungumzo ya Uhuru Kenyatta anayetajwa kuwa mmoja wa Wapatanishi wa EAC-SADC kwa mchakato wa kuleta amani mashariki mwa DRC na mwenyeji wake Pal Kagame yalijikita zaidi kwenye juhudi zinazoendelea ili kufanikisha kuleta suluhu kwa mzizo huko Kivu Kaskazini na Kusini pamoja na kutafuta njia za kuleta amani ya kudumu na kufafanua sababu za msingi za mzozo usioisha huko Mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩.
..✍🏼Unahisi undani wa kikao hicho cha wawili hao ulikuwa kutafuta suluhu ili kurejesha amani mashariki mwa DRC ao yapo mengine yao ya nyuma ya pazia?