11/16/2025
Mvutano mpya wazuka kati ya Japan na China kuhusu hatma ya Taiwan!
Waziri Mkuu wa Japan, Sanae Takaichi, ametangaza wazi kuwa endapo China itaivamia Taiwan, basi Japan haitasita kuisaidia Taiwan hadi mwisho wa vita. Takaichi amesema hayo akisisitiza dhamira ya taifa lake kulinda usalama wa eneo la Asia Mashariki.
“Tutasaidia Taiwan mpaka mwisho wa vita.”
Kauli hiyo imezua taharuki Beijing, ambako Wizara ya Mambo ya Nje ya China imejibu kwa ukali, ikisema: “Japan wasijiingize katika mgogoro huu. Watakutana na mapigo ambayo hawajawahi kuyakutana nayo kabla.”
Katika historia, baada ya mashambulizi ya mabomu ya nyuklia ya Hiroshima na Nagasaki mwaka 1945, Japan imekuwa mshirika wa karibu wa Marekani katika ukanda wa Asia, pamoja na Korea Kusini.
Je, kauli hii ya Waziri Mkuu wa Japan ni onyo kwa China, au ni tiketi ya kuanzisha mzozo mkubwa wa kijeshi?
Endelea kuwa nasi kwa taarifa zaidi, hapa hapa MWK TV, Ukweli uko hapa.
Toa maoni yako