Banza Media "Burudani | Gossip | Lifestyle
đź“© DM for Ads & Collabs
🎬 New content daily" Asante kwa sapoti yenyu
Bado kwa zidi kusonga mbele
(3)

Staa wa Bongo Fleva, Juma Jux, na mpenzi wake mrembo Priscilla Ajoke wameweka wazi kuwa wanatarajia kupata mtoto wa kium...
21/08/2025

Staa wa Bongo Fleva, Juma Jux, na mpenzi wake mrembo Priscilla Ajoke wameweka wazi kuwa wanatarajia kupata mtoto wa kiume. Taarifa hiyo imetangazwa kupitia sherehe ya kuvutia ya gender reveal iliyofanyika kwa mbwembwe na rangi nyingi.

Msanii Wa rap Nchini Kenya  ametia verse kwenye Wimbo Maarufu Wa   Copy & paste Je remix inaitajikaVipi amepita vizuri a...
21/08/2025

Msanii Wa rap Nchini Kenya ametia verse kwenye Wimbo Maarufu Wa Copy & paste
Je remix inaitajika

Vipi amepita vizuri ama amechapa ?

Video 👇

Msanii maarufu wa Bongo Fleva nchini, Yammitz, ametangaza rasmi ujio wa EP yake mpya yenye jina “After All”, ambayo inat...
21/08/2025

Msanii maarufu wa Bongo Fleva nchini, Yammitz, ametangaza rasmi ujio wa EP yake mpya yenye jina “After All”, ambayo inatarajiwa kutoka Ijumaa hii. EP hiyo imejaa ladha ya kipekee na ina jumla ya nyimbo 6 k**a ifuatavyo:

1. Arenare

2. Sijafunzwa (feat. Mdogo Sajent)

3. Pole

4. Doze Doze

5. Unanichukia

6. Na Enjoy

Swali kwa mashabiki: Ni wimbo gani unausubiri kwa hamu zaidi kutoka kwenye EP hii?

20/08/2025

Diamond platnumz akizungumuzia safari ya maisha Yake

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Lava Lava, amefunguka kuhusu changamoto anazokutana nazo kila anapotoa kazi mpya za muziki....
20/08/2025

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Lava Lava, amefunguka kuhusu changamoto anazokutana nazo kila anapotoa kazi mpya za muziki. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Lava Lava ameeleza kuwa licha ya jitihada zake, amekuwa ni miongoni mwa wasanii wanaokumbwa na fitna mara kwa mara, jambo analodai limekuwa likijirudia kila wakati.

Hata hivyo, Lava Lava amesema hana hofu kwani anaamini Mungu yupo pamoja naye na ataendelea kusimama imara katika safari yake ya muziki.

"Mpaka sasa mimi ndio msanii pekee ninayeongoza kwa kufanyiwa fitna kila ninapotoa kazi zangu mpya, ila Mungu yupo na mimi," ameandika Lava Lava.

Hivi karibuni msanii huyo ameachia EP yake mpya iitwayo TimeEP, akiwahakikishia mashabiki wake burudani ya kipekee licha ya changamoto anazokumbana nazo.

Msanii maarufu wa Bongo Fleva, Marioo, amewashukuru mashabiki wake kwa sapoti huku akitumia ukurasa wake wa mitandao ya ...
19/08/2025

Msanii maarufu wa Bongo Fleva, Marioo, amewashukuru mashabiki wake kwa sapoti huku akitumia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii kuwakumbusha mchango wake mkubwa katika tasnia ya muziki wa Tanzania.

Katika ujumbe wake, Marioo amesema anajiandaa kuachia wimbo mpya ambao utakuwa ni GLOBAL SONG, utakaopatikana ndani ya albamu yake “The God Son Deluxe.”

