10/12/2025
RDC : Serikali yathibitisha mashambulizi ya mabomu kutoka Rwanda, mamia ya maelfu wakimbia makazi yao
Msemaji wa Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Patrick Muyaya, amesema kupitia RTNC kwamba mabomu yanayorushwa kutoka eneo la Buragama, upande wa Rwanda, yamelenga maeneo ya raia katika njia ya Kamanyola–Uvira.
Kwa mujibu wa taarifa za awali:
• Zaidi ya watu 200,000 wamelazimika kukimbia makazi yao,
• Zaidi ya vifo 80 vimeripotiwa hadi sasa,
• Serikali inasema inaendelea kufuatilia hali kwa karibu.
Muyaya ameeleza kuwa anasubiri takwimu kamili kutoka kwa Gavana Purusi, ambaye anaratibu taarifa za maafa na idadi ya walioathirika.
Ametoa wito kwa raia wote “kuendelea kuwa watulivu lakini waendelea kubaki macho na kushik**ana” mbele ya tishio linaloendelea mashariki mwa nchi.
🖊️ Mwandishi: MecaMedia Africa – Desk ya Ulinzi & Usalama
📌 Soma Zaidi: Mecamediaafrica.com
🏷️ Tags: