The Two Cast

The Two Cast News platform 󱢏
Writer 󱢏
Digital Content Creator󱢏
(2)

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟏𝟗𝐓𝐇 𝐃𝐄𝐂 𝐒𝐎𝟒𝐄𝐏𝟑-𝟒 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟏Mambo yashachemka, Saida ashapigiwa simu kuwa Asha ameshikwa alafu sasa Jem...
18/12/2025

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟏𝟗𝐓𝐇 𝐃𝐄𝐂 𝐒𝐎𝟒𝐄𝐏𝟑-𝟒 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒

𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟏
Mambo yashachemka, Saida ashapigiwa simu kuwa Asha ameshikwa alafu sasa Jemimah na yeye akapiga simu kwa AL, akamwambia AL k**a uko kwa nyumba hepa! Dem wa Ray ameshikwa na najua ataenda kumtaja Ray na akimtaja Ray, Ray lazima atantaja mimi. AL akamuuliza madam sasa unataka tucheze vipi? Jemimah akamwambia sikiliza, nenda kavitafute vile vibaka wa Umoja uongee na huyo kiongozi wao wa nywele nyingi mwenye huwa anatembea k**a mwanamke, umwambie wafanye juu chini, Ray aulizwe (ashughulikiwe) kabla Asha hajamtaja. aah! Makosa. Jemimah ameamua kufuta nyayo sasa. Ray akawekwa wanted na magaidi wengine kwa sababu Jemimah anajua, mradi tu Asha ameshikwa, Ray lazima atatajwa na Ray akishikwa atabanwa vizuri aseme kila kitu, kitu ambacho Jemimah hawezi kutaka kuhatarisha.
Wakati sasa Saida wanatoka na Tyrone kukimbia kituo cha polisi cha Central, acha wafungue lango, wamuone Asha, akilia tu... najua hata pia mnashangaa Asha amefikaje hapa wakati anapaswa kuwa kituo cha polisi... acha sasa niwarudishe nyuma, saa moja lililopita.
Tuliona Asha akiwa ameshikwa anaenda kuwekwa kwenye gari lakini wakati aliangalia nyuma, alimuona Ray.. wakati Asha aliwekwa kwenye gari aliambia polisi sikilizeni, mimi ni msichana tu niliyeingia kwenye mapenzi ya kijinga, mimi hizi pesa si mimi niliyeiba, ni mpenzi wangu ndiye mwizi na mimi si mwizi, mimi ni mtoto wa Daktari Tyrone. Kwanza polisi wakashtuka, wakamuuliza wewe ndio umekuwa unatafutwa? Asha akawaambia ni mimi,. ona sasa mshajua na kwa sababu sitaki kubeba msalaba wa mtu mwingine, mpenzi wangu yuko nyuma ya nyumba amejificha hapo, ningekuwa ninyi ningeenda huko sasa hivi.
Wueh! Mapolisi kusikia hivyo, ndani ya dakika chache walikuwa washamfikia Ray. Ray akakiri akasema yeah hizo pesa Asha hahusiki hivyo Asha akaachiliwa, kisha Ray akawekwa ndani lakini Ray akawaambia kitu kimoja, "siko peke yangu, tuko wengi" polisi akamwambia tutajulia mbele kwa sasa twende.
Hivyo ndio Asha aliachiliwa, akarudi nyumbani na ndio huyu langoni sasa, alafu Jemimah akidhani Ray yuko mbioni (anatoroka), Ray ashashikwa tayari.. mako! Makosa sana, alafu sasa acha niwashtue kitu kingine, leo sijapata taarifa mpya nimekaa nikaona hakuna namna mtalala bila kupenda (like) chapisho langu, nikaamua niandike kitu ambacho hakipo sasa fanyeni hivi, ukiona nimekosa sana, njoo kwangu unipige, univunje-vunje macho na unitoboe mikono.
Follow us The Two Cast part two inakuja

