The Two Cast

The Two Cast News platform 󱢏
Writer 󱢏
Digital Content Creator󱢏
(2)

05/05/2026

Ladies be careful

Endorsed by UDA, M , and the wife. As a voter, share your perspective.
07/02/2026

Endorsed by UDA, M , and the wife. As a voter, share your perspective.

Huyu kijana alishikwa na kisu akieda shuleni na akiulizwa akasema amechoka kupigwa na wenzake na amejaribu kuambia mwali...
26/01/2026

Huyu kijana alishikwa na kisu akieda shuleni na akiulizwa akasema amechoka kupigwa na wenzake na amejaribu kuambia mwalimu lakini hakuna hatua inachukuliwa...
Were you bullied in school?

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟏𝟑𝐓𝐇 𝐉𝐀𝐍 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄 𝟏Saida na Asha wameshapika chajio, tayari kula lakini punde si punde, mwenye nyumb...
12/01/2026

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟏𝟑𝐓𝐇 𝐉𝐀𝐍 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒
𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄 𝟏
Saida na Asha wameshapika chajio, tayari kula lakini punde si punde, mwenye nyumba akaingia. Sabina akawauliza, bado mnafanya nini hapa? Ona vile mshapika chakula kingi kana kwamba ni chenu. Saida alimwambia Sabina sikiliza, pia sisi tunaishi hapa, na hapa hatutoki... na mmeona Sabina amekuja na Robert... kumbe hawajakuja kucheza.
Robert alitoa miwani akaweka kando, akawaambia Saida na Asha, si mmeambiwa mtoke ama nimesikia vibaya? Saida akasema hatutoki hapa, na Asha pia akasema kutoka kwa chumba chako sitoki. Nakuambia Robert akiwa na Sabina, waliwashikanisha Saida na Asha, mbio sana hadi nje ya lango na wakafunga lango. Saida na Asha wakatupwa nje.
Lakini tazama, wakati Saida walitolewa nje, Sabina alikuja akapiga simu, akampigia mtu akamwambia nimeshamuachilia mlengo (target), wamalize hao sasa... nani amepigiwa simu... amini usiamini, ni Ray.. aah! Makosa. Ray akakubali na akamwambia Sabina, kazi itafanyika vile inavyofaa, hadi Ray ana bastola hapo kwenye gari.
Ray aliwaona akina Asha na hata akashuka kwenye gari wakaongea hapo lakini Asha akauliza Ray unafanya nini? Saida akamwambia ni mimi nimemuita aje baada ya sisi kufukuzwa. Ray akawaambia k**a mnataka mahali pa kukaa naweza wasaidia lakini Saida akamwambia usijali, tunaenda kwa Annaliza na kwa kuwa una gari labda utushushe huko. Ray akapeleka Asha na Saida kwa Annaliza na usisahau, hawa hawa ndio amelipwa kuwamaliza.
Annaliza aliwakaribisha lakini akiwa amekasirika sana na Robert na Sabina baada ya kuambiwa waliwafurusha akina Saida. Annaliza hakuvumilia, alimpigia simu Robert, akamuuliza, wewe ni mnyama wa aina gani hata huna huruma na mtoto wa watu mnawafukuza usiku huu? Robert akasema ni kwa sababu sikuwa na njia nyingine, lakini Anna akamwambia mshikaji unahitaji kukua (grow up), sijui huyo mwanamke anakupa nini lakini unahitaji kukua mzee... kumbe Sabina amemsikia Robert akiongea kwa simu na Annaliza 😂😂😂😂
𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄 𝟐
