MWK TV

MWK TV Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MWK TV, Media, Winnipeg, MB.

MWK TV is a modern online television channel that provides National and International News, Sports, Music,Films, Gossips, Documentaries, and more.

- YouTube: MWK TV
- FB : MWK TV
- IG: mwanawekaayatv
- TikTok: mwanawekaaya
- X: MWK TV

Mvutano mpya wazuka kati ya Japan na China kuhusu hatma ya Taiwan!Waziri Mkuu wa Japan, Sanae Takaichi, ametangaza wazi ...
11/16/2025

Mvutano mpya wazuka kati ya Japan na China kuhusu hatma ya Taiwan!

Waziri Mkuu wa Japan, Sanae Takaichi, ametangaza wazi kuwa endapo China itaivamia Taiwan, basi Japan haitasita kuisaidia Taiwan hadi mwisho wa vita. Takaichi amesema hayo akisisitiza dhamira ya taifa lake kulinda usalama wa eneo la Asia Mashariki.

“Tutasaidia Taiwan mpaka mwisho wa vita.”

Kauli hiyo imezua taharuki Beijing, ambako Wizara ya Mambo ya Nje ya China imejibu kwa ukali, ikisema: “Japan wasijiingize katika mgogoro huu. Watakutana na mapigo ambayo hawajawahi kuyakutana nayo kabla.”

Katika historia, baada ya mashambulizi ya mabomu ya nyuklia ya Hiroshima na Nagasaki mwaka 1945, Japan imekuwa mshirika wa karibu wa Marekani katika ukanda wa Asia, pamoja na Korea Kusini.

Je, kauli hii ya Waziri Mkuu wa Japan ni onyo kwa China, au ni tiketi ya kuanzisha mzozo mkubwa wa kijeshi?

Endelea kuwa nasi kwa taarifa zaidi, hapa hapa MWK TV, Ukweli uko hapa.

Toa maoni yako

Mbunge wa Kigoma Mjini, Mheshimiwa Clayton Recocatus Chipando maarufu k**a Baba Levo, ameleta neema kwa wakazi wa Kigoma...
11/16/2025

Mbunge wa Kigoma Mjini, Mheshimiwa Clayton Recocatus Chipando maarufu k**a Baba Levo, ameleta neema kwa wakazi wa Kigoma wanaotarajia kufunga ndoa!

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Baba Levo ametangaza kuwa amenunua gari aina ya Jeep kwa ajili ya wananchi wote wa Kigoma Mjini litakalotumika k**a usafiri wa siku ya harusi, bure kabisa!

"Ndugu zangu wa Kigoma Mjini, kwa sasa mtu yeyote akitaka kuao au kuolewa nimewanunulia gari bureee…!! Hata k**a ni ndoa ya mkeκα. Njoo uweke mafuta ya elfu 13 mwende kanisani, ukumbini au msikitini."

Ndiyo Mfuatiliaji wetu! Unaleta tu mafuta ya elfu 13, na safari ya harusi inafanyika kwa heshima! Wananchi wengi wamepongeza hatua hii ya Mbunge wao, wakisema ni ishara ya kiongozi anayegusa maisha ya watu moja kwa moja.

Ukiwa Kigoma, harusi siyo tena shida! Endelea kufuatilia kurasa zetu hapa hapa MWK TV, Ukweli uko hapa.

Toa maoni yako

Karibu tena Mfuatiliaji wetu, tukikuletea matukio moto moto kutoka kwa Mastaa wa Afrika Mashariki!  Na sasa twende hadi ...
11/16/2025

Karibu tena Mfuatiliaji wetu, tukikuletea matukio moto moto kutoka kwa Mastaa wa Afrika Mashariki!
Na sasa twende hadi nchini Kenya ambako Mwanamuziki maarufu Sanaipei Tande ametoa kauli iliyozua gumzo mitandaoni.

“Kuolewa si lazima. Unaweza kuchagua kutofanya hivyo. Hakuna ubaya kwa mwanaume kukosa pesa kitu k**a hicho kinaweza kubadilika wakati wowote.”

Naam, umesikia mwenyewe! Sanaipei amesema hana tatizo kuwa kwenye uhusiano na Mwanaume asiye na fedha, mradi kuna upendo wa kweli na maelewano.

Ameongeza kuwa pesa sio kipimo pekee cha thamani ya Mwanaume na kwamba yeye yuko tayari kumpa nafasi yeyote anayeonyesha nia ya dhati hata k**a hana uwezo wa kifedha kwa sasa.

Sanaipei tena: “Ndio, naweza kumpa nafasi mwanaume ambaye hana pesa.”

Ni kauli ya kishujaa au utata?

