MWK TV

MWK TV Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MWK TV, Media, Winnipeg, MB.

MWK TV is a modern online television channel that provides National and International News, Sports, Music,Films, Gossips, Documentaries, and more.

- YouTube: MWK TV
- FB : MWK TV
- IG: mwanawekaayatv
- TikTok: mwanawekaaya
- X: MWK TV

Nyumba mbili za kifahari London zinahusishwa na Kiongozi Mkuu wa Iran zauzwa kwa mamilioni ya pauni.LONDON, Uingereza.Ny...
09/07/2026

Nyumba mbili za kifahari London zinahusishwa na Kiongozi Mkuu wa Iran zauzwa kwa mamilioni ya pauni.

LONDON, Uingereza.

Nyumba mbili za kifahari katika eneo la Kensington, London, zinazodaiwa kumilikiwa na Kiongozi Mkuu wa Iran, Mojtaba Khamenei, zimeanza kuuzwa baada ya Mfanyabiashara na Mwanabenki wa Iran, Ali Ansari, ambaye ametajwa kuwa Mtu muhimu wa mtandao wa kifedha wa Khamenei, kushindwa kulipa mikopo ya mali hizo.

Kwa mujibu wa ripoti ya The Sunday Times iliyochapishwa Septemba 6, 2026, nyumba hizo ziko katika jengo la 3a Palace Green, katika moja ya maeneo ya kifahari zaidi ya Kensington, na ziko umbali wa takribani mita 45 kutoka ubalozi wa Israel nchini Uingereza.

Mali hizo, zilizonunuliwa mwaka 2014 na 2016 kupitia Ansari, zina thamani ya pamoja ya takribani pauni milioni 35.75. Moja ilinunuliwa kwa pauni milioni 19 mwaka 2016 na sasa inauzwa kwa takribani pauni milioni 12, huku nyingine iliyonunuliwa kwa pauni milioni 16.75 mwaka 2014 ikiwa haina bei ya wazi ya kuanzia katika tangazo la mauzo.

Kila nyumba ina vyumba vya Wafanyakazi pamoja na eneo binafsi la juu la jengo, huku mali hizo zikiwa karibu na Kensington Palace, eneo linalohusishwa na makazi rasmi ya Prince na Princess of Wales.

- Uhusiano na mtandao wa Khamenei.

Uchunguzi wa awali wa Bloomberg umehusisha mali hizo na mtandao mpana wa uwekezaji unaodaiwa kuwa chini ya ushawishi au udhibiti wa Mojtaba Khamenei. Uchunguzi huo ulieleza kuwa mali kadhaa nchini Uingereza na sehemu nyingine za Ulaya zilisajiliwa kupitia Kampuni na watu wa kati badala ya kuwekwa moja kwa moja kwa jina la Khamenei.

Ansari ametajwa na vyanzo vya Magharibi k**a mmoja wa watu muhimu katika mtandao huo, lakini amekanusha vikali kuwa na uhusiano wowote wa kifedha au binafsi na Mojtaba Khamenei, kupitia Wakili wake.

- Mali hizo zafuatiliwa baada ya vikwazo.

Mamlaka za Uingereza zilimwekea Ansari vikwazo mwaka 2025, hatua iliyosababisha mali zake nchini Uingereza kuzuiliwa. Serikali ya Uingereza pia imethibitisha Bungeni kwamba hatua za vikwazo dhidi ya Ansari ziliathiri mali zake nchini humo, zikiwemo mali isiyohamishika.

Ripoti za hivi karibuni zinaeleza kuwa baada ya Ansari kushindwa kutimiza malipo ya mikopo ya nyumba hizo, mali hizo ziliingia katika mchakato wa receivership, na sasa zimewekwa sokoni. Fedha zitakazopatikana kutokana na mauzo hayo zinatarajiwa kubaki chini ya masharti ya vikwazo wakati Ansari akiendelea kuwa kwenye orodha ya waliowekewa vikwazo.

- Eneo la nyumba hizo laibua maswali ya usalama.

