Imani Philosophy

Imani Philosophy Habari na matukio mbalimbali katika jamaii Ulimwenguni kote. Follow ili uwe wa kwanza kufikiwa na habari zote.

MFUASI WA RAILA ODINGA AOMBA MSAADA KUHUDHURIA MAZISHI YA KIONGOZI WAKENuru Okanga, anayejulikana k**a mfuasi sugu wa Ra...
17/10/2025

MFUASI WA RAILA ODINGA AOMBA MSAADA KUHUDHURIA MAZISHI YA KIONGOZI WAKE

Nuru Okanga, anayejulikana k**a mfuasi sugu wa Raila Odinga, amewaomba Wakenya msaada wa shilingi 50,000 za Kenya (sawa na takribani Tsh. 950,000 za Tanzania) ili aweze kusafiri kuhudhuria mazishi ya kiongozi huyo wa ODM.

Taarifa hizo zimesambaa mitandaoni, zikidai kuwa Okanga yuko katika hali ngumu kifedha na anahitaji msaada wa dharura kufanikisha safari hiyo.

🚨 OFFICIAL: Kikosi cha Yanga SC kinachosafiri kuelekea Malawi kwaajili ya Mchezo wa hatua ya pili ya awali ya Klabu Bing...
16/10/2025

🚨 OFFICIAL: Kikosi cha Yanga SC kinachosafiri kuelekea Malawi kwaajili ya Mchezo wa hatua ya pili ya awali ya Klabu Bingwa Barani Afrika dhidi ya Silver Striker ya Malawi 🇲🇼

🚨_|| 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒 : Nipo tayari kufundisha timu za Yanga Sc na Simba Sc ila sio k**a kocha msaidizi hilo hapana""Nishakaa san...
16/10/2025

🚨_|| 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒 :

Nipo tayari kufundisha timu za Yanga Sc na Simba Sc ila sio k**a kocha msaidizi hilo hapana"

"Nishakaa sanaa kwenye ukocha msaidizi na kwa malengo niliyonayo kwasasa popote pale ni kuwa kocha mkuu sio msaidizi tena nishatoka huko"

Kocha mkuu wa klabu ya Jkt Tanzania Ahmad Ally kuhusu uwezekano wa yeye kwenda kufundisha vilabu vya Yanga Sc na Simba Sc k**a yupo tayari.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa taarifa ya kuufungia uwanja wa Sokoine, Mbeya kutumika kwa michezo y...
15/10/2025

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa taarifa ya kuufungia uwanja wa Sokoine, Mbeya kutumika kwa michezo ya Ligi kwa kukosa vigezo vya kikanuni na sheria za mpira wa miguu.

Kwa mujibu wa TFF miundombinu ya uwanja huo haikidhi matakwa ya Kanuni k**a ilivyoainishwa kwenye masharti ya Kanuni ya Leseni za Klabu.

Kufuatia uamuzi huo, timu zinazotumia uwanja huo kwa michezo yao ya nyumbani zitalazimika kutumia uwanja mwingine k**a Kanuni inavyoelekeza mpaka uwanja wao utakapofunguliwa, baada ya kufanyiwa marekebisho na kukaguliwa na TFF.

Aidha TFF imezikumbusha Klabu zote kuendelea kutunza na kuboresha miundombinu ya viwanja.

KUNDI LA P SQUARE WAUNGANA TENAP Square sasa wamerudi pamoja RASMI baada ya miaka 4 ya kutengana.   Hatimaye wameamua ku...
14/10/2025

KUNDI LA P SQUARE WAUNGANA TENA

P Square sasa wamerudi pamoja RASMI baada ya miaka 4 ya kutengana. Hatimaye wameamua kuwasikiliza mashabiki wao , walielewa ukuu wao ulitokana na wao kuwa pamoja na kutojaribu kuudhihirishia ulimwengu nani bora . Kaka yao Jude aliwaunganisha huku akitaka washerehekee siku yao ya kuzaliwa mwaka huu pamoja.

Nani mwingine alikosa nyimbo nzuri za P square? Mchanganyiko huu haujawahi kushindwa. Kuanzia vibonzo hadi taswira nzuri.

Mshambuliaji wa Yanga SC, Clement Mzize amerejea uwanja wa mazoezi baada ya kupona jeraha lililomweka nje kwa muda wa wi...
14/10/2025

Mshambuliaji wa Yanga SC, Clement Mzize amerejea uwanja wa mazoezi baada ya kupona jeraha lililomweka nje kwa muda wa wiki mbili.

Mzize is back 💯

 Part 8Mhe. Lissu: Sasa tuambie wewe ulikuwa na mash*taka gani? Kaaya: Mimi sikuwa na mash*taka. Mhe. Lissu: Kwanini huk...
13/10/2025



Part 8

Mhe. Lissu: Sasa tuambie wewe ulikuwa na mash*taka gani?

