Mecamedia Informations de contact, plan et itinéraire, formulaire de contact, heures d'ouverture, services, évaluations, photos, vidéos et annonces de Mecamedia, Chaîne de télévision, Kinshasa.

🎥 Karibu MECAMEDIA!
📰 Habari, ⚽ Michezo, 📜 Historia na 🎬 Burudani za kipekee.
📅 Maudhui mapya kila siku!
👉 Bonyeza Subscribe kwa updates bora!

10/12/2025

RDC : Serikali yathibitisha mashambulizi ya mabomu kutoka Rwanda, mamia ya maelfu wakimbia makazi yao

Msemaji wa Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Patrick Muyaya, amesema kupitia RTNC kwamba mabomu yanayorushwa kutoka eneo la Buragama, upande wa Rwanda, yamelenga maeneo ya raia katika njia ya Kamanyola–Uvira.

Kwa mujibu wa taarifa za awali:
• Zaidi ya watu 200,000 wamelazimika kukimbia makazi yao,
• Zaidi ya vifo 80 vimeripotiwa hadi sasa,
• Serikali inasema inaendelea kufuatilia hali kwa karibu.

Muyaya ameeleza kuwa anasubiri takwimu kamili kutoka kwa Gavana Purusi, ambaye anaratibu taarifa za maafa na idadi ya walioathirika.

Ametoa wito kwa raia wote “kuendelea kuwa watulivu lakini waendelea kubaki macho na kushik**ana” mbele ya tishio linaloendelea mashariki mwa nchi.

🖊️ Mwandishi: MecaMedia Africa – Desk ya Ulinzi & Usalama

📌 Soma Zaidi: Mecamediaafrica.com

🏷️ Tags:

Baada ya kuona video zao zikiwa tunazisambaza kwenye group la WhatsApp la MecaMedia, watutsi wameamua kuripoti group hil...
10/12/2025

Baada ya kuona video zao zikiwa tunazisambaza kwenye group la WhatsApp la MecaMedia, watutsi wameamua kuripoti group hilo ili lifungwe.

Kwasababu , photo hizo zilionyesha uongo na mabadiliko (edit) waliokuwa wakitengeneza ili kudanganya umma kuhusu hali ya usalama Uvira.

Wakazi wa uvira tuna Towa wito kwa umma kutodanganywa na propaganda hizo, waasi hawako sehemu yoyote ndani ya Uvira k**a wanavyodai kwenye mitandao.

Wananchi wanaendelea kuomba Mungu na kuwaombea Wazalendo waendelee kushikilia mistari ya ulinzi, ili Uvira ibaki salama k**a ilivyo sasa.

🖊 Mwandishi : MecaMedia Africa – Uvira Desk
📌 Soma zaidi : Usalama Mashariki mwa DRC, M23, Wazalendo, Propaganda za Mtandaoni

🏷 Tags :

🇧🇮🇨🇩 Burundi lamkemea vikali Rwanda na M23 : “Hii ni fedheha kwa Marekani na Rais Trump”IHI — mecamediaafrica.comSerikal...
10/12/2025

🇧🇮🇨🇩 Burundi lamkemea vikali Rwanda na M23 : “Hii ni fedheha kwa Marekani na Rais Trump”
IHI — mecamediaafrica.com

Serikali ya Burundi imetoa kauli kali leo Jumatano, ikisema kwamba kusonga mbele kwa waasi wa M23, chini ya wiki moja tangu kutiwa saini kwa makubaliano ya kusitisha vita nchini DRC, ni “tusi kubwa kwa Marekani na fedheha isiyo na kifani kwa Rais Donald Trump.”

Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi, Edouard Bizimana, ameliambia shirika la habari la AFP kuwa hatua ya waasi hao—wanaotuhumiwa kuungwa mkono na Rwanda—kuchukua mji wa kimkakati wa Uvira, ilhali makubaliano mapya yamesainiwa, ni ishara kwamba M23 na Kigali hawana nia ya amani.

