09/22/2025
Katika Mahak**a Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam, shauri la uhaini linalomkabili mwanasiasa mashuhuri Tundu Lissu limeendelea kusikilizwa leo.
Katika hatua hiyo ya awali, upande wa Jamhuri ulisoma orodha ya mashahidi na vielelezo vitakavyotumika katika kesi hiyo. Baada ya hapo, Lissu alipewa nafasi ya kutoa maoni yake.
Lissu amesema hana pingamizi na vielelezo vya Jamhuri, akieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuokoa muda wa mahak**a na kuepuka mabishano yasiyo ya lazima.
Hata hivyo, aliwasilisha orodha ya mashahidi wake, wakiwemo viongozi wakuu wa nchi akiwataja Rais Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, IGP Camilius Wambura, pamoja na Viongozi wa Chadema na wale wa kimataifa k**a Martha Karua na Dkt. W***y Mutunga kutoka Kenya.
Lissu alisisitiza kesi ianze mara moja akisema: “Mimi sikai hotelini, niko Magereza na nakaa na watu wa kunyongwa. Shauri lianze sasa!”
Kwa upande wa mashtaka, Wakili Katuga aliomba muda zaidi kwa maelezo kuwa walifika mahak**ani kwa ajili ya hatua ya awali tu.
Majaji walikubaliana na pande zote na kutangaza kuwa shauri hilo litaanza kusikilizwa rasmi tarehe 6 Oktoba 2025, kuanzia saa 3:00 asubuhi kila siku, kwa mtiririko.
Endelea kuwa nasi kwa taarifa zaidi za kesi hii ya kihistoria.
Toa maoni yako