DW Kiswahili

DW Kiswahili Tunakuletea yaliyomuhimu. Unatupa fikra yako: Jadiliana nasi habari kutoka Afrika na ulimwengu mzima.

Katika kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi mkuu visiwani Zanzibar, gharama kubwa za maisha zimekuwa moja ya mada kuu zi...
09/10/2025

Katika kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi mkuu visiwani Zanzibar, gharama kubwa za maisha zimekuwa moja ya mada kuu zinazojadiliwa na wananchi wanapokutana na wagombea wa urais, wakieleza matumaini yao kwa viongozi watakaopunguza mzigo wa maisha.

09/10/2025

Wanamgambo wa Hamas kuwaachilia mateka wa Israel wanaoshikiliwa huko Gaza huku Israel ikitarajiwa kuwaachilia huru takriban wafungwa 2,000 wa Kipalestina.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron atamteua waziri mkuu mpya katika kipindi cha saa 48 zijazo. Hayo yamesemwa na ofisi yak...
09/10/2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron atamteua waziri mkuu mpya katika kipindi cha saa 48 zijazo. Hayo yamesemwa na ofisi yake jana Jumatano, baada ya kujiuzulu kwa waziri mkuu anayeondoka Sebastien Lecornu kuashiria nchi hiyo kuingia katika mzozo wa kisiasa.
Lecornu aliiambia TV ya Ufaransa katika mahojiano mapema kwamba alitarajia waziri mkuu mpya kutajwa badala ya uchaguzi wa mapema wa wabunge kuitishwa au Macron kujiuzulu katika jitihada za kuutatua mgogoro huo.

Mnamo Jumatatu wiki hii Macron alimpa Lecornu hadi Jumatano jioni kutafuta njia ya kutoka kwa kipindi kigumu cha miezi kadhaa ya msuguano juu ya bajeti ya kubana matumizi.
Lecornu alijiuzulu mapema Jumatatu baada ya kuwa madarakani kwa chini ya mwezi mmoja.

Rais wa Marekani Donald Trump amesema Israel na Hamas wametia saini awamu ya kwanza ya mpango wa amani ya Gaza.Kundi la ...
09/10/2025

Rais wa Marekani Donald Trump amesema Israel na Hamas wametia saini awamu ya kwanza ya mpango wa amani ya Gaza.

Kundi la Hamas linatarajiwa kuwaachilia huru mateka 'hivi karibuni' likisema mateka wa Israel walio hai watabadilishwa kwa karibu wafungwa 2,000 wa kipalestina.

Trump alisema Jumatano kwamba anaamini mateka wote walioshikiliwa huko Gaza, ikiwa ni pamoja na miili ya marehemu, "watarudi" Jumatatu.

Israel nayo itawaondoa wanajeshi wake kwa njia iliyokubaliwa. Msemaji wa serikali ya Israel ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba Israel inatarajia mateka wake wataanza kuachiwa Jumamosi.

Msemaji huyo hakusema iwapo serikali inatarajia mateka wote 48 waliosalia, wanaoishi na waliokufa, wataachiliwa wote mara moja.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu atakutana na baraza lake la mawaziri leo Alhamisi ili kuidhinisha mpango wa kuachiliwa kwa mateka wanaoshikiliwa huko Gaza.

09/10/2025

Yaliyomo kwenye DW Kiswahili Habari za Ulimwengu | Podcast | Leo Asubuhi | Oktoba 09, 2025 | Swahili Habari:
- Trump asema Isreal na Hamas wamesaini awamu ya kwanza ya mkataba wa amani.
- Macron kumtaja waziri mkuu mpya wa Ufaransa.
Ukitaka kupata habari zetu kila siku, bonyeza 'subscribe' kwenye chaneli yetu ya DW Kiswahili.

Ripoti mpya iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Uhasibu nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imeonesha makampuni ya kuchi...
08/10/2025

Ripoti mpya iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Uhasibu nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imeonesha makampuni ya kuchimba madini ambayo mengi ni ya kigeni hayakutoa hesabu kamili ya mapato ya kila mwaka kwa karibu miaka mitano.

Ripoti hiyo imesema, ufichuzi huo umedhihirisha matendo yanayokiuka sheria yanayofanywa na makampuni yanayochimba utajiri huo wa Kongo. Zaidi ya dola bilioni 16.8 za mapato hazikuripotiwa kwenye ukaguzi wa hesabu kati ya mwaka 2018 hadi 2023 , mwenendo ulioinyima serikali mapato na hata jamii zinazozunguka migodi.

