Banza Media "Burudani | Gossip | Lifestyle | Politics
📩 DM for Ads & Collabs
🎬 New content daily" Asante kwa sapoti yenyu
Bado kwa zidi kusonga mbele
(1)

wanaowania tuzo za mwaka 2026, zitakazotolewa Februari 1, 2026 nchini Marekani 🇺🇸.Miongoni mwa waliotajwa ni Eddy Kenzo ...
08/11/2025

wanaowania tuzo za mwaka 2026, zitakazotolewa Februari 1, 2026 nchini Marekani 🇺🇸.

Miongoni mwa waliotajwa ni Eddy Kenzo kutoka Uganda, ambaye aliweka historia mwaka 2022 k**a msanii wa kwanza kutoka nchini humo kupata Grammy nomination. Safari hii ameibuka tena kwa mara ya pili mfululizo, akishindania kipengele cha Best African Performance pamoja na majina makubwa ya muziki barani Afrika.

Wanaowania kipengele cha Best African Performance ni:
🎵 Burna Boy 🇳🇬 – LoVe
🎵 Eddy Kenzo 🇺🇬 & Mehran Martin – Hope & Love
🎵 Ayra Starr & Wizkid 🇳🇬 – Gimme Dat
🎵 Tyla 🇿🇦 – Push To Start
🎵 Davido & Omah Lay 🇳🇬 – With You

Swali ambalo wengi wamejiuliza ni kwa nini wasanii kutoka Tanzania 🇹🇿 hawajafanikiwa kuingia kwenye orodha hii mwaka huu?

Je, ni ukosefu wa international strategy, usimamizi hafifu wa kazi, au muziki wetu bado haujapata msukumo wa kimataifa unaohitajika kufikia viwango vya Grammy?

🗣️ Tuambie maoni yako — unadhani nini kimekwamisha wasanii wa Tanzania kufika hatua hii?

Mfanyabiashara Jennifer Jovin, maarufu k**a Niffer, amefikishwa katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Sa...
07/11/2025

Mfanyabiashara Jennifer Jovin, maarufu k**a Niffer, amefikishwa katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, leo Novemba 7, 2025.

Hii inakuja wiki moja baada ya Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kuthibitisha kuwa lilikuwa likimshikilia Niffer kwa tuhuma za kuhamasisha wananchi kufanya fujo siku ya kupiga kura.

Msanii wa k**e Wa kizazi kipya pipijojo ameachia video Yake ya Kwanza ya Wimbo CHAKACHA Baada ya Wimbo huo kufanya vizur...
07/11/2025

Msanii wa k**e Wa kizazi kipya pipijojo ameachia video Yake ya Kwanza ya Wimbo CHAKACHA
Baada ya Wimbo huo kufanya vizuri inje na Ndani ya tanzania

Mtangazaji wa kituo cha kimataifa cha CNN, Larry Madowo ambaye ni raia wa Kenya, amewaomba Watanzania waliokuwa na bahat...
07/11/2025

Mtangazaji wa kituo cha kimataifa cha CNN, Larry Madowo ambaye ni raia wa Kenya, amewaomba Watanzania waliokuwa na bahati ya kurekodi video za matukio ya vurugu zilizotokea nchini Tanzania kati ya Oktoba 29 hadi 31, kuzishiriki ili ulimwengu uweze kuona hali halisi ya machafuko hayo.

Madowo amesema hatua hiyo inalenga kusaidia jamii ya kimataifa kufahamu ukweli wa yaliyojiri nchini humo, hasa baada ya vyombo vingi vya habari vya ndani kushindwa kuripoti kwa uhuru kutokana na hofu na vikwazo vya kisheria.

07/11/2025

Mama wa mfanyabiashara maarufu Niffer ameonekana kwenye video akimuombea msamaha mtoto wake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kupitia video hiyo ambayo imeenea mtandaoni, mama huyo amejitokeza kwa hisia kubwa, akiomba Rais Samia amsamehe Niffer kutokana na matamshi au matendo yake yaliyosababisha sintofahamu katika siku za hivi karibuni.

Tukio hilo limezua maoni mseto mtandaoni, huku baadhi ya watumiaji wakisifu hatua ya mama huyo k**a ya hekima na upendo wa mzazi.

Msanii wa Muziki Nchini alikiba aomba msamaha Kwa mashabiki Zake Walio kwazika na Kitendo cha yeye Ku- support CCM
06/11/2025

Msanii wa Muziki Nchini alikiba aomba msamaha Kwa mashabiki Zake Walio kwazika na Kitendo cha yeye Ku- support CCM

UJUMBE WANGU KWA TAIFASalaam.Kwanza, nitoe pole za dhati kwa wote waliofikwa na misiba, majeraha au hasara kutokana na v...
06/11/2025


UJUMBE WANGU KWA TAIFA

Salaam.

