28/11/2025
Umoja wa Afrika umesimamisha uwanachama wa Guinea-Bissau kufuatia mapinduzi ya wiki hii katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi. Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Afrika Mahamoud Ali Youssouf amesema Guinea Bissau imeondolewa mara moja kwenye vyombo vyake vikuu vya maamuzi. Hatua hiyo imejiri baada ya Jumuiya ya Kiuchumi ya Magharibi mwa Afrika, ECOWAS pia kusimamisha nchi hiyo.