MWK TV

MWK TV MWK TV, Notre TV en ligne Tv De Confiance et D’efficacité Qui Nous Donne des Informations Fiables Et Independente De Notre Communauté

https://youtu.be/ax3AmuYYSEIJOHN HECHE AHUTUBIA WANANCHI BAADA YA KESI YA TUNDU LISSU LEO HII/ MAJAJI/ SEREKALI/ WANAMUO...
09/22/2025

https://youtu.be/ax3AmuYYSEI
JOHN HECHE AHUTUBIA WANANCHI BAADA YA KESI YA TUNDU LISSU LEO HII/ MAJAJI/ SEREKALI/ WANAMUOGOPA

Toa maoni yako



MWKT TV is a modern online television channel that provides National and International News, Sports, Music,Films, Gossips, Documentaries, and more.- YouTube:...

https://youtu.be/CUi9g0ptjvcJ. HECHE AFUNGUKA NAMNA VIONGOZI WA CHADEMA WALIVYOZUILIWA KUSAFIRI NJE YA NCHI NA SHTUMA RW...
09/22/2025

https://youtu.be/CUi9g0ptjvc
J. HECHE AFUNGUKA NAMNA VIONGOZI WA CHADEMA WALIVYOZUILIWA KUSAFIRI NJE YA NCHI NA SHTUMA RWA RAIS

Toa maoni yako


MWKT TV is a modern online television channel that provides National and International News, Sports, Music,Films, Gossips, Documentaries, and more.- YouTube:...

Katika ulimwengu wa kandanda ya EPL, historia inaandikwa tena na hakuna mwingine bali ni Mohamed Salah!Nyota huyo wa Liv...
09/22/2025

Katika ulimwengu wa kandanda ya EPL, historia inaandikwa tena na hakuna mwingine bali ni Mohamed Salah!

Nyota huyo wa Liverpool ameweka rekodi kali baada ya kuingia rasmi kwenye orodha ya wachezaji 10 bora kwa upande wa mabao na assist katika Ligi Kuu England!

Kwa upande wa mabao, Salah anashikilia nafasi ya nne, akiwa na mabao 188, akiwapita mastaa wakubwa k**a Andrew Cole, Aguero na hata Thierry Henry. Anafuatia tu kina Alan Shearer, Harry Kane na Wayne Rooney.

Lakini si hapo tu! Salah pia amejiunga na top 10 ya assist, akiwa na pasi za mabao 89, akigawana nafasi ya tisa na James Milner. Juu yao wapo kina Ryan Giggs, Kevin De Bruyne na Cesc Fabregas.

Jamani, huyu ndiye Salah, Mfungaji, Mtengenezaji, na Mfalme wa Anfield! Na ni mchezaji pekee kutoka Afrika aliyeingia kwenye listi hizi zote mbili!

Je, ataweza kupanda hadi nafasi ya tatu au hata zaidi? Wakati ndio utasema...Tutazidi kufuatilia!

Toa maoni yako


Kutokea Pyongyang, Korea Kaskazini, Kiongozi wa taifa hilo, Kim Jong Un, amesema kuwa yuko tayari kwa mazungumzo na Mare...
09/22/2025

Kutokea Pyongyang, Korea Kaskazini, Kiongozi wa taifa hilo, Kim Jong Un, amesema kuwa yuko tayari kwa mazungumzo na Marekani, lakini kwa masharti madhubuti.

Katika hotuba yake mbele ya bunge siku ya Jumapili, Kim amesema kuwa kamwe hatoridhia kuachana na silaha za nyuklia, hata k**a Marekani itaahidi kuondoa vikwazo vya kiuchumi dhidi ya nchi yake.

"Silaha hizi ni kinga ya taifa letu. Mazungumzo yanawezekana, lakini si kwa shinikizo," alisema Kim kwa msisitizo.

Marekani kwa muda mrefu imekuwa ikihimiza Korea Kaskazini kusitisha mpango wake wa nyuklia, lakini kauli hii mpya ya Kim inaashiria kuwa mazungumzo yoyote yajayo yatakuwa kwenye msingi wa usawa, si masharti.