Kwanza, nitoe pole za dhati kwa wote waliofikwa na misiba, majeraha au hasara kutokana na vurugu zilizotokea. Kurudishiana maumivu si utu, wala si msingi wa taifa letu. Tofauti za kisiasa hazitufanyi tuache kuwa jamii moja kwani kabla ya itikadi, sisi ni binadamu na ni Watanzania.

Mimi ni mhanga wa fujo hizo, Na Ofisi yangu imechomwa na mali zangu zimeteketea. Wapo wanaoonekana kufurahia, wakidai “nilistahili” kwa sababu ya msimamo wangu wa kisiasa. Lakini ukweli ni huu: sijawahi kumtukana mtu, sijawahi kumdhuru mtu nimekuwa tu muumini wa siasa ninayoiamini kupitia Chama Changu CCM.

Lakini je, wale wasio na chama walioumizwa je? Nani anawatetea? Hili linaonesha wazi kuwa fujo hazitofautishi bali ni uharibifu usio na mantiki.

Kwa hivyo wakati huu si muda wa kutafutana mchawi, wala kushindana kutupiana lawama. Ni wakati wa busara.

Nawabariki na kuwasamehe wote waliohusika katika uharibifu wa biashara yangu huku wakiwa wamedhamiria kunirudisha nyuma.
Muhimu ni kwamba Mwenyenzi Mungu ameendelea kuniruzuku UHAI basi ninaamini MALI zinaweza kurejeshwa kwa juhudi na kupambana pasipo KUKATA TAMAA lakini pumzi ya uhai haina mbadala. Alhamdulillah!!

Naiombea nchi yangu. Namuombea Rais wangu, Mama Samia, pamoja na Serikali yake katika kuendeleza Awamu ya Sita katika kipindi chake cha pili. Kwani ninamani kuwa huu ni wakati wa kuimarisha Umoja na Upendo kwa taifa letu ni muhimu sana tukawaunga mkono Viongozi wetu.

Na mimi sitarudi nyuma katu, Nitaendelea kuamini, kutetea na kusimama na imani safi ya chama changu CCM, licha ya majaribu, vitisho na hasara niliyopata.

Ninashauri tusimamie katika nguzo ya hekima, maridhiano, uvumilivu na utatuzi wa hoja bila fujo.

Kwa walionijulia hali baada ya Kuzushiwa Kifo: Poleni kwa namna mlivyojisikia baada ya habari zile. Asanteni kwa kujali. Mali zilizopotea ni hasara kubwa sana na nimeumia, ila haziwezi kuwa na thamani kuliko uzima huu Mungu alionipa, Alhamdullilah.

Tuchague Amani.
Tuchague Umoja.
Tuchague Busara.

Mungu Ibariki Tanzania 🇹🇿

05/11/2025

Msanii marioo inje na mzuki Naha huwezo Wa kunyowa na kutengeneza Gari Kwa kipindi cha vurugu Nchini Tanzania alifanya kazi ya kumunyowa boss wake abbah

Siku mbili baada ya huduma ya intaneti kurejeshwa nchini Tanzania, wananchi wameanzisha kampeni ya mass-unfollowing dhid...
05/11/2025

Siku mbili baada ya huduma ya intaneti kurejeshwa nchini Tanzania, wananchi wameanzisha kampeni ya mass-unfollowing dhidi ya wasanii waliomuunga mkono Rais Samia Suluhu katika kampeni na uchaguzi mkuu.

Miongoni mwa wasanii waliokumbwa na hatua hiyo ni Diamond Platnumz, ambaye amepoteza zaidi ya wafuasi 100,000 ndani ya saa 12 pekee. Pia, Harmonize ni miongoni mwa waliolengwa na wananchi mitandaoni.

Watanzania wanawatuhumu wasanii hao kutumia ushawishi wao kuunga mkono kile kinachoitwa utawala wa kidikteta unaoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Maneno ya kuwatia nguvu Wa Tanzania kutoka Kwa Msanii diamond platnumz baada ya vurugu zilizo tokea Nchini Tanzania Kwa ...
04/11/2025

Maneno ya kuwatia nguvu Wa Tanzania kutoka Kwa Msanii diamond platnumz baada ya vurugu zilizo tokea Nchini Tanzania Kwa siku Tatu zilizo pita

Adresse

Thika
Uvira
00100

Téléphone

+254774652712

Site Web

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque Banza Media publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Contacter L'entreprise

Envoyer un message à Banza Media:

Partager