🇧🇮 Burundi yafunga mpaka na DRC

Kutokana na hali hiyo, Burundi imetangaza kufunga mpaka wake na Congo, baada ya M23 kusogea karibu na mji wa Bujumbura.
Kwa mujibu wa Bizimana, hatua hii ni ya kulinda usalama wa taifa na kuzuia athari za mapigano kuvuka mipaka.

🇷🇼 Rwanda lawindwa na mwito wa vikwazo

Waziri Bizimana ameomba Rwanda iwekwe chini ya vikwazo vya kimataifa, akisema Kigali inachochea vurugu Mashariki mwa DRC kupitia msaada kwa M23 — tuhuma ambazo Rwanda imekuwa ikikanusha mara kwa mara.

“Rwanda haionyeshi nia ya kusitisha vita. Inaendelea kuiunga mkono M23 bila kuficha. Hili ni tishio kwa amani ya ukanda mzima,” — alisema Bizimana.

🇺🇸 Aibu kwa Marekani?

Burundi inaona kwamba kuendelea kwa mashambulizi haya, siku chache baada ya mchakato wa amani unaounga mkono Marekani, ni pigo kubwa kwa juhudi za Washington, na hasa kwa Rais Donald Trump, ambaye amejitosa k**a msuluhishi mkuu kati ya Kinshasa na Kigali.

🖋️ Mwandishi: Musa Ruvubika
📌 Soma zaidi kwenye: mecamediaafrica.com

🏷️ Tags:

Njo kweli ya iyo photo iyo mwache panique✍️ Mwandishi: MecaMedia Africa📚 Soma zaidi: mecamediaafrica.com
10/12/2025

Njo kweli ya iyo photo iyo mwache panique

✍️ Mwandishi: MecaMedia Africa
📚 Soma zaidi: mecamediaafrica.com

10/12/2025

UVIRA : Wazalendo waimarisha ulinzi, wakikanusha madai ya waasi kuingia mjini

Hali ya usalama mjini Uvira (Sud-Kivu) inaendelea kuwa tulivu huku wanamovement wa Wazalendo wakithibitisha kuwa wako katika maeneo yote ya kimkakati ya mji huo na kwamba hakuna “repli stratégique” wala uwepo wa waasi wa AFC/M23 ndani ya Uvira.

Katika ujumbe wao kwa wananchi, Wazalendo wamesisitiza kuwa mji uko chini ya udhibiti wao kamili, wakikanusha vikali tetesi kwamba waasi wamesogea au kuingia Uvira.

Wakati huohuo, madai mazito yameelekezwa kwa baadhi ya wanajeshi wa FARDC wanaotuhumiwa “kusaliti wananchi”, jambo lililoongeza hasira na msimamo mkali wa makundi ya kujilinda ya raia.

Wazalendo wamewataka wakazi wa Uvira na WatCongolais wote ulimwenguni kudumisha utulivu na kuendelea kuwa na ujasiri, wakisema wamedhamiria kulinda mji bila kurudi nyuma.

✍️ Mwandishi: MecaMedia Africa
📚 Soma zaidi: mecamediaafrica.com

10/12/2025

Uvira yatikisika: Wazalendo wathibitisha uwepo mkubwa wa kijeshi ndani ya mji

Hali ya taharuki imetanda katika mji wa Uvira, baada ya taarifa kuenea kwamba viongozi wakuu wa vikundi vya Wazalendo wamewasili na kuanza kujipanga kijeshi katika maeneo mbalimbali ya mji huo.

Katika ujumbe ulioenea kwenye mitandao ya kijamii Ijumaa hii, inaelezwa kuwa:
• Jenerali Muzalendo James Fyeka Aduwi yupo Uvira kwa ufuatiliaji wa operesheni.
• Jenerali Muzalendo Makanaki Kasimbira John anaripotiwa kuwepo maeneo ya Bonde la Ruzizi.
• Jenerali René Itongwa na Jenerali Rady Mutoto pia wanatajwa kuwa katika maeneo tofauti ya mkoa huo.

Ujumbe huo umetangaza kuwa vikosi vya Wazalendo vimesambazwa maeneo mbalimbali ya Uvira, hatua inayokuja wakati mvutano wa kiusalama ukiendelea kuongezeka mashariki mwa nchi.