Tutaendelea kukufahamisha kadri taarifa mpya zinavyotufikia.

Endelea kufuatilia ukurasa wetu kwa habari motomoto duniani kote!

Toa maoni yako



Msanii Nguli wa muziki kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, ambaye amewahi kuwa na uhusiano na Wanawake mbalimbali, sasa a...
09/22/2025

Msanii Nguli wa muziki kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, ambaye amewahi kuwa na uhusiano na Wanawake mbalimbali, sasa ametoa ushauri mzito kwa Wanaume kuhusu jinsi ya kujiheshimu na kujilinda wanapokutana na Wasichana Warembo.

Kupitia ujumbe wake, Diamond amewashauri Wanaume wajifunze kuheshimu miili yao na kulinda mali zao, kwa kujiepusha kuingia kwenye uhusiano usiyo wa lazima na Wasichana wazuri wanaoweza kuwapotezea mwelekeo.

Diamond amesema kuwa kuwa na Mpenzi mmoja ni jambo bora sana, na ameungwa mkono na Watu wengi wanaoamini kuwa uaminifu na uhusiano wa Mtu mmoja ni aina ya usafi wa maisha.

"Ni vizuri kuwa na Mpenzi mmoja. Ni jambo linaloonyesha nidhamu, usafi wa moyo na heshima binafsi," amesema Staa huyo ambaye amekuwa na uhusiano na Mastaa mbalimbali barani Afrika.

Kauli hii imeibua mijadala mitandaoni, hasa kutokana na historia ya uhusiano wa Diamond ambao umekuwa ukigonga vichwa vya habari mara kwa mara.

Je, unakubaliana na ushauri huu wa Diamond Platnumz?

Toa maoni yako


Katika Mahak**a Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam, shauri la uhaini linalomkabili mwanasiasa mashuhuri Tundu Lissu l...
09/22/2025

Katika Mahak**a Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam, shauri la uhaini linalomkabili mwanasiasa mashuhuri Tundu Lissu limeendelea kusikilizwa leo.

Katika hatua hiyo ya awali, upande wa Jamhuri ulisoma orodha ya mashahidi na vielelezo vitakavyotumika katika kesi hiyo. Baada ya hapo, Lissu alipewa nafasi ya kutoa maoni yake.

Lissu amesema hana pingamizi na vielelezo vya Jamhuri, akieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuokoa muda wa mahak**a na kuepuka mabishano yasiyo ya lazima.

Hata hivyo, aliwasilisha orodha ya mashahidi wake, wakiwemo viongozi wakuu wa nchi akiwataja Rais Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, IGP Camilius Wambura, pamoja na Viongozi wa Chadema na wale wa kimataifa k**a Martha Karua na Dkt. W***y Mutunga kutoka Kenya.

Lissu alisisitiza kesi ianze mara moja akisema: “Mimi sikai hotelini, niko Magereza na nakaa na watu wa kunyongwa. Shauri lianze sasa!”

Kwa upande wa mashtaka, Wakili Katuga aliomba muda zaidi kwa maelezo kuwa walifika mahak**ani kwa ajili ya hatua ya awali tu.

Majaji walikubaliana na pande zote na kutangaza kuwa shauri hilo litaanza kusikilizwa rasmi tarehe 6 Oktoba 2025, kuanzia saa 3:00 asubuhi kila siku, kwa mtiririko.

Endelea kuwa nasi kwa taarifa zaidi za kesi hii ya kihistoria.

Toa maoni yako


Ameandika Rosa Ree, Msanii wa muziki wa Hip-hop Tanzania."MFUNGO DAY 1 Habari za Asubuhi….. Leo tunaanza na Sala ya “TOB...
09/22/2025

Ameandika Rosa Ree, Msanii wa muziki wa Hip-hop Tanzania.

"MFUNGO DAY 1

Habari za Asubuhi….. Leo tunaanza na Sala ya “TOBA”. Kibinadamu tunafanya mengi ambayo yanatuchafua na kutufanya hatustahili kusimama mbele ya MUNGU wetu mtakatifu. Hivyo, k**a Musa alivyotakiwa kuvua viatu kabla ya kuzungumza na MUNGU kwenye kichaka kilichowaka moto Mlima Horebu (Kutoka 3:5) basi nasi lazima tuvue viatu vyetu vya mizigo yote inatotutia najis kabla ya kuongea na MUNGU.