Mahali zilipo nyumba hizo kumeongeza mvutano wa suala hilo kwa sababu ziko karibu sana na Ubalozi wa Israel Mjini London, ambao unalindwa kwa kiwango kikubwa kutokana na mazingira ya kiusalama.

Ripoti ya The Standard iliwahi kueleza kuwa Nyumba hizo zina mwonekano wa moja kwa moja kuelekea sehemu ya nyuma ya ubalozi, jambo lililoibua wasiwasi miongoni mwa Wataalamu wa usalama.

Kwa upande mwingine, uchunguzi wa Bloomberg umeonyesha kuwa suala la mali za London ni sehemu ya mtandao mpana zaidi wa uwekezaji unaodaiwa kuhusishwa na Khamenei, ukiwa na mali katika maeneo ya kifahari k**a Hampstead's “Billionaires’ Row” na maeneo mengine ya Ulaya na Mashariki ya Kati.

Mauzo hayo sasa yanaweka katika mtazamo mpana zaidi mjadala kuhusu jinsi mitandao ya watu wenye nguvu nchini Iran ilivyoweza kuwekeza katika mali za thamani kubwa katika nchi za Magharibi licha ya vikwazo vya muda mrefu dhidi ya Tehran.

Toa maoni yako

Susan Sarandon: “Bado naondolewa kwenye filamu kwa sababu ya msimamo wangu kuhusu Israel na Palestina”.Mwigizaji Mkongwe...
09/07/2026

Susan Sarandon: “Bado naondolewa kwenye filamu kwa sababu ya msimamo wangu kuhusu Israel na Palestina”.

Mwigizaji Mkongwe wa Marekani na Mshindi wa Tuzo ya Oscar, Susan Sarandon, amesema bado anakabiliwa na kile anachoeleza kuwa ni kulipiziwa kisasi kikazi na kufutiwa nafasi katika filamu kutokana na msimamo wake wa wazi dhidi ya hatua za Israel huko Gaza na mshik**ano wake na Palestina.

Sarandon aliyasema hayo Jumapili hii Septemba 6, 2026 alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari katika Tamasha la Filamu la Venice, ambako alikuwa akitangaza filamu yake mpya The Echo Chamber.

Mwigizaji huyo alisema amekuwa akishinikizwa ndani ya tasnia ya burudani nchini Marekani kutokana na kukosoa hadharani sera na vitendo vya Israel pamoja na uungaji mkono wa Marekani kwa Israel.

Kwa mujibu wa Sarandon, baadhi ya Mawakala wa Wasanii na Viongozi wa kampuni za burudani wamekuwa wakijaribu kuzuia asipate nafasi za kuigiza katika filamu.

“Bado hivi karibuni nimeondolewa kwenye baadhi ya filamu kwa sababu kuna mashirika ya uwakala ambayo bado yanawaambia watu wasiniajiri. Lakini huo ndio mfumo wa nguvu. Nadhani miongoni mwa watu, na hasa kimataifa, ninahisi ninakaribishwa.”

Sarandon amekuwa miongoni mwa Wasanii mashuhuri wa Hollywood wanaotoa matamshi ya wazi kuhusu vita vya Gaza na kuunga mkono haki za Wapalestina.

Msimamo huo umekuwa ukizua mjadala mkubwa katika tasnia ya burudani ya Marekani, huku baadhi ya Wasanii wakidai kuwa uhuru wa kutoa maoni kuhusu vita vya Gaza unaweza kuwa na athari katika taaluma zao, wakati wengine wakitetea haki ya Wasanii kutoa maoni yao ya kisiasa.

Kauli ya Sarandon inakuja wakati vita vya Gaza na uhusiano wa Marekani na Israel vikiendelea kuwa miongoni mwa masuala yanayogawa maoni ndani ya Marekani na katika Jumuiya ya kimataifa.

Toa maoni yako

LAMBERT MENDE: “TATIZO LA CONGO LILIANZA 1996, TSHISEKEDI SI CHANZO CHA MGOGORO”.Mbunge wa Kitaifa wa Jamhuri ya Kidemok...
09/07/2026

LAMBERT MENDE: “TATIZO LA CONGO LILIANZA 1996, TSHISEKEDI SI CHANZO CHA MGOGORO”.

Mbunge wa Kitaifa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Mwenyekiti wa CCU, Lambert Mende, ambaye pia ni Msemaji na Waziri wa mawasiliano wa zamani wa Serikali ya Serikali ya Joseph Kabila, amesema mzizi wa mgogoro wa mashariki mwa DRC unapaswa kutafutwa hadi mwaka 1996, akipinga madai kwamba Rais Félix Tshisekedi ndiye chanzo cha matatizo yanayoikabili DRC.

Mende amesema mashambulizi dhidi ya Congo yalianza wakati Mobutu Sese Seko akiwa madarakani, miaka 23 kabla ya Tshisekedi kuingia madarakani. Katika kauli yake, amemtaja Rais wa Rwanda, Paul Kagame, akidai kuwa alihusika katika mashambulizi ya mwaka 1996 na katika kuingia madarakani kwa Laurent-Désiré Kabila.

Akieleza msimamo wake, Mende amesema: "Tulishambuliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1996. Je, Tshisekedi alikuwa madarakani? Tatizo hili tunalolitatua lilianza mwaka 1996. Mobutu ndiye aliyekuwa madarakani. Kagame aliishambulia Congo mwaka 1996. Alimweka Laurent-Désiré Kabila madarakani mwaka 1996, na baadaye akamuua Laurent-Désiré Kabila, na leo anaishambulia tena Congo."

"Kwa hiyo, tunaanzia mwaka 1996, na kudai kwamba Tshisekedi ndiye tatizo la mwaka 1996 ni kusema uongo, kwa sababu hilo lilikuwa miaka 23 kabla hajafika madarakani."

"Tshisekedi si tatizo! Je, ni yeye aliyekwenda kumwambia Kagame aishambulie Congo mwaka 1996?”

Kauli hiyo inakuja wakati mgogoro wa muda mrefu katika mashariki mwa DRC ukiendelea kuhusisha masuala ya usalama, makundi yenye silaha na uhusiano wenye mvutano kati ya Kinshasa na Kigali.

Toa maoni yako

Marekani yakanusha Iran kushambulia Meli ya Marekani katika Mlango wa Hormuz.Jeshi la Marekani limekanusha vikali madai ...
09/06/2026

Marekani yakanusha Iran kushambulia Meli ya Marekani katika Mlango wa Hormuz.

Jeshi la Marekani limekanusha vikali madai ya Iran kwamba vikosi vya Tehran vimefanikiwa kushambulia meli ya kijeshi ya Marekani isiyo na rubani katika Mlango wa Hormuz, likisema taarifa hiyo haina ukweli.

Vyombo vya habari vinavyomilikiwa na serikali ya Iran vilidai kuwa vikosi vya Iran vililenga meli hiyo baada ya kujaribu kuingia katika eneo ambalo Tehran imelieleza kuwa ni sehemu iliyowekewa vikwazo ndani ya njia hiyo muhimu ya kimataifa ya majini.

Hata hivyo, Msemaji wa Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM), Kapteni Tim Hawkins, ameyapuuza madai hayo na kuyaelezea k**a “uongo mtupu”, kwa mujibu wa taarifa iliyoripotiwa na Associated Press.

Madai hayo yameibuka wakati mvutano wa kijeshi kati ya Washington na Tehran ukianza kupanda tena baada ya kipindi cha utulivu wa kiasi. Mlango wa Hormuz umeendelea kuwa kitovu cha mzozo huo kutokana na umuhimu wake katika usafirishaji wa mafuta na biashara ya kimataifa.

Masaa kadhaa kabla ya madai hayo ya Iran, Marekani ilitangaza kuwa vikosi vyake vilishambulia meli tatu za mafuta za Iran, hatua ambayo Washington ilisema ilikuwa majibu ya shambulio la makombora lililolenga meli mbili za kivita za Marekani.