Toa maoni yako

Katika tukio la aina yake lililotokea mwaka 2020 kwenye mchezo wa Kombe la Carabao kati ya Chelsea na Tottenham Hotspur,...
11/16/2025

Katika tukio la aina yake lililotokea mwaka 2020 kwenye mchezo wa Kombe la Carabao kati ya Chelsea na Tottenham Hotspur, Eric Dier alilazimika kuacha Uwanja na kukimbilia chooni wakati timu yake ilikuwa nyuma kwa bao 1-0!

Chelsea walikuwa wakiongoza kwa bao la Timo Werner, lakini dakika 25 kabla ya mpira kumalizika, Dier alihisi haja ya dharura na kutoka Uwanjani bila ruhusa. Hali hiyo ilimkera kocha wake wa wakati huo, José Mourinho, ambaye bila kusita alimfuata chooni kumrudisha haraka Uwanjani!

Kwa bahati nzuri kwa Spurs, Chelsea hawakutumia vyema muda huo, na baada ya Dier kurejea, Erik Lamela alisawazisha bao. Mchezo ukaenda hadi mikwaju ya penati na Tottenham wakatinga hatua inayofuata.

Eric Dier alitangazwa kuwa Mchezaji Bora wa Mechi na kuweka picha kwenye mitandao ya kijamii akiwa na tuzo yake juu ya choo!
Nukuu yake ikisema: “Mwanaume halisi wa mechi.”

Na huo ndio ushuhuda kwamba hata chooni unaweza kuandika historia!

Endelea kufuatilia habari moto moto za michezo hapa hapa MWK TV, Ukweli uko hapa.

Toa maoni yako

Msanii chipukizi anayezidi kung'ara katika anga la muziki wa Afrika Mashariki, Kirikou Akili, ameibuka mshindi wa shinda...
11/15/2025

Msanii chipukizi anayezidi kung'ara katika anga la muziki wa Afrika Mashariki, Kirikou Akili, ameibuka mshindi wa shindano la Super Beat na kutunukiwa gari jipya kabisa!

Ushindi huu umetokana na wimbo wake maarufu "Aha Nihe!?", ambao umevuma kwa kasi kubwa kwenye mitandao ya kijamii na majukwaa ya muziki. Kirikou ameonyesha wazi kuwa muziki wa Burundi unazidi kupenya kimataifa!

Kirikou alinukuliwa akisema: "Nashukuru Mungu na mashabiki wangu wote. Ushindi huu ni wetu sote. Burundi tumefika, na tutaendelea kufika mbali!"

Katika shindano hilo, hakukosekana ushindani mkali kutoka kwa Wasanii wengine wakali k**a Alvella Muhimbare na Yannick Utar, lakini mwisho wa siku, Kirikou ndiye aliyewika zaidi!

Kwa hiyo k**a ulikuwa hujamfahamu Kirikou, basi sasa ndio muda wa kufuatilia kazi zake maana safari yake ya muziki inapaa juu zaidi!

Endelea kufuatilia kurasa zetu kwa habari zaidi.

Toa maoni yako

Habari kutoka Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo!Ubalozi wa Ubelgiji umeingia kwenye lawama baada ya miadi 1000 ...
11/15/2025

Habari kutoka Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo!

Ubalozi wa Ubelgiji umeingia kwenye lawama baada ya miadi 1000 ya maombi ya visa iliyotolewa saa 8 (mbili) usiku kutoweka ndani ya sekunde 30 tu!

Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka ubalozi huo, kuna hofu kuwa teknolojia haramu k**a virusi na ‘bots’ zinatumika kuk**ata nafasi hizo zote na baadaye kuuzwa kwa watu wengine.

Ubalozi wa Ubelgiji umesema, nanukuu: “Tunaamini kuwa miadi hiyo inachukuliwa kwa kutumia programu maalum zisizo halali, na hivyo kuathiri haki ya upatikanaji kwa raia wa kawaida.”

Raia wa Kinshasa wameonyesha kukerwa, wakisema sasa imekuwa vigumu kupata miadi kwa njia ya kawaida, huku wengine wakilazimika kulipia nafasi hizo kwa bei ya juu mtaani.

Wataalamu wa teknolojia na uhamiaji wanashauri maboresho ya haraka ya mfumo huo ili kuzuia udanganyifu.

Tunaendelea kufuatilia taarifa hii kwa kina… Endelea kuwa nasi kwa habari zaidi.

Toa maoni yako

Habari njema kutoka Doha, Qatar.Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kundi la waasi la AFC/M23, leo wametia s...
11/15/2025

Habari njema kutoka Doha, Qatar.

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kundi la waasi la AFC/M23, leo wametia saini makubaliano ya awali ya amani, yanayolenga kumaliza mzozo uliodumu kwa muda mrefu mashariki mwa nchi hiyo.

Lakini dakika chache tu baada ya saini hiyo, ujumbe kutoka upande wa M23 umetolea ufafanuzi uliozusha hisia mseto.

