18/12/2025
𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟏𝟗𝐓𝐇 𝐃𝐄𝐂 𝐒𝐎𝟒𝐄𝐏𝟑-𝟒 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒
𝐏𝐀𝐑𝐓 𝟏
Mambo yashachemka, Saida ashapigiwa simu kuwa Asha ameshikwa alafu sasa Jemimah na yeye akapiga simu kwa AL, akamwambia AL k**a uko kwa nyumba hepa! Dem wa Ray ameshikwa na najua ataenda kumtaja Ray na akimtaja Ray, Ray lazima atantaja mimi. AL akamuuliza madam sasa unataka tucheze vipi? Jemimah akamwambia sikiliza, nenda kavitafute vile vibaka wa Umoja uongee na huyo kiongozi wao wa nywele nyingi mwenye huwa anatembea k**a mwanamke, umwambie wafanye juu chini, Ray aulizwe (ashughulikiwe) kabla Asha hajamtaja. aah! Makosa. Jemimah ameamua kufuta nyayo sasa. Ray akawekwa wanted na magaidi wengine kwa sababu Jemimah anajua, mradi tu Asha ameshikwa, Ray lazima atatajwa na Ray akishikwa atabanwa vizuri aseme kila kitu, kitu ambacho Jemimah hawezi kutaka kuhatarisha.
Wakati sasa Saida wanatoka na Tyrone kukimbia kituo cha polisi cha Central, acha wafungue lango, wamuone Asha, akilia tu... najua hata pia mnashangaa Asha amefikaje hapa wakati anapaswa kuwa kituo cha polisi... acha sasa niwarudishe nyuma, saa moja lililopita.
Tuliona Asha akiwa ameshikwa anaenda kuwekwa kwenye gari lakini wakati aliangalia nyuma, alimuona Ray.. wakati Asha aliwekwa kwenye gari aliambia polisi sikilizeni, mimi ni msichana tu niliyeingia kwenye mapenzi ya kijinga, mimi hizi pesa si mimi niliyeiba, ni mpenzi wangu ndiye mwizi na mimi si mwizi, mimi ni mtoto wa Daktari Tyrone. Kwanza polisi wakashtuka, wakamuuliza wewe ndio umekuwa unatafutwa? Asha akawaambia ni mimi,. ona sasa mshajua na kwa sababu sitaki kubeba msalaba wa mtu mwingine, mpenzi wangu yuko nyuma ya nyumba amejificha hapo, ningekuwa ninyi ningeenda huko sasa hivi.
Wueh! Mapolisi kusikia hivyo, ndani ya dakika chache walikuwa washamfikia Ray. Ray akakiri akasema yeah hizo pesa Asha hahusiki hivyo Asha akaachiliwa, kisha Ray akawekwa ndani lakini Ray akawaambia kitu kimoja, "siko peke yangu, tuko wengi" polisi akamwambia tutajulia mbele kwa sasa twende.
Hivyo ndio Asha aliachiliwa, akarudi nyumbani na ndio huyu langoni sasa, alafu Jemimah akidhani Ray yuko mbioni (anatoroka), Ray ashashikwa tayari.. mako! Makosa sana, alafu sasa acha niwashtue kitu kingine, leo sijapata taarifa mpya nimekaa nikaona hakuna namna mtalala bila kupenda (like) chapisho langu, nikaamua niandike kitu ambacho hakipo sasa fanyeni hivi, ukiona nimekosa sana, njoo kwangu unipige, univunje-vunje macho na unitoboe mikono.
Follow us The Two Cast part two inakuja