Kwa mujibu wa taarifa za Marekani, meli hizo za kivita hazikupata madhara wala wanajeshi wa Marekani hawakujeruhiwa katika shambulio hilo la makombora.

Tukio hilo linaongeza hofu kwamba mvutano kati ya Marekani na Iran unaweza kuendelea kuongezeka katika eneo la Ghuba, huku Mlango wa Hormuz ukiwa katika hatari zaidi kutokana na shughuli za kijeshi na vitisho kwa usafirishaji wa kibiashara.

Kwa sasa, madai ya Iran kuhusu kushambuliwa kwa meli ya Marekani hayajathibitishwa na pande huru, huku Washington ikiendelea kuyakataa vikali.

Toa maoni yako

Iran yaionya Marekani: “Mashambulizi mapya yatajibiwa kwa kasi, uzito na maumivu zaidi”.TEHRAN, IRAN.Spika wa Bunge la I...
09/06/2026

Iran yaionya Marekani: “Mashambulizi mapya yatajibiwa kwa kasi, uzito na maumivu zaidi”.

TEHRAN, IRAN.

Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, ameitoa onyo kali kwa Marekani, akisema mashambulizi yoyote mapya dhidi ya Iran yatakabiliwa na majibu makubwa zaidi kuliko yaliyotolewa awali.

Ghalibaf amesema Tehran haitazingatia tena kile alichokiita “majibu yenye uwiano”, akisisitiza kuwa mazingira ya mapambano yamebadilika na kwamba Iran iko tayari kujibu kwa nguvu zaidi iwapo maslahi au usalama wake vitatishiwa.

Katika ujumbe wake, Ghalibaf amesema: “Iran imefanya kila juhudi iwezekanavyo kuhakikisha kuwa Marekani inaelewa kwamba masharti ya mchezo yamebadilika. Ikiwa hawajaelewa hadi sasa, wanapaswa kuelewa kabla haijawa kuchelewa kwamba sheria za mchezo zimebadilika.”

Akaongeza: “Mashambulizi yoyote mapya dhidi ya maslahi na usalama wa Iran yatakabiliwa na jibu la haraka zaidi, zito zaidi na lenye maumivu zaidi. Kipindi cha majibu yenye uwiano kimekwisha.”

Kauli hiyo inakuja wakati mvutano kati ya Tehran na Washington ukiendelea kuongezeka, huku pande hizo mbili zikikabiliana kijeshi na kutoleana vitisho vya kulipiza kisasi.

Marekani imesema hatua zake za kijeshi zinalenga kulinda wanajeshi, mali na usafirishaji wa kibiashara katika eneo hilo, wakati Iran ikisisitiza kuwa haitakubali kulazimishwa kurudi nyuma kupitia shinikizo la kijeshi au kiuchumi.

Onyo la Ghalibaf linaashiria mabadiliko katika lugha ya Tehran kuhusu namna itakavyojibu mashambulizi ya Marekani. Badala ya majibu yanayolingana na ukubwa wa shambulio lililotangulia, Iran sasa inatishia kuchukua hatua za haraka, nzito na zenye madhara makubwa zaidi.

Mvutano huo umeendelea pia kuibua wasiwasi kuhusu usalama wa Mlango wa Hormuz, mojawapo ya njia muhimu zaidi za usafirishaji wa mafuta duniani. Hatua yoyote ya kijeshi inayozuia au kuvuruga usafirishaji kupitia eneo hilo inaweza kuathiri masoko ya mafuta na biashara ya kimataifa.

Wachambuzi wa masuala ya Mashariki ya Kati wanaonya kuwa ikiwa vitisho hivyo vitafuatwa na mashambulizi mapya, mzozo kati ya Iran na Marekani unaweza kuingia katika awamu hatari zaidi, huku uwezekano wa mapigano kuenea katika maeneo mengine ya Mashariki ya Kati ukiongezeka.

Kwa sasa, kauli ya Ghalibaf imeongeza uzito kwenye ujumbe wa Tehran kwamba shambulio lolote jipya dhidi ya Iran halitapokelewa kwa majibu ya kiwango kilekile, bali linaweza kuchochea hatua kali zaidi za kijeshi.