Baada ya Ray kuwafikisha, kuna kitu Saida alishuku akaja akauliza Ray, ulikuwa unafanya nini hapo, kwa sababu nilisema nilikuita ili kukutetea... ulikuwa umekuja kufanya nini ama kutuua vile Sabina alikutuma? Ray akamwambia hapana, mimi nilikuwa nimekuja tu kumwona Asha kwa sababu namkumbuka sana. Ray alidanganya kwa sababu ni kweli yeye alitumwa kumuua Asha... Saida akamwambia Ray unaona sasa vile Sabina anatupeleka, na nikikuambia umuue unaona ni kazi ngumu. Ray akamwambia kumuua Sabina si suluhisho.
Asha alikuja akauliza mamake kuna mpango gani kati yako na Ray? Saida akasema nahofia tu asiende hivi aache kutusaidia kwanza ni kwa vile hajui humtaki. Asha akamwambia mama, usinichanganye akili, kuna njama gani yako na Ray kwa sababu nashuku sana unanificha. Saida hawezi jaribu kumwambia Asha ukweli kwa sababu wueh.... ataharibu mambo. Vyovyote vile, wamekaribishwa kwa Annaliza.
Siku iliyofuata, kwa Chris, ameketi mezani na mkewe, wanakula chai na mahindi ya kuchoma. Maisha yamekuwa magumu sana kwa Chris. Chris aliuliza Jemimah k**a anaenda kortini kusikiliza kesi ya Tyrone lakini Jemimah akamwambia hapana, sitaki kwenda huko nimwone Robert, kwa sababu ananiudhi sana. Punde si punde, Jemimah akapigiwa simu, akaamka akaenda kuipokea huko nje. Huyo alikuwa Ray na anataka sana wakutane.
Jemimah akarudi akadanganya Chris akamwambia naenda kumwona rafiki yangu, anataka kufanya harusi hivyo alitaka nimsaidie kuchagua nguo. Chris akakubali tu lakini ndani kabisa anaona aaai... hapa mko na uhakika sichezewi wakuu.. Chris akashuku kitu.. aah! Makosa.
Wakati tu Jemimah ametoka hivi, Chris pia naye kwa sababu amekuwa akishuku mkewe anakutana na mwanaume akaamua kumfuata Jemimah sasa... wah! Makosa sana kwa sababu Jemimah anaenda kukutana na Ray.
Walikutana wakaja kwenye hoteli fulani wakaketi wakaanza kuongea huku Ray anamwambia Jemimah husikii kuwa Sabina anataka niue Saida na hata ameshawafukuza jana. Jemimah akamuuliza, umekubali kufanya hiyo kazi? Ray akamwambia hapana, ndio maana niko hapa tukutane uniambie hatua ya kufuata. Kumbe Chris pia, aliwafuata ameketi hapo anasikiliza kila kitu. Chris haamini huyu ni mkewe wanaongea kuhusu kumuua mtu.
Chris ndio anazidi kuchanganyikiwa kwa sababu sasa amesikia Ray akisema vile anampenda Asha hivyo ameshajua huyu hawezi kuwa mpenzi wa mkewe, huyu ni mshirika wa uhalifu (partner in crime). Jemimah aliuliza Ray, sasa ulitaka nifanye nini? Ray akamwambia kwa sababu wewe ni mkubwa wetu, piga simu tujue nani mwingine amepewa kazi ya kumuua Saida kwa sababu najua si mimi peke yangu. Wakati mazungumzo haya yakiendelea, Chris anasikia kila kitu.
Punde si punde, Sabina alimpigia simu Ray, akamuuliza mbona bado Asha yuko hai? Ray akamwambia hapana, kazi ilikuwa kumuua Asha lakini jana alikuwa na mamake na mimi sipendi kuwa na shahidi kwa kazi yangu. Sabina akamwambia usinifanye mjinga wewe, nataka kufikia leo usiku Asha awe ameuawa.. sawa? Ray akamwambia ni sawa, nitafanya hivyo. wueh! Mambo yamechemka. Kuna kitu Ray anajua, asipofanya hii kazi, kuna mtu mwingine atapewa kazi ya kumuua Asha...
Je, ungependa kupata daily updates? Tufollow The Two Cast

