I7N Media

I7N Media Home of , , , and | Tunakuletea dunia kiganjani |
X (Twitter): i7NMedia

 Israel imekubali kuwaachilia wafungwa mia saba (700) hadi mia nane (800) wa Kipalestina badala ya mateka arobaini (40) ...
25/03/2024


Israel imekubali kuwaachilia wafungwa mia saba (700) hadi mia nane (800) wa Kipalestina badala ya mateka arobaini (40) wa Israel ambao bado wanashikiliwa na Hamas.
Iwapo watafanikiwa, mabadilishano hayo yatakuwa sehemu ya makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Hamas, ambayo yameingia mwezi wa tano (5) sasa.

 Urusi imeshusha bendera nusu mlingoti kwa siku moja (1) ya maombolezo baada ya watu kadhaa kupigwa risasi na silaha za ...
25/03/2024


Urusi imeshusha bendera nusu mlingoti kwa siku moja (1) ya maombolezo baada ya watu kadhaa kupigwa risasi na silaha za moja otomatik kwenye tamasha la muziki wa rock nje ya miji mkuu Moscow katika shambulio baya zaidi kwa miongo miwili (2).
Rais Vladimir Putin alitangaza siku ya kitaifa ya maombolezo Jumapili baada ya kuahidi kuwasaka na kuwaadhibu wale wote waliohusika na shambulio hilo, ambapo watu wasiopungua mia moja thelathini na saba (137) waliuawa, wakiwemo watoto watatu (3), na zaidi ya mia moja na hamsini (150) kujeruhiwa.

 Hesabu za kwanza katika vituo vya kupigia kura katika uchaguzi wa rais uliocheleweshwa nchini Senegal, Jumapili, zinaon...
25/03/2024


Hesabu za kwanza katika vituo vya kupigia kura katika uchaguzi wa rais uliocheleweshwa nchini Senegal, Jumapili, zinaonyesha mgombea wa upinzani Bassirou Diomaye Faye (umri 44) akiongoza.
Wafuasi wake walianza kusherekea mitaani baada ya siku ya amani ya uchaguzi ambayo wengi wanatumaini utaleta mabadiliko.

 Watu kumi na moja (11) waliuawa katika mashambulizi mawili (2) karibu na mji wa Beni mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokra...
25/03/2024


Watu kumi na moja (11) waliuawa katika mashambulizi mawili (2) karibu na mji wa Beni mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Jumamosi usiku.
Afisa katika mtaa Augustin Kapupa amewatuhumu waasi wa ADF kuhusika na shambulio hilo.

 Rais wa Urusi anasema: "tutalipiza kisasi kila mmoja. Na wale ambao wanahusika katika mashambulizi, bila kujali nchi ya...
24/03/2024


Rais wa Urusi anasema: "tutalipiza kisasi kila mmoja.
Na wale ambao wanahusika katika mashambulizi, bila kujali nchi ya asili na hali.
Kwa sasa ndio lengo halali na lengo kuu la taifa.”

24/03/2024


Niite Collie, nimetimia ndoto yangu ya kuwa mnyama.
(Soma POST ILIYOPITA …)
Kwa video ya dakika tatu (3Min) tembelea ukurasa wetu wa TRUTH SOCIAL/i7NMedia

 Baada ya kutumia zaidi ya dola elfu kumi na nne ($14,000) kuwa Mbwa, anatimiza ndoto yake ya kutembezwa kwenye kamba.Mw...
24/03/2024


Baada ya kutumia zaidi ya dola elfu kumi na nne ($14,000) kuwa Mbwa, anatimiza ndoto yake ya kutembezwa kwenye kamba.
Mwanaume anayejulikana kwa jina la Toco huko nchini Japani ambaye alijigeuza kuwa mbwa anasema: “Mabadiliko hayakuwa tu kuvaa vazi la mbwa; bali ilikuwa ni kukumbatia utambulisho ambao ilikuwa ni ndoto niliyoiota tangu utotoni. Kwa sasa niite collie, nimetimiza ndoto yangu ya kuwa mnyama ... Leo, nitatoka na kutembea."
Toco alielezea katika video ambayo imekusanya zaidi ya watazamaji elfu kumi na saba (17,000) kwenye chaneli yake ya YouTube, ambayo pia iliiongezea subscribers karibu watu elfu thelathini (30,000).

(Ona video -POST INAYOFUATA …)

 Iran inatoa wito kwa nchi zote za Kiislamu kusitisha uhusiano wa kidiplomasia na Israel.
19/03/2024


Iran inatoa wito kwa nchi zote za Kiislamu kusitisha uhusiano wa kidiplomasia na Israel.

 China inasema iko tayari kuingilia kijeshi ikiwa Marekani au NATO itashambulia Urusi.
17/03/2024


China inasema iko tayari kuingilia kijeshi ikiwa Marekani au NATO itashambulia Urusi.

   atatunukiwa nyota ya Hollywood Walk of Fame.Chama cha Biashara cha Hollywood kilitangaza mipango yao ya kumheshimu mw...
13/03/2024


atatunukiwa nyota ya Hollywood Walk of Fame.
Chama cha Biashara cha Hollywood kilitangaza mipango yao ya kumheshimu mwanzilishi wa N.W.A. na nyota katika kitengo cha Kurekodi. Nyota ya Dre itakuwa karibu na swahiba wake wa muda mrefu in-rhyme , ambaye alipokea nyota yake mwaka 2018.

 Hair, nails, .POLA BEAR   ,  ,
13/03/2024


Hair, nails, .POLA BEAR
, ,

 Mamia ya watu walikuwa wamekusanyika katika eneo la kutazama kurushwa kwa roketi ya Space One ya Kairos katika eneo la ...
13/03/2024


Mamia ya watu walikuwa wamekusanyika katika eneo la kutazama kurushwa kwa roketi ya Space One ya Kairos katika eneo la Wakayama magharibi mwa Japani.
Lakini sekunde chache baada ya kurushwa, roketi hiyo ililipuka na kuwaka moto, na kusababisha moshi kutanda katika eneo la mbali la milimani.
Kampuni hiyo yenye makao yake makuu Tokyo imekuwa ikijaribu kuwa kampuni ya kwanza ya kibinafsi ya Japani kuweka satelaiti kwenye obiti.

Address

Bujumbura

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when I7N Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to I7N Media:

Share