Benjamin Mbonimpa, Mjumbe wa AFC/M23 aliyeshiriki mazungumzo hayo amesema, na tunamnukuu: “Hakutakuwa na mabadiliko yoyote ya hali kwenye uwanja wa mapambano, wala shughuli yoyote ile. Wananchi wetu wanapaswa kuwa na subira, safari bado ni ndefu.”

Kauli hiyo imepokewa kwa tahadhari kubwa na wachambuzi wa masuala ya usalama, huku wengine wakisisitiza kuwa bado kuna safari ndefu kufikia amani ya kudumu.

Itakumbukwa kuwa makubaliano haya ya Doha ni hatua ya kwanza kuelekea mkataba mpana wa amani kati ya pande hizo mbili.

Tutaendelea kufuatilia kwa karibu matukio haya ya kidiplomasia kwa niaba yako.

Endelea kufuatilia kurasa zetu kwa taarifa zaidi kupitia kituo hiki cha MWK TV, Ukweli uko hapa.

Toa maoni yako

TAMKO RAMSI LA BARAZA MAASKOFU TEC KUHUSU JUU YA UCHAGUZI, MAANDAMANO, UTEKAJI, POLISI KUTUMIA NGUVU https://youtu.be/DB...
11/15/2025

TAMKO RAMSI LA BARAZA MAASKOFU TEC KUHUSU JUU YA UCHAGUZI, MAANDAMANO, UTEKAJI, POLISI KUTUMIA NGUVU
https://youtu.be/DBg-_MVUmns?si=whN3g6KHOy3jQNNE

Toa maoni yako

MWKT TV is a modern online television channel that provides National and International News, Sports, Music,Films, Gossips, Documentaries, and more.- YouTube:...

kutoka Doha, Qatar, Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kundi la Waasi la AFC/M23 wamesaini rasmi mkataba wa...
11/15/2025

kutoka Doha, Qatar, Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kundi la Waasi la AFC/M23 wamesaini rasmi mkataba wa mfumo wa amani, hatua ya kwanza muhimu kuelekea makubaliano ya kina ya kumaliza mzozo wa muda mrefu katika maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi, mkataba huo wa awali unalenga kuweka msingi wa usitishaji mapigano, urejeshaji wa wakimbizi, na ujumuishaji wa wapiganaji wa zamani katika jamii au jeshi la taifa.

“Serikali ya Congo na AFC/M23 wamesaini makubaliano ya mfumo wa amani, hatua ya mwanzo kuelekea mkataba wa kina wa kudumu,” imesema taarifa hiyo kutoka Doha.

Mkataba huu unatajwa kuwa hatua ya matumaini kwa mamilioni ya raia wa Kongo waliokumbwa na machungu ya vita kwa zaidi ya miaka kumi.

Mashirika ya kimataifa k**a Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika yamekaribisha hatua hii na kutoa wito kwa pande zote kuendeleza majadiliano kwa dhati hadi amani ya kudumu itakapopatikana.

Endelea kufuatilia matangazo yetu kwa taarifa zaidi juu ya maendeleo ya mkataba huu wa kihistoria.

Toa maoni yako

Katika hii dunia inayozidi kuendeshwa na tamaa ya faida, kuna shujaa mmoja aliyesimama kidete kwa ajili ya uhuru wa tekn...
11/15/2025

Katika hii dunia inayozidi kuendeshwa na tamaa ya faida, kuna shujaa mmoja aliyesimama kidete kwa ajili ya uhuru wa teknolojia na huyo si wingine bali ni Jean-Baptiste Kempf, Muundaji na kiongozi wa programu maarufu ya VLC Media Player.

Akiwa na miaka 18, Jean-Baptiste alijiunga na timu ya wanafunzi waliokuwa wakiitengeneza VLC. Miaka mitatu baadaye, alipokuwa na miaka 21, alipewa uongozi wa mradi huo. Ndipo majaribu yakaanza!

Kampuni kubwa yakamtolea ofa ya hadi dola milioni 10 ili waununue programu hiyo au waweke matangazo na kukusanya data za watumiaji. Lakini Jean-Baptiste alikataa kwa msimamo mkali: “Hapana. VLC itabaki huru milele.”

Akaanzisha shirika lake la VideoLAN ambalo hadi leo halina matangazo, halikusanyi taarifa binafsi, na VLC bado ni bure kwa kila Mtu duniani.

Kwa zaidi ya miaka 16, amekuwa akitoa huduma hii ya kipekee bila malipo yoyote. Na sasa, kila unapofungua filamu au muziki kupitia VLC, kumbuka Mtu mmoja alikataa mabilioni, kwa ajili yako.

Toa maoni yako

Address

Winnipeg, MB

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MWK TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MWK TV:

Share

Category