08/11/2025
wanaowania tuzo za mwaka 2026, zitakazotolewa Februari 1, 2026 nchini Marekani 🇺🇸.
Miongoni mwa waliotajwa ni Eddy Kenzo kutoka Uganda, ambaye aliweka historia mwaka 2022 k**a msanii wa kwanza kutoka nchini humo kupata Grammy nomination. Safari hii ameibuka tena kwa mara ya pili mfululizo, akishindania kipengele cha Best African Performance pamoja na majina makubwa ya muziki barani Afrika.
Wanaowania kipengele cha Best African Performance ni:
🎵 Burna Boy 🇳🇬 – LoVe
🎵 Eddy Kenzo 🇺🇬 & Mehran Martin – Hope & Love
🎵 Ayra Starr & Wizkid 🇳🇬 – Gimme Dat
🎵 Tyla 🇿🇦 – Push To Start
🎵 Davido & Omah Lay 🇳🇬 – With You
Swali ambalo wengi wamejiuliza ni kwa nini wasanii kutoka Tanzania 🇹🇿 hawajafanikiwa kuingia kwenye orodha hii mwaka huu?
Je, ni ukosefu wa international strategy, usimamizi hafifu wa kazi, au muziki wetu bado haujapata msukumo wa kimataifa unaohitajika kufikia viwango vya Grammy?
🗣️ Tuambie maoni yako — unadhani nini kimekwamisha wasanii wa Tanzania kufika hatua hii?