DW Kiswahili

DW Kiswahili Tunakuletea yaliyomuhimu. Unatupa fikra yako: Jadiliana nasi habari kutoka Afrika na ulimwengu mzima.

Hujambo na karibu tena kweye vipindi vyetu vya DW Noa Bongo Jenga Maisha Yako katika mchezo unaoangazia Elimu ya Kidijit...
03/01/2026

Hujambo na karibu tena kweye vipindi vyetu vya DW Noa Bongo Jenga Maisha Yako katika mchezo unaoangazia Elimu ya Kidijitali. Ni kipindi cha Pili kwenye mfululizo wa mchezo wetu wa redio unaoitwa Suluhisho la Kidijitali. Hadithi hii inaelezea umuhimu wa kukuza elimu na ujuzi wa kidijitali unaohitajika kukabiliana na changamoto za kidijitali. Katika kipindi kilichotangulia, tulikutana na Faith, mwalimu wa shule ya Inzuna ambaye anaishi na binamu zake Rahim, na Jennifer. Rahim ametawaliwa na teknolojia ya habari na hutumia muda mwingi kwenye kompyuta yake. Jennifer hutegemea kipato chake kutokana na ubunifu wa ushawishi katika mitandao ya kijamii. Shule ya Inzuna, ambako Faith anafanya kazi, inashiriki katika shindano la ubunifu wa kidijitali baina ya shule chini ya maudhui Teknolojia ya Kidijitali katika sekta ya elimu.
Walimu wengi walishangaa kuona kuwa Faith ndiye aliyeteuliwa kuwa mratibu na kuwaongoza wanafunzi katika mradi huo wa shule kwenye shindano hilo, badala ya rafiki yake Nina. Licha ya kufurahia uteuzi huo, je, Faith anafahamu changamoto zake? Pia katika kipindi kilichopita, mama yake Jennifer aliwatembelea nyumbani kwao bila ya kutoa taarifa. Je ziara hii ya ghafla ilikuwa na ujumbe gani? Hebu tusikie yanayojiri katika kipindi hiki cha leo kwa jina Uvumbuzi. Tuskimalizie uhondo, jiunge nasi na utuandikie maoni yako!

03/01/2026

Huenda ukawa umeshasikia au unafahamu kwamba dhahabu ni kinga dhidi ya mfumuko wa bei katika taifa lenye utajiri wa aina hiyo ya madini.
Hapa mchimbaji mdogo wa madini, Ashraf aneleza namna kauli hii inavofanya kazi.

Rais wa Marekani Donald Trump ameandika kwenye mtandao wake wa Truth Social kwamba Rais wa Venezuela Nicolas Maduro na m...
03/01/2026

Rais wa Marekani Donald Trump ameandika kwenye mtandao wake wa Truth Social kwamba Rais wa Venezuela Nicolas Maduro na mkewe wamek**atwa na kusafirishwa nje ya taifa hilo.

Usiku wa kuamkia Jumamosi jiji la Caracas lilitikiswa na milipuko, ikiambatana na kelele za helikopta. Trump amesema operesheni hii imefanyika kwa kuzingatia utekelezaji wa Sheria za Marekani.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Christopher Landau, amesema Venezuela imepata "mapambazuko mapya" na mtawala wa kiimla hayupo tena na kwamba hatimaye atakabiliwa na mkono wa sheria kutokana na makosa yake.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi imelaani kitendo cha Marekani cha uchokozi wa kutumia silaha dhidi ya Venezuela .

03/01/2026

Yaliyomo kwenye DW Kiswahili Habari za Ulimwengu | Podcast | Leo Mchana | Januari 03, 2026 | Swahili Habari:

Milipuko yasikika katika mji mkuu wa Venezuela

Ukraine kufanya mkutano na washauri wa usalama mjini Kiev

Na Polisi Iran yaonya kuhusu maandamano ya kutumia silaha

Ukitaka kupata habari zetu kila siku, bonyeza 'follow' kwenye chaneli yetu ya DW Kiswahili.