Toa maoni yako

Nchi 8 za Kiarabu na Kiislamu zalaani mpango wa kuondoa Wapalestina Gaza.Nchi nane za Kiarabu na Kiislamu zimeungana kul...
09/06/2026

Nchi 8 za Kiarabu na Kiislamu zalaani mpango wa kuondoa Wapalestina Gaza.

Nchi nane za Kiarabu na Kiislamu zimeungana kulaani vikali kauli na mapendekezo ya Mawaziri wawili wakuu wa Israel, Waziri wa Usalama wa Taifa Itamar Ben-Gvir na Waziri wa Ulinzi Israel Katz, kuhusu mpango wa kuwaondoa Wapalestina kwa wingi kutoka Ukanda wa Gaza.

Taarifa hiyo ya pamoja imetolewa na Mawaziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia, Jordan, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Qatar, Misri, Uturuki, Indonesia na Pakistan, ambao wameonya kwamba kauli hizo zinaweza kuongeza mvutano na kudhoofisha juhudi za amani katika eneo hilo.

Hatua hiyo ya kidiplomasia imekuja siku chache kabla ya uchaguzi mkuu wa Israel unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2026, huku Mawaziri wenye msimamo mkali katika serikali ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu wakitoa mapendekezo ya kuwawezesha Wapalestina kuondoka Gaza kwa kile wanachokiita "uhamiaji wa hiari." Reuters imeripoti kuwa Ben-Gvir na Katz wameongeza wito huo wakati kampeni za uchaguzi zikizidi kushika kasi.

Siku ya Alhamisi, Ben-Gvir aliwasilisha waraka wenye kurasa 20 wenye kichwa "Mpango Kazi wa Kitaifa wa Uhamiaji wa Hiari kutoka Ukanda wa Gaza", akieleza mpango unaolenga kuwawezesha Wapalestina kuondoka katika eneo hilo na kuhamia nchi nyingine.

Vyombo vya habari vya kimataifa vimeripoti kuwa mpango huo unaelezwa kulenga kuondoka kwa sehemu kubwa ya Wakazi wa Gaza kwa kipindi cha miaka kadhaa, huku Ben-Gvir akidai kuwa utekelezaji wake unaweza kuanza kwa kuwaondoa mamia ya maelfu ya watu katika mwaka wa kwanza.

- Katika taarifa yao ya pamoja, nchi hizo nane zilisema:

"Tunalaani kwa nguvu kauli zilizotolewa na Waziri wa Usalama wa Taifa wa Israel, Itamar Ben-Gvir, na Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz, kuhusu kuwaondoa watu wa Palestina kutoka Ukanda wa Gaza, ikiwa ni pamoja na mapendekezo ya mipango na mifumo inayolenga kuwaondoa Wapalestina kwa nguvu kutoka katika ardhi yao."

"Kauli na mapendekezo hayo ni uchochezi na yanawakilisha ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa na kanuni za msingi za haki za binadamu."

"Tunasisitiza kwamba watu wa Palestina wana haki ya kubaki katika ardhi yao na kwamba jaribio lolote la kuwahamisha kwa nguvu linatishia juhudi za amani na usalama katika eneo hilo."

"Tunathibitisha tena msimamo wetu wa kukataa kabisa uhamishaji wa lazima wa Wapalestina na kusisitiza umuhimu wa kuheshimiwa kwa haki zao, ikiwa ni pamoja na haki yao ya kujitawala na kuanzisha dola yao huru ya Palestina."

"Tunatoa wito kwa Jumuiya ya kimataifa kuendelea kupinga hatua na kauli zozote zinazolenga kuwahamisha Wapalestina kutoka katika ardhi yao na kuchukua hatua zinazohitajika kuhakikisha utekelezaji wa sheria za kimataifa."Taarifa hiyo imekuja wakati mvutano wa kidiplomasia kuhusu mustakabali wa Gaza ukiongezeka. Waziri Katz amekuwa akisisitiza kwamba "uhamiaji" wa Wapalestina ni sehemu ya suluhisho analoliona kwa Gaza, huku Marekani ikisema hakuna mpango wa kuwalazimisha Wapalestina kuondoka dhidi ya matakwa yao.