Wananchi wamehimizwa kuwa makini, huku hali ya wasiwasi ikiongezeka miongoni mwa wakaazi wanaohofia uwezekano wa mapigano mapya.

Soma zaidi kwenye: mecamediaafrica.com
Mwandishi: Meca Media Africa

Tags:

10/12/2025

Wazalendo watuliza hali Uvira, wakilaumu FARDC kwa “kuwasaliti” katika mapambano

Katika ujumbe unaosambaa kwenye mitandao, wapiganaji wa Wazalendo wameeleza kuwa mji wa Uvira bado uko chini ya udhibiti wao, licha ya kile wanachokiita “kukata tamaa” kutoka kwa baadhi ya maafisa wa FARDC.

Wakiongozwa na Jenerali Muzalendo Makanaki Kasimbira John, Wazalendo wanadai kuimarisha vizuizi na ulinzi kwenye maeneo kadhaa ya Plain de la Ruzizi, wakisisitiza kuwa wako tayari kuendelea kupambana kwa ajili ya nchi.

Kwa mujibu wa ujumbe huo, Wazalendo wanasema waliwahi kuwa karibu kuikomboa Bukavu wiki iliyopita, lakini juhudi zao zilikwama kutokana na kile walichotaja k**a “ujumbe wa kuwadhoofisha” kutoka baadhi ya wanajeshi wa FARDC.

Wamewataka wakazi wa Goma na Bukavu kubaki na matumaini, wakidai kuwa mapambano yao bado yanaendelea.

Hadi sasa hakuna tamko rasmi kutoka FARDC kuthibitisha au kukanusha madai haya.

Mwandishi: Mecamedia Africa

Soma zaidi kwenye: mecamediaafrica.com

Tags:

Pas de panique à Uvira : les images virales sont générées par l’IALa population ya Uvira imetakiwa kutokuwa na hofu baad...
10/12/2025

Pas de panique à Uvira : les images virales sont générées par l’IA

La population ya Uvira imetakiwa kutokuwa na hofu baada ya kusambaa kwenye mitandao picha mbili zinazoonyesha vurugu na machafuko muka mjini. Taarifa rasmi zinabainisha kuwa picha hizo zimetengenezwa na intelligence artificielle (AI) na hazihusiani kabisa na hali halisi.

Kwa mujibu wa vyanzo vya usalama, mji wa Uvira uko shwari na chini ya udhibiti wa mamlaka. Wananchi wanaombwa kutokubali taarifa za kupotosha na kuzingatia tu chanzo cha habari kinachoaminika.

Mecamedia Africa inakumbusha kuwa teknolojia ya AI inaweza kutengeneza picha zenye uhalisia mkubwa, hivyo tahadhari inahitajika kabla ya kusambaza taarifa zozote.

Mwandishi: Mecamedia Africa
Soma zaidi: https://mecamediaafrica.com

Tags:

Kinshasa–Limete : Wafanyakazi wa kiwanda cha kutibu maji walaani mazingira hatarishi ya kaziWafanyakazi wa kibarua katik...
10/12/2025

Kinshasa–Limete : Wafanyakazi wa kiwanda cha kutibu maji walaani mazingira hatarishi ya kazi

Wafanyakazi wa kibarua katika kiwanda cha kutibu maji cha Limete wameibua kilio kikubwa kuhusu mazingira hatarishi wanayofanyia kazi, wakisema wanapoteza afya zao kila siku bila ulinzi wowote wa kitaalamu.

Katika ziara ya Jumanne 9 Novemba, wafanyakazi hao walisema kuwa licha ya kushughulikia kemikali hatari zinazotumika kusafisha maji ya matumizi ya wananchi, hawapati vifaa vya kujikinga k**a vile glavu, barakoa, miwani au mavazi maalum ya kazi.

Baadhi wameanza kupata vipele, matatizo ya kupumua, na kizunguzungu, bila msaada wa kitabibu kutoka mamlaka husika.

