08/10/2025
: Chama kikuu cha upinzani visiwani Zanzibar cha ACT-Wazalendo kimezundua ilani yake ya uchaguzi mahsusi kwa visiwa hivyo kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025. Kwenye uzinduzi huo, chama hicho kupitia mgombea wake wa kiti cha urais Othman Masoud Othman kimesema ilani yake imejikita kwenye misingi mikuu minne ya uchumi, mamlaka kamili, upatikanaji wa haki na masuala ya kijamii, huku suala la haki za Zanzibar kwenye Muungano likipewa umuhimu wa pekee. Ikiwa ni mpiga kura huko visiwani Zanzibar, kipaumbele kipi kimekuvutia zaidi?