BundafmTz

BundafmTz Ngurumo ya Jamii 92.1mhz

Ni kweli wanafunzi watafanya vizuri kazi ya upandaji miti kuliko watu wengine kwa sababu wao hawana kazi nyingine zaidi ...
17/06/2025

Ni kweli wanafunzi watafanya vizuri kazi ya upandaji miti kuliko watu wengine kwa sababu wao hawana kazi nyingine zaidi ya kusoma? Naomba maoni yako kwenye comment.

”Upandaji miti ni njia mojawapo ya utunzaji wa mazingira,kupata kivuri na upatikanaji wa matunda ya kutosha katika jamii yetu” Tegemeo Masiti mhifadhi misitu Wilaya ya Bunda. Na Witness Joseph Akizungumza na Bunda Fm Radio kwenye kipindi cha ukurasa mpya mhifadhi…

BUNDA.Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Mjini BUNDA (BUWSSA) imetambulisha mradi mpya  wa maji  katika kata ya ...
05/12/2024

BUNDA.

Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Mjini BUNDA (BUWSSA) imetambulisha mradi mpya wa maji katika kata ya Wariku Halmashauri ya mji wa bunda.

Mradi huo unatarajia kugharimu shilingi bilioni 1,620,121,364.90 mpaka kukamilika kwake , utekelezaji wake ni wa muda wa miezi sita umeanza tarehe 1 mwezi wa 12 , 2024 mpaka tarehe 31 mwezi wa 5 ,2025 hadi sasa umefikia asilimia 8.

Akitambulisha mradi huo Katika mkutano wa hadhara uliofanyika mtaa wa Kamkenga ,Mkurugenzi wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Mjini bunda ,Esther Gilyoma amesema kupitia wizara ya maji inaendelea kutekeleza na kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama pia mradi huo utaenda kunufaisha jumla ya wakazi 33,088 katika kata ya wariku.

Gilyoma amesema kuwa kazi zitakazotekelezwa katika mradi huo ,uchimbaji wa mtaro km 40, ununuzi wa bomba,ujenzi wa tangi la maji lenye ujazo wa lita 200,000,ununuzi wa pampu ya kusukuma maji ,na tayari mzabuni ameshapeleka bomba za maunganisho mapya kwa wateja mia moja hamsini

Naye Katibu Tawala wilaya ya bunda SALUM MTELELA kwa Niaba ya mkuu wa wilaya ya bunda, ametoa tahadhari kwa watu wote wanaojipanga kuhujumu miundombinu inayotekelezwa na serikali amesema kuwa serikali haita sita kuwachukulia hatua za kisheria watakaobainika kufanya hivyo

KWA upande wa wakazi wa kata ya wariku wameishukuru serikali kwa kuleta mradi huo ambao utawasaidia kupata maji kwa wakati hasa nyakati za kiangazi .

Mradi huo ukikamilika utasaidia maeneo ya nyandago, kamkenga, kangetutya, na mumanyago kupitia tangi lenye ujazo wa lita 200,000 linalojengwa shule ya msingi wariku mtaa wa mumanyago .

17/07/2024

: Alhamisi tarehe 18.7.2024 katika kipindi cha Shujaa, tuambie kwa nini wanaume awapima VVU., faida za kupima VVU na athari za kutopima VVU.
Pia k**a una maoni au maswali tutumie hapa kwenye Ukurasa wetu nasi tutasoma hewani kwenye kipindi.
Usikose kusikiliza KIPINDI CHA SHUJAA, kila siku za Jumanne na Alhamisi saa 10:30 hadi saa 11:00 jioni ndani ya Bunda Fm radio 92.1.
.1 YA JAMII

15/07/2024

: Jumanne tarehe 16.7.2024 katika kipindi cha Shujaa, tuambie kuhusu umuhimu wa wanajamii kupima VVU.
Pia k**a una maoni au maswali tutumie hapa kwenye Ukurasa wetu nasi tutasoma hewani kwenye kipindi.
Usikose kusikiliza KIPINDI CHA SHUJAA, kila siku za Jumanne na Alhamisi saa 10:30 hadi saa 11:00 jioni ndani ya Bunda Fm radio 92.1.
.1 YA JAMII

04/07/2024

: Alhamis tarehe 4.7.2024 katika kipindi cha Shujaa, tuambie kuhusu umuhimu wa mama aishie na VVU kumpima Mtoto wake VVU baada ya kujifungua.
Pia k**a una maoni au maswali tutumie hapa kwenye Ukurasa wetu nasi tutasoma hewani kwenye kipindi.
Usikose kusikiliza KIPINDI CHA SHUJAA, kila siku za Jumanne na Alhamisi saa 10:30 hadi saa 11:00 jioni ndani ya Bunda Fm radio 92.1.
.1 YA JAMII

01/07/2024

: Jumanne tarehe 2.7.2024 katika kipindi cha Shujaa, tuambie kuhusu umuhimu wa mama aishie na VVU kukamilisha mahudhurio yote ya Kliniki ya Mama na Mtoto baada ya kujifungua.
Pia k**a una maoni au maswali tutumie hapa kwenye Ukurasa wetu nasi tutasoma hewani kwenye kipindi.
Usikose kusikiliza KIPINDI CHA SHUJAA, kila siku za Jumanne na Alhamisi saa 10:30 hadi saa 11:00 jioni ndani ya Bunda Fm radio 92.1.
.1 YA JAMII