Kaaya: Mimi sikuwa na mash*taka.

Mhe. Lissu: Kwanini hukupanda cheo wewe? Maana umetumia miaka 15 kupanda cheo na sio 9 kwa mujibu wa PGO?

Kaaya: Sio mimi tu.

Mhe. Lissu: nataka wewe hao wengine tutajua.

Kaaya: Mimi sijajua anayepandisha cheo sio mimi.

Mhe. Lissu: Mimi sikusema lolote kuhusu utendaji kazi wako mzuri. Umepandishwa cheo umesema ni utendaji mzuri hujapandishwa unasema anajua muajiri kwanini?

Kaaya: Sielewi kwakweli.

Mhe. Lissu: Naomba nimsomeee Apendix A PGO 53. Vigezo vya kupandishwa vyeo ni seniority, utendaji yaani sifa, na possession on educational qualification yaani kisomo na utaaluma.

Unakubaliana na hii?

Kaaya: Hiyo ni general rule.

Mhe. Lissu: Additional Qualification to be considered ni good conduct, education, professional knowledge, good manner, sobriety yaani usiwe mlevi. Na hii unaisemeaje?

Kaaya: Hiyo nayo ni general rule.

Mhe. Lissu: Hukupandishwa cheo kwa miaka 15 kwasababu hufai?

Kaaya: sio kweli.

Mhe. Lissu: ulisema una shahada ya chuo kikuu ya sheria na umepata advanced diploma ya air condition hukupandishwa cheo?

Kaaya: inategemea nilipata lini hivyo visomo.

Mhe. Lissu: Sasa nikurudishe kwenye maelezo yako. Waheshimiwa Majaji apewe D1 shahidi.

Ushahidi wa Tarehe 09 October ukiwa hapa mahak**ani ulibaini kuwa ile video ina viashiria vya jinai?

Kaaya: Ni kweli.

Mhe. Lissu: kwahiyo kwenye hili maneno yako ya kizimbani na polisi yanalingana?

Kaaya: Ni kweli.

Mhe. Lissu: Sasa swali langu umesema wewe ni mwanasheria waeleze majaji matamashi yenye viashiria vya jinai ni kosa gani kwenye sheria za Tanzania.

Kaaya: Hakuna nililosema kwamba hilo ni kosa.

Mhe. Lissu: Nakuuliza viashiria vya jinai ni kosa gani kwa mujibu wa sheria za Tanzania?

Kaaya: sijasema k**a kulikuwa na kosa.

Mhe. Lissu: Kwahiyo ni kosa gani?

Kaaya: hadi nivi identify ni viashiria gani?

Mhe. Lissu: k**a wewe ni Laweyer unawezaje kusema kitu kikachunguzwe k**a hujaona k**a ni kosa?

Kaaya: mimi sikuainisha makosa. Baada ya Upelelezi ndio ingejulikana.

Mhe. Lissu: je kwenye patrol yako ulisema unaperuzi ili kung'amua makosa ya jinai?

Kaaya: Ni kweli

Mhe. Lissu: Sasa tuambie uling'amua makosa gani?

Kaaya: Niliona kuna false information. Nikaona niwamabie hii taarifa ya kweli au sio kweli.

Mhe. Lissu: Kwahiyo wewe uling'amua kosa?

Kaaya: Ndio taarifa za uongo.

Mhe. Lissu: Je kwenye maelezo yako yote ulisema wapi kuna kosa la uhaini?

Kaaya: Kwenye maelezo yangu sijaandika kosa la uhaini.

Mnaenjoy au hamuenjoy wajameni. 😂 Shahidi amelegea k**a mlenda hapa kizimbani. Anageuzwa geuzwa sanaa.

Mhe. Lissu: Je kwenye maelezo yako yote umeeleza kwamba kuna kosa la Kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni?

Kaaya: Sijaandika kosa lolote na hilo halipo.

Mhe. Lissu: Kwa vile wewe umedai ni Mwanasheria ni sawa au sio sawa kusema unafahamu kifungu cha sheria nilichosh*takiwa nacho yaani S. 39(2)(d) ya Penal Code?

Kaaya: Nafahamu.

Mhe. Lissu: Waeleze majaji k**a unafahamu kwamba mtu anayesambaza maneno ya kihaini sio yule alaiyeanzisha. Na yeye anakuwa amefanya kosa la uhaini? Waeleze majaji k**a unafahamu.

Kaaya: inategemea

Mhe. Lissu: Inategemea nini?

Kaaya: Inategemea na upelelezi. Sheria inategemea na Upelelezi.