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟏𝟖𝐓𝐇 𝐃𝐄𝐂 𝐒𝐄𝟎𝟒𝐄𝐏𝟎𝟏-𝟐 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟏Saida alijua mara moja, ni Tinah aliyefuta ile namba na anayo. Saida alik...
17/12/2025

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟏𝟖𝐓𝐇 𝐃𝐄𝐂 𝐒𝐄𝟎𝟒𝐄𝐏𝟎𝟏-𝟐 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒
𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟏
Saida alijua mara moja, ni Tinah aliyefuta ile namba na anayo. Saida alikuja kwa chumba cha Tinah k**a umeme na hataki mchezo, akamwambia nataka hiyo namba uliyotoa kwenye simu ya Beka na ukaifuta. Tinah akamwambia mimi sina namba lakini Saida alimwambia nitakupiga wewe kufikia wakati unanipa namba utakuwa umeona moto.
Walianza kubishana hapo, Beka akaona kana kwamba sasa awakataze lakini Tinah na Saida kwa pamoja wakamwambia "shut up." 😂😂😂 Beka akajifunza kunyamaza. Punde si punde, Tyrone akafika.
Tyrone alikuja akakalisha kila mtu chini akiwemo Beka akamuuliza, Aisha alisema nini? Beka akasema alisema anajutia kutoka huku na akasema nisalimie mamake. Tyrone akauliza Saida na wewe mbona unasema Tinah alifuta namba? Saida akamwambia huyu Tinah hataki Aisha apatikane na najua alifuta hiyo namba. Tinah akaweka drama fulani hapo hadi akalia ndio aaminike tu lakini Saida akaambia Tyrone huyu mtoto anajifanya tu ndio umuamini. Ni kweli Tinah anajifanya tu lakini ameongea na Asha.
Ray naye kufika nyumbani, akidhani kila kitu kiko sawa, hana habari Asha alishapata zile barakoa... Asha akauliza Ray, hizi ni nini, barakoa ni za nini? Ama umeanza kuibia watu? Ray akasema mpenzi mimi hizi vitu sijui si unajua hii nyumba si yangu, labda ni za rafiki yangu. Asha alimwambia usinione mjinga Brayson.... Ray ameruka sana anasema hizi vitu hajui na lazima ni za rafiki yake... lakini Asha alikataa. 😂 😂
Asha akauliza k**a ni za rafiki yako, kwa hivyo ina maana rafiki yako ni jambazi? Ray akasema hapana, hizi ni za kuvaa mtu akiendesha pikipiki na rafiki yangu hufanya kazi ya pikipiki. 😂 😂 Asha ijapokuwa anaambiwa kitu kinachokaa k**a ukweli, lakini alimwambia Ray usijaribu kunihadaa.
Ray kuona Asha anaelekea kujua ukweli, akamwambia basi, k**a ni hivyo mimi na wewe basi imekwisha, ndio usiwe unakaa na mimi... Asha akamwambia basi pole mpenzi, nilikuwa nauliza tu. Asha alimshika akamlalia akamwambia mpenzi nakupenda na nilikuwa nauliza tu... 😂 😂 😂
AL naye amemsubiri Ray aje ampe sehemu yake ya pesa aende lakini akatumiwa ujumbe akaambiwa jambazi, ondoka sasa hivi huku ni kubaya kiasi tutakutana baadaye. 😂 😂 😂 Raty alituma ule ujumbe akiwa ameufuta kwa haraka sana. K**a ni pesa bado wanazo na Asha kwa bahati tu hajapata zile pesa.
𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟐
Tinah leo ameshapika chakula cha jioni na Tyrone hawezi kuacha kuvutiwa na binti yake. Yaani Tinah amekuwa mzuri hadi babake anamwambia sasa wewe ni binti yangu.
