DW Kiswahili

DW Kiswahili Tunakuletea yaliyomuhimu. Unatupa fikra yako: Jadiliana nasi habari kutoka Afrika na ulimwengu mzima.

Umoja wa Afrika umesimamisha uwanachama wa Guinea-Bissau kufuatia mapinduzi ya wiki hii katika nchi hiyo ya Afrika Magha...
28/11/2025

Umoja wa Afrika umesimamisha uwanachama wa Guinea-Bissau kufuatia mapinduzi ya wiki hii katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi. Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Afrika Mahamoud Ali Youssouf amesema Guinea Bissau imeondolewa mara moja kwenye vyombo vyake vikuu vya maamuzi. Hatua hiyo imejiri baada ya Jumuiya ya Kiuchumi ya Magharibi mwa Afrika, ECOWAS pia kusimamisha nchi hiyo.

Tanzania imepuuzilia mbali azimio la Bunge la Ulaya linalotaka nchi hiyo isipewe ufadhili kutoka Umoja wa Ulaya kufuatia...
28/11/2025

Tanzania imepuuzilia mbali azimio la Bunge la Ulaya linalotaka nchi hiyo isipewe ufadhili kutoka Umoja wa Ulaya kufuatia madhila ya uchaguzi Mkuu. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mahmoud Thabit Kombo amesema Watanzania hawatakufa kutokana na njaa wala kusimama kwa shughuli za maendeleo kutokana na hatua hiyo ya EU kwani Tanzania ina vyanzo luluki vya mapato. Kauli ya Waziri Kombo ameitoa wakati Umoja wa Ulaya ukiwa umepanga kuipa Tanzania zaidi ya uero milioni 150 sawa na Tsh 400 bilioni, fedha za miradi ya maendeleo kwa Tanzania katika kipindi cha mwaka 2026.

K**a una mpango wa kwenda Marekani kwa sasa, itabidi utafakari upya. Rais Donald Trump amesema "atasitisha kabisa uhamia...
28/11/2025

K**a una mpango wa kwenda Marekani kwa sasa, itabidi utafakari upya.

Rais Donald Trump amesema "atasitisha kabisa uhamiaji" wa watu kwenda Marekani kutoka "nchi zote maskini na zinazoendelea duniani". Rais huyo wa Marekani hajatoa maelezo ya mpango wake huo au kutaja ni nchi zipi zinaweza kuathiriwa. Hii inajiri siku moja baada ya raia wa Afghanistan kutuhumiwa kwa kuwapiga risasi wanajeshi wawili wa Kikosi cha Walinzi wa Taifa huko Washington DC, na kumuuwa mmoja wao.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, nchini Tanzania Ridhiwani Kikwete ameagi...
28/11/2025

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, nchini Tanzania Ridhiwani Kikwete ameagiza kuwa Viongozi wote wanaolalamikiwa na Wananchi waitwe wahojiwe ikiwemo yeye mwenywe juu ya tuhuma zinazowakabili. Ridhiwani amesisitiza kuwa ni vyema taarifa za Watumishi wa Umma zikawa wazi na Viongozi wenye tuhuma wahojiwe na amesema hata yeye aitwe ahojiwe juu ya tuhuma za umiliki wa kituo cha mafuta cha Lake Oil ili ukweli ujulikane. Ameongeza kuwa wenye ushahidi wajitokeze kuuweka wazi ili kuisaidia serikali.

28/11/2025

: Sikiliza Dunia Yetu Leo Jioni Novemba 28, 2025 kutoka Idhaa ya Kiswahili ya DW, Bonn. Haya ni miongoni mwa tuliyokuandlia:

- Waziri Mkuu wa Senegal Ousmane Sonko asema mapinduzi ya Guinea Bissau sio halali

- Ulaya na Afrika wajadili usalama na malighafi ili kukabili ushawishi wa China

- Wauguzi katika eneo la Uvira jimbo la Kivu Kusini wagoma wakidai malipo na utambuzi wa serikali

/Ukitaka kupata habari zetu kila siku, bonyeza 'subscribe' kwenye chaneli yetu ya DW Kiswahili.