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟗𝐓𝐇 𝐉𝐀𝐍 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄 𝟏Leo ni siku ya mahak**ani, Sabina na Robert wamekuja na wakili wao, Saida na Annal...
09/01/2026

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟗𝐓𝐇 𝐉𝐀𝐍 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒
𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄 𝟏
Leo ni siku ya mahak**ani, Sabina na Robert wamekuja na wakili wao, Saida na Annaliz wamekuja na wakili wao. Angalia jinsi wakili wa Sabina alivyochangamka 😂😂 kumbuka huyu wakili alikuwa wakili wa Tyrone lakini kwa sababu ya pesa, ameshamsaliti Tyrone, sasa hivi ni wakili wa Sabina.
Tyrone aliletwa kizimbani, anamwangalia Robert akiwa haamini. Sabina alisimama kizimbani, anaonekana mwenye machozi, majonzi na huzuni sana lakini yote haya ni michezo tu anayocheza. Yaani Tyrone alimwangalia Robert hivi hadi akaanza kulia, anashindwa huyu ni rafiki wa aina gani, unichukulie mke kisha usimame mahak**ani dhidi yangu tena.. dunia haina huruma. Fikiria Tyrone alilia.
Chris naye kwake kumechafuka, alikuja akamuuliza Jemimah, kwahiyo wewe na Robert mnafanya kazi pamoja, anakupea pesa ili ufanye shopping alafu mimi nionekane sifai sindio? Jemimah akamwambia sijui unaongelea nini wewe... kwahiyo kwa sababu nafanya shopping kwangu ni vibaya ama? Chris akamuuliza mbona basi ameninyima mkopo na wewe anakupea? Jemimah akamwambia Robert ni kaka yangu, si lazima akikupa mimi akupe wewe, we twende tukale mzee, alah. Jikubali umefilisika usaidiwe. Sikiliza, Jemimah pesa anayotumia ni zile walizoiba na Ray, si ati amepewa na Robert.
Huku mahak**ani, ilifika wakati wa Tyrone kuulizwa maswali, anaulizwa, unasema bastola ilifyatuka yenyewe, nini kilifanya ifyatuke yenyewe? Tyrone alishindwa kujibu, alianza kulia, akasema "I didn't mean to shoot my daughter." Fikiria wakili anamuuliza haya maswali, ni wakili aliyekuwa wake, wakili wake binafsi siku chache zilizopita lakini ameshanunuliwa na Sabina.
Kikao cha kwanza kiliisha watu wakatoka nje. Wakili wa akina Saida alikuja akasema hii kesi itakuwa ngumu kiasi lakini Annaliz akasema haifai kuwa ngumu na tumekulipa, kwa hiyo chaguo ni gani? Wakili akawaambia kuna machaguo mawili tu, la kwanza Tyrone akubali kuwa ilikuwa jaribio la mauaji (attempted murder) ili apunguziwe miezi ya kukaa jela.. Saida akamuuliza na chaguo la pili? Wakili akasema chaguo la pili labda kungojea miujiza ifanyike Tyrone aachiliwe 😂😂😂😂
𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄 𝟐
Wakili wa Robert na Sabina alikuja akawaambia Sabina, mambo yanaenda vizuri na kuna uwezekano Tyrone atakaa ndani kwa miaka mingi sana... Robert akamuuliza muda gani? Akaambiwa mradi tu ninyi wawili mwe na amani ya akili.
Sabina na Robert wakisikia hivyo, wanafurahia sana, kwa sababu wanataka Tyrone aozee gerezani na kile Sabina anataka sana ni kuwa na uwezo wa kumiliki kila mali anayomiliki Tyrone. Je, watafanikiwa? Tuone.
Huku hospitalini, kwa mara ya kwanza, Celestine akapata nafuu alafu ajabu wakati alipoamka kitu cha kwanza alitaka kuona ni babake. Sasa hapa kuna kuchanganyikiwa, hatujui anataka kuona baba mlezi au baba mzazi.. mzazi ni yule aliyepanda mbegu, mlezi ni yule aliyekaa naye 😂😂 tunachojua ni Tinah alitaka kuona mama yake na baba yake. Mbio mbio muuguzi akakimbia akamuita Sabina akamwambia Tinah anataka kukuona wewe na baba yake. Robert na Sabina wakaja mbio... Tinah akaona mama yake akatabasamu, kisha akaona Robert pia akamgeukia mama yake akamuuliza "yuko wapi baba yangu?".. Robert akashindwa, kwani baba yako si mimi niliye hapa? Hadi Sabina akamwambia Tinah, Tyrone alikupiga risasi na sasa hivi yuko jela na hivi karibuni atapelekwa gerezani kabisa. Tinah akasema hapana, mbona ak**atwe na hakukusudia,... nataka kumuona. Sabina na Robert hawataki hivi, kwani sasa wasomaji acha niwaambie mapema, miujiza ya kumtoa Tyrone ndani ni Celestine.
Robert akiwa kwenye mizunguko yake kumbe Jemimah alikuja kumfokea. Jemimah akamwambia Robert sikiliza, k**a huwezi tusaidia basi kaa mbali na familia yangu.. mbona umemwambia Chris ati huwezi msaidia hadi nimuache? Robert akamwambia nilikuwa mkweli tu na k**a unataka nikusaidie, basi nitafanya hivyo tu k**a Chris hatakuwa sehemu ya maisha yako. Jemimah akamwambia sasa sikiliza punda wewe, Chris ni mwanaume wangu, k**a huwezi msaidia akiwepo basi baki na msaada wako... au niseme msaada wa Sabina.
Sabina alisikia akaja akauliza kuna nini tena huku Jemimah, mbona nasikia mnagombana? Jemimah akamwambia hatugombani, nilikuwa naongea na baba wa mtoto wako (baby daddy) 😂😂
Eish angalia Asha na Ray, inaonekana penzi linarudi lakini Asha hafanyi hivi kwa sababu anamjali sana Ray, anafanya hivi kwa sababu wanataka kumtumia Ray kwa manufaa yao. Asha aliletwa hadi nyumbani na akamwambia Ray usijali, ikiwa tutafukuzwa twende Mombasa, nitahakikisha nimekuja kukuona lakini tafadhali, unahitaji kubadilika, hasa wewe na Jemimah na tabia zako za wizi... Ray akashtuka huyu amejua vipi habari zangu na Jemimah, lakini ni Saida aliyemwambia Asha.
Ray alimwambia Asha, niko tayari kubadilika kuwa mwema kabisa mpenzi wangu (empress) bora tu ujue nakupenda, nitabadilika na nitakuwa mtakatifu k**a Nandwa na kazi zake za mtandaoni za takataka 😂😂😂😂 Ghia yaani Ray anaita kazi zangu za takataka jamani na ninyi mmenyamaza tu 🥲🥲

𝐇𝐈𝐕𝐈 𝐍𝐃𝐈𝐕𝐘𝐎 𝐈𝐋𝐈𝐕𝐘𝐎𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝐓𝐀𝐑𝐄𝐇𝐄 𝟖 𝐉𝐀𝐍𝐔𝐀𝐑𝐈 𝟐𝟎𝟐𝟔𝐅𝐈𝐑𝐒𝐓 𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄Chris amerudi nyumbani akiwa na hasira sana, akauliza ...
07/01/2026