“Tunatoa huduma muhimu kwa wananchi, lakini tunafanya kazi k**a watu wasiokuwa na thamani,” alisema mmoja wao kwa masharti ya kutotajwa jina.

Wanatoa wito kwa REGIDESO na Wizara ya Afya kuchukua hatua za haraka ili kulinda maisha ya wafanyakazi, na kuhakikisha viwango vya usalama vinazingatiwa.

🖊 Mwandishi: MecaMedia Africa
📌 Soma zaidi: www.mecamediaafrica.com

🏷️ Tags:

Kinshasa : Operesheni ya Usafi Yafichua Zaidi ya Wafanyakazi 3,800 Heu Katika Sekta ya UsafiriOperesheni maalum ya uhaki...
10/12/2025

Kinshasa : Operesheni ya Usafi Yafichua Zaidi ya Wafanyakazi 3,800 Heu Katika Sekta ya Usafiri

Operesheni maalum ya uhakiki wa watumishi iliyoanzishwa na Waziri wa Usafiri wa Jiji la Kinshasa, Jésus-Noël Sheke, imebaini udanganyifu mkubwa ndani ya utawala wa usafiri wa jiji hilo.

Kwa mujibu wa ripoti ya ukaguzi iliyotolewa Jumanne, tarehe 9 Desemba, kati ya majina 7,293 yaliyokaguliwa, ni wafanyakazi 3,067 pekee waliothibitishwa kuwa halali—wakati 3,845 wamegundulika kuwa ni hewa, waliopenyishwa kwa kutumia hati feki na ushirikiano wa baadhi ya maafisa wa ndani.

Takwimu zilizokuwa zikitolewa awali na idara husika zilionekana kutofautiana pakubwa na uhalisia, jambo lililothibitisha kuwepo kwa uvurugaji mkubwa wa orodha za wafanyakazi.

Waziri Sheke ameahidi hatua kali kwa wote waliohusika na udanganyifu huo na kusisitiza kuwa zoezi la kusafisha sekta ya usafiri litaendelea ili kurejesha uwazi na nidhamu ya kiutawala.

✍️ Mwandishi: MecaMedia Africa
📌 Soma zaidi: www.mecamediaafrica.com

🔖 Tags:

📰 Ituri : Watu 4 wauawa na watutsi wa ADF saa chache baada ya kufunguliwa kwa barabara ya RN4Saa chache baada ya serikal...
10/12/2025

📰 Ituri : Watu 4 wauawa na watutsi wa ADF saa chache baada ya kufunguliwa kwa barabara ya RN4

Saa chache baada ya serikali kutangaza kufunguliwa tena kwa Barabara Kuu ya RN4, kipande cha Luna–Komanda, mashambulizi mapya ya watutsi wa ADF-MTM yameutikisa tena mkoa wa Ituri.

Jioni ya Jumanne, 9 Desemba 2025, waasi walivamia kijiji cha Idohu, kilichopo kando ya barabara hiyo. Kulingana na CRDH, kupitia kwa koordinator wake Christophe Munyanderu, watu wanne waliuawa, akiwemo mtoto mchanga, huku wengine watatu wakipigwa risasi walipokuwa wakitoka shambani.

Mashambulizi haya yametokea licha ya uimarishaji wa operesheni za pamoja kati ya jeshi la Congo (FARDC) na lile la Uganda (UPDF), zilizolenga kurejesha usalama na kufufua shughuli za uchumi katika eneo hilo lililokuwa limefungwa kwa zaidi ya miaka mitatu.

Watu wa eneo hilo pamoja na mashirika ya haki za binadamu wamelaani tukio hilo, wakisema linaendelea kuhatarisha maisha ya raia na kuzuia maendeleo ya Ituri.

✍️ Mwandishi: MecaMedia Africa

🔗 Soma zaidi kwenye: mecamediaafrica.com

10/12/2025

Sikiliza ivi video kwa makini

✍️ Mwandishi: MecaMedia Africa
📌 Soma zaidi: www.mecamediaafrica.com

Adresse

Kinshasa

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque Mecamedia publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Contacter L'entreprise

Envoyer un message à Mecamedia:

Partager