MWK TV

MWK TV Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MWK TV, Media, Winnipeg, MB.

MWK TV is a modern online television channel that provides National and International News, Sports, Music,Films, Gossips, Documentaries, and more.

- YouTube: MWK TV
- FB : MWK TV
- IG: mwanawekaayatv
- TikTok: mwanawekaaya
- X: MWK TV

Israel yatingisha diplomasia, mataifa yazidi kupinga utambuzi wa Somaliland!Katika kile kinachoonekana k**a mlipuko wa k...
12/27/2025

Israel yatingisha diplomasia, mataifa yazidi kupinga utambuzi wa Somaliland!

Katika kile kinachoonekana k**a mlipuko wa kidiplomasia, Israel hivi karibuni ilitangaza kuitambua rasmi Somaliland k**a taifa huru, hatua ambayo imeibua upinzani mkali kutoka kwa mataifa mbalimbali pamoja na mashirika ya kimataifa.

Mpaka sasa, waliopinga hatua hiyo ya Israel ni pamoja na:

Umoja wa Afrika, ambao umesisitiza kuwa unayatambua mipaka ya Somalia k**a ilivyokuwa baada ya ukoloni. "AU inaunga mkono mamlaka kamili ya Somalia juu ya ardhi yake yote."

Saudi Arabia nayo imelaani uamuzi huo kwa kusema: "Tunapinga hatua yoyote inayovunja umoja na mamlaka ya Somalia."

Misri haijabaki nyuma, ikitoa kauli kali ikisema: "Hatua hii ni kinyume na sheria za kimataifa na inaleta hatari ya mivutano katika ukanda."

Somalia yenyewe imetoa tamko rasmi la kulaani vikali, ikisema: "Hatukubali kugawanywa. Israel imekiuka misingi ya mamlaka ya taifa letu."

Mataifa mengine yaliyopinga ni Uturuki, Djibouti, na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, wakisisitiza kuwa utambuzi wa Somaliland ni uvunjaji wa sheria na misingi ya Umoja wa Mataifa.

Kwa sasa hali bado ni tete, huku mazungumzo ya kidiplomasia yakitarajiwa kuendelea katika siku zijazo.

Endelea kufuatilia kurasa za MWK TV kwa taarifa zaidi!

Toa maoni yako

Tyler Perry katikaoto wa tuhuma mpya za unyanyasaji wa kijinsia!Mtayarishaji maarufu wa filamu za Hollywood, Tyler Perry...
12/27/2025

Tyler Perry katikaoto wa tuhuma mpya za unyanyasaji wa kijinsia!

Mtayarishaji maarufu wa filamu za Hollywood, Tyler Perry, amejikuta katika kashfa mpya nzito baada ya kush*takiwa kwa madai ya unyanyasaji wa kijinsia na Mwigizaji aliyecheza kwenye moja ya filamu zake!

Katika habari iliyoripotiwa kutoka jimbo la California, Mwigizaji Mario Rodriguez, aliyewahi kushiriki katika filamu "Boo! A Madea Halloween", amemfungulia kesi Tyler Perry, akimtuhumu kwa unyanyasaji wa kijinsia unaodaiwa kutokea kati ya mwaka 2018 na 2019.

Rodriguez anadai kuwa Tyler Perry alimvamia kimwili, akamkumbatia kwa nguvu na kumguza sehemu zisizofaa wakati wa mkutano wa kazi. Kesi hiyo imewasilishwa rasmi Mahak**ani, huku Rodriguez akitaka alipwe fidia ya takribani dola milioni 77 za Kimarekani.

Rodriguez amesema: "Vitendo hivyo viliniacha nikiwa na majeraha ya kisaikolojia, vimeniharibia taaluma yangu na kunitia aibu kubwa."

Hadi sasa, Tyler Perry hajatoa tamko lolote kuhusu tuhuma hizo, na mashabiki wake wanasubiri kwa hamu kuona hatma ya kesi hiyo.

Endelea kufuatilia kurasa zetu kwa taarifa kamili pindi kesi hii itakapoendelea!

Toa maoni yako

Hiba Abouk aomba msamaha kwa Hakimi, lakini mashabiki wasema: ‘Ni kisa cha mkataba mpya!’Ni habari inayotikisa mitandao ...
12/27/2025

Hiba Abouk aomba msamaha kwa Hakimi, lakini mashabiki wasema: ‘Ni kisa cha mkataba mpya!’