Kwa upande mwingine, Viongozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu wameendelea kusisitiza kwamba suluhisho la mgogoro wa Gaza linapaswa kuheshimu haki za Wapalestina na kuepuka uhamishaji wa watu kutoka katika ardhi yao.

Toa maoni yako

DOMINICAN REPUBLIC YATWAA TAJI YA MISS WORLD 2026.Mrembo Joheirry Mola Dominguez kutoka Jamhuri ya Dominika (Dominican R...
09/06/2026

DOMINICAN REPUBLIC YATWAA TAJI YA MISS WORLD 2026.

Mrembo Joheirry Mola Dominguez kutoka Jamhuri ya Dominika (Dominican Republic) ametwaa taji la Miss World 2026, baada ya kuibuka mshindi katika mashindano hayo makubwa ya urembo yaliyowakutanisha Warembo 111 kutoka mataifa mbalimbali duniani.

Mashindano hayo yalifikia kilele Jumamosi, Septemba 5, 2026, katika hafla iliyofanyika 2 April Square, Mjini Nha Trang, Nchini Vietnam, ambapo Warembo hao walichuana kuwania taji hilo la kimataifa.

Mola Dominguez alichukua nafasi hiyo kutoka kwa Opal Suchata Chuangsri wa Thailand, aliyekuwa akishikilia taji la Miss World. Kwa ishara ya makabidhiano ya taji, Chuangsri ndiye aliyemvika Mola taji baada ya kutangazwa Mshindi.

Ushindi huo unaiweka Dominican Republic katika nafasi ya juu zaidi kwenye ramani ya mashindano ya urembo duniani, huku Mola akianza rasmi safari yake k**a Miss World 2026.

Mashindano ya Miss World ni miongoni mwa mashindano makubwa zaidi ya urembo duniani na huvutia washiriki kutoka sehemu mbalimbali za dunia kila mwaka.

Toa maoni yako

Iran yadaiwa kuandaa shambulio la pamoja dhidi ya Israel kutoka pande nyingi.TEHRAN/TEL AVIV.Iran inadaiwa kuandaa opere...
09/06/2026

Iran yadaiwa kuandaa shambulio la pamoja dhidi ya Israel kutoka pande nyingi.

TEHRAN/TEL AVIV.

Iran inadaiwa kuandaa operesheni kubwa ya kijeshi dhidi ya Israel ambayo inaweza kuhusisha mashambulizi ya wakati mmoja kutoka maeneo mbalimbali ya Mashariki ya Kati, kwa kutumia vikosi vyake pamoja na washirika wake wenye silaha, kwa mujibu wa tathmini za kijasusi za Israel zilizoripotiwa na The Jerusalem Post.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, mpango huo unahusisha Hezbollah nchini Lebanon, Hamas, Wahouthi nchini Yemen pamoja na makundi yenye uhusiano na Iran nchini Iraq, huku Tehran ikidaiwa kutaka kuhakikisha mashambulizi hayo yanafanyika kwa uratibu mkubwa tangu mwanzo.

Mkakati huo unatofautiana na shambulio la Hamas la Oktoba 7, 2023, ambapo Hamas ilifanya mashambulizi makubwa dhidi ya Israel huku maeneo mengine yaliyokuwa yakihusishwa na Iran yakiwa hayajaanzisha mashambulizi makubwa kwa wakati mmoja.

Tathmini za Israel zinaeleza kuwa Iran sasa inajaribu kuzuia hali hiyo kujirudia kwa kuunganisha kile kinachojulikana k**a mtandao wake wa washirika wa kijeshi katika operesheni moja yenye kulenga kuishinikiza Israel kutoka kaskazini, kusini na maeneo mengine ya ukanda huo kwa wakati mmoja.