𝐇𝐈𝐕𝐈 𝐍𝐃𝐈𝐕𝐘𝐎 𝐈𝐋𝐈𝐕𝐘𝐎𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝐓𝐀𝐑𝐄𝐇𝐄 𝟖 𝐉𝐀𝐍𝐔𝐀𝐑𝐈 𝟐𝟎𝟐𝟔
𝐅𝐈𝐑𝐒𝐓 𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄
Chris amerudi nyumbani akiwa na hasira sana, akauliza Jemimah, "Wewe mwanamke shida yako ni nini? Au madharau yameanza kwa sababu umejua nimeanza kufilisika?" Jemimah akamuuliza Chris, "Shida ni nini? Sikuelewi." Chris akamwambia, "Mbona Celestine alipigwa risasi na hukuniambia na ulikuwa unajua?" Jemimah akacheka 😂😂 akamwambia, "Sikia ng'ombe huyu, kwani kwa sababu mpenzi wako wa kando alipigwa risasi, ni kazi yangu mimi kukuambia? Sindio?" 😂😂😂
Chris anaamini Jemimah anamcheat pia, hadi anamwambia, "Naona mwanaume uliyeanza kudate naye anakuvimbisha kichwa sana." Jemimah anacheka tu, kwa sababu anajua hakuna kitu kingine. 😂😂
Maskini Becka, alifunga vitu vyake ili aondoke, lakini Saida na Asha wakamuona, wakamuuliza, "Unaenda wapi?" Becka akawaambia, "Ni Sabina amenifukuza, narudi zangu Mombasa." Saida akamwambia, "Nenda tu sasa utafanya nini." Becka akawauliza, "Au ni ninyi mmenisaliti nikafukuzwa? Kwa sababu najua sana hamnipendi." 😂😂😂 Saida alicheka tu akamwambia Becka, "Tungetaka utoke huku ungetoka kitambo sana, hatujahusika." Hadi Saida akampea nauli akamwambia, "Hii utanunua machungwa hapo Emali."
Flora alimpigia Sabina simu, akamwambia, "Yule kijana Ray amekuwa huku na akampa Saida pesa, nashuku kuna njama wanapanga." Flora huwa anafanya kazi kisiri (undercover) kwa hii familia na anamwambia Sabina kila kitu. Sabina akajua mara moja kuwa Saida anacheza mchezo fulani.
Jemimah alikuja kwa Ray. Kumbuka baada ya kumwibia yule mzee, pesa Ray alibaki nazo, hivyo Jemimah amekuja kuchukua fungu lake. Sikiliza, mzee aliibiwa pesa taslimu na kadi ya ATM, hivyo Ray alienda ATM akatoa pesa zote za huyo mzee na ndizo hizi anajaribu kuzipanga hapa.
Alimpa Jemimah fungu lake lakini Jemmy akamwambia hata hazitoshi, kwa sababu mahitaji yake ni mengi sana. Ray akamwambia, "Tunaweza kufanya kazi nyingine pia kwa sababu niko tayari kwa lolote." 😂😂😂
Annaliza, Saida na Asha walikuja kwa mwanasheria waongee naye wajue jinsi Tyrona atakavyotoka gerezani. Lakini mwanasheria kumuona tu Asha, akashindwa alimuona wapi, akamuuliza, "Wewe, msichana si wewe ndiye ulikuwa mwanafunzi bora (top student) wa KCSE?" Asha akamwambia, "Ndiyo." Huyu mwanasheria sasa ndiye atawasaidia waone k**a Tyrone atapewa dhamana (bail).
𝐒𝐄𝐂𝐎𝐍𝐃 𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄
Robert akiwa hospitalini aliitwa na muuguzi akamwambia kuna mtu ambaye si wa familia ya Tinah anataka kumuona Celestine, ni mwanaume. Robert akashangaa sana huyu ni nani... kumbe ni Becka! 😂😂
Becka kabla hajaenda Mombasa alikuja kumuona Tinah, na Robert anamjua Becka lakini akamuuliza, "Sabina anajua kuwa umekuja huku?" Bila shaka hapana, kwa sababu Sabina alikuwa ameshafukuza Becka. Becka aliomba sana hadi Robert akamhurumia akamruhusu kumuona Tinah.
Mwanasheria ameshapewa pesa zake na akaahidi atasimama na Tyrone. Lakini mwanasheria akauliza Annaliza, "Nakujua wewe ni rafiki yangu, unafanya haya yote kwa sababu umefukuzwa kazi au unataka Tyrone apate haki?" Anna hakumficha mwanasheria, akamwambia, "Ninafanya hivi ili Robert asishinde baada ya kila kitu alichonifanyia."
Maskini Becka, alikuja akamuona Tinah na huwa anamuita tajiri. Akamwambia, "Nakuhurumia sana tajiri wangu, mimi naondoka na huenda hatutaonana tena. Mamako ashanifukuza, na hata senti moja hajanipa ila namwachia Mungu tu." Haya yote Robert anasikia na anashangaa tu, ni shetani wa aina gani huyu? 😂😂😂
Haya! Saida na Asha kufika nyumbani, Sabina amewasubiri. Akawauliza, "Mbona mnaleta magaidi kwangu? Ray alikuwa anafanya nini hapa?" Saida akamwambia, "Alikuwa amekuja kumuona Asha, kuna shida hapo?" Sabina akawaambia, "Msijaribu upuuzi huo tena." Saida anataka kumpiga Sabina lakini Asha anamshika. 😂😂😂 Saida alijua mara moja ni Flora aliwachongea.
Robert alikuja kwa Sabina. Sabina akamuuliza, "Mbona hukusema unakuja labda nikuandalie chajio?" Robert akamwambia, "Hata sijakuja kula. Nimekuja kukuuliza, shida yako ni nini Sabina?" Sabina akamuuliza, "Ni nini?" Robert akamwambia, "Hata k**a unataka kuwa mshindi wa mchezo huu, mbona unafukuza kila mtu kazi?" Sabina akamwambia, "Ooh, kwa hiyo ni kwa sababu ya Annaliza?" Robert akamwambia, "Hapana, ni Becka. Amekuja hospitali kumuona Tinah na akasema jinsi ulivyomfuta kazi." Sabina akakasirika sana, akamwambia Robert, "Wewe pia ondoka hapa, ukitaka kuwafuata wafuate!" 😂😂😂 Saida na Asha wakiona hivyo, wanafurahia sana.
Siku iliyofuata, Chris ameamka anapata mtoto wake hajala kwa sababu nyumba haina chakula; Chris amefilisika. Chris alikuja kwa Robert akamwambia, "Kaka, najua nilikufanyia vibaya, nisaidie bwana. Ongea na Sabina, najua ni mpenzi wako anaweza kukusikiliza uniokoe." Robert alimwambia, "Kaka, ulisubiri hospitali iishe ukaichukua hisa, kwa hiyo nenda ukafie mbali huko."
Siku ya mahak**ani imefika. Wanaenda mahak**ani wajue k**a Tyrone atatoka au hatatoka. Saida na Asha walitangulia. Sabina anawaambia, "Si ninyi mchukue tu vitu vyenu mwende kuliko kulingoja niwafukuze k**a mbwa?" Saida akamwambia, "Hawa unaowaita mbwa hawatabiriki hata kidogo... chunga sana mdomo wako!" 😂😂😂