Chini ya kanuni za uchimbaji madini za Kongo za mwaka 2018, mbali ya kulipa kodi, makampuni ya madini yanapaswa kuchangia asilimia 0.3 ya mapato ya mwaka kwa ajili ya maendeleo ya jamii katika maeneo migodi iliko. Fedha hizo hutumika kugharamia miradi ya elimu, afya na maji.

Taswira ya hisia mseto kabla na baada ya kudaiwa kutekwa na watu wasiojulikana kwa Humphrey Polepole nchini Tanzania. Mt...
08/10/2025

Taswira ya hisia mseto kabla na baada ya kudaiwa kutekwa na watu wasiojulikana kwa Humphrey Polepole nchini Tanzania. Mtizamo huo ni kutoka kwa mchora vibonzo wetu Said Michael 'Wakudata' . Nawe unasemaje, unakubaliana nao?

08/10/2025

Unaujua msemo wa waswahili wa "kuponea chupuchupu"? Basi hicho ndio kimetokea kwa Chui dume mmoja huko Brazil alijeruhiwa kwa risasi na huenda angekufa k**a asingepata msaada. Umemwona lakini Chui alivyokuwa mtulivu akifahamu kwamba anaokolewa?

08/10/2025

Kwa baridi hiyo ungestahamili kwa muda gani kabla hujaanza kutoa wosia? 🥶🥶🥶

 : Chama kikuu cha upinzani visiwani Zanzibar cha ACT-Wazalendo kimezundua ilani yake ya uchaguzi mahsusi kwa visiwa hiv...
08/10/2025

: Chama kikuu cha upinzani visiwani Zanzibar cha ACT-Wazalendo kimezundua ilani yake ya uchaguzi mahsusi kwa visiwa hivyo kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025. Kwenye uzinduzi huo, chama hicho kupitia mgombea wake wa kiti cha urais Othman Masoud Othman kimesema ilani yake imejikita kwenye misingi mikuu minne ya uchumi, mamlaka kamili, upatikanaji wa haki na masuala ya kijamii, huku suala la haki za Zanzibar kwenye Muungano likipewa umuhimu wa pekee. Ikiwa ni mpiga kura huko visiwani Zanzibar, kipaumbele kipi kimekuvutia zaidi?

08/10/2025

Tumaini letu umekuwa na mchana mwema haya ni miongoni mwa utakayoyasikia katika Dunia Yetu Leo Jioni:-

- Misri yasema lipo tumaini katika mazungumzo ya kusitisha mapigani Ukanda wa Gaza

- Chama Kikuu cha upinzani Zanzibar ACT-Wazalendo chazindua ilani yake katikati mwa kampeni za uchaguzi mkuu wa Tanzania.

  : Serikali ya Ethiopia imeituhumu nchi jirani ya Eritrea kwamba inajipanga kuanzisha vita. Waziri wa Mambo ya Kigeni w...
08/10/2025

: Serikali ya Ethiopia imeituhumu nchi jirani ya Eritrea kwamba inajipanga kuanzisha vita. Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Ethiopia amemwandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kumfahamisha kwamba Eritrea hivi sasa inashirikiana na kundi la waasi wa TPLF walio na nguvu katika jimbo la Ethiopia la Tigray kwa lengo la kuanzisha vita. Mahusiano kati ya nchi hizo mbili jirani yamekuwa mabaya tangu Eritrea ilipojipatia uhuru kutoka Ethiopia mwaka 1993. Ziliwahi kupigana vita mwaka 1998 hadi 2000. Chanzo cha msuguano wa sasa ni ugomvi kuhusu eneo la bandari na madai ya kila upande kuwa na malengo ya kuhujumu usalama wa mwingine

Adresse

Bonn
53113

Webseite

https://tinyurl.com/2bvkbetv

Benachrichtigungen

Lassen Sie sich von uns eine E-Mail senden und seien Sie der erste der Neuigkeiten und Aktionen von DW Kiswahili erfährt. Ihre E-Mail-Adresse wird nicht für andere Zwecke verwendet und Sie können sich jederzeit abmelden.

Service Kontaktieren

Nachricht an DW Kiswahili senden:

Teilen