Ni habari inayotikisa mitandao duniani kote! Mke wa zamani wa Nyota wa soka wa PSG, Achraf Hakimi, Bi. Hiba Abouk, ameripotiwa kuomba msamaha na kueleza kuwa anajutia kuomba talaka kutoka kwa Staa huyo wa Morocco!

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kupitia vyanzo vya karibu, Hiba amesema alichukua uamuzi kwa mihemko na baada ya kushauriwa vibaya na marafiki zake. “Nimekosea, natamani Hakimi anirudie,” amesema Hiba kwa uchungu.

Lakini vipi muda wa kauli hizi? Hapo ndipo mashaka yanapoanza. Kwa sababu, ni kipindi hiki hiki ambapo PSG imetangaza kumwongezea Hakimi mkataba mpya wa thamani ya pauni milioni 28 kwa mwaka, ukilinganisha na ule wa zamani wa pauni milioni 10.

Watazamaji na mashabiki wamejaa mitandaoni wakihoji: Je, huu ni msamaha wa dhati au kuna maslahi ya kifedha nyuma ya pazia?

Tutakuletea ripoti zaidi kadri simulizi hili linavyoendelea kuchukua sura mpya. Endelea kufuatilia kurasa zetu kwa taarifa nyingine moto moto hapa hapa kwenye kituo chako pendwa!

Toa maoni yako

Moto wa vita wawaka Uvira! Jeshi la Congo larumisha makombora kwenye ngome kuu ya Waasi wa M23.Huko Uvira, mashariki mwa...
12/26/2025

Moto wa vita wawaka Uvira! Jeshi la Congo larumisha makombora kwenye ngome kuu ya Waasi wa M23.

Huko Uvira, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, moto wa mapigano umechacha tena! Jeshi la FARDC limefanya mashambulizi makali ya anga dhidi ya kambi kuu ya waasi wa AFC/M23 iliyoko katika eneo la Kala, ambapo awali kulikuwa na kambi ya MONUSCO.

Taarifa rasmi kutoka kwa vyanzo vya usalama zinasema kuwa mashambulizi hayo yamelenga kusambaratisha ngome ya Waasi hao ambao wamekuwa wakituhumiwa kwa kuvuruga amani na usalama katika eneo hilo.

Jeshi la Congo limesema linaendelea na operesheni ya kuhakikisha maeneo yote yaliyotwaliwa na waasi yanarejeshwa mikononi mwa serikali.
"Haya ni mashambulizi ya kulenga kwa lengo la kurejesha mamlaka ya serikali na kulinda raia," imethibitishwa na Msemaji wa FARDC.

Mpaka sasa hakuna taarifa rasmi kutoka kwa kundi la waasi la M23 kuhusu athari za mashambulizi haya ya anga.

Endelea kuwa nasi kwa taarifa zaidi kuhusiana na hali ya usalama mashariki mwa DRC.

Toa maoni yako

wa vita wawaka Uvira! Jeshi la Congo larumisha makombora kwenye ngome kuu ya Waasi wa M23.

Huko Uvira, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, moto wa mapigano umechacha tena! Jeshi la FARDC limefanya mashambulizi makali ya anga dhidi ya kambi kuu ya waasi wa AFC/M23 iliyoko katika eneo la Kala, ambapo awali kulikuwa na kambi ya MONUSCO.

Taarifa rasmi kutoka kwa vyanzo vya usalama zinasema kuwa mashambulizi hayo yamelenga kusambaratisha ngome ya Waasi hao ambao wamekuwa wakituhumiwa kwa kuvuruga amani na usalama katika eneo hilo.

Jeshi la Congo limesema linaendelea na operesheni ya kuhakikisha maeneo yote yaliyotwaliwa na waasi yanarejeshwa mikononi mwa serikali.
"Haya ni mashambulizi ya kulenga kwa lengo la kurejesha mamlaka ya serikali na kulinda raia," imethibitishwa na Msemaji wa FARDC.

Mpaka sasa hakuna taarifa rasmi kutoka kwa kundi la waasi la M23 kuhusu athari za mashambulizi haya ya anga.

Endelea kuwa nasi kwa taarifa zaidi kuhusiana na hali ya usalama mashariki mwa DRC.