19/06/2024

: Alhamis tarehe 20.6.2024 katika kipindi cha Shujaa, tuambie kuhusu umuhimu wa mwanamke kuwahi kliniki mara tu anapohisi ujauzito na kukamilisha mahudhurio yote 8 ya Kliniki ya wajawazito.
Pia k**a una maoni au maswali tutumie hapa kwenye Ukurasa wetu nasi tutasoma hewani kwenye kipindi.
Usikose kusikiliza KIPINDI CHA SHUJAA, kila siku za Jumanne na Alhamisi saa 10:30 hadi saa 11:00 jioni ndani ya Bunda Fm radio 92.1.
.1 YA JAMII

12/06/2024

: Alhamis tarehe 13.6.2024 katika kipindi cha Shujaa, tuambie kuhusu nafasi yako wewe mzazi au mlezi katika kumuhamasisha kijana wako mwenye umri wa kuanzia miaka 15 na kuendelea kufanya tohara ya hiari ya kitabibu ya wanaume.
Pia k**a una maoni au maswali tutumie hapa kwenye Ukurasa wetu nasi tutasoma hewani kwenye kipindi.
Usikose kusikiliza KIPINDI CHA SHUJAA, kila siku za Jumanne na Alhamisi saa 10:30 hadi saa 11:00 jioni ndani ya Bunda Fm radio 92.1.
.1 YA JAMII

10/06/2024

: Jumanne tarehe 11.6.2024 katika kipindi cha Shujaa, tuambie kuhusu nafasi yako wewe mzazi au mlezi katika kumuhamasisha kijana wako mwenye umri wa kuanzia miaka 15 na kuendelea kufanya tohara ya hiari ya kitabibu ya wanaume.
Pia k**a una maoni au maswali tutumie hapa kwenye Ukurasa wetu nasi tutasoma hewani kwenye kipindi.
Usikose kusikiliza KIPINDI CHA SHUJAA, kila siku za Jumanne na Alhamisi saa 10:30 hadi saa 11:00 jioni ndani ya Bunda Fm radio 92.1.
.1 YA JAMII

05/06/2024

: Alhamisi tarehe 6.6.2024 katika kipindi cha Shujaa, tuambie kuhusu nafasi ya mwanamke katika kumuhamasisha mwenza wake kufanya tohara ya hiari ya kitabibu ya wanaume.
Pia k**a una maoni au maswali tutumie hapa kwenye Ukurasa wetu nasi tutasoma hewani kwenye kipindi.
Usikose kusikiliza KIPINDI CHA SHUJAA, kila siku za Jumanne na Alhamisi saa 10:30 hadi saa 11:00 jioni ndani ya Bunda Fm radio 92.1.
.1 YA JAMII

02/06/2024

: Jumanne tarehe 4.6.2024 katika kipindi cha Shujaa, tuambie kuhusu umuhimu wa kufanya Tohara ya Hiari ya kitabibu ya wanaume na sio Tohara ya Jadi. Pia k**a una maoni au maswali tutumie hapa kwenye Ukurasa wetu nasi tutasoma hewani kwenye kipindi.
Usikose kusikiliza KIPINDI CHA SHUJAA, kila siku za Jumanne na Alhamisi saa 10:30 hadi saa 11:00 jioni ndani ya Bunda Fm radio 92.1.
.1 YA JAMII

DC. ANNEY ATOA ONYO KALI KWA WAKOPESHAJI WANAOCHUKUA KADI ZA BENKI ZA WATUMISHI WILAYANI BUNDAJumatano 29.05.2024Mheshim...
30/05/2024

DC. ANNEY ATOA ONYO KALI KWA WAKOPESHAJI WANAOCHUKUA KADI ZA BENKI ZA WATUMISHI WILAYANI BUNDA

Jumatano 29.05.2024

Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda Dkt. Vicent Anney ametoa Onyo kali kwa Taasisi au Watu Binafsi wanaochukua Kadi ZA Benki za Watumishi wanaokopa kwao kinyume na taratibu za ukopeshaji.

Dkt. Anney Ameyasema hayo Leo wakati akiongea na Taasisi/Watu Binafsi wanaotoa huduma ya Mikopo ya fedha katika Ukumbi wa Ofisi yake.

Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya amesema "Kufanya hivyo ni Utapeli na wengine wamekua wa wakiongeza Tiba bila Utaratibu, wengine wanaongeza Mikopo baada ya Mkopo wa mteja kuisha tena bila Utaratibu. Mkuu wa Wilaya ameagiza tabia hizo kukoma.

Aidha Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ameelekeza Taasisi au Watu Binafsi wanaokopesha ambao hawajasajiliwa kujisajili kabla hajaanza kufanya opareshi ya kukagua.

Sambamba na hilo Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ametoa Onyo kwa wanaowalaghai Wastaafu kwa kuwapa Mikopo isiyoeleweka na kuchukua fedha zao na pia amekataza kuk**ata Mali ya mteja bila kibali Cha Polisi.

Mwisho Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya amewaelekeza wafanyabiashara hao kufuata Utaratibu wa ukopeshaji uliotolewa na kwamba yeyote atakaekiuka atachukuliwa hatua za kisheria. Aidha amesema Mikopo yote lazima ihusishe salary slip ya mtumishi na mkataba uoneshe muda wa marejesho, makato pamoja na riba.

Kwa upande wao wafanyabiashara wamemshukuru Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya kwa kukaa pamoja nao kutoa elimu na kusikiliza kero zao ambapo Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ameahidi kuzifanyia kazi.

Address

Mapumulo

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BundafmTz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to BundafmTz:

Share