🎤 Marioo aliandika:

> “Watanzania mnanidai tu GLOBAL SONG na naenda kuwapa soon kwenye hii hii The God Son Deluxe. Lakini tofauti na hapo, kwa kutia hizi hit back-to-back kwa generation hii, hakuna dogo anayeweza toka Mama Amina mpaka leo. Sijapoa, sijaboa, na mkumbuke sijawahi kubebwa na label yoyote kubwa wala kuandikiwa wimbo, na bado kuna wasanii wametoka kupitia mimi. Mnasahau haraka sana, nimeona niwakumbushe na nawakumbusha nikiwa na wimbo namba moja nchini na nikiwa k**a mmiliki wa tuzo ya Msanii Bora wa Mwaka (Bongo Fleva) kwa miaka kadhaa. Nasubiri tuzo yangu ya mwaka jana na mwaka huu, na nina uhakika hakuna mtu anaweza kuchukua hiyo tuzo k**a siyo mimi. Asanteni kwa support.”

Kwa miaka ya karibuni, Marioo amekuwa miongoni mwa wasanii wachache walioweza kujiweka kileleni bila msaada wa label kubwa, na bado ametoa hits zilizotikisa anga la muziki.

👉 Hivi sasa, akiwa na wimbo namba moja nchini, Marioo anaendelea kuthibitisha nafasi yake k**a mmoja wa nguzo kuu za kizazi kipya cha Bongo Fleva.

Je Yuko sahihi kudai kuwa hakuna Msanii Anae muweza Kwasasa ?

Nyota mkubwa wa muziki barani Afrika, Wizkid, ameonekana aki-vibe na wimbo maarufu wa Harmonize uitwao “Single Again”, j...
19/08/2025

Nyota mkubwa wa muziki barani Afrika, Wizkid, ameonekana aki-vibe na wimbo maarufu wa Harmonize uitwao “Single Again”, jambo lililozua msisimko mkubwa miongoni mwa mashabiki wa muziki wa Bongo Fleva na Afrika kwa ujumla.

“Single Again” ni moja ya nyimbo zilizotikisa Afrika Mashariki na kimataifa tangu ilipotolewa rasmi mwaka 2023. Ngoma hiyo imekuwa na mafanikio makubwa kwenye majukwaa ya kidijitali, ambapo YouTube audio pekee imevutia zaidi ya watazamaji milioni 10, huku Spotify ikirekodi zaidi ya streams milioni 13.

Kuvutiwa kwa msanii mkubwa k**a Wizkid ni ushahidi wa namna muziki wa Bongo Fleva unavyoendelea kupenya kwenye anga la kimataifa na kuthibitisha hadhi ya Harmonize k**a mmoja wa wasanii wenye ushawishi mkubwa barani Afrika.

👉 Wewe unaionaje collabo ya Wizkid na Harmonize ikitokea?

Video below 👇

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, amefunguka kuhusu safari yake ya muziki na mchango mkubwa aliopata kuto...
19/08/2025

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, amefunguka kuhusu safari yake ya muziki na mchango mkubwa aliopata kutoka kwa mama yake mzazi, Mama Dangote, alipokuwa akianza kutafuta nafasi kwenye tasnia ya muziki.

Akizungumza kupitia , Diamond alisema kuwa mama yake aliwahi kumpa yeye na kaka yake Pete la dhahabu ili waiuze , kwa ajili ya kujipatia fedha. Sehemu ya fedha hizo alitumia kulipia session ya studio na kurekodi wimbo wake wa kwanza.

Kwa mujibu wake, wimbo huo haukufanikiwa sana kutokana na kukosa uzoefu, lakini ulikuwa chanzo cha watu kugundua kipaji chake na hatimaye kumpa nafasi ya kuanza kuandaa albamu yake ya kwanza. Hata hivyo, msaidizi wake wa mwanzo alipata matatizo ya kifedha na kumlazimu Diamond kuendelea kujihangaikia peke yake.

Akiendelea kusimulia, Diamond alikumbuka siku moja alipokuwa akimsaidia rafiki yake kutoa maji nyumbani kwao, ghafla akaanza kuimba kutokana na msongo wa mawazo. Rafiki mmoja alimsikia na kumwunganisha na mtu aliyemsaidia zaidi katika safari yake ya muziki.