Wakiwa mezani, Tyrone akagundua Saida hayupo, akauliza mmeshamwambia Saida kuna chakula cha jioni? Tinah akadanganya akasema ndio nilimwambia lakini ni k**a hana hamu ya kula. Tyrone akaamka kwenda kumuita lakini Sabina akamwambia, k**a hataki kula achana naye lakini Tyrone alimwambia tafadhali huwezi kuelewa ni mimi pekee ninayeelewa. Sabina anahisi vibaya sana kuona Tyrone anamjali Saida.
Wakati Tyrone ameenda, Tinah akaambia mamake "unahisi vibaya na jinsi wewe na Robert mnavyofinyana nyuma ya mgongo wa baba yangu?" 😂 😂 😂
Tyrone alikuja akaambia Saida tafadhali, twende tukale na nikikuona ukiwa hivi inaniumiza sana. Tyrone alimshika Saida akampangusa machozi, akamwambia usilie, ukilia unanifanya nilie pia mimi. Saida akamwambia Tyrone, nilifanya makosa kumleta Asha huku, sasa nisingekuwa hivi. Saida hajamzoea Asha wake kuwa hivi, anashangaa tu nini kimempata binti yake.
Sabina pia akiwa hapo alimwambia Tinah sikiliza, najua ulifuta hiyo namba kwenye simu ya Beka. Tinah akamuuliza na kisha? Sabina akamuuliza mbona ukafanya hivyo? Tinah akamwambia namchukia Asha, na hastahili kuishi huku. Sabina akamwambia vizuri angalau mimi na wewe tuko upande mmoja kwa sababu pia nataka sana huyo Saida atoke kwenye hii nyumba. Tinah akaambia mamake sikiliza, hatuko upande mmoja, kwa sababu una hadi kesho asubuhi niwe nimepata mahitaji yangu la sivyo baba atajua kila kitu.
Huku kwa Chris nako, alipigiwa simu kutoka kituo cha polisi akaambiwa tuna dalili za mmoja wa washukiwa. Jemimah alikuwa hapo akasikia, akauliza wamesema nini? Chris akamwambia walichukua alama za vidole na ni k**a wanajua mahali mmoja wa washukiwa alipo.
Jemimah kusikia hivyo, akampigia simu AL lakini kosa ni AL amelala, simu inaita lakini haipokelewi. Jemimah akampigia Ray lakini kumbe Ray alikuwa ameenda kununua mahitaji, kwa hivyo ni Asha ndiye aliyepokea simu, akamwambia Jemimah, Ray hayupo ametoka kidogo.
Lakini kidogo tu hivi, kabla hata Asha hajamaliza kuongea, alishtukia mlango umepigwa teke vibaya sana. Polisi wameshafika.
Asha alishtuka sana kuona polisi kumbe Ray ndiye alikuwa anakuja akaona polisi ikabidi akimbie. Polisi wakauliza Asha, pesa mlizoiba ziko wapi? Asha akamwambia mimi sijui kitu mnaongelea lakini polisi mwingine akaingia chini ya kitanda akapata pesa kwa hivyo moja kwa moja Asha akawa mshukiwa mkuu kwa sababu pesa zimepatikana akiwa peke yake.
Asha aliwaambia tafadhali hata mnaweza kumpigia mama yangu lakini wapi, akachukuliwa... Asha akiingia kwenye gari alichungulia akamuona Ray, akajua tu kwa kweli nilijua tu wewe ni gaidi. Wah! Makosa sana.
Taarifa ikamfikia Chris akaambiwa wameshamk**ata msichana na zile pesa anaitwa Asha. Jemimah yeye anamjua Asha kwa hivyo alimpigia Saida akamwambia Asha amepatikana, lakini amek**atwa na anapelekwa kituo kikuu cha polisi (Central Police Station)... Saida hajawahi kushtuka kiasi hicho. Ukimaliza, wacha comment na utufollow The Two Cast for daily updates

Mbona hawa wanadada wanatrend?
16/12/2025

Mbona hawa wanadada wanatrend?