Ukraine leo itakuwa mwenyeji wa mazungumzo mafupi ya washauri wa masuala ya kiusalama kutoka nchi kadhaa wakati nchi hiy...
03/01/2026

Ukraine leo itakuwa mwenyeji wa mazungumzo mafupi ya washauri wa masuala ya kiusalama kutoka nchi kadhaa wakati nchi hiyo ikisisitiza kuwa mazungumzo ya amani yanaelekea kufikia makubaliano.

Wengine watakaohudhuria mkutano huo ni wawakilishi wa Umoja wa Ulaya na Jumuiya ya Kujihami NATO, huku wajumbe wa Marekani wakijiunga kwa njia ya video.

Mazungumzo ya leo yanafanyika baada ya Zelensky awali kutangaza kwamba mpango ulioidhinishwa na Marekani uko tayari kwa "asilimia 90", lakini akaonya kuwa masuala muhimu ya kimaeneo bado yamekwama.

Wanamgambo wa kundi la ADF, wanaohusishwa na kundi linalojiita Dola la Kiislamu IS,  walishambulia ndani ya eneo la kilo...
03/01/2026

Wanamgambo wa kundi la ADF, wanaohusishwa na kundi linalojiita Dola la Kiislamu IS, walishambulia ndani ya eneo la kilomita saba kaskazini magharibi mwa jimbo la Kivu Kaskazini.

Watu 15 waliuawa na nyumba 13 kuchomwa moto. Jeshi la Kongo limesema askari wake wawili pia wameuawa.

Kwa mujibu wa kiongozi mmoja wa eneo hilo Macaire Sivikunula, mashambulizi hayo yalisababisha wanakijiji kuingiwa na hofu huku milio ya risasi ikisikika kati ya saa mbili usiku hadi saa kumi alfajiri.

Mashuhuda wameripoti kuona moshi ukifuka kutoka kwenye vituo vya kijeshi. Serikali ya Venezuela imeishutumu moja kwa moj...
03/01/2026

Mashuhuda wameripoti kuona moshi ukifuka kutoka kwenye vituo vya kijeshi. Serikali ya Venezuela imeishutumu moja kwa moja Marekani kwa kushambulia vituo vyake vya kiraia na kijeshi.

Lakini hadi sasa wizara ya ulinzi ya Marekani Pentagon pamoja na Ikulu ya White House hazijatoa kauli kuhusu tukio hilo.

Venezuela tayari imetangaza hali ya dharura kufuatia matukio hayo.

02/01/2026

Mwigizaji wa maarufu wa Marekani Angelina Jolie ametembelea upande wa Misri wa kivuko cha mpaka cha Rafah kuelekea Ukanda wa Gaza. Alitembelea Shirika la Msalaba Mwekundu la Misri ili kupata muhtasari wa juhudi za misaada zinazoendelea kwa eneo la pwani lililofungwa, kwa mujibu wa vyanzo ndani ya shirika hilo siku ya Ijumaa. Jolie alipokelewa na gavana wa eneo hilo, ambaye alimfuatilia katika ziara yake. Vyombo vya habari vimeripoti kuwa mwakilishi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani pia alikuwepo. Baadaye, Jolie aliripotiwa kusaidia kupakia vifaa vya misaada kwa Gaza k**a ishara ya mshik**ano, na alieleza shukrani zake kwa juhudi za Misri. Pia alisifu jukumu muhimu linalofanywa na wanaojitolea, wafanyakazi katika usambazaji wa misaada kwa ufanisi licha ya changamoto nyingi. Jioni, alitarajiwa kutembelea hospitali katika mji wa karibu wa al-Arish. Kwa mujibu wa vyanzo vya Misri, anapanga kukutana na Wapalestina waliojeruhiwa kutoka Ukanda wa Gaza. Jolie alikuwa mjumbe maalum wa Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) kwa miaka mingi. Leo, anaendelea kutembelea maeneo yenye migogoro na misukosuko duniani ili kuvutia umakini wa umma kutokana na mateso ya raia. Rafah ndicho kivuko pekee cha mpaka katika Ukanda wa Gaza ambacho hakielekei moja kwa moja Israel. Kivuko hicho kilifungwa wakati wa vita vya Gaza. Mashirika ya misaada yamekuwa yakitoa wito kwa muda mrefu wa kivuko hicho kifunguliwe.