Nyaraka za ndani za Hamas zilizok**atwa Gaza baada ya mashambulizi ya mwaka 2023 ziliripotiwa kuonyesha kuwa Yahya Sinwar, aliyekuwa kiongozi wa Hamas, alikuwa akitafuta namna ya kuhusisha maeneo mengine ya mapambano, yakiwemo Lebanon, Syria na Sinai.

Hata hivyo, tathmini zilizowahi kutolewa na Marekani na Israel zilisema Iran na Hezbollah hazikuwa na taarifa kamili kuhusu muda na maelezo ya operesheni ya Oktoba 7 kabla haijaanza. Sinwar alitarajiwa kuwa mafanikio ya awali ya Hamas yangesababisha maeneo mengine kuingia kwenye mapambano kwa nguvu zaidi.

Sasa, kwa mujibu wa tathmini mpya, Tehran inaonekana kutaka uratibu huo uwe sehemu ya mpango wenyewe, badala ya kusubiri washirika wengine kuamua kujiunga baada ya mapigano kuanza.

Ripoti hizo pia zinadai kuwa maafisa wa ngazi ya juu wa Kikosi cha Quds, tawi la operesheni za nje la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran, wamekuwa na mawasiliano na mak**anda kutoka Hezbollah, Wahouthi na makundi yenye uhusiano na Iran nchini Iraq kuhusu namna ya kupanua mapambano.

Madai hayo yanaibuka wakati mvutano kati ya Israel na Hezbollah ukiendelea. Israel imeendelea kufanya mashambulizi katika maeneo ya kusini mwa Lebanon, huku Hezbollah ikiendelea kufanya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani dhidi ya maeneo ya Israel. Reuters imeripoti kuwa mashambulizi ya Israel nchini Lebanon Jumapili, Septemba 6, yalisababisha vifo vya watu saba, huku Hezbollah ikiwa imetajwa kuhusika na mashambulizi ya awali ya droni.

Iran yenyewe pia imekuwa ikiongeza onyo kwamba shambulio kubwa la Israel dhidi ya maeneo yanayohusishwa na Hezbollah nchini Lebanon linaweza kusababisha jibu kubwa la kijeshi. Reuters iliripoti wiki hii kuwa Tehran ilikuwa imeifikishia Marekani ujumbe kwamba shambulio kubwa la Israel katika eneo la kimkakati kusini mwa Lebanon lingeweza kusababisha Iran kulipiza kisasi kwa kiwango kikubwa.

Iwapo madai haya ya kijasusi yatathibitika na mpango huo kutekelezwa, wachambuzi wanaonya kwamba ungeweza kufungua mzunguko mpana zaidi wa vita katika Mashariki ya Kati, kwa kuhusisha Iran, Israel, Lebanon, Gaza, Yemen na Iraq kwa wakati mmoja.

Hata hivyo, hadi sasa hakuna uthibitisho huru kwamba Iran imeweka tarehe maalumu ya kuanza mashambulizi hayo, na taarifa hizo zinategemea zaidi tathmini za kijasusi za Israel pamoja na ripoti za vyombo vya habari

Toa maoni yako

FARDC na Wazalendo wawarudisha nyuma Waasi wa M23 katika eneo la Fizi.KINSHASA, DRC.Vikosi vya Jeshi la Jamhuri ya Kidem...
09/06/2026

FARDC na Wazalendo wawarudisha nyuma Waasi wa M23 katika eneo la Fizi.

KINSHASA, DRC.

Vikosi vya Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (FARDC), vikisaidiwa na Wapiganaji wa Wazalendo, vimefanikiwa kuwasukuma nyuma Wapiganaji wa Waasi wa Twirwaneho na Red Tabara, yanayoshirikiana na Muungano wa M23-ARC/AFC, katika eneo la Angùle, Wilaya ya Fizi, Mkoani Sud-Kivu.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, operesheni hiyo imefanyika leo hii Jumapili Septemba 6, 2026 huku mapigano yakisababisha Wapiganaji wa Twirwaneho kurudi nyuma kuelekea eneo la Até 'Avocat baada ya kukabiliwa na mashambulizi kutoka kwa vikosi vinavyounga mkono serikali.