Mioyo yetu ikawe safi kutokana na dhambi za kimwili, za kiakili na za kiroho. Damu ya YESU ikatusafishe na kutujaza roho mtakatifu maana hatuwezi kuwa watakatifu pekee yetu kwa matendo yetu mpaka kustahili kuwa karibu na Utakatifu wa MUNGU….

Unposali Sala ya TOBA, kumbuka kujirudi kwa yaliyomo moyoni mwako ili uweze kuepukana na roho za hasira, uzinzi, chuki, wivu, fitina, visasi, kujikweza na mizigo mingine iliyo moyoni mwako ambayo nafsi yako inaifahamu. Tunapotubu, lazima tutue mizigo yote, tunyenyekee tukijua sisi hatuna nguvu bila kuwezeshwa na MUNGU na tusalimu amri kwake, Muumba wa mbinguni na nchi na mwenye mamlaka yote!

NAWATAKIA MFUNGO MWEMA! 🇹🇿✊🏾"

Toa maoni yako


Habari za michezo Mfuatiliaji wetu, tukianzia barani Afrika, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeendelea kutamba katika ...
09/22/2025

Habari za michezo Mfuatiliaji wetu, tukianzia barani Afrika, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeendelea kutamba katika viwango vya ubora wa soka katika ukanda wa CACAFA, na sasa imechukua nafasi ya juu kabisa katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Kwa mujibu wa viwango vipya vya FIFA vilivyotangazwa hivi karibuni, DRC imepanda hadi nafasi ya 60 duniani, na kuongoza ukanda wa CECAFA, ikiwa ni ishara ya maendeleo makubwa ya kandanda nchini humo.

Uganda haikubaki nyuma! Nchi hiyo imepanda kwa nafasi sita, na sasa inak**ata nafasi ya pili ukanda huu, ikithibitisha kuwa soka la Uganda linaendelea kupata umaarufu na nguvu kimataifa.

Kwa upande mwingine, hali si shwari kwa majirani wa DRC, Kenya na Tanzania ambao wameporomoka katika viwango hivyo. Tanzania sasa inashika nafasi ya 107, huku Kenya ikiwa nafasi ya 111 duniani, hali inayotokana na matokeo mabaya katika mechi zao za kufuzu Kombe la Dunia la mwaka 2026.

Je, Kenya na Tanzania watarejea kwenye ubora wao wa awali? Au DRC itaendelea kutawala ukanda huu? Tuambie maoni yako!

Endelea kufuatilia ukurasa wetu kwa taarifa zaidi za michezo, hapa hapa MWK TV.

Toa maoni yako


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amesema kinachotokea huko Gaza ni miongoni mwa matukio mabaya zaidi y...
09/22/2025

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amesema kinachotokea huko Gaza ni miongoni mwa matukio mabaya zaidi ya vifo na uharibifu kuwahi kushuhudiwa katika maisha yake yote, si k**a Katibu Mkuu tu, bali hata k**a binadamu.

Guterres amesema, na ninamnukuu: “Iwapo tutafanya au hatutafanya yale tunayopaswa kufanya, uhuni wa Israel utaendelea. Angalau sasa tuna nafasi ya kuihamasisha jamii ya kimataifa kuongeza presha ili wasifanikiwe.”

Ameendelea kusema kwamba kiwango cha mateso, uharibifu na umwagaji damu kimekuwa cha kusikitisha mno, akisisitiza haja ya jamii ya kimataifa kuchukua hatua za haraka kukomesha mzozo huo na kurejesha amani ya kudumu.

Hii ni sauti ya onyo kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Je, dunia itasikia?

Endelea kubaki nasi kwa taarifa zaidi…

Toa maoni yako



Leo tunamulika staa wa Bongo Movie na mama wa Watoto, Aunty Ezekiel, ambaye ameweka wazi namna alivyokutana na mpenzi wa...
09/22/2025

Leo tunamulika staa wa Bongo Movie na mama wa Watoto, Aunty Ezekiel, ambaye ameweka wazi namna alivyokutana na mpenzi wake ambaye pia ni Baba wa Watoto wake Kusah, Msanii wa muziki wa kizazi kipya.

Aunty amesema kuwa walikutana kwa njia ya mtandao wa Instagram, baada ya yeye kushiriki challenge ya wimbo wa Kusah. Muda si mrefu, Kusah alimwandikia DM na hapo ndipo safari yao ya mapenzi ilipoanza.

Lakini si yote yalikuwa rahisi! Aunty anasema kuna Watu walimshauri aachane na Kusah wakidai anamikosi, lakini yeye hakuwasikiliza, kwani hakuwahi kuamini katika imani hizo.

"Nilikutana na baba Nono kupitia Instagram… lakini watu walikuwa wakisema ana mikosi. Sikuwapa nafasi kabisa, sikuamini katika hilo," amesema Aunty kwa kujiamini.

Staa huyo anayefahamika kwenye filamu k**a "Prison Revenge" na "Pumba Jungu La Urithi", anazidi kuthibitisha kuwa mapenzi ya kweli yanaweza kuanza hata kupitia DM!

Je, wewe unaamini mapenzi ya mitandaoni yanaweza kuzaa matunda?

Endelea kufuatilia MWK TV kwa Burudani hii, tupo kwa ajili yako!

Toa maoni yako


Msanii wa filamu na pia video vixen anayefanya vizuri kwenye tasnia ya Bongo Movie, Caren Simba, amefunguka kwa mara ya ...
09/22/2025

Msanii wa filamu na pia video vixen anayefanya vizuri kwenye tasnia ya Bongo Movie, Caren Simba, amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu hali ya kihisia aliyowahi kupitia kwenye mahusiano ya kimapenzi.

Caren amesema wazi kuwa yeye ni mtu mwenye wivu mkubwa, na mara kadhaa hilo limekuwa chanzo cha matatizo kati yake na wanaume aliowahi kuwa nao.

"Mimi ni mtu mwenye wivu sana kwenye mapenzi kwani huwa napenda kweli. Nimepigwa sana na wanaume kisa wivu wangu."

Lakini kilichoacha wengi wameguswa, ni pale aliposema kuwa matatizo ya mapenzi yalimsababisha kupata stress kali, kuanza kulewa, na hata kufikia hatua ya kutamani kupotea duniani.

"Nimewahi kupata stress kwenye mapenzi, nikaanza kulewa tu, pia nilitamani hata kupotea duniani."

Aaah, kweli mapenzi sio lelemama!

Je, wewe Mfuatiliaji wetu, una mtazamo gani kuhusu hali k**a hizi kwenye uhusiano?

Usiende mbali, burudani inaendelea hapa hapa MWK TV.

Toa maoni yako



Karibu kwenye taarifa ya burudani... na sasa, habari inayotikisa mitandao ya kijamii kutoka kwa mwanadada maarufu Siwema...
09/22/2025

Karibu kwenye taarifa ya burudani... na sasa, habari inayotikisa mitandao ya kijamii kutoka kwa mwanadada maarufu Siwema Edson, mama wa mtoto wa msanii Nay wa Mitego.

Katika ukurasa wake, Siwema amesema kwa uwazi kuwa hana mpango wa kuolewa kamwe. Amedai kuwa ndoa huondoa uhuru wa mwanamke, hasa kwenye kazi na malengo ya binafsi. Siwema alinukuliwa akisema:

"Nachukia sana kitu kinachoitwa ndoa na sina mpango wa kuolewa kwenye maisha yangu. Ndoa itanipunguzia uhuru wa kufanya kazi zangu. Wanaume wengi wamekuwa wakitaka kunioa lakini mimi nakataa, sitaki kupata maumivu ya kuumizwa nikiwa ndani ya ndoa."

Kauli hiyo imeibua mijadala moto mitandaoni. Je, ndoa bado ina nafasi kwenye maisha ya mwanamke wa kisasa?

Baki nasi kwa habari zaidi.

Toa maoni yako



Address

Winnipeg, MB

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MWK TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MWK TV:

Share

Category