02/01/2026

Raia wa Sudan wanasubiri kwa shauku kubwa pambano la timu yao ya taifa dhidi ya miamba wa soka barani Afrika, Senegal, katika mechi ya raundi ya 16 bora ya AFCON 2025. Licha ya taifa hilo kukumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe, Sudan imeendelea kubeba matumaini ya mashabiki wake kupitia matokeo chanya katika mashindano hayo. Swali linalojitokeza sasa ni iwapo hali inayoendelea mjini Khartoum itawapa motisha ya ziada nyota wa Sudan kupata ushindi dhidi ya Simba wa Teranga. Msikilize na kumtazama kocha wa Sudan, Kwesi Appiah na kisha Winga wa Kushoto wa Sudan, Bakhit Khamis. Lakini na wewe tupe mtazamo wako kwa mchezo huo.

Polisi ya Nigeria imemfungulia mashtaka manne dereva wa gari lililohusika kwenye ajali iliyomjeruhi bingwa wa zamani wa ...
02/01/2026

Polisi ya Nigeria imemfungulia mashtaka manne dereva wa gari lililohusika kwenye ajali iliyomjeruhi bingwa wa zamani wa uzito wa juu duniani kutoka Uingereza, Anthony Joshua, na kuua marafiki zake wawili wa karibu. Adeniyi Mobolaji Kayode, mwenye umri wa miaka 46, alifikishwa mbele ya Mahak**a ya Hakimu ya Sagamu siku ya Ijumaa kuhusiana na ajali hiyo iliyotokea kwenye barabara ya Lagos-Ibadan Expressway, kwa mujibu wa taarifa ya Kamandi ya Polisi ya Jimbo la Ogun. Polisi waliiambia Reuters kuwa Kayode ameshtakiwa kwa makosa manne, ikiwemo kusababisha kifo kwa kuendesha gari kwa uzembe. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Januari 20. Reuters haikuweza kumpata Kayode au wakili wake mara moja. Kayode hajatoa maoni hadharani kuhusu kesi hiyo. Joshua, mwenye umri wa miaka 36, alipata majeraha madogo wakati gari la kifahari aina ya Lexus SUV alilokuwa akisafiria lilipogongana na gari jingine siku ya Jumatatu. Marafiki zake wawili Sina Ghami na Latif Ayodele, walikufa katika ajali hiyo.

  Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt Mwigulu Nchemba amesema serikali kuahirisha safari za usafiri wa treni za mwendokasi za SG...
02/01/2026

Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt Mwigulu Nchemba amesema serikali kuahirisha safari za usafiri wa treni za mwendokasi za SGR ni kulinda usalama wa raia pale hitilafu za hali za hewa zikijitokeza.

Mwigulu ameyasema hayo wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa Bwawa la Maji la Kidunda lililopo Mkoa wa Morogoro nchini Tanzania na amesisitiza kuwa hali hio ni ya kawaida hata kwa nchi zilizoendelea.

02/01/2026

Mikanda ya usalama kwenye magari huokoa maisha lakini mamilioni bado hawajifungi. Kwa nini watu wanahatarisha maisha, hata kwa safari fupi?

Adresse

Bonn
53113

Webseite

https://tinyurl.com/2bvkbetv

Benachrichtigungen

Lassen Sie sich von uns eine E-Mail senden und seien Sie der erste der Neuigkeiten und Aktionen von DW Kiswahili erfährt. Ihre E-Mail-Adresse wird nicht für andere Zwecke verwendet und Sie können sich jederzeit abmelden.

Service Kontaktieren

Nachricht an DW Kiswahili senden:

Teilen