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟕𝐓𝐇 𝐉𝐀𝐍 𝟐𝟎𝟐𝟔 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒𝐅𝐈𝐑𝐒𝐓 𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄Ni mwendo wa saa mbili na nusu usiku nyumbani kwa Tyrone. Saida anahisi A...
07/01/2026

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟕𝐓𝐇 𝐉𝐀𝐍 𝟐𝟎𝟐𝟔 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒
𝐅𝐈𝐑𝐒𝐓 𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄
Ni mwendo wa saa mbili na nusu usiku nyumbani kwa Tyrone. Saida anahisi Asha hayuko sawa, na kweli Asha ana msongo wa mawazo kwa sababu hataki mambo ya Ray. Asha analazimishwa kuwa karibu na Ray ili Ray awasaidie kupata pesa za wakili; na si kwamba Ray ni tajiri fulani, la hasha, yeye ni mwizi tu k**a mpenzi wako, lakini kwa sababu anataka kukufurahisha, ndiyo maana anaiba.
Ray na Jemimah wamefika mahali kazi ilipo, na ungejiuliza sana ni mpango gani wanaoendesha, lakini usijali, nawaeleza sasa hivi. Hivi ndivyo mambo yanavyokwenda:
Jemimah na Ray waingie kwenye baa, kisha wajifanye ni wapenzi. Walipoingia, kumbe lengo lao liko huko—kuna mwanamume mmoja tajiri ambaye anapenda sana wanawake. Mpango ni Ray ajifanye Jemimah ni mpenzi wake lakini Jemimah amkatae ili huyu tajiri aone fursa ya kumnyakua 🤣🤣.
Na kweli, wakaona yule mzee anawatazama sana hadi Ray akamwambia Jemimah, "Wallahi wewe ni mrembo sana," kisha akasema anataka kwenda nje kidogo ili mzee huyo aje kumtongoza Jemimah.
Hapo hapo! Ray alipotoka tu, kana kwamba ilikuwa imepangwa, mzee huyo akaja na divai pale Jemimah alipoketi na kumuuliza, "Mrembo k**a wewe mbona unakaa na vijana wadogo wakati mimi niko hapa? Kwa majina naitwa Paul." Wakaanza kupiga gumzo, na hapa ndipo mpango ulipoanza... Ray akarudi na kumuuliza Paul, "Unafanya nini na mpenzi wangu?" Paul akasema, "Kijana tulia, tunazungumza tu." Ray akakasirika na kusema hata halipi bili hiyo kisha akaondoka. Paul akamwambia Jemimah, "Tulia mrembo, mimi nitagharamia kila kitu" 🤣🤣🤣.
Paul akidhani amepata bahati, hajui tayari ameshanaswa.
Ilimchukua Jemimah dakika ishirini tu akawa ameshamuibia Paul pesa kiasi cha shilingi laki moja na hamsini elfu, kisha akatoka nje ya baa, akakutana na Ray na wakaenda zao. Ilikuwa ni mbinu iliyopangwa vyema.
Muda ulienda hadi saa saba ya usiku na ndipo Jemimah anarudi kwake. Kumbuka alitoka kwa siri bila Chris kujua 🤣🤣 lakini siku za mwizi ni arobaini. Kumbe Chris aliamka, akagundua mke wake hayupo, akaketi kitandani kumngoja 🤣🤣.
Jemimah kufika tu, akakutana na Chris mbele yake! Chris akamuuliza, "Umetoka wapi saa hizi?" Jemimah akadanganya, "Nimetoka nje kutembea kidogo." Chris akamwambia, "Usinifanye mjinga, unataka kunidhalilisha, sivyo?" Chris alikuwa amekasirika sana, karibu ampige Jemimah, k**a si mtoto wao kusikia kelele na kuja, Jemimah angekiona cha mtema kuni 🤣🤣.
𝐒𝐄𝐂𝐎𝐍𝐃 𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄
Becka naye alikuja kumuuliza Sabina hali ya Tinah, lakini Sabina akamwambia, "Usinifanye mjinga, najua unashirikiana na Saida." Becka akajitetea, "Hapana mama, mimi nakuheshimu tu, sishirikiani na Saida hata kidogo."
Sabina akamwambia Becka, "Sikiliza, aliyekukubalia uishi hapa yuko gerezani, huyo ni Tyrone. Aliyekuleta hapa yuko chumba cha wagonjwa mahututi (ICU), huyo ni Celestine. Hivyo basi, mambo ni mawili: uende gerezani kwa Tyrone au uende ICU kwa Celestine. Hapa kwangu nakupa dakika tano tu uwe umeondoka." Maskini Bakari! 🤣🤣
Chris naye alikuwa hajui yanayojiri hospitalini. Alipofika huko, akamkuta Robert na kumwambia, "Tafadhali ndugu yangu, nataka kuongea na Tyrone anikopeshe pesa kidogo, mambo si mazuri huku." Robert akamjibu, "Tyrone yuko gerezani kwa kumpiga risasi Tinah, hivyo hutapata msaada."
Chris alishangaa sana; alifika na kumwona Tinah akiwa katika hali ya kupoteza fahamu (coma), lakini kabla hajakaa sana, Sabina akafika akiwa na hasira kali. Akamfukuza Chris na kumwambia Robert asiwahi kumruhusu huyu mtu kumkaribia mtoto wake.
Kumbe Ray naye, katika zile pesa walizomuibia yule mzee, alipewa laki moja. Mapema asubuhi, Ray alienda kwa Saida, akampa pesa hizo na kumwambia ni laki moja. Lakini kosa walilofanya au jambo wasilolijua ni kwamba Flora, yule mfanyakazi wa ndani, ni mja wa Sabina. Hivyo kila kitu walichozungumza na pesa alizopewa Saida, Flora alisikia na kuona. Kosa kubwa sana! 🤣🤣 Saida aligundua Flora anawachungulia, akamwambia, "Ole wako mtu asikie jambo hili, utaona cha moto."
Robert, baada ya kusikia Chris amefilisika, alimpigia simu Jemimah na kumuuliza, "Shida iko wapi? Nasikia Chris amekwama sana." Jemimah akamwambia, "Ndiyo, yuko kwenye matatizo kidogo, alinaswa na sakata la utapeli." Robert akamwambia, "Basi ondoka hapo, wewe na Ivy." Jemimah akamjibu, "Mimi si k**a wewe ambaye naweza kuwaacha watu ninaowapenda." Robert akamuuliza, "Hivyo unajaribu kusema nini?" Jemimah hakumficha, akamwambia, "Mimi si msaliti k**a wewe ambaye unaweza kuwageuka marafiki zako. K**a unataka kumsaidia Chris msaidie, k**a sivyo, usijiingize kwenye mambo ya familia yangu." Lo! Hali ni mbaya...
Saida na Annaliz wanajitahidi kutafuta wakili atakayekwenda kumtoa Tyrone gerezani.
Huku nje, Ray alikuja kumuomba Asha msamaha kwa jinsi alivyomtendea vibaya, lakini Asha akamwambia, "Usijali, nilishakusamehe tayari, usikuwe na wasiwasi." Ray anashangaa imekuwaje amesamehewa haraka hivyo 🤣🤣 hajui kuwa ni mchezo tu Asha anacheza kwa sababu wanahitaji msaada wake. Maskini Ray! 🤣🤣
Mwisho tufollow The Two Cast for daily updates

Vikosi maalumu vya Marekani vimeiteka meli hii inayohusishwa na Urusi baada ya msako mrefu kuanzia nchini Venezuela.Mare...
07/01/2026

Vikosi maalumu vya Marekani vimeiteka meli hii inayohusishwa na Urusi baada ya msako mrefu kuanzia nchini Venezuela.
Marekani imeituhumu meli hiyo kuwa sehemu ya kundi linalojiita "shadow fleet" (msafara wa kivuli) wa meli haramu za mafuta zinazotumiwa na Venezuela pamoja na washirika wao.
Meli hiyo ilipoondoka Venezuela, ilikuwa ikipeperusha bendera ya Guyana. Lakini baada ya msako mrefu wa vikosi vya Marekani vilivyokuwa vimepania kuiteka, ilianza kupeperusha bendera ya Urusi.
Chini ya sheria za kimataifa, meli huwa chini ya ulinzi wa nchi ambayo bendera yake inapeperushwa. Hivyo basi, kwa kutupa bendera ya Guyana na kuchukua bendera ya Urusi baharini, meli hiyo iliingia chini ya ulinzi wa Urusi.
Kutokana na hali hiyo, asubuhi ya leo Putin alituma nyambizi na meli za kivita kwa haraka ili kujaribu kuilinda meli hiyo wakati ikijaribu kukwepa kuk**atwa karibu na Iceland.
Hata hivyo, jitihada za Putin za kuilinda meli hiyo ya siri zilikwama wakati wanajeshi wa Marekani walipoivamia na kuingia ndani mchana wa leo, huku nyambizi na meli nyingine za kijeshi za Urusi zilizokuwa zimewasili eneo hilo zikitazama kwa mbali.
Helikopta ya kijeshi ya Marekani ilionekana ikikaribia meli hiyo.
Ilikuwa ni upinzani mkubwa wa kukatisha tamaa katika Bahari ya Atlantiki.

Ni addiction gani ngumu sana kuwacha?
05/01/2026

Ni addiction gani ngumu sana kuwacha?

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟔𝐓𝐇 𝐉𝐀𝐍 𝟐𝟎𝟐𝟔 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒𝐅𝐈𝐑𝐒𝐓 𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄Sasa ni siku ya pili. Tinah bado hajazinduka kutoka kwa hali ya kupoteza ...
05/01/2026

𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟔𝐓𝐇 𝐉𝐀𝐍 𝟐𝟎𝟐𝟔 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒
𝐅𝐈𝐑𝐒𝐓 𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄
Sasa ni siku ya pili. Tinah bado hajazinduka kutoka kwa hali ya kupoteza fahamu (comma). Sabina alikuja akamuuliza Robert, "Mtoto wangu atapata nafuu kweli?" Robert akamwambia tuwe na imani, kwa sababu Tinah alipoteza damu nyingi sana wakati alipopigwa risasi na wakati wa upasuaji. Sabina alisema wallahi Tyrone atalipia kwa kumweka binti yake katika hali hii... lakini Robert akamwambia, "Ni binti yetu, si wako pekee yako." 😂😂
Baadaye Sabina alikuja katika ofisi ya Tyrone, akaanza tu kutabasamu hadi akaenda kuketi kwenye kiti hicho cha Tyrone. Robert akamuuliza, "Mipango yako ni gani kwa sababu sasa umekalia kiti cha CEO?" Sabina akamwambia, "Sikiliza Robert, Tyrone nahakikisha anaozea jela, hivyo basi hospitali hii ni yangu mimi na wewe." Robert alimwambia awe mwangalifu, Tyrone ana ushawishi na watu wengi.
Robert akamuuliza, "Pia mpenzi, samahani, mbona ukamfuta kazi Annaliza? K**a unataka kuendesha hospitali hii, angekuwa na msaada mkubwa." Sabina akamuuliza, "Msaada mkubwa kwangu ama kwako wewe?" 😂😂😂
Ray naye namba aliyopewa na Tinah haipatikani. Alijaribu kupiga lakini haipatikani, akaamua kuenda mlangoni kubisha. Beckah ndiye aliyefungua mlango, akamuuliza, "Unafanya nini hapa?" Ray akamwambia, "Nataka kuongea na Celestine." Beckah alimwambia, "Wacha upuzi, unataka kuongea na Tinah ama Asha?" Ray akamwambia, "Mimi nataka kuongea na Tinah." Beckah akamwambia Tinah alipigwa risasi na saa hii yuko hospitali.
Ray alikuwa hajui k**a Tinah alipigwa risasi. Akauliza, "Na Asha yuko wapi?" Beckah akamwambia, "Unaona, nilijua tu ni Asha ulitaka kuona alafu unajifanya hapa." Ray akamuuliza, "Asha yuko wapi?" Beckah kwa kiburi akamwambia, "Sikuambii, fanya unachotaka." Ndani ya dakika chache 😂😂😂 Beckah alikuwa ameinuliwa juu na Ray vibaya sana. Ray akamwambia, "Niambie ama ujue mimi ni jambazi."
Asha na mamake walikuwa wameshafika hospitalini huko kwa sababu wameshindwa kupata wakili anayeweza kusaidia Tyrone atolewe, kwani wakili wa Tyrone ameshanunuliwa na Sabina na yuko upande wake. Annaliza pia alisikia maneno hayo, akaambia Asha na Saida, "Kuna rafiki yangu wakili, ngoja nimtafute." Annaliza ana kinyongo na Sabina.
Ray alijileta hospitalini akawapata kina Asha hapo, akasema yeye hajaja kwa ubaya, amesikia tu Tinah alipigwa risasi na amekuja kuona hali yake na pia kuangalia k**a Asha yuko sawa. Saida akamwambia, "Basi ushamuona Asha yuko sawa, unaweza kwenda sasa."
𝐒𝐄𝐂𝐎𝐍𝐃 𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄
Bwana na Bibi Chris ndio wanatoka kituo cha polisi. Mambo hayakuenda vizuri, hadi Jemimah amekasirika sana. Kumbe Chris ameshajulikana kuwa ni tapeli na serikali inamfuatilia sana. Jemimah anamuuliza Chris, "Mbona ukatueka katika maisha haya sasa?" Chris akamwambia, "Nyamaza, nilifanya hivyo ili muishi vizuri, ama wakati mlikuwa mnaishi vizuri hamkujua pesa zinatoka wapi?" 😂😂😂
Saida alifikiria akaona kuwa kwa sasa hafai kuwa na adui k**a Ray. Alimuita Ray akamuuliza, "Si ulisema unampenda Asha na unaweza kufanya chochote?" Ray akasema, "Ndiyo, naweza kufanya chochote kumpata Asha." Saida akamwambia, "Sasa tuko na shida ya pesa, na kwa sababu umesema unaweza kufanya chochote, basi fanya jambo tupate pesa tumtoe mzee gerezani."
Saida ameona ni Ray tu anayeweza kuwasaidia kwa sababu anajua anaweza kwenda kuiba.
Sabina alimwambia Robert, "Sasa hii yote itakuwa yetu kwa sababu nitahakikisha Tyrone anakaa jela kabisa." Robert anamuuliza, "Una uhakika? Kwa sababu Tinah bado anamjua Tyrone k**a babake." Sabina akamwambia ni kwa sababu anahudumiwa vizuri, hivyo akimshughulikia vyema atakuwa sawa.
Saida yuko makini sana, alimwambia Asha, "Nimeshaongea na Ray atumie njia zake apate pesa atusaidie, na wewe ujifanye unampenda kisha baada ya hapo unaweza kumuacha." 😂 In kifupi, Saida anataka tu Ray aende kuiba.
Jemimah naye alikuja kwa Ray, akamwambia kuwa kuna kazi anataka wafanye. Ray akaona hii ni nafasi nzuri kwa sababu yeye pia alikuwa anatafuta sana njia ya kupata pesa, na sasa fursa imejileta yenyewe. 😂😂😂
Robert alimwambia Sabina aende nyumbani, yeye atafanya kazi usiku kucha huku akimwangalia mtoto wao.
🤣🤣🤣🤣 Umeshawahi kuwa umelala kisha mke wako anakuangalia? 🤣🤣🤣 Hivyo ndivyo Jemimah anavyomwangalia Chris; kumbe alikuwa amepanga Chris alale kisha yeye atoke. Huku nje ya lango, Ray alikuwa anamngoja Jemimah. Ungeshangaa sana wanaenda wapi.
Kumbe Robert alimpigia simu Annaliza wakutane, akamwambia, "Tafadhali naomba unisamehe kwa jinsi Sabina alivyokufukuza, mimi si mtu mbaya." Annaliza akamwambia, "Wewe ni mnyama, unawezaje kumgeuka rafiki yako na kutembea na mke wake? Hakika?" Robert akamwambia, "Sijakuita kwa ajili ya hayo, nimekuita kukuambia nakupenda sana."
Annaliza akacheka akamwambia Robert, "Sasa sikiliza, sijakataa kuwa unanipenda, lakini fanya jambo moja: mpite Sabina aje hapa, uniambie unanipenda mbele yake." Robert anajua hawezi kufanya kitu k**a hicho. Annaliza akamwambia, "Ndiyo, nilijua tu 🤣🤣🤣 wewe ni tumbo la nguruwe." Annaliza akaondoka.

Hadithi ya Mercy NjeriKando ya barabara ya kuelekea Kabarak, kilomita chache kutoka mji wa Nakuru, kimesimama kituo cha ...
04/01/2026

Hadithi ya Mercy Njeri
Kando ya barabara ya kuelekea Kabarak, kilomita chache kutoka mji wa Nakuru, kimesimama kituo cha kibiashara cha Mercy Njeri. Katikati ya kituo hiki chenye shughuli nyingi, kuna Shule ya Msingi ya Mercy Njeri, ambayo zamani ilijulikana k**a Shule ya Msingi ya Kiamunyi. Watu wengi hudhania kuwa jina hilo ni la kiongozi mwenye nguvu au tajiri fulani. Lakini Mercy Njeri hakuwa mmoja wapo. Alikuwa mtoto tu.
Aliyezaliwa Kiamunyi mnamo mwaka wa 1975, Mercy alikuwa mwenye afya hadi alipotimiza umri wa miaka sita. Kisha alianza kupata matatizo ya kupumua na kuugua mara kwa mara. Baadaye madaktari walimgundua kuwa na ugonjwa wa moyo (rheumatic heart disease), ambao kwa kawaida hujulikana k**a tatizo la "tundu kwenye moyo."
Mnamo mwaka wa 1985, madaktari walipendekeza afanyiwe upasuaji wa haraka wa moyo nchini Uingereza. Gharama ilikuwa Shilingi 500,000, pesa ambazo familia yake haikuwa nazo. Michango kadhaa iliandaliwa, lakini kiasi kidogo tu ndicho kilichopatikana. Familia hiyo ilianza kukata tamaa polepole.
Kisha, mnamo tarehe 4 Februari 1985, Rais Daniel arap Moi alisimama katika Shule ya Msingi ya Kiamunyi, ambapo Mercy alikuwa mwanafunzi wa Darasa la Tatu. Mwalimu mkuu alielezea hali ya Mercy na kusimulia ndoto yake ya kuwa daktari. Hadithi hiyo ilimgusa Rais sana.
Rais Moi mara moja alichangisha fedha na kumwalika babake Mercy katika Ikulu ya Nakuru. Alilipia gharama zote za upasuaji na safari. Mnamo tarehe 14 Machi 1985, Mercy alisafiri kwa ndege kuelekea Uingereza akiwa amejawa na matumaini.
Mnamo tarehe 29 Machi 1985, Mercy alifanyiwa upasuaji mrefu na mgumu wa moyo uliodumu kwa saa 12. Kwa kusikitisha, alifariki usiku huohuo.
Mazishi yake yalifanyika tarehe 6 Aprili 1985 nyumbani kwa familia yake kule Kiamunyi. Katika hali isiyo ya kawaida, Rais Moi alihudhuria mazishi hayo. Wakati wa ibada, mwalimu mkuu aliomba shule hiyo ipewe jina jipya kwa heshima ya Mercy. Rais alikubali.
Leo hii, jina la Mercy linaendelea kuishi kupitia Shule ya Msingi ya Mercy Njeri, Shule ya Upili ya Mercy Njeri, Kituo cha Kibiashara cha Mercy Njeri, na Barabara ya Mercy Njeri. Jamii nzima imebeba jina la mtoto huyu.

Address

Gandhinagar

Opening Hours

Monday 7:30pm - 8pm
Tuesday 7:30pm - 8pm
Wednesday 7:30pm - 8pm
Thursday 7:30pm - 8pm
Friday 7:30pm - 8pm
Saturday 4pm - 7pm

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Two Cast posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share