Toa maoni yako

DADA YAKE DIAMOND AMTETEA VIKALI BAADA YA MADAI YA KUPAKA LIPSTICK!Katika hali ya kuonyesha upendo wa familia na kusimam...
12/25/2025

DADA YAKE DIAMOND AMTETEA VIKALI BAADA YA MADAI YA KUPAKA LIPSTICK!

Katika hali ya kuonyesha upendo wa familia na kusimamia ukweli, dada wa Msanii maarufu Diamond Platnumz, Esma Platnumz, ameibuka na kumtetea kaka yake kufuatia mjadala mzito unaoendelea mitandaoni kuhusu picha zake zinazodaiwa kuonesha amepaka lipstick.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Esma amesema kinachoonekana kwenye midomo ya Diamond siyo lipstick, bali ni lip balm ya kawaida ambayo Diamond hupata kutoka kwa mjomba wa mtoto wake Tahiya, pindi anaposafiri au kwa kuagiza kutoka Uingereza.

“Acheni ushabiki nawajibu sasa. Hii ni lip balm ambayo Uncle wake Tahiya huwa anamnunulia akisafiri au ana-order. Zinapatikana sana UK. K**a mnataka na nyinyi mtajiwe jina, ni nzuri kwa lips, ina-moisturize vizuri tu. Ila binadamu, nachoka mimi 😢”, ameandika Esma kwa hisia kali.

Diamond mwenyewe hajajibu chochote kuhusu tuhuma hizo, lakini dada yake ameshachukua nafasi hiyo kuweka wazi kila kitu, na kufunga mjadala huo kwa sasa.

Endelea kufuatilia kurasa zetu kwa habari na burudani hapa hapa MWK TV Ukweli uko hapa, tunakuletea yote moto moto!

Toa maoni yako

Machozi afunguka: "Fumanizi Mwanza liloacha alama maishani Mwangu!"Katika taarifa inayowagusa wengi, Msanii wa Bongo Fle...
12/25/2025

Machozi afunguka: "Fumanizi Mwanza liloacha alama maishani Mwangu!"

Katika taarifa inayowagusa wengi, Msanii wa Bongo Fleva maarufu kwa wimbo wa Utaipenda, Hussein Rashid almaarufu Hussein Machozi, amefunguka kuhusu tukio moja la kusisimua lililotokea miaka ya nyuma, tukio ambalo anasema halitamsahaulika maishani mwake.

Akizungumza na vyombo vya habari, Machozi amesema: “Dah! Ilikuwa ni pande za Mwanza, siku hiyo shori fulani aliniingiza ndani kwake, kabla ya kufanya chochote ghafla demu wangu na kampani yake walizama ndani kunifumania,” amesema Machozi kwa hisia nzito.

Tukio hilo la fumanizi linadaiwa kuwa limemfundisha mengi kuhusu maisha ya kimapenzi na kumuacha akiwa na kumbukumbu ya kudumu.

Mashabiki wake wamepokea simulizi hiyo kwa mshangao huku wengi wakimsifia kwa ujasiri wa kuweka wazi hali ambayo Wasanii wengi wangependelea kuficha.

Machozi ambaye amewahi kutamba na nyimbo kali kwenye chati za muziki, anaonekana kurejea tena kwenye vichwa vya habari, safari hii si kwa muziki, bali kwa simulizi ya tukio lililobadilisha maisha yake.

Endelea kufuatilia kurasa zetu kwa taarifa zaidi kuhusu Mastaa wako pendwa, hapa hapa MWK TV, Ukweli uko hapa.

Toa maoni yako

12/25/2025

Nabii Eboh Noah atinga na Benz mpya ya milioni 232, adai Mungu amesogeza mafuriko!

Katika kile kinachoonekana k**a mchanganyiko wa imani na utata wa kiuchumi, Nabii Eboh Noah kutoka Ghana ameibua mjadala mkali baada ya kuonekana na gari jipya la kifahari aina ya Mercedes Benz la mwaka 2025, linalokadiriwa kugharimu dola 89,000 za Kimarekani.

Kwa mujibu wa taarifa, Nabii huyo anadaiwa kuwalazimisha baadhi ya wafuasi wake kuuza mali zao na kumpa fedha, kwa madai ya kujiandaa na mafuriko ya kiroho yaliyokuwa yanakuja.

