21/08/2026
TUNDU LISSU ANAENDELEA
Na nilitumikia nafasi hiyo hadi tarehe 29 Juni 2019.
Ilikuwaje nikatumikia kabla ya kipindi kuisha?
Narudi kwenye tarehe 7 Septemba 2017, ambapo nikiwa Dodoma kwenye vikao vya Bunge, nilifuatwa kutoka Bungeni mpaka kwenye makazi yangu rasmi na kushambuliwa kwa risasi, risasi nyingi sana, na watu ambao Serikali ya Tanzania inawaita watu wasiojulikana.
Kufuatia shambulio hilo, nilikimbizwa Hospitali ya Dodoma na siku hiyo hiyo nikasafirishwa Nairobi, Kenya, ambako nilikaa hospitalini mpaka tarehe 4 Januari 2018.
Baada ya hapo nilipelekwa Ubelgiji kwa matibabu zaidi katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven.
Nilikuwa nikihudhuria matibabu mpaka Januari 2022. Kati ya Nairobi na Ubelgiji nilifanyiwa operesheni 25; operesheni 17 katika Hospitali ya Nairobi na operesheni nane katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven.
Waheshimiwa Majaji, mkiona navuta mguu na kuchechemea, ni kwa sababu ya tukio hilo.
Nikiwa hospitalini, tarehe 29 Juni 2019, aliyekuwa Spika wa Bunge, marehemu Job Ndugai, alitangaza kunifuta ubunge, kwa kuwa nilikuwa mtoro na sijaonekana Bungeni kwa miaka miwili.
Miaka miwili inafika, hajui nilipo. Ndiyo maneno aliyoyasema.
Hiyo ndiyo sababu iliyopelekea nisimalize term ya pili ya ubunge wangu.
Na kwenye hili niongeze, kwa sababu ni muhimu katika kesi hii: licha ya kuwa Mbunge na kuumizwa vibaya nikiwa Bungeni, Bunge na Serikali ya Tanzania ilikataa kata-kata kulipa gharama za matibabu. Sikupewa hata senti moja ya matibabu, licha ya sheria ya uendeshaji wa Bunge inayoelekeza kuwa Mbunge akipata changamoto yoyote ya kiafya ana haki ya kutibiwa na Bunge. Bunge lile lilikataa.
Waheshimiwa Majaji, kwa kuwa naelezea masuala ya personal record, kipindi nikiwa Bungeni nilikuwa Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, effectively kiongozi namba mbili katika uongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, wa kwanza akiwa Mwenyekiti wa Kambi Rasmi ya Upinzani, ambaye wakati huo alikuwa Mheshimiwa Mbowe.
Vilevile, Waheshimiwa Majaji, nilikuwa msemaji mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni wa masuala ya Katiba na sheria, masuala ya Muungano, pamoja na Mwanasheria Mkuu Kivuli (Shadow Attorney General).
Waheshimiwa Majaji, Mahak**a irekodi kuwa nimefanya kazi yangu ya ubunge kwa uaminifu mkubwa na kwa umahiri.
Kipindi hicho, kuanzia 2011 hadi 2014/2015, nilikuwa mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba.
Na kwa kipindi hicho, Waheshimiwa Majaji, Bungeni niliongoza harakati za kupigania Katiba mpya na mfumo huru wa uchaguzi. Kilichonileta hapa kwa ushahidi wangu si uhaini, bali ni mgogoro mkubwa wa kisiasa wa kupigania Katiba mpya na mfumo huru wa uchaguzi.
Tuliongoza mapambano haya Bungeni kwa uaminifu mkubwa na umahiri.
Nje ya ubunge, nimekuwa Rais wa Chama cha Wanasheria cha Tanganyika tangu mwezi Machi au Aprili 2017 mpaka Septemba 2017 niliposhambuliwa.
Nilichaguliwa na mawakili wa nchi hii kuwa Rais wao.
Hauwi Rais wa Chama cha Mawakili wa nchi hii k**a wewe ni mtu wa hovyo hovyo, laini laini.
Nje ya uongozi wa mawakili wenzangu, hapa nilipo, Waheshimiwa Majaji, ni Makamu Mwenyekiti wa Vyama vya Kidemokrasia Duniani, kwa Kiingereza International Democrat Union (IDU).
Shirikisho linalounganisha zaidi ya vyama 80 vya siasa around the world.
IDU ni muunganiko wa vyama vya kidemokrasia kutoka takribani nchi 80 mbalimbali duniani; Ulaya, Afrika, Amerika na Asia, ikiwepo vyama kadhaa vinavyotawala duniani.
Ni Makamu Mwenyekiti wa IDU na mjumbe wa K**ati yake Kuu ya Kitaifa.