Hata hivyo, hali ya usalama katika eneo hilo bado inaendelea kuzua hofu miongoni mwa wakazi, kutokana na kuwepo kwa makundi yenye silaha katika maeneo yanayozunguka Angùle, Na'ehele, Mulima na Abala.

Taarifa zinaeleza kuwa Raia wengi wamekimbia makazi yao kwa haraka na kuelekea Elumbé, wakitafuta usalama kutokana na mapigano yanayoendelea.

Udhibiti wa maeneo hayo unaonekana kuwa na umuhimu mkubwa kwa usalama wa Mkoa wa Sud-Kivu na Mkoa jirani wa Tanganyika, kwa kuwa yanatoa njia muhimu kuelekea katikati ya eneo la Fizi na Mji wa Baraka.

Iwapo makundi ya Waasi yatafanikiwa kuyateka maeneo hayo, hatua hiyo inaweza kuwapa njia ya kusonga mbele kuelekea katikati ya Fizi na Baraka, huku pia ikiongeza shinikizo kwenye njia inayounganisha Sud-Kivu na Tanganyika.

Maendeleo hayo yanaweza pia kuongeza tishio dhidi ya Uvira, Mji muhimu kimkakati ulioko karibu na mpaka wa DRC na Burundi.

Kwa sasa, hali ya usalama katika maeneo hayo bado sio nzuri sana, huku Raia wakiendelea kuhama kutoka maeneo yaliyoathiriwa na mapigano.

Toa maoni yako

SIMBA YAANZA VIZURI AFRIKA, YAIANGUSHA MIGHTY WANDERERS MALAWI.Simba SC imeanza kwa kishindo kampeni yake ya kuwania Lig...
09/06/2026

SIMBA YAANZA VIZURI AFRIKA, YAIANGUSHA MIGHTY WANDERERS MALAWI.

Simba SC imeanza kwa kishindo kampeni yake ya kuwania Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions League) baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mighty Wanderers ya Malawi katika mchezo wa kwanza wa raundi ya awali.

Mchezo huo umechezwa katika Uwanja wa Bingu National Stadium Jijini Lilongwe, ulikuwa wa ushindani mkubwa huku kipindi cha kwanza kikimalizika bila timu yoyote kupata bao.

Baada ya mapumziko, Simba SC iliongeza kasi ya mashambulizi na juhudi zake zilizaa matunda dakika ya 66, pale Mshambuliaji Anicet Oura alipofunga bao lililoipa Simba uongozi wa 1-0. Bao hilo ndilo lililodumu hadi filimbi ya mwisho.

Ushindi huo ni muhimu kwa Mnyama, ambaye sasa anarejea Dar es Salaam akiwa na faida ya bao moja kabla ya mchezo wa marudiano. Simba SC ilikuwa ikilenga kupata matokeo chanya ugenini ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele.

Kwa upande wa Malawi, Mighty Wanderers ilikuwa ikitegemea zaidi faida ya kucheza nyumbani, huku mashabiki wa Simba waliokuwa Lilongwe wakitoa sapoti kubwa kwa timu yao. Idadi kubwa ya Watanzania na mashabiki waliotoka Tanzania waliijaza sehemu ya Bingu National Stadium kwa rangi nyekundu za Simba SC.

Mchezo wa marudiano kati ya Simba na Mighty Wanderers utachezwa Tanzania kati ya Septemba 11-13, 2026, huku mshindi wa jumla akiendelea na hatua inayofuata ya mashindano hayo.

FT: 🇲🇼 Mighty Wanderers 0-1 Simba SC 🇹🇿
⚽ Anicet Oura : 66'

Simba sasa ina kazi moja: kulinda faida hiyo ya bao moja katika mchezo wa marudiano na kuhakikisha inafuzu kwenda hatua inayofuata ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Toa maoni yako

Address

Winnipeg, MB

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MWK TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MWK TV:

Shortcuts

Share

Category