28/11/2025

Mahak**a Kuu ya Tanzania imetupilia mbali shauri la maombi ya kuidharau Mahak**a lililokuwa linawakabili Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, John Heche, Katibu Mkuu John Mnyika na wenzao. Ni kuhusu madai ya kukiuka amri yake ya kukizuia chama hicho kufanya shughuli za kisiasa na kutumia mali za chama hicho hadi hapo kesi ya mgogoro wa mgawanyo wa rasilimali baina ya Chadema Bara na Chadema Zanzibar itakapoamuliwa.

  Utupaji takataka ovyo ni tatizo ambalo limeshuhudiwa kwenye maeneo mengi ulimwenguni na kuchochea changamoto ya uharib...
28/11/2025

Utupaji takataka ovyo ni tatizo ambalo limeshuhudiwa kwenye maeneo mengi ulimwenguni na kuchochea changamoto ya uharibifu wa mazingira, madhara kwa wanyama huku wakati mwengine kusababisha. Ni kwa nini jamii inaendeleza suala la utupaji taka ovyo?

Wizara ya afya nchini Uganda imethibitisha vifo vya watoto kumi na moja kutokana na ugonjwa wa surua au Ukambi. Vifo hiv...
28/11/2025

Wizara ya afya nchini Uganda imethibitisha vifo vya watoto kumi na moja kutokana na ugonjwa wa surua au Ukambi. Vifo hivi vimetokea kwenye kanda ya Karamoja ambako mlipuko wa ugonjwa huo ulioripotiwa tarehe 19 mwezi huu. Tangu wakati huo visa 74 vimeripotiwa katika eneo hilo.

Kenya imeorodheshwa k**a soko lenye vikwazo vingi zaidi miongoni mwa nchi zinazolinganishwa na nchi hiyo, huku biashara ...
28/11/2025

Kenya imeorodheshwa k**a soko lenye vikwazo vingi zaidi miongoni mwa nchi zinazolinganishwa na nchi hiyo, huku biashara zikizidi kufunga milango kutokana na mazingira magumu. Ripoti ya hivi karibuni ya Benki ya Dunia inaonyesha kuwa sera za kibiashara zisizofaa na wingi wa mashirika ya umma yenye ushawishi mkubwa yanakandamiza ushindani na fursa za ajira.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema wajumbe wa nchi yake na wale wa Marekani watakutana wiki hii ili kujadili kwa...
28/11/2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema wajumbe wa nchi yake na wale wa Marekani watakutana wiki hii ili kujadili kwa kina mpango wa kusitisha mapigano na Urusi uliopendekezwa na rais wa Marekani Donald Trump.

28/11/2025

Rais wa Guinea-Bissau aliyepinduliwa madarakani Umaro Sissoco Embaló amekimbilia katika nchi jirani ya Senegal, baada ya jeshi kumuapisha hapo jana Jenerali Horta Nta Na Man k**a rais wa mpito atakaeshikilia wadhifa huo kwa kipindi cha mwaka mmoja.

28/11/2025

Bunge la Ulaya limelaani vikali hapo jana ukandamizaji ulioshuhudiwa baada ya uchaguzi nchini Tanzania. Katika kikao maalum, wabunge wa Ulaya wamekosoa matumizi ya nguvu kubwa iliyofanywa na mamlaka za Tanzania.

Adresse

Bonn
53113

Webseite

https://tinyurl.com/2bvkbetv

Benachrichtigungen

Lassen Sie sich von uns eine E-Mail senden und seien Sie der erste der Neuigkeiten und Aktionen von DW Kiswahili erfährt. Ihre E-Mail-Adresse wird nicht für andere Zwecke verwendet und Sie können sich jederzeit abmelden.

Service Kontaktieren

Nachricht an DW Kiswahili senden:

Teilen