Kwa Diamond, hii ni hadithi inayoonyesha namna ambavyo Mama Dangote aliweka kando mitazamo hasi ambayo wazazi wengi hujihusisha nayo kuhusu muziki na kumsaidia kijana wake kufuata ndoto zake.

Mwanadada msanii wa muziki wa Bongo Flava, Yasiruni Shabani maarufu k**a , ameandaa hadithi maalum itakayogusia safari y...
19/08/2025

Mwanadada msanii wa muziki wa Bongo Flava, Yasiruni Shabani maarufu k**a , ameandaa hadithi maalum itakayogusia safari yake ya maisha na muziki kwa ujumla.

Hadithi hiyo yenye kusisimua ameipa jina la “AFTER ALL” kwa Kiswahili ikimaanisha “BAADA YA YOTE”. Kupitia kazi hii, Yammitz ataeleza mambo yaliyotokea kabla na baada ya safari yake ya muziki, akifichua undani wa changamoto na mafanikio aliyoyapitia.

Mashabiki wake wanasubiri kwa hamu kufahamu, ni nini hasa kilichotokea nyuma ya pazia na kipi kinachomsubiri mbele.

👉 Wewe unadhani Yammitz atafichua nini? Toa maoni yako.

Naona unalazimisha kuhitilafiana na mimi, nikuongezee mwendo, okay wacha nikuridhishe…Kwanza kabisa, sikutaka mitandaoni...
18/08/2025

Naona unalazimisha kuhitilafiana na mimi, nikuongezee mwendo, okay wacha nikuridhishe…

Kwanza kabisa, sikutaka mitandaoni. Niliku-pigia simu na kukutumia meseji na tulipokutana niliongea na wewe kwa hekima na ushahidi namna gani nimekua sipendezewi.

Nimekua nikimsema Baba Levo, anachokifanya tena nikikuonyesha kwa ushahidi na nikuambia kuwa hakina faida kwangu zaidi ya kunitia tu ubaya!

Lakini pia nilikuambia, msanii anapotoka kwenye lebo usitegemee wote watakuwa na reaction za kufanana. Wengine watakuwa na reaction mbalimbali:

Kuna wengine wanaweza wakaona wanareact vitu ambavyo siyo vizuri kwa maumivu ya kukupenda tu.

Kuona “dah, ndugu yetu kaio kutoka kwenye team…”

Nikakuambia: jitahidi kutumia busara, maana hayo ni mambo ya kawaida. Na unapaswa kujua binadamu wako hivyo — usipokua makini utaona kila mtu katumwa na Diamond.

Then utaishia kunichukia na kugombana na mimi bila sababu.

Nikakutolea mfano, hai kua ata wewe alipokuwa Rayvanny ulikuja nyumbani kwangu na hasira kuniambia maneno kedekede ya kumchukia Rayvanny, na ulipinga kabisa nisifanye naye nyimbo ya Nitongoze na wala nisisirikiane nae kwa lolote.

Nikakuambia: hapana, si vyema mtu kutoka kwenye lebo sio adui. Ni jambo la kawaida, kuna time itafika ata wewe utapaswa pia kutoka kwa lebo kuanza maisha ya kujitegemea.

Haikuishia hapo, na kila nilipofanya nae wimbo ulinnuna na mara zote kuchukia kwanini nampasupport kazi zake!

Diamond Platnumz vs Mbosso: Mgogoro Waibuka Kuhusu Wimbo “Pawa”Beef kubwa limezuka kati ya Diamond Platnumz na aliyekuwa...
18/08/2025

Diamond Platnumz vs Mbosso: Mgogoro Waibuka Kuhusu Wimbo “Pawa”

Beef kubwa limezuka kati ya Diamond Platnumz na aliyekuwa msanii wa lebo yake, Mbosso, baada ya rafiki wa karibu wa Diamond, Baba Levo, kudai hadharani kwamba Diamond anastahili kupewa asilimia 50 ya sifa za wimbo mkubwa wa Mbosso, Pawa. Baba Levo alienda mbali zaidi akisema: “Tupe melodi yetu.”

Mbosso Ajibu

Mbosso hakusita kujibu kwa hasira, akisisitiza kwamba Pawa ameandika mwenyewe kwa asilimia 100, na mchango wa Diamond ulikuwa mdogo sana. Aidha, alimlaumu Diamond kwa kutoshughulikia kauli za Baba Levo, huku akikanusha vikali kwamba Diamond ndiye aliyeandika wimbo huo.
Licha ya kueleza kwamba bado anamuheshimu Diamond, Mbosso alieleza hatakubali kipaji chake kudharauliwa kwa mtu mwingine kupewa sifa zisizo zake.

Diamond Ajitokeza

Diamond Platnumz alijibu kupitia mfululizo wa posti ndefu kwenye Instagram, akikanusha wivu au wazo la kupora sifa. Alisema hakutaka jambo hilo lifike mtandaoni kwani tayari alikuwa amempigia simu Mbosso na kumtumia ujumbe akimpa ushahidi:
“Sikutaka mitandao… nilikupigia simu na kukutumia messages… nilikuonyesha kwa ushahidi kuwa hakuna faida kwangu zaidi ya kunitia tu ubaya.”

Diamond aliongeza kuwa migongano ndani ya lebo ni jambo la kawaida, na si kila msanii akiondoka lazima aendelee na uhusiano mzuri:
“Msanii anapotoka kwenye lebo usitegemee wote watakua na reaction zinazofanana… wengine wanaweza wakawa wanareact vitu ambavyo sio vizuri.”

Alimkumbusha Mbosso kuwa hata yeye mwenyewe aliwahi kumzuia kushirikiana na Rayvanny, lakini Diamond hakumkataza, akithibitisha kwamba kushirikiana na wasanii wa nje ya Wasafi si usaliti.

Mashtaka na Utetezi

Kuhusu wivu, Diamond alihoji:
“Mie nikuonee wewe wivu kwa kitu gani haswa? Itanisaidia nini? Nitake sifa kupitia Pawa? Pawa imehit kuliko nyimbo ya Sele nchini? Je Sele uliandika pekeako?”

Diamond pia alidai kuwa yeye ndiye aliyechangia kwa kiwango kikubwa kwenye nyimbo nyingi za Mbosso:
“Takribani 90% ya nyimbo zako zote nimeandika… kuanzia asilimia 40%, 50%, zingine hadi asilimia 90% viitikio, verses, michezesho na kadharika.”

Zaidi ya muziki, Diamond alifichua msaada wa kifedha aliompatia Mbosso wakati akiwa Wasafi:
“Umetoka Wasafi licha ya sijakutoza hata shilingi mia… nilikua nakudai milioni 323,250,000/= ya kukukopesha toka mfukoni mwangu, na vyote nilikuachia nikakuambia huo ni mchango wangu kwako kaanzie maisha.”

Kuhusu “Pawa”

Diamond alisisitiza kwamba hakutaka kumnyang’anya Mbosso sifa, ila aliongeza nguvu kwenye chorus ya Pawa, jambo ambalo kwa mtazamo wake lilisaidia wimbo huo kufanikisha mafanikio makubwa.

📌 Hitimisho:
Sakata hili limeonesha jinsi migongano ya kimaslahi na mchango wa wasanii ndani ya lebo inaweza kuzua mjadala mkali. Hata hivyo, mashabiki sasa wanasubiri kuona k**a Diamond na Mbosso watafanikisha maridhiano au k**a huu ndio mwanzo wa mgawanyiko wa kudumu kati ya mastaa hawa wawili.

Diamond Platnumz vs Mbosso: Mgogoro Waibuka Kuhusu Wimbo “Pawa”Beef kubwa limezuka kati ya Diamond Platnumz na aliyekuwa...
18/08/2025

Diamond Platnumz vs Mbosso: Mgogoro Waibuka Kuhusu Wimbo “Pawa”

Beef kubwa limezuka kati ya Diamond Platnumz na aliyekuwa msanii wa lebo yake, Mbosso, baada ya rafiki wa karibu wa Diamond, Baba Levo, kudai hadharani kwamba Diamond anastahili kupewa asilimia 50 ya sifa za wimbo mkubwa wa Mbosso, Pawa. Baba Levo alienda mbali zaidi akisema: “Tupe melodi yetu.”

Mbosso Ajibu

Mbosso hakusita kujibu kwa hasira, akisisitiza kwamba Pawa ameandika mwenyewe kwa asilimia 100, na mchango wa Diamond ulikuwa mdogo sana. Aidha, alimlaumu Diamond kwa kutoshughulikia kauli za Baba Levo, huku akikanusha vikali kwamba Diamond ndiye aliyeandika wimbo huo.
Licha ya kueleza kwamba bado anamuheshimu Diamond, Mbosso alieleza hatakubali kipaji chake kudharauliwa kwa mtu mwingine kupewa sifa zisizo zake.

Diamond Ajitokeza

Diamond Platnumz alijibu kupitia mfululizo wa posti ndefu kwenye Instagram, akikanusha wivu au wazo la kupora sifa. Alisema hakutaka jambo hilo lifike mtandaoni kwani tayari alikuwa amempigia simu Mbosso na kumtumia ujumbe akimpa ushahidi:
“Sikutaka mitandao… nilikupigia simu na kukutumia messages… nilikuonyesha kwa ushahidi kuwa hakuna faida kwangu zaidi ya kunitia tu ubaya.”

Diamond aliongeza kuwa migongano ndani ya lebo ni jambo la kawaida, na si kila msanii akiondoka lazima aendelee na uhusiano mzuri:
“Msanii anapotoka kwenye lebo usitegemee wote watakua na reaction zinazofanana… wengine wanaweza wakawa wanareact vitu ambavyo sio vizuri.”

Alimkumbusha Mbosso kuwa hata yeye mwenyewe aliwahi kumzuia kushirikiana na Rayvanny, lakini Diamond hakumkataza, akithibitisha kwamba kushirikiana na wasanii wa nje ya Wasafi si usaliti.

Mashtaka na Utetezi

Kuhusu wivu, Diamond alihoji:
“Mie nikuonee wewe wivu kwa kitu gani haswa? Itanisaidia nini? Nitake sifa kupitia Pawa? Pawa imehit kuliko nyimbo ya Sele nchini? Je Sele uliandika pekeako?”

Diamond pia alidai kuwa yeye ndiye aliyechangia kwa kiwango kikubwa kwenye nyimbo nyingi za Mbosso:
“Takribani 90% ya nyimbo zako zote nimeandika… kuanzia asilimia 40%, 50%, zingine hadi asilimia 90% viitikio, verses, michezesho na kadharika.”

Zaidi ya muziki, Diamond alifichua msaada wa kifedha aliompatia Mbosso wakati akiwa Wasafi:
“Umetoka Wasafi licha ya sijakutoza hata shilingi mia… nilikua nakudai milioni 323,250,000/= ya kukukopesha toka mfukoni mwangu, na vyote nilikuachia nikakuambia huo ni mchango wangu kwako kaanzie maisha.”

Kuhusu “Pawa”

Diamond alisisitiza kwamba hakutaka kumnyang’anya Mbosso sifa, ila aliongeza nguvu kwenye chorus ya Pawa, jambo ambalo kwa mtazamo wake lilisaidia wimbo huo kufanikisha mafanikio makubwa.

📌 Hitimisho:
Sakata hili limeonesha jinsi migongano ya kimaslahi na mchango wa wasanii ndani ya lebo inaweza kuzua mjadala mkali. Hata hivyo, mashabiki sasa wanasubiri kuona k**a Diamond na Mbosso watafanikisha maridhiano au k**a huu ndio mwanzo wa mgawanyiko wa kudumu kati ya mastaa hawa wawili.

Adresse

Thika
Uvira
00100

Téléphone

+254774652712

Site Web

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque Banza Media publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Contacter L'entreprise

Envoyer un message Ă  Banza Media:

Partager