Katika kauli yake ya hivi karibuni, Nabii huyo amesema: “Watu wengi wameshindwa kuelewa maono ya Mungu. Lakini natangaza, Mungu amesema siku ya mafuriko imeahirishwa hadi tarehe nyingine!”

Kauli hiyo imeibua taharuki na hisia tofauti miongoni mwa jamii ya waumini na mitandaoni, huku baadhi wakimtetea kuwa ni mtu wa maono na wengine wakimtuhumu kwa kutumia jina la Mungu kujitajirisha.

Waumini wake wameendelea kusimama imara nyuma yake, wakisema: “Tunamwamini Nabii wetu. K**a Mungu kasema, basi tunangoja.”

Endelea kufuatilia taarifa zetu kwa habari zaidi kuhusu sakata hili la "Benz na Mafuriko ya Kiroho!"

Toa maoni yako


MOTO MPYA MPAKANI! Israel yashambulia gari, watu wawili wauawa karibu na mpaka wa Syria na Lebanon.Taarifa tulizozipokea...
12/25/2025

MOTO MPYA MPAKANI! Israel yashambulia gari, watu wawili wauawa karibu na mpaka wa Syria na Lebanon.

Taarifa tulizozipokea hivi punde kutoka Mashariki ya Kati zinaeleza kuwa watu wawili wamepoteza maisha kwenye shambulio la anga lililofanywa na Israel dhidi ya gari moja karibu na mpaka wa Lebanon na Syria.

Kwa mujibu wa vyanzo vya usalama kutoka eneo hilo, shambulio hilo lilitokea muda mfupi uliopita na lilikilenga gari lililokuwa likisafiri kwenye barabara inayotumiwa na raia na vikundi vya kijeshi.

"Gari lililolengwa liliteketea kabisa kwa moto baada ya kushambuliwa na kombora la angani, watu wawili waliokuwa ndani waliaga dunia papo hapo," chanzo kimoja cha usalama kimethibitisha.

Hadi sasa hakuna tamko rasmi kutoka kwa jeshi la Israel kuhusu shambulio hilo, lakini hatua k**a hizi zimekuwa zikifanyika mara kwa mara katika juhudi za Israel kuzuia ushawishi wa wapinzani wake wa kijeshi kwenye mipaka yake.

Mpaka sasa haijajulikana k**a waliouawa ni wanachama wa kundi la kijeshi au raia wa kawaida.

Hali bado ni ya taharuki na majeshi ya pande zote yameripotiwa kuwa katika hali ya juu ya ulinzi.

Endelea kufuatilia kurasa zetu kwa taarifa zaidi kadri tutakavyozipokea.

Toa maoni yako


Msiba Msikitini Maiduguri: Watu 7 wafariki Dunia katika mlipuko mkubwa!Kutokea moja kwa moja nchini Nigeria, Msikiti uli...
12/24/2025

Msiba Msikitini Maiduguri: Watu 7 wafariki Dunia katika mlipuko mkubwa!

Kutokea moja kwa moja nchini Nigeria, Msikiti uliopo ndani ya soko la Gamboru, katika Mji wa Maiduguri, umetikiswa na mlipuko mkubwa uliosababisha vifo vya watu saba waliokuwa wakiabudu.

Tukio hilo la kusikitisha limetokea, ambapo waumini wa Kiislamu walikuwa katika ibada, kabla ya mlipuko huo kutokea ghafla. Mashuhuda wamesema mlio huo ulikuwa wa kutisha na ulitokea ndani kabisa ya eneo la kuswalia.

Taarifa kutoka vyombo vya usalama zimethibitisha vifo hivyo na kueleza kuwa uchunguzi umeanzishwa mara moja.

“Hadi sasa hakuna kundi lolote lililodai kuhusika na tukio hili,” amesema Msemaji wa usalama wa mkoa huo.

Katika tukio la pili hili, kundi la waumini wa Kiislamu limeripotiwa kutekwa na watu wasiojulikana waliokuwa na silaha, na juhudi za kuwaokoa zinaendelea.

Serikali ya Nigeria imetoa wito kwa wananchi kuwa watulivu huku vyombo vya usalama vikiendelea na uchunguzi.

Endelea kufuatilia kurasa zetu kwa taarifa zaidi kuhusu tukio hili la kusikitisha.

Toa maoni yako

Address

Winnipeg, MB

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MWK TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MWK TV:

Share

Category