Mhe. Lissu: Kuna watu wamesambaza hayo maneno ikiwemo Jambo TV instagram na YouTube?

Kaaya: Ni kweli.

Mhe. Lissu: Ilipelekwa Arusha one Digital?

Kaaya: Ni kweli

Mhe. Lissu: ilipelekwa clouds media instagram?

Kaaya: sikumbuki.

Mhe. Lissu: ilipelekwa Mwanzo TV youtube?

Kaaya: Ni kweli nakumbuka.

Mhe. Lissu: Waeleze majaji k**a unafahamu au hufahamu k**a ninakabiliwa na kesi mahak**a ya kisutu ya kusambaza taarifa za uongo?

Kaaya: Nafahamu.

Itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.@

Cc

Mahak**a Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali pingamizi lililowekwa na upande wa Jamhuri dhidi ya ma...
13/10/2025

Mahak**a Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali pingamizi lililowekwa na upande wa Jamhuri dhidi ya maombi ya msh*takiwa Tundu Lissu ya kutaka maelezo ya maandishi ya shahidi wa pili kupokelewa mahak**ani.

Mahak**a imesema mshtakiwa amefuata taratibu zote zinazohitajika kisheria katika kuomba kielelezo hicho kupokelewa Mahak**ani.

Kutoka kwenye insta Story ya Paula 🙄
12/10/2025

Kutoka kwenye insta Story ya Paula 🙄

11/10/2025

╱◥██████◣
│∩│🌠▤│▤▤│
K**a simu yako ni original copy hii 🤣🤣🤣

Katika kujiandaa na mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Silver Strikers ya Malawi, klabu ya Yanga Sc Jana Oktoba 10, 202...
11/10/2025

Katika kujiandaa na mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Silver Strikers ya Malawi, klabu ya Yanga Sc Jana Oktoba 10, 2025 imecheza mechi ya kirafiki dhidi ya TRA United kwenye uwanja wa Gymkana na kumalizika kwa sare tasa.

FT: Yanga Sc 0-0 TRA United

Yanga Sc itachuana na miamba hiyo ya Malawi Oktoba 18, 2025 kwenye mchezo huo wa raundi ya pili ya CAFCL ambapo itakuwa ugenini kabla ya kurudiana nyumbani Oktoba 25, 2025.

Romuald Rakotondrabe Kocha Mpya wa Yanga, Yanga SC Yamteua Romuald Rakotondrabe Kuwa Kocha Mpya | Achukua Mikoba ya Roma...
09/10/2025

Romuald Rakotondrabe Kocha Mpya wa Yanga, Yanga SC Yamteua Romuald Rakotondrabe Kuwa Kocha Mpya | Achukua Mikoba ya Romain Folz.

Klabu ya Young Africans SC (Yanga SC) imeripotiwa kufikia makubaliano ya kumteua Romuald Rakotondrabe, kocha wa Timu ya Taifa ya Madagascar, kuwa Kocha Mkuu mpya wa klabu hiyo, akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Romain Folz raia wa Ufaransa.

Romuald Rakotondrabe Kocha Mpya wa Yanga
Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vya kuaminika, Rakotondrabe, mwenye umri wa miaka 60, anatarajiwa kuwasili nchini Tanzania hivi karibuni kwa ajili ya kukamilisha taratibu za mwisho za usajili na kusaini mkataba wa miaka miwili na mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kocha huyo ana uzoefu mkubwa katika soka la Afrika, hasa kutokana na mafanikio aliyoyapata akiwa na Barea, timu ya taifa ya Madagascar, ambayo aliiongoza kufuzu hatua muhimu katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON). Uwezo wake wa kujenga timu zenye nidhamu na kucheza soka la ushindani umekuwa sababu kuu ya kuvutia uongozi wa Yanga SC.

Romuald Rakotondrabe Kocha Mpya wa Yanga
Romuald Rakotondrabe Kocha Mpya wa Yanga
Wakati huo huo, Romain Folz (35) anatarajiwa kuvunjiwa rasmi mkataba wake na klabu hiyo, hatua itakayofunga ukurasa wake wa muda mfupi ndani ya Yanga SC. Folz, ambaye aliwahi kufundisha klabu kadhaa barani Afrika ikiwemo AmaZulu FC na Azam FC, ameshindwa kufikia matarajio ya mashabiki na uongozi wa klabu hiyo kongwe ya Jangwani.

Uongozi wa Yanga SC una matumaini kuwa ujio wa Rakotondrabe utaleta mwelekeo mpya na kuongeza nguvu ya ushindani wa timu katika mashindano ya ndani na kimataifa, hususan katika Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions League) na NBC Premier League.

Address

London

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Imani Philosophy posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share