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟏𝟕𝐓𝐇 𝐃𝐄𝐂 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟏Robert alikuwa kwenye simu na Saida akimwambia, "Unataka niache kazi zangu nianze ku...
16/12/2025

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟏𝟕𝐓𝐇 𝐃𝐄𝐂 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒

𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟏
Robert alikuwa kwenye simu na Saida akimwambia, "Unataka niache kazi zangu nianze kumtafuta Asha? Unajua hilo haliwezekani." Punde si punde, Annaliza akaja na kumuuliza Robert, "Umeongea na Tyrone?" Robert akamjibu, "Hapana, kwani yupo?" Ann akamwambia kuwa wanapaswa kuwa na mkutano lakini Tyrone hajatokea. Sisi tunajua kuwa Tyrone yuko mikononi mwa polisi.
Kule polisi, Sabina anamtazama Jemimah na kuona kuwa mama huyu haaminiki kabisa. Muda mfupi baadaye, Ray akampigia simu Jemimah na kumwambia kuwa anapaswa kuja kuchukua pesa hizo kwani ni hatari sana kukaa nazo. Jemimah akamwambia atulie hadi mambo yatakapopoa.
Huku Sabina na Saida wakimngoja Tyrone atoke, Saida anawaambia ana uhakika kuwa Tyrone hawezi kufanya kitu k**a hicho. Tyrone alipotoka, aliwaambia, "Jamani mimi sina hatia, huyu mzee ana hasira tu kwa sababu binti yangu alimwacha."
Chris naye akamuuliza Jemimah, "Nilikiona kwa Tyrone, ulikuwa unafanya nini?" Jemimah akasema alikuwa ameenda kumwona Tinah, kwani alitaka kumwona na akamwomba msamaha. Chris hana habari kuwa adui yake mkubwa yuko karibu naye.
Ripoti ilimfikia Robert kuhusu jinsi Chris alivyosema kuwa Tyrone alituma wahuni kumuibia, lakini kwa vyote vile, hakuna ushahidi wowote.
Maisha ya Asha yanazidi kuwa magumu. Ameshaambiwa asiwe anaenda kazini; yeye abaki, afagie nyumba na kulala huku Ray akienda kazini. Lakini wakati anafagia, aliona kitu kwenye mfuko wa kubebea (carrier bag) akashindwa ni nini. Alipokitoa, alishtuka hadi akakiangusha. Makosa makubwa.
Jemimah alikuja kukutana na akina Ray na AL na kuwaambia, "Mnaweza kuchukua sehemu yenu, lakini mjue ninajua kuwa mliiba pesa hizo, kwa hivyo msijaribu hata noti moja maana tutakosana vibaya sana."
Asha aliamua kumpigia Beka kwa sababu anayo namba yake. Beka akapokea akijiuliza namba hii ngeni ni ya nani, lakini aliposikia sauti tu akajua ni Asha. Akamuuliza, "Uko wapi Asha?" Asha akamuuliza, "Mama yangu anaendeleaje?" Beka akamwambia, "Mama hayuko sawa, na hukufanya vizuri kuondoka; mamako analia sana kila siku."
Asha alimuuliza Beka, "Je, mnaona k**a nilifanya makosa kutoroka? Maana nimechanganyikiwa sana." Beka akamwambia, "K**a unataka msaada niambie, hata k**a hutaki wazazi wako wajue." Asha alimwambia tu, "Tafadhali usiambie mtu kuwa tumeongea, na umsalimie mamangu." Kumbe Tinah alikuwa akimsikiliza Beka akiongea kwenye simu. Asha anajuta sasa kwa sababu anajua alifanya kosa kutoroka na Ray.

𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟐
Tinah alikuja na kumuuliza Beka, "Ulikuwa unaongea na nani?" Beka akajaribu kujitetea kidogo lakini Tinah tayari alishajua ni Asha. Pamoja na hayo, Tinah alipigiwa simu kuwa mzigo wake wa manguo ya Gikomba umewasili.
Kazini k**a kawaida, Robert anajipendekeza sana kwa Annaliza, hadi Anna akamuuliza, "Mbona kila saa unakuja kuniangalia na kunialika kwa chakula cha jioni? Unataka nini hasa, natumai hujaribu kunitongoza?" Robert akamwambia, "Tulia, ni chakula tu, nakuahidi hakuna kitakachofanyika."
Tinah ameshapata nguo zake za kuuza, hadi Beka akamwambia, "Yule jamaa anakuuzia nguo nzuri sana, unapaswa kumshikilia." Tinah akamwambia hata baba yake anampa msaada mkubwa. Beka akamwambia, "Heri wewe una wazazi wazuri, sisi wengine hatukubahatika." Tinah akamuuliza, "Unamaanisha nini?" Beka akamwambia, "Ni vile sisi wengine wazazi wetu hawakutu..." Kabla amalize, akamwona Saida akiwasikiliza.
Beka alimfuata Saida kwa sababu kuna ujumbe anapaswa kumpa kutoka kwa Asha. Lakini kosa alilofanya Beka ni kuacha simu yake pale; Tinah akaichukua, akaiondoa namba aliyotumia Asha kumpigia na kuiweka kwenye simu yake.
Beka alikuja na kumwambia Saida, "Unajua nimeongea na Asha?" Saida akamwambia, "Usitaje jina la mtoto wangu wakati wewe ndiye uliyesababisha haya." Beka akamwambia, "Nimeongea naye na alikuwa analia akisema anajuta sana." Saida akajua mara moja kuwa lazima huyo kijana amemfanyia Asha kitu kibaya, akamwambia Beka, "Nipe namba hiyo." Hapo ndipo Beka alipotambua kuwa aliacha simu yake mahali Tinah alipokuwa.
Saida na Beka walikuja kuangalia namba hiyo kwenye simu ya Beka lakini kumbe, wakati Tinah aliichukua namba hiyo, aliifuta kwenye simu ya Beka. Kwa hivyo Beka hana namba sasa, lakini Tinah anayo.
Tinah aliipigia namba hiyo na kumwambia Asha, "Sikiliza, hata k**a hutaongea. Huku ulishasahaulika na hata mamako hataki kusikia jina lako likitajwa. Kwa hivyo ningekuwa wewe, nisingerudi huku." Tinah anaongea huku Asha akisikiliza tu. Tinah akamwambia, "Kaa mbali nasi." Asha akamuuliza, "Namba hii umeipata wapi?" Tinah akamwambia, "Usiwe mjinga, si umempigia Beka na hapo ndipo amenipa namba? Tumia akili!"
Asha sasa amejua kuwa ana dhamira moja tu: kupambana na Tinah. Na hawezi kupambana naye akiwa mafichoni; atapambana naye wakiwa wote kwenye jumba la kifahari. Basi... Tinah? Asha anakuja kwa ajili yako. Tufollow The Two Cast for daily updates.

16/12/2025

Small plane carrying 10 people crashes into building in Toluca, west of Mexico City. killing everyone on board

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟏𝟔𝐓𝐇 𝐃𝐄𝐂 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟏Jemimah alipigiwa simu na Ray, akamuuliza ni kwa nini hakumwambia Chris alikuwa na b...
15/12/2025

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟏𝟔𝐓𝐇 𝐃𝐄𝐂 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒

𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟏
Jemimah alipigiwa simu na Ray, akamuuliza ni kwa nini hakumwambia Chris alikuwa na bunduki. Jemimah akamjibu hakuwa anajua k**a angeibeba (bunduki). Kisha Jemimah akamuuliza kuhusu pesa, "Mko nazo?" Ray akamwambia "Ndio," lakini hajui pa kuziweka. Jemimah akamshauri, "Kaa nazo hadi mambo yatulie." Ray alijaribu kumwambia, "Yoh, siwezi kaa na hizi pesa," lakini Jemimah akakata simu kwa haraka, kwa sababu Chris aliingia.
Chris amefika akiwa ameumia sana. Jemimah anajifanya kumhurumia sana lakini yeye ndiye bongo (mastermind). Akamuuliza k**a aliwaona wale wezi lakini Chris akamwambia "Zii, sikuwaona, lakini shida yangu tu ni walijuaje niko na pesa." Angalia Jemimah vile anajifanya na kusema, "Na kweli, walijuaje?" Kosa ambalo akina Ray walifanya ni kuacha pikipiki (motorbike) hapo.
Ray ilibidi arudi nyumbani. Shida ni hajui ataambia Asha aliumia akifanya nini, na bado yuko na zile pesa, mamillion ya pesa. Alifika wakati Asha alikuwa amelala. Akaingia chumbani pole poooole na kuziweka chini ya kitanda. Lakini Asha hakuwa amelala, alikuwa macho na akaona kile kimewekwa chini ya kitanda. Alipomuuliza Ray, Ray akasema ni vitu vya kazi (job).
Asha akanotice kidonda kwenye mkono wa Ray, akamwambia "Babe, yafaa twende hospitali," lakini Ray akamwambia "Yoh, mi niko sawa babe, usiwe na wasiwasi."
Kumbe Chris naye alisuspect mtu, naye ni Tyrone. Chris alimcall Tyrone na akamwambia, "Najua ni wewe uliwatuma watu waniibie pesa na utalipa kwa hilo." Tyrone alishangaa, "Sasa hii imetoka wapi?" Kwani kusema ukweli, hana habari Chris anazungumza nini.
Ray ashatulia, amefungwa mkono, huku Asha anamwambia "Babe, siwezi taka kitu kibaya ikufanyikie ama ufanye kitu kibaya." Ray anamwambia "Tulia babe, siwezi fanya kitu kibaya na nitamake sure unakaa maisha mazuri." Punde si punde, walipokuwa wanakunywa chai, mlangoni kukabishwa (kuligongwa).
Ray akauliza, "Wewe ni nani anabisha?" Kumbe ni yule jamaa mwenye walikuwa na yeye jana. Angalau roho ya Ray ikatulia. Lakini angalia: wakati Ray ameenda kuongea na rafiki yake anayeitwa Along Lilo (AL), hapo na hapo, Asha akafanya kosa moja kubwa sana; akaenda kuangalia ni nini Ray alieka chini ya kitanda jana usiku. Aah! Kosa. Hata k**a ni mumeo, as long as ushajua yeye ni gaidi na asuspect unaeza mset, manze wewe ni kwisha maneno. Asha, ashajitangazia Kang'o (shida kubwa).
𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟐
AL alikuja kuongea na Ray kujua venye ako, na Ray akamwambia "Mnaona shida mumenieka?" AL akamwambia "Tulia, angalau uko sawa."
Ray hana habari Asha ashachukua begi. Kisha AL akaambia Ray, "Unajua hiyo pikipiki waliipata?" Ray akamwambia "Unaona, sasa si tutashikwa?" AL akamwambia "Tulia, hiyo piki niliiba, so wakifanya uchunguzi watamshika tu mwenye pikipiki lakini si sisi."
Ray akaambia AL achukue zile pesa aende nazo lakini AL akamwambia "Si unajua mi huwa siishi pahali (hamishi makazi), so kaa tu na hizo pesa."
Wacha Ray arudi kwa nyumba, ampate Asha ako na ile begi. Lakini ajabu ni kuwa Ray hakushtuka. Kwa nini? Kumbe, akili ni mali, begi halisi la pesa haliko hapa. Begi halisi la pesa Ray alificha (siku ya kwanza) akaja na begi ingine yenye imejaa nyundo, koromeo na kokobilo. (Hizo ni vifaa vya mjengo, msishangae).
Swali, alibadilisha saa ngapi? Usiku, wakati Asha alikuwa amelala, Ray aliamka pole poooole, akachukua zile pesa akaeka kwa begi tofauti, na begi yenye Asha aliona akaeka vile vifaa vya mjengo. Hivyo ndivyo Asha alivyochezwa.
Tinah naye shughuli baada ya shughuli. Kwanza leo anaenda Gikomba na ashaitisha Uber. Lakini mwenye Uber anamchelewesha sana (anamchezesha), akafanya Tinah akachelewa hadi akakutana na Tinah (Tinah mwingine, labda).
Jemimah alimpata Tinah na akamuuliza, "Niliambiwa unanitafuta?" Tinah akamwambia "Ndio, nilitaka tu kuomba msamaha." Jemimah akamuuliza "Vipi k**a ni mpango wako na Chris nidhani mumeachana kumbe mnanicheza?" Tinah akamwambia "Kwa kweli, kwa kweli, nina maana (I mean it)."
Lakini punde si punde, Jemimah akaona makarao (polisi) wanaenda kwa Tyrone na Chris ako ndani. Jemimah akajua mara moja ni Tyrone ndiye anayedhulumiwa.
Tyrone yeye hana habari kinachokuja. Ashaoga anaenda kazini. Lakini punde si punde, makarao wakafika na Chris. Akawauliza "Shida ni nini?" Chris akasema "Ni huyu, alitumana watu waniibie pesa zangu." Tyrone yeye hajui chochote... amekuja tu kushikwa.
Jemimah pia alifika na akauliza "Chris, ujinga gani unafanya?" Chris akasema "Huyu ndiye alituma watu waniibie kwani ni yeye alijua nimelipwa shares zangu." Tyrone alikosa njia nyingine (otherwise) wakaenda polisi kuandika statement (taarifa), lakini Tyrone alimtazama Jemimah kwa macho na akamwambia "Sikiza Jemimah, sina uhusiano wowote na hili (I have nothing to do with this)." Jemimah anajua "Ndio, si Tyrone," kwani ni yeye k**a Jemimah ndiye alitumana (watu wa Ray).
Tufollow The Two Cast for daily updates

15/12/2025

🫡🫡

Siku yako ikifika imefika☺️
15/12/2025

Siku yako ikifika imefika☺️

15/12/2025

President William Ruto having a chat with Truphena Muthoni

14/12/2025

Mshtuko Watamu huku mwanamke akinaswa akifukua kaburi la mtoto katika tukio la usiku wa manane.

Nabii David Owuor, yule mtu wa miujiza anayeponya kila kitu, alitembelea Hospitali ya "G. Fogliani" huko Milazzo (ME), n...
14/12/2025

Nabii David Owuor, yule mtu wa miujiza anayeponya kila kitu, alitembelea Hospitali ya "G. Fogliani" huko Milazzo (ME), nchini Italia. Sababu? Kufanyiwa upasuaji wa goti!
Kwa kweli, nguvu zake hazikuwa na uwezo wa kurekebisha goti lake tu hapa Kenya.

Atarudi hivi karibuni akiwa amepona na ameongeza nguvu mpya za kuponya wagonjwa na viwete wote ambao yeye mwenyewe hakuweza kujiponya goti lake.

Si unaona nyinyi ndio mko na wivu😂😂Mulamwa and Carol Muthoni Co-parenting.
14/12/2025

Si unaona nyinyi ndio mko na wivu😂😂
Mulamwa and Carol Muthoni Co-parenting.

Address

Gandhinagar

Opening Hours

Monday 7:30pm - 8pm
Tuesday 7:30pm - 8pm
Wednesday 7:30pm - 8pm
Thursday 7:30pm - 8pm
Friday 7:30pm - 8pm
Saturday 4pm - 7pm

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Two Cast posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share