12/27/2025
Israel yatingisha diplomasia, mataifa yazidi kupinga utambuzi wa Somaliland!
Katika kile kinachoonekana k**a mlipuko wa kidiplomasia, Israel hivi karibuni ilitangaza kuitambua rasmi Somaliland k**a taifa huru, hatua ambayo imeibua upinzani mkali kutoka kwa mataifa mbalimbali pamoja na mashirika ya kimataifa.
Mpaka sasa, waliopinga hatua hiyo ya Israel ni pamoja na:
Umoja wa Afrika, ambao umesisitiza kuwa unayatambua mipaka ya Somalia k**a ilivyokuwa baada ya ukoloni. "AU inaunga mkono mamlaka kamili ya Somalia juu ya ardhi yake yote."
Saudi Arabia nayo imelaani uamuzi huo kwa kusema: "Tunapinga hatua yoyote inayovunja umoja na mamlaka ya Somalia."
Misri haijabaki nyuma, ikitoa kauli kali ikisema: "Hatua hii ni kinyume na sheria za kimataifa na inaleta hatari ya mivutano katika ukanda."
Somalia yenyewe imetoa tamko rasmi la kulaani vikali, ikisema: "Hatukubali kugawanywa. Israel imekiuka misingi ya mamlaka ya taifa letu."
Mataifa mengine yaliyopinga ni Uturuki, Djibouti, na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, wakisisitiza kuwa utambuzi wa Somaliland ni uvunjaji wa sheria na misingi ya Umoja wa Mataifa.
Kwa sasa hali bado ni tete, huku mazungumzo ya kidiplomasia yakitarajiwa kuendelea katika siku zijazo.
Endelea kufuatilia kurasa za MWK TV kwa taarifa